UCHAMBUZI WA TAMTHILIYA YA MACHOZI YA MWANAMKE

 

 IKISIRI 

Utafiti huu umechunguza kauli ya utendwa katika Machozi ya Mwanamke. Kazi kubwa ilikuwa ni kuchunguza jinsi fani na maudhui vinavyohusiana katika kuelezea dhamira ya mwandishi. Mtafiti alikusanya sentensi, akazipa namba, kisha akazichambua kwa kutumia mbinu zilizopendekezwa na (Haliday na Hasan, 1976) na (Kahigi, 1997) huku kukiwa na mabadiliko madogomadogo. Data yetu ilichambuliwa kwa kutumia nadharia za elimu mitindo na naratolojia. Utafiti uligundua kuwa, matumizi ya utendwa yalichochewa na upekee wa lengo la mwandishi, mada iliyokuwa inazungumziwa, pamoja na mazingira ya muktadha wa wakati kitabu kinatungwa. Pia, utafiti uligundua nafsi zote tatu zikitumika katika simulio. Nafsi ya kwanza na ya pili (umoja na wingi) huonesha ukaribu wa nafsi ya mwandishi au wakala wake katika jambo linalozungumziwa; na nafsi ya tatu (umoja na wingi) huonesha umbali wa nafsi ya mwandishi au wakala wake katika jambo linalozungumziwa. 

Kwa hiyo kuna haja ya kufanywa utafiti mwingine katika nyanja mbalimbali ambazo hazikushughulikiwa katika kazi hii kama vile: uandishi wa kitaaluma; masuala ya kisheria; uandishi wa ripoti za vikao; hatua za utafiti wa kisayansi katika maabara; maamuzi mbalimbali ya kiserikali au kiutawala; lugha za magazetini; na kwingineko ili kuona ni kwa nini hutumika lugha ya utendwa badala ya utenda. Vilevile, tafiti zijazo zinaweza kutafiti matumizi ya utendwa kwa kutumia mikabala mingine ambayo siyo elimu mitindo wala naratolojia.  

UTANGULIZI  SURA YA KWANZA 

1.1 Utangulizi 

Mwandishi Ibrahim Ngozi katika uhai wake aliandika kazi kama vile: Mwaka wa George (1987) Ushuhuda wa Mifupa (1990), na Machozi ya Mwanamke (1977). Tamthiliya ya Mwaka wa George ilitokana na kitabu cha George Owel (1984) kilichotokana na Shamba la Wanyama. Ushuhuda wa Mifupa ni tamthiliya inayohusu maradhi ya UKIMWI. Machozi ya Mwanamke inahusiana na harakati za ukombozi wa wanawake. 

Kwanini Ibrahim Ngozi aliita tamthilia yake “Machozi ya Mwanamke?” Machozi ya binadamu hufanana yawe ya mwanaume au mwanamke; kwanini basi tamthiliya hii inayachomoza machozi ya mwanamke kama kitu tofauti? Maswali haya yalinifikirisha zaidi nilipoangalia mwaka ilipoandikwa tamthiliya hii na kusoma marejeleo mbalimbali na kukumbuka yaliyotokea katika kipindi ilipoandikwa tamthiliya hii. Ingelikuwa na mantiki na kuendana sana na matukio ya wakati huo kuhusu ukombozi wa mwanamke kama tamthiliya ingeliitwa “furaha au ushindi wa mwanamke.” Kwa hiyo, kuipa tamthiliya kichwa cha “machozi” kuliongeza udadisi na kudhaniwa kuwa kinachoongelewa hapa ni zaidi ya kile kinachoonekana na kubebwa na kichwa cha tamthiliya. 

Kwa hiyo, maswali kadhaa yalizuka kuhusu kazi hii: Je, ni tamthiliya inayolenga kumtetea mwanamke, na hivyo inajiunga na harakati za wanajamii mbalimbali katika utetezi huo? Lakini kama tamthiliya ingelikuwa inamtetea mwanamke, kwanini itumie “machozi?” Na tena mchoraji wa picha iliyopo katika jalada la tamthilia hii aliamua kuwaonesha wasomaji, mwanamke anayetiririkwa na machozi. Lugha ya picha na lugha ya maneno - vyote vinaonesha kinyume cha mambo yanayodhaniwa yangelijenga muktadha unaosawiri yaliyojiri wakati kitabu hiki kinaandikwa. Je, ni nini mwandishi alitaka kuwaeleza wasomaji? Maswali haya yalichochea ari yangu ya kutaka kuichambua zaidi tamthiliya hii na hasa nikiangalia lugha yake na uhusianao wake na dhamira kuu. Kutokea katika mtazamo huu, uchambuzi na uhakiki ambao uliteuliwa uliegemea katika nadharia inayoangalia jinsi lugha inavyoumba dhamira. Wanazuoni wamejadili mikabala mbalimbali ya kuchambua na kuhakiki kazi za fasihi. Baadhi yao ni kama vile (Jameson, 1971); (Williams,1977); (Eagleton, 1978); hawa wameangalia zaidi kwa mkabala wa Kimarx katika uchambuzi wa kazi za kifasihi. Kwa kifupi, waliangalia kazi za kifasihi kama zao la matabaka likionesha ukinzani na mivutano miongoni mwa matabaka katika jamii, na wanafasihi (waandishi) kama wanaotetea tabaka moja wanaloliandikia dhidi ya tabaka jingine. Kwa upande mwingine, (Senkoro, 1987); na (Spivak, 1990); tukionesha kwa uchache tu, ni wanafasihi waliojikita kuchambua na kuhakiki wakitumia zaidi mikabala ya Kibaadaukoloni; na (Wamitila, 2001) yeye ameangalia mikabala mbalimbali kwa pamoja. Kila mkabala huwa na kaida zake na malengo yake. Katika mikabala hii waandishi, huchambua kwa kuzingatia fani au maudhui ya kazi husika, au vipengele vinavyotokana navyo. 

Katika mikabala hii pia huangaliwa uhusiano na athari za jamii na waandishi wa kazi hizo za kifasihi; au mwingiliano kati ya kazi na kazi nyingine na athari zake katika jamii. Utafiti huu unakusudia kuchambua tamthiliya ya Machozi ya Mwanamke (Ngozi,1977) kwa kutumia mikabala miwili ambayo ni: mkabala wa kielimu mitindo, na mkabala wa kinaratolojia. Kwa ujumla wake, na kama itakavyoangaliwa kwa undani baadaye, elimu  mitindo inaangalia lugha inavyojishughulisha katika kuiwakilisha dhamira ya mwandishi. Hasa, elimu mitindo inahusisha misingi ya kiisimu katika kuchambua kazi ya fasihi. Katika utafiti huu, kipengele cha kiisimu kinachohusika ni matumizi ya kauli ya utendwa, na namna kauli hii inavyojipambanua katika fasihi ya Kiswahili kupitia katika tamthiliya ya Machozi ya Mwanamke; na kwa upande mwingine mkabala wa kinaratolojia huchambua usimuliaji wa hadithi kwa kubaini nafsi mbalimbali na utambuzi wa msemaji katika simulizi inayohusika. 

Utumiaji wa nafsi hudhihirisha ukaribu au umbali wa nafsi ya mwandishi katika simulio. Kwa kutumia mikabala hii miwili, madhumuni ni kuangalia uhusiano uliopo kati ya dhamira za mwandishi katika tamthilia hiyo na kauli za utendwa anazozitumia. Sentensi ya utendwa ni mtiririko wa taarifa kwenye sentensi unaoonyesha kuwa kiima ni mtendwa. Jambo hili linatokeza maswali kadhaa kuhusiana na dhamira na wahusika au wasemaji katika kazi hii ya kifasihi. Ni mambo gani humfanya mtumiaji wa lugha kuchagua utendwa badala ya utenda katika mazingira ambamo kauli yoyote ingeliweza kufaa? Kwa muktadha wa utafiti huu, swali jingine la kujiuliza ni je, ni vipengele na mazingira gani yalimfanya mwandishi wa tamthilia ya Machozi ya Mwanamke kuchagua zaidi utendwa kuliko utenda katika kuwapa lugha ya majibizano wahusika wake? Uchaguzi huo wa mwandishi unaangaliwa katika utafiti huu kama suala la elimu mtindo. Tunauangalia mtindo wa mwandishi na jinsi unavyoweza kuathiri, sio tu mawasiliano na mahusiano baina ya wahusika, lakini hata pengine ujumbe na dhamira zibebwazo na wahusika wenyewe. Hapa ndipo matumizi ya nadharia ya naratolojia yanapojitokeza. Je nafsi ambazo msomaji anakutana nazo katika usomaji wa tamthilia hii zinamwakilisha nani katika  jamii? Katika kuumba kauli za utendwa kutoka katika hali ambayo ingeliweza kuwa ni utenda, kunatokea pia mabadiliko ya maumbo; mabadiliko ya mpangilio wa maneno na sentensi; na mabadiliko ya uelekezi yanayoambatana na kauli ya utendwa. Mabadiliko haya yanaathiri namna utolewaji wa kazi yenyewe unavyokuwa na hata kuzielekeza dhamira katika mwelekeo fulani.

Kwa ujumla, tutakachofanya hapa ni kuchambua ili kutambua uteuzi huo wa kauli moja badala ya nyingine unaendana na nini katika sentensi azitumiazo mwandishi. Je, katika tamthilia inayochambuliwa, uteuzi wa matumizi ya kauli ya utendwa unategemea mhusika anayesema ni nani? Je, ujenzi wa sentensi za mhusika fulani katika tamthilia umejitokeza kwa kufuata utaratibu maalumu au la? Kama ilivyoelezwa hapo juu, kauli ya utenda na ile ya utendwa huelezea taarifa inayofanana kidhana na sio kimguso. Katika utafiti huu, kinachozingatiwa zaidi ni athari za kimawasiliano baina ya wahusika kwa kuangalia matumizi ya utendwa yakitofautishwa na yale ya utenda. Kwa vyovyote vile, athari inayojitokeza kisentensi kutokana na kauli hizo mbili ni ile ya mwonekano wa vijenzi, ambao unahusisha mabadiliko ya maumbo; mabadiliko ya mpangilio; na mabadiliko ya uelekezi kama itakavyogusiwa katika sura ya pili. Mabadiliko haya yanaweza kuangaliwa kama tabia ya mnyambuliko ya lugha, tabia ambayo ni mojawapo ya sifa za kiisimu za lugha ya Kiswahili. Tabia hii ya mnyambuliko wa lugha ndiyo kiini cha tofauti za kimtindo. Mnyambuliko huu ndio unaowezesha kusema kitu kilekile kwa namna tofauti. Dhana ya “namna tofauti” ndiyo inayobeba uzito wa kiini cha utafiti huu. Kiini ambacho kinalenga kujua ni kwa nini hutokea  namna tofauti za uzungumzaji wa jambo lile lile mbali na mabadiliko ya mpangilio wa maneno na sentensi.

Katika utafiti huu, kinachoangaliwa ni kauli hizi za utendwa kama suala la mtindo wa mwandishi. Kwamba, wahusika wanaotoa kauli za utendwa wanabeba dhamira iliyojificha ambayo ni sauti ya jamii katika harakati za ukombozi wa mwanamke. Yaani, kwa kuangalia dhamira za mwandishi na uhusiano wake na mtindo anaoutumia kutolea dhamira hizo, imewezesha kuuona upekee wa mwandishi katika kazi yake. Upekee huu unatokana na uteuzi au uchaguzi wa kipengele kimoja badala ya kingine, katika mazingira ambamo kimoja au kingine kingeliweza kufaa. Jambo hili la mtindo kama suala la uchaguzi limeshughulikiwa na wataalamu kadhaa. Kwa mfano, (Halliday & Hasan, 1976), na (Leech & Short, 1981) wanauelezea mtindo kuwa ni uteuzi au uchaguzi wa kipengele kimoja badala ya kingine.

Kwa kutumia mawazo ya wataalamu hawa na wengine waliotafiti suala la mtindo katika lugha ya Kiswahili, kazi hii imeichambua Tamthilia ya Machozi ya Mwanamke, ikiangalia uhusiano kati ya yale yasemwayo na namna yanavyosemwa. Je, mwandishi anasukumwa na nini katika kuteua kauli moja na kuacha nyingine? Katika kujibu swali hili na mengine yaliyoulizwa hapo kabla, kazi hii imegawanywa katika sura tano. Sura ya kwanza imeshughulikia kiini cha utafiti kwa ujumla. Inatoa utangulizi wa kile kinacholengwa kutafitiwa na sababu zake ikigusia vipengele vya: maswali ya utafiti, tatizo linalotafitiwa au wazo kuu la utafiti, malengo na umuhimu wa utafiti, na kisha, mipaka ya utafiti huu. Kiini hiki cha utafiti kimetokana na yale yaliyoonwa katika sura ya pili. Katika sura ya pili, utafiti unapitia marejeo na tafiti mbalimbali zilizoandika kuhusu mawazo  na vipengele muhimu vinavyojenga kazi hii. Katika kupitia marejeo, uhakiki umefanywa kuona ni yapi yamefanywa kuhusiana sio tu na suala la utendwa na utenda, bali pia tafiti kuhusu elimu mitindo na lugha ya Kiswahili kwa ujumla, na kuhusu nadharia ya naratolojia. Kutokana na yale yaliyoonwa katika sura ya pili, kazi hii imechagua nadharia zitakazotumiwa na mbinu za utafiti ili kutimiza malengo ya utafiti. Mbinu za utafiti zilizotumika zimeelezwa katika sura ya tatu.

Katika sura ya tatu, kinachoangaliwa ni mbinu za utafiti ikiwa ni pamoja na njia za ukusanyaji data, data zilizotumiwa, mahali zilipopatikana data hizo, na mbinu za uchambuzi wa data husika. Vipengele hivi vyote vimeangaliwa kupitia katika viunzi vya kinadharia vilivyochaguliwa ili kujenga hoja za utafiti huu. Hoja hizi ambazo ni matokeo ya utafiti zinajenga mjadala katika sura ya nne. Sura ya nne, ni mjadala ambao unalenga kujibu maswali ya jumla yaliyoulizwa katika utafiti huu, na hasa majibu ya maswali matatu mahususi. Ni sura inayowasilisha matokeo, inayafafanua na kuyachambua, ikijenga mjadala kuhusu matumizi ya utendwa kama suala la mtindo katika kazi ya Machozi ya Mwanamke. Kutokana na mjadala huu, sura ya tano inakuwa ya hitimisho na mapendekezo kwa ajili ya tafiti za baadaye. Kazi hii yenye sura tano imeongozwa na mawazo kuwa Ibrahim Ngozi alichagua na kuwapatia wahusika wake katika Machozi ya Mwanamke kauli za utendwa huku akijaribu kupambana na mfumo uliomkuza kama mwandishi wa dhamira ya ukombozi wa mwanamke. Vilevile, tamthiliya hii imechambuliwa na (Mtiro, 2005) akiangalia taswira ya mwanamke kama mnyanyaswaji, mdhulumiwa, asiyejiamini, na msomi. Hata hivyo, tuangalie kwanza tatizo la kiutafiti tunalolishughulikia.

1.2 Tatizo la utafiti 

Waandishi wa kazi za kifasihi ni zao la jamii mahususi. Yale wayaandikayo katika kazi hizo, sio tu huchotwa kutoka jamii hiyo, bali pia huakisi kwa kiasi kikubwa hali ya jamii waliyomo. Hali hiyo huchangamana ikiwa na masuala ya kijamii na kiutamaduni, kiuchumi au hata kisiasa. Mchangamano huo wa kazi ya kifasihi unaumbwa kutokana na uteuzi wa lugha na tamathali mbalimbali kwa kadri anavyotaka mwanafasihi, yaani mwandishi wa kazi husika. Katika mfumo dume, lugha nayo huwa ni nyenzo mojawapo ya kuendelezea mfumo huu. Jamii hutumia lugha ambayo huwakandamiza jinsia moja na kuiinua jinsia nyingine kwa njia isiyo ya moja kwa moja. Wakati mwingine jambo hili hutokea kwa kukusudia, lakini mara nyingi lugha hutumika bila ya makusudi hayo na watumiaji hawatambui athari za matumizi yao ya lugha fulani katika mawasiliano. Kwa mfano, katika Machozi ya Mwanamke, ingawa mwandishi amejitoa kuongelea ukombozi wa mwanamke, ni kwa kiasi gani lugha yake anayoitumia inaakisi mawazo na dhamira yake hiyo ya ukombozi? Kwa kutumia nadharia ya naratolojia, je, mwandishi ana uchaguzi kiasi gani kuitumia lugha anayoitaka kuumba dhamira za kazi yake ya kifasihi? Kwa maneno mengine, je, mwanafasihi huyu ambaye ni zao la jamii huongozwa na nini katika uteuzi wake wa lugha ya kutumia katika kazi yake? Je huongozwa na kaida zilizomo katika lugha au huvutwa na masuala yaliyo nje ya lugha – kama ya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni? Ni kwa njia gani mhakiki wa kazi ya kifasihi anaweza kuthibitisha kuwa mwandishi fulani aliongozwa na jambo moja au jingine katika uteuzi wa lugha ili kuufikisha ujumbe uliomo katika kazi yake? Maswali haya yanaweza kuangaliwa kwa njia nyingine: je, ikiwa mwandishi ana uhuru wa  kuchagua, kuna sababu yoyote inayoweza kuelezwa kuwa kigezo cha uchaguzi wa maneno fulani, au muundo wake, na kuacha maneno mengine au muundo wake? Kwa mfano, ikiwa lugha ina miundo ya utendwa na utenda, je kwa nini na ni katika mazingira yapi mwandishi atateua na kupendelea matumizi ya muundo mmoja zaidi ya muundo mwingine? Maswali haya ambayo yanajenga kiini cha tatizo linalojadiliwa katika kazi hii, ni maswali ya kielimu mitindo, lakini pia yanagusa nadharia ya usimulizi au naratolojia. Kwa mujibu wa uelewa wa mtafiti, na kutokana na kupitia marejeo mbalimbali, suala la elimu mitindo limeangaliwa na wanazuoni mbalimbali. Hata hivyo, hakuna aliyeangalia matumizi ya utendwa kama suala la uchaguzi katika Tamthilia za Kiswahili. Yaani, nadharia ya elimu mitindo haikuwahi kutumika katika kuchambua vigezo vya uteuzi wa utendwa katika kazi ya kifasihi ya Kiswahili. Utafiti huu, una lengo la kuchangia mkabala huu kwa kutumia tamthilia ya I. Ngozi ijulikanayo kama Machozi ya Mwanamke. 1.3. Maswali ya Utafiti 1. Je kuna uhusiano wowote kati ya dhamira kuu ya mwandishi na matumizi yake ya kauli za utendwa? 2. Je ni katika mazingira gani mwandishi anawafanya wahusika wake kutumia kauli za utenda na utendwa? 3. Je, kuna uhusiano gani kati ya dhamira ya mwandishi na ujenzi wa maonesho na sehemu za tamthilia? 20 1.4. Malengo ya utafiti Utafiti huu umeongozwa na malengo ya aina mbili ambayo ni ya jumla na mahsusi. 1.4.1 Lengo la jumla Kuangalia uhusiano uliopo kati ya dhamira kuu ya mwandishi na matumizi ya utendwa ambayo yanachochewa na upekee wa lengo la mwandishi, muktadha, na mada inayozungumziwa. 1.4.2 Malengo mahususi 1. Kuchambua dhamira kuu ya mwandishi na uhusiano wake na kauli ya utendwa. 2. Kuelezea muktadha au mazingira ya ujitokezaji wa kauli za wahusika za utenda na utendwa. 3. Kufafanua jinsi mfuatano wa maonyesho na sehemu za tamthilia ulivyo na uhusiano na lugha na dhamira kuu. 1.5 Umuhimu wa Utafiti Utafiti huu umekusudia kuongeza uelewa kuhusu uhusiano wa maudhui na fani katika kazi ya fasihi kwa mkabala wa kielimu mitindo na utambuzi wa nafasi ya mwandishi kama msimulizi katika kuisemea jamii. Katika maudhui, kazi inachagua dhamira kuu na katika fani, utafiti unaangalia lugha na hasa kipengele cha kauli ya utendwa ili kubaini uhusiano huo. Katika kuangalia uhusiano huo, utafiti huu umetumia nadharia za elimu mitindo na naratolojia ili kujenga kiunzi cha uchanganuzi na mjadala katika kuchambua kauli za utendwa. Kwa kufanya hivyo, utafiti huu unajenga hoja kuwa kauli ya utendwa inaweza kuangaliwa nje ya 21 matumizi ya kawaida ya kiisimu, ikatumika kama mbinu ya kielimu mitindo; katika kuchambua kazi za kifasihi kama ilivyofanywa kwenye tamthilia hii ya Machozi ya Mwanamke. Hii ni nyongeza katika mbinu za uchambuzi wa kazi za fasihi ambayo inaweza kuwasaidia wachambuzi katika viwango mbalimbali. 1.6 Mipaka ya Utafiti Utafiti huu unazungumzia matumizi ya kauli ya utendwa, kama mbinu ya kimitindo katika tamthilia ya Machozi ya Mwanamke. Ingawa kwa ujumla wake uhusiano unaoangaliwa unagusa dhana za fani na maudhui, utafiti huu haukukusudia kuichambua tamthilia hii kwa mikabala ya fani na maudhui. Dhana hizo zinatajwa tu kwa kuwa ndizo zinazobeba lugha ambamo kipengele cha utendwa kimo ndani yake; na upande wa maudhui ndio unaobeba kipengele cha dhamira ambacho uhusiano wake unaangaliwa. Kwa hiyo, tathmini ya utafiti huu iwe katika wigo huu wa kielimu mitindo na sio nje ya hapo. Vilevile, kauli za utendwa zilizohusishwa katika utafiti huu ni zote mbili: yaani utendwa wa hiari na ule wa lazima. Kauli za utendwa wa hiari ni zile zinazompa uhuru mtumiaji, wa ama kutumia kauli ya utendwa, au kauli ya utenda. Kauli za utendwa wa lazima ni zile zisizotoa uhuru (au uchaguzi) kwa wasemaji kutumia kauli zote mbili (yaani kauli za utendwa wa lazima kama yalivyo matendo yenye mahusiano ya kingono). Kwa hiyo, kauli hizi za utendwa wa lazima zimehusishwa kwa kuzingatia suala la utamaduni ambao humtaka mwanamke na mwanaume wawe na namna tofauti za kuzungumzia maswala hayo. Kwa hiyo, katika lugha kuna uhuru, lakini katika utamaduni hakuna uhuru. Hii inalenga kumwangalia mwandishi kama msimulizi kwa kutumia nadharia ya usimulizi (naratolojia) ili kubaini nafasi yake katika kuisemea jamii. 22 1.7 Hitimisho Katika sehemu hii ya utangulizi, umewekwa msingi wa utafiti ambao ni matumizi ya kauli ya utendwa kama mbinu ya kielimu mitindo. Limejadiliwa tatizo, malengo, umuhimu, na mipaka ya utafiti huu. Katika sehemu inayofuata yamejadiliwa mapitio mbalimbali ya makala na vitabu ambayo yameshughulikia kazi kielimu mitindo, na matumizi ya kauli ya utendwa katika lugha mbalimbali. Vilevile, katika sura hiyo, kumejadiliwa kiunzi cha nadharia zinazotumika katika uchambuzi huu. Nadharia hizo ni: elimu mitindo, na naratolojia au usimulizi ili kubaini nafasi ya mwandishi kama msimulizi na nafsi anazozitumia kupitia wahusika wake.

SURA YA PILI MAPITIO YA MAREJEO NA KIUNZI CHA NADHARIA

2.1 Utangulizi 

Katika sura hii, marejeo yanayoongelea utendwa yatachambuliwa ili kubaini jinsi wataalamu walivyouangalia utendwa kwa mikabala mbalimbali. Aidha, machapisho mbalimbali yanayozungumzia nadharia za elimu mtindo na naratolojia yatarejelewa na kuhakikiwa ili kujenga mkabala tutakaoutumia katika utafiti huu. Katika sehemu 2.2 tutaangalia kazi zilizoshughulikia utendwa nje ya lugha ya Kiswahili. Katika sehemu 2.3 tutaangalia kazi zilizoshughulikia utendwa katika Kiswahili. Sehemu 2.4 tutaangalia kazi zilizoshughulikia elimu mitindo. Katika sehemu 2.5 tutajadili kiunzi cha nadharia, nadharia ya elimu mitindo itajadiliwa katika sehemu 2.5.1. Nadharia ya mtindo kama uchaguzi au uteuzi itajadiliwa katika sehemu 2.5.1.1 , na nadharia ya mtindo kama utofauti itajadiliwa katika sehemu 2.5.1.2. Katika sehemu 2.5.2 tutajadili nadharia ya naratolojia. Wahusika katika kazi za fasihi watajadiliwa katika sehemu 2.6. Wahusika katika nadharia ya naratolojia watajadiliwa katika sehemu 2.7, na katika sehemu 2.8 litafanywa hitimisho. 2.2. Kazi zilizoshughulikia utendwa nje ya lugha ya Kiswahili Katika lugha kama vile Kiingereza, kauli ya utendwa inatumika kwa sababu mbalimbali kama vile: kwanza, kukwepa lawama ya kutotaja mhusika wa tukio fulani hasa katika kutoa taarifa za kiuchunguzi na kiupelelezi. Pili, ni mbinu ya kuficha haiba ya mtu hasa kama ni kiongozi wa kisiasa mwenye kashfa fulani. Tatu, kuna urahisi wa kutumia kauli ya utendwa kuliko 24 kutumia kauli ya utenda katika mazungumzo ya kila siku. Nne, ni kama humjui mtenda wa jambo fulani ni bora kutumia kauli ya utendwa. Tano, ni katika ripoti za kiutafiti kwenye maabara ambapo kauli ya utendwa husisitiza jambo na si mtu (Hansard,1995, para.2). Kwenye lugha ya Kirusi, kauli ya utendwa inatumika sana kuliko inavyotumika katika Kiingereza. Sababu za kutumia kauli ya utendwa katika Kirusi ni kutokana na ukweli kwamba, watumiaji wa lugha hii hupendelea kuzungumzia mambo mbalimbali kwa kutumia nafsi ya tatu; badala ya nafsi ya kwanza na ya pili. Hii ni kwa kuwa, utendwa husaidia kuondoa nafsi ya mtenda (Russian Language Centre, 2008, para.2). Ikichunguzwa lugha ya Kispaniola, muundo wa kauli ya utendwa unafanana na ule wa kauli ya utendwa katika Kiingereza kwamba, kunakuwa na umbo la “ser” likifuatiwa na hali timilifu ya kitenzi. Na katika lugha hii ya Kispaniola, kauli ya utendwa si maarufu sana kama ilivyo katika Kiingereza, kwani wataalamu wa uandishi husisitiza kutoitumia. Badala yake wanasisitiza kutumia kauli ya utenda ambayo inawezesha kueleweka vizuri bila uvulivuli wa maana (Erichsen, 2008, para 7). Katika lugha ya Kijerumani, kauli ya utenda na ile ya utendwa zinatumika zote katika kuelezea jambo lile lile ila tofauti inakuwa ni namna au mbinu inayotumika katika kuelezea. Kwa maana hiyo, kunakuwa na tofauti ya mtazamo. Kauli ya utendwa inatumika sana katika lugha ya Kijerumani na aina hii ya lugha inapatikana sana katika kazi za kitaaluma kwa sababu kuu mbili ambazo ni: kwanza, kuondoa taasubi ili utafiti ujisemee wenyewe; na pili, ni mtindo wa uandishi ambao hauhusishi nafsi ya mwandishi (Verhuist, 2005, para. 1). 25 Vilevile, kauli ya utendwa katika Kijerumani inatumika pale ambapo mtenda wa jambo si muhimu na kilicho muhimu ni kitendo alichofanya. Na mwisho kabisa matumizi haya ya utendwa katika lugha ya Kijerumani yanatokana na kiima cha sentensi kuwa kirefu, ambapo kiima hiki hupelekwa mwishoni mwa sentensi. Kwa maneno mengine, mtenda anapelekwa mwishoni mwa sentensi na yambwa ndiyo inayokaa katika sehemu ya kiima (Verhuist, 2005, para 1). Kwenye lugha ya Kiitaliano, kauli ya utendwa haitumiki sana kama ilivyo katika lugha ya Kiingereza. Katika lugha hii, kauli ya utendwa hutumika kama silaha ya kukwepa lawama. Pia inasisitizwa sana katika maandishi kwa kuwa ndivyo inavyoshauriwa na wataalamu wa maswala ya uandishi. Katika lugha ya mazungumzo, kauli ya utenda ndiyo inayotumika (Picarazzi, 2006, para.2). Katika lugha ya Kifaransa, matumizi ya utendwa huepukwa pale inapobidi hasa mtenda wa jambo akiwa anajulikana. Na inapotokea mtenda hajulikani, basi hapo ndipo inashauriwa kutumia kauli ya utendwa (Stein, 2004:167). Hali hii si tofauti katika lugha zote ambazo tumezijadili hapo juu - yaani katika Kijerumani, Kirusi, Kiingereza, Kiitaliano, na Kifaransa. Matumizi ya kauli ya utendwa yanatumika sambamba na matumizi ya kauli ya utenda kwa kuzingatia njia ya mawasiliano inayotumia (kama ni uandishi au mazungumzo). Vilevile inatokana na uamuzi wa mzungumzaji kusema wazo lake kwa namna anayoitaka. Ila katika Kispaniola, hali ni tofauti kwani inashauriwa kutotumia kauli ya utendwa badala yake kinachosisitizwa ni matumizi ya kauli ya utenda. 26 Hansard (1995) anaeleza kuwa: Kauli ya utendwa ni kitendo kinachojitokeza katika vitenzi elekezi ambapo nafasi ya mtenda huweza kudondoshwa kutokana na sababu mbalimbali kama vile kutokuona umuhimu wa kumjua mhusika aliyetenda jambo fulani (para.1). Kwa maana hiyo, nafasi ya mtenda hudondoshwa kutokana na kutokuona umuhimu wake katika mazungumzo kwa sababu kilicho muhimu ndicho kinatajwa. Mara nyingine nafasi hii ya mtenda hudondoshwa kutokana na sababu ya kutofahamika kwake. Hivyo, badala ya wazungumzaji kutaja wahusika wa jambo ambalo hawana uhakika nalo, hujikuta wakimdondosha mtenda. The Writing Center (1998) inaeleza kuwa Matumizi ya kauli ya utendwa si kosa la kisarufi bali ni aina ya lugha ambayo inatumika sana katika ripoti za maabara. Hapa msomaji anahitaji kujua hatua zinazofuatwa katika utendekaji wa jambo na hahitaji kujua nani ni mhusika wa jambo fulani au nani katenda kitendo husika (para.1). Hii ina maana kuwa, katika ripoti za uchunguzi unaofanywa maabara, hatua za kufanya utafiti huo huandikwa kwa kutumia kauli ya utendwa. Vilevile hutumia nafsi ya tatu badala ya nafsi ya kwanza, na vitenzi vyenye udhahania ndivyo hutawala katika uwanja huu. Kwa kufanya hivyo, mwandishi hujiondoa nafsi yake katika ripoti ya kiutafiti, na jambo hili linaupa utafiti uhuru ili ujisemee wenyewe. 27 Alfreld, Alred, Brusaw, na Oliu (2006) wanadai kuwa: Kauli ya utendwa hutumika katika maandishi ya kisayansi na kiufundi ambayo yanapaswa kuungwa mkono kwa sababu huweza kuifanya kazi kutohusishwa na mtu wala taasisi yoyote ile, na hivyo inakuwa mbali na mwandishi au mtu. Hii ni tabia ya lugha ya kisayansi au kiufundi ambayo huondoa taasubi katika taarifa au ripoti ya utafiti (para.1). Ufafanuzi wa sababu hii ya matumizi ya kauli ya utendwa unaweza kufanana kidogo na hapo juu tulipoeleza kuhusu ripoti za kimaabara, kwani vyote hivi vinahusiana. Hii ni kwa kuwa, viko katika kundi moja - yaani maswala ya utafiti wa kimaabara na ripoti za kisayansi na kiufundi. The Writing Centre (1999) inaeleza kuwa: Matumizi ya kauli ya utendwa yanaweza kuwa ni ya kisiasa zaidi kwa maana kuwa, kauli ya utendwa hujitokeza pale ambapo mtenda wa jambo hatajwi ili kuficha haiba yake kwa lengo la kumhifadhi asidhalilike mbele za watu. Kwa hali hiyo, muktadha unajibainisha wazi kuwa ni nani anasemwa (para.1). Hii ina maana kwamba, maswala ya kisiasa yanagubikwa na kashfa mbalimbali zinazotokana na upotovu wa maadili ya baadhi ya viongozi wa kisiasa. Hivyo, wanapokumbwa na kashfa hizo inakuwa ni vigumu sana kuandika wazi kuwa mwanasiasa huyo amefanya jambo gani. Hii ni kutokana na sababu kwamba, mambo hayo hayaleti picha nzuri kwa jamii ambayo 28 anaiongoza. Hivyo, matumizi ya kauli ya utendwa husaidia kumstahi kwa kutokumtaja. Kolln (1994) anadai kuwa, kutumika kwa utendwa: Ni kwa lengo la kuondokana na lawama zinazoambatana na mamlaka aliyo nayo mtu katika kazi au majukumu ya kutoa uamuzi wenye athari kiutendaji. Badala ya kutumia kauli ya utenda kutoa maamuzi basi, kauli ya utendwa hutumika ili kutokujihusisha au kutokujifungamanisha na utendaji wa tukio lenyewe. Hii ni mbinu ya kukwepa lawama (para.5). Suala la kutoa uamuzi wa kiutendaji ni gumu kwa baadhi ya watu kwa kuwa wanaogopa kufungamanishwa au kuhusishwa na maamuzi hayo. Mbinu nzuri inayowezesha kukwepa lawama hizi ni kwa kujiondoa ili usijibainishe wazi kuwa wewe ndiye uliyetoa uamuzi fulani. Na yote haya yanawezekana kwa kutumia kauli ya utendwa ambayo inakuwezesha kusema kile unachotaka kukisema pasipo na ulazima wa kubainisha nafsi yako. Hansard (1995) anaeleza kuwa: Kauli ya utendwa ni uchaguzi mzuri mara nyingi husisitiza wazo la msingi. Msisitizo unawekwa mwanzoni, kwa hiyo kauli ya utendwa ndiyo inayowezesha kusisitiza jambo badala ya kusisitiza mtendaji wa jambo. Huu unaweza kuwa ni mchomozo katika sentensi (para.1). Jambo hili la kudakiza mbele kile kinachosemwa limekuwa ni la kawaida sana katika lugha 29 mbalimbali duniani kwa kuwa watu wanataka kusikia taarifa zinazohusu tukio lilivyofanyika au litavyofanyika na sio kumjua aliyefanya au atakayefanya tukio hilo. Kwa maneno mengine, inawezekana kusema kuwa, jambo la msingi ndilo linalowekwa sehemu ya mwanzo wa sentensi na yale yanayowekwa mwishoni ni kwamba yana umuhimu mdogo/hafifu. Hansard (1995) anafafanua matumizi ya utendwa kuwa “ni pale ambapo hujui nani amefanya jambo fulani, kwa hiyo ni vema kutumia kauli ya utendwa kwa sababu huna uhakika wa mtenda wa jambo unalolisema”. Sababu hii inaweza kufafanuliwa kuwa, inapotokea humjui mhusika wa jambo fulani ambalo limetokea, ni bora kutomtaja mtu yeyote kwani huna uhakika na taarifa hiyo. Jambo hili linaweza kuwa na maana sana kama tukio lililotokea ni baya mfano wa ajali za barabarani, na kama aliyesababisha ajali hiyo hafahamiki. Kwa hiyo, inakuwa ni bora kuzungumza kwa kutumia kauli ya utendwa kama vile mtu amegongwa badala ya kusema fulani amemgonga mtu kwani kwa kubainisha huyo fulani ambaye huna uhakika naye, utakuwa umejiingiza kwenye matatizo kwa sababu za kiupelelezi ili kuisaidia polisi. Hansard (1995) anadai kuwa, matumizi haya ya utendwa hutokana na “kama wasomaji wako hawahitaji kujua nani kafanya jambo, bali wanachotaka kujua nini kimefanyika, basi ni vema kutumia kauli ya utendwa”. Wakati mwingine wasomaji au wasikilizaji wa taarifa fulani, hawataki au hawahitaji kumjua mtu aliyefanya jambo fulani, ila tu wanataka kujua jambo hilo lililofanyika au litakavyofanyika. Katika muktadha huu, mzungumzaji hana budi kufanya 30 hivyo kulingana na hadhira yake inayomsikiliza. Jaspersen “alikuwa ni miongoni mwa wanaisimu wa mwanzo kabisa kushughulikia jambo hili la matumizi ya kauli ya utendwa. Wanaisimu waliofuata baadae waliiga tu aliyoyasema Jaspersen, kwa maneno mengine, hawakuwa na jambo jipya waliloliibua” (kama ilivyonukuliwa katika Mkude, 2005:171). Jaspersen alibainisha mazingira yafuatayo ambayo yanasababisha matumizi ya kauli ya utendwa ambayo ni: kwanza, ni “kama mtenda halisi wa jambo hajulikani au habainiki kwa urahisi”. Pili, ni “kama mtenda halisi wa jambo anatambulika kutokana na muktadha wa mazungumzo”. Jaspersen anaendelea na sababu ya tatu kuwa, ni “kutokumtaja mtenda wa jambo kwa lengo la kuonesha adabu kwa mtu unayezungumza naye kama amekuzidi umri au kama ni mtu unayemheshimu sana kutokana na wadhifa wake”. Nne, ni “kutokana na uchaguzi wa matumizi ya kauli ya utendwa kuliko kauli ya utenda kwani inasadia kuepuka kumtaja mtenda wa jambo na hii inaepusha matatizo kama vile lawama”. Tano, ni “kurahisisha muunganiko wa sentensi moja na nyingine” (kama ilivyonukuliwa katika Mkude, 2005:171). Shibatani anaona kauli ya utendwa inaweza kutumika katika mazingira yafuatayo: kwanza, “utendwa hautaji mhusika wa jambo, kwa hiyo kauli ya utendwa ni nzuri kwa mazingira fulani ya kiusalama”. Pili, “utendwa unaleta mada ya mjadala kuwa sehemu ya kiima”. Tatu, “utendwa unajenga kiini (egemeo) cha kisintaksia” (kama ilivyonukuliwa katika Mkude, 2005:172). 31 Palmer ana matumizi haya ya kauli ya utendwa ambayo ni: kwanza, “inakweza nafasi isiyo ya kiima kuwa kiima kwa ajili ya egemeo la kisintaksia”. Pili, “inakweza nafasi isiyokuwa ya mtenda kwa ajili ya msisitizo wa mada”. Tatu, “mtenda akiondolewa, utendwa unatumika mahali ambapo mtenda hajulikani au kama si muhimu kumtaja”. Nne, “katika lugha nyingine utendwa unatumika kwa sababu ya sheria zilizopo katika suala zima la kitu gani kina hadhi ya kukaa kwenye nafasi ya kiima cha kauli ya utenda” (kama ilivyonukuliwa katika Mkude, 2005:172). Kama tutakavyoona baadaye, mbinu hii ya kuangalia namna utendwa unavyoweza kuangaliwa, ikiangaliwa kwa jicho la kinaratolojia itabainika kuwa msemaji anayepewa utendwa anaweza kuwa anaisemea jamii kwa nia na lengo fulani mahususi, ama akisema hivyo kwa kutambua nia hiyo, au bila kutambua. Kwa kuhitimisha sehemu hii, utafiti umeonesha jinsi wachambuzi mbalimbali katika lugha mbalimbali walivyoishughulikia kauli ya utendwa. Katika kazi hizo, hakuna hata mchambuzi mmoja aliyetumia kauli ya utendwa kama mbinu ya uchambuzi wa kifasihi. Kazi zao zilijikita katika kuelezea sababu za matumizi ya kauli ya utendwa; ambapo imeonekana kuna ulandano wa mawazo katika kazi za (Alfred, Alred, Brusaw na Oliu, 2006; Mkude, 2005; The Writing Centre, 1998; Hansard, 1995; Palmer, 1994; Kolln, 1994; Shibatani, 1985; na Jespensen, 1924). Baada ya kuangalia kazi zilizoshughulikia kauli ya utendwa katika lugha nyinginezo – sasa tuangalie zile zilizoshughulikia kauli ya utendwa katika Kiswahili. 2.3. Kazi zilizoshughulikia utendwa katika lugha ya Kiswahili Kauli ya utendwa imechambuliwa kwa namna mbalimbali na wachambuzi wa lugha ya 32 Kiswahili. Wachambuzi hawa ni pamoja na: (Kabudi,1974; Mazrui, 1983; Khamis, 1988; Mdee, 1988; Massamba, Kihore na Hokororo, 1999; Massamba, Kihore, na Msanjila, 2001; Bearth, 2003; Habwe, 2004; na Mkude, 2005 tukitaja kwa uchache tu). Wengi wa wachambuzi hawa wameangalia zaidi utendwa kama kategeoria ya kisarufi. Kwa kutumia mkabala wa kisarufi, wamechunguza utendwa wakibainisha mabadiliko ya maumbo, mabadiliko ya mpangilio, na mabadiliko ya uelekezi. Kwa mfano, Kabugi (1974) anaielezea kauli ya utendwa kuwa inatokana na nini kinazungumzwa wakati huo ama kimaandishi ama kwa njia ya mdomo. Anaelezea kuwa umbo {-w} linapachikwa kabla ya irabu ishilizi lakini inategemea na aina ya irabu zilizopo mwishoni mwa kitenzi husika mfano “–aa”; “-ea”; “-oa”; vitachukua umbo la {li} …WA {le}…WA. Zaidi ya hayo ametoa mfano wa neno na kulibadilisha kuwa katika kauli ya utendwa, kwa mfano :- “piga -pigwa”; “oa”-“olewa”. Mazrui (1983) anaelezea mazingira ya kauli ya utendwa kuwa yanategemea asili ya kitenzi kama ni Kibantu au Kiarabu. Katika Kibantu umbo la mwishoni litakuwa {wa} wakati neno lenye asili ya Kiarabu litahitaji mnyambuliko wa {l} kabla ya kupachika umbo la utendwa ambalo ni {-iwa; au -ewa}. Sawa na waliomtangulia, Khamisi (1988) ameangalia utendwa kwa kufafanua mazingira ya kitenzi cha Kiswahili yanayoweza kuchukua maumbo mbalimbali. Aliongezea kuwa, vitenzi vyenye asili ya Kibantu mwishilizo utachukua umbo {-wa} wakati vile vyenye asili ya Kiarabu ambavyo mwishoni vinaishia na irabu {-i; -e; -u} vitachukua umbo la {-l-} kabla 33 ya kuongeza umbo hili {-iwa; -ewa} mwishoni mwa kitenzi. Mdee (1996) anaongezea kuwa vitenzi vya kutenda vinaponyambulishwa na kuwa katika kauli ya kutendwa, huambishwa kiambishi {–wa} cha hali ya kutendwa baada ya kudondosha kiambishi tamati {–a}. Massamba, Kihore, na Msanjila (2001) wanatafsiri kauli ya utendwa kuwa ni kanuni ya kiambishi nyambulishi {-w-} cha kitenzi katika kuunda maneno ya lugha ya Kiswahili. Wametoa mfano wa maneno mbalimbali na jinsi kanuni hii inavyowezesha kunyambulishwa kutoka katika kauli ya utenda na kuwa katika kauli ya utendwa. Kwa mfano sentensi namba 21: (a) ach-w-a (b) ach-i-w-a (2001:147) Kitenzi hicho katika kauli ya utenda ni “acha” kinaponyambulishwa katika kauli ya utendwa, kunakuwa na uundwaji wa maneno mbalimbali. Bearth (2003) anazungumzia kauli ya utendwa katika Kiswahili kuwa, hutokea kwa kubadilishana nafasi ya kiima inayokaliwa na mtendwa katika kauli ya utendwa. Habwe na Karanja (2004) wanaeleza kuwa sentensi ya utenda ina uhusiano wa karibu na sentensi ya utendwa kwa kuwa zote zinatokana na umbo moja la ndani ambalo limefanyiwa 34 mabadiliko na kuwa umbo la nje. Wanaongezea kuwa mofu {-w} hupachikwa kabla ya irabu ishilizi na kiunganishi “na” kabla ya kumtaja mtenda wa jambo ambaye ataonekana mwishoni mwa sentensi. Wachambuzi wote hapo juu, wameelezea kauli ya utendwa kwa mkabala wa kimofolojia – yaani mabadiliko ya maumbo ya vitenzi katika kauli ya utendwa. Linapozungumziwa suala la mabadiliko ya maumbo, kinachomaanishwa ni uchopekaji wa kiambishi nyambulishi {-w} kabla ya irabu ishilizi. Mabadiliko haya yalitegemea asili ya vitenzi kwa kuwa vile vyenye asili ya Kiarabu vilihusisha mchakato tofauti kabla ya kuchopeka mofu hiyo ya utendwa. Inabidi maumbo haya ya utendwa yachukue mnyambuliko mwingine ambao ni {-li-} au {-le- } kabla ya kuchopeka kiambishi nyambulishi cha utendwa ambacho ni {-wa} mwishoni mwa neno. Uchambuzi wao ni wa msingi kwa kuwa unawezesha kuielewa kauli ya utendwa kwa mapana yake. Mbali na maumbo, au mofolojia, kuna mkabala mwingine ambao unauangalia utendwa kwa kuzingatia nafasi ya kiima na yambwa. Mabadiliko ya mpangilio yanayohusisha kubadilishana nafasi kwa sehemu ya kiima na ile yambwa (au sintaksia) katika kauli ya utenda na ile ya utendwa yameangaliwa na wanaisimu kadhaa kuhusiana na lugha ya Kiswahili. Wazo hili limeshughulikiwa katika kazi za (Massamba, Hokororo, na Msanjila, 1999; na Mkude, 2005). Mabadiliko kama haya yanaendana na maana ambazo wazungumzaji wameweka kutokana na suala la dhamira, ambapo, jambo linalowekwa mwanzoni mwa sentensi ndilo linaloonekana lina umuhimu; na lile linalopelekwa mwishoni halina umuhimu mkubwa. Jambo hili linalopelekwa mwishoni ni sawa na taarifa ya ziada ambayo, kuwepo au kutokuwepo kwake hakuathiri mawazo makuu. 35 Massamba, Kihore, na Hokororo wanaifasili kauli ya utendwa kwa mkabala wa kisintaksia wakimaanisha - ni kwa jinsi gani nafasi ya mtenda (halisi wa jambo) katika kauli ya utenda inachukuliwa na mtendwa (wa jambo) katika kauli ya utendwa (1999:61). Kazi hii imeshughulikia kipengele cha kauli ya utendwa kwa mkabala wa Noam Chomsky wa sarufi geuza maumbo zalishi (1957), na kuona jinsi sentensi ya utenda na ile ya utendwa zinavyohusiana kwa kuwa zinatokana na umbo moja la ndani ambalo linafanyiwa mabadiliko na kupata umbo la nje. Kwa mfano sentensi namba 25: (a) Malima amempiga Juma (b) Juma amepigwa na Malima Katika sentensi hiyo, kiima halisi cha kauli ya utenda kimebadilika na kuwa cha yambwa ya kauli ya utendwa; na yambwa ya kauli ya utenda imechukua nafasi ya kiima cha kauli ya utendwa. Wachambuzi hawa wameelezea mabadiliko ya mpangilio kama suala la kisintaksia zaidi. Wameonyesha jinsi kiima na yambwa vinavyoweza kubadilishana nafasi wakitaka kudhihirisha kuwa, kauli ya utenda na ile ya utendwa zinatokana na umbo moja la ndani. Kwa maneno mengine, kinachowekwa mwanzoni mwa sentensi ndicho kinachoonekana kuwa na umuhimu mkubwa – na kile kinachopelekwa mwishoni mwa sentensi kinapunguziwa umuhimu au hadhi. 36 Kwa upande wake, Mkude (2005) ndiye aliyechambua kauli ya utendwa katika lugha ya Kiswahili kwa kina zaidi. Kazi yake hasa ilifafanua dhana ya kauli ya utendwa, na kuelezea mabadiliko ya maumbo ya utendwa, mabadiliko ya mpangilio wa viambajengo vya sentensi, na mabadiliko ya uelekezi wa kitenzi. Katika kujadili mabadiliko ya mpangilio wa viambajengo katika sentensi, anaelezea kubadilishana nafasi kwa kiima (cha kauli ya utenda) na chagizo (cha kauli ya utendwa). Hii ina maana kuwa, kiima asilia cha kauli ya utenda kilibadilika hadhi, na kuwa chagizo katika kauli ya utendwa; na yambwa katika kauli ya utenda ilipanda hadhi na kuwa kiima cha kauli ya utendwa. Suala la hadhi linaloongelewa hapa ni ule mchakato wa kubadili kiima cha sentensi na kuwa chagizo; na yambwa kuwa kiima cha sentensi. Mkude (kama hapa juu) ana sababu sita za matumizi ya kauli ya utendwa ambayo ni: kwanza, “umuhimu wa mada ambayo husababisha msisitizo kuwekwa kwenye mada na sio mtenda wa jambo”. Pili, “kudondosha mtenda wa jambo - katika sababu hii, mtenda wa jambo hatajwi kutokana na sababu mbalimbali kama vile kujulikana kwake, au kutokujulikana”. Tatu, ni “utengenezaji wa egemeo la kisintaksia”. Nne, ni “kuzingatia itifaki ya nini kikae sehemu ya kiima na nini kisikae”. Tano, “ni mbinu ya kuondoa utata”, na mwisho, ni sababu ya “fokasi ni mtenda ikimaanisha kuwa utendwa hutumika kumchomoza mtenda” (Mkude, 2005). Hivyo ubainishaji wa (Mkude, 2005) kuhusu sababu za matumizi ya kauli ya utendwa umeweza kujumuisha sababu zote ambazo zilitajwa na watafiti wa mwanzoni pamoja na mpya alizoziongezea. 37 Hata hivyo, kazi hizo zote hazikuangalia utendwa kama mbinu ya kielimu mitindo anayoweza kuitumia mwandishi wa kazi ya fasihi katika kuibua dhamira zake. Kazi hizi ziliuangalia utendwa kama suala la kiisimu tu. Na kwa kuwa kazi hizo hazikutumia kauli ya utendwa kama mbinu ya uchambuzi wa kifasihi, kazi hii imeliziba pengo hilo. Kwa kuhitimisha sehemu hii, utafiti umeonesha jinsi wachambuzi mbalimbali katika lugha ya Kiswahili walivyoishughulikia kauli ya utendwa. Katika kazi hizo, hakuna hata mchambuzi mmoja aliyetumia kauli ya utendwa kama mbinu ya uchambuzi wa kifasihi. Kazi zao zilijikita katika kuchambua kauli hii kwa mtazamo wa kimofosintaksia, yaani kimofolojia na kisintaksia tu. Baada ya kuangalia dhana za utendwa, tuangalie sasa kazi zilizochambuliwa kielimu mitindo na wale walioshughulikia dhana na nadharia ya elimu mitindo. 2.4 Kazi zilizoshughulikia Elimu mitindo Kwa kuchunguza marejeo yaliyochambua mitindo na elimu mitindo hasa katika fasihi, tutaweza kuweka msingi imara wa utafiti wetu. Maw (1974) ndiye alikuwa mtu wa mwanzo kabisa kuchunguza mtindo katika lugha ya Kiswahili. Kazi hii ililenga kuchunguza mtindo katika nyanja tatu tofauti za matumizi ya lugha zikiwemo: mazungumzo ya kisiasa, hadithi simulizi, na habari ya gazetini. Lengo likiwa ni kuchambua na kutofautisha sifa muhimu za lugha ya mazungumzo na lugha ya maandishi. Kipengele cha uchambuzi kilichotumika ni cha kiisimu. Kipengele hiki kinadadisi jinsi gani sentensi inashikamana kutokana na mahusiano ya viambajengo vyake. Uchambuzi wa kazi hii haukuegemea katika fasihi ya Kiswahili, bali lugha kwa ujumla. 38 Badhi ya wahakiki wa kazi za fasihi ya Kiswahili wamefanya uchambuzi wao kwa kuziangalia tanzu za fasihi kama vile riwaya, ushairi, na tamthilia wakizingatia vipengele vya fani na maudhui. Katika uchambuzi huo kwa ujumla, mambo yanayoangaliwa ni kwa vipi mwandishi wa kazi ya fasihi ameiumba kazi yake kwa kuzingatia uhusiano wa vipengele katika fani na katika maudhui. Uchambuzi wa aina hii ingawa ni wa maana na hutokeza udadisi wa wanafasihi katika kuichunguza kazi husika, bado sio toshelezi. Kuna vipengele kadhaa ambavyo ikiwa vingeliangaliwa kwa undani, mhakiki au mchambuzi angeliielewa na kuifafanua kazi ya fasihi vizuri zaidi. Hapa ndipo mkabala wa kielimu mitindo unapokuwa na mashiko, na kutupeleka hatua moja zaidi katika ubora wa uchambuzi wa kazi za kifasihi. Wanaelimu mitindo katika fasihi ya Kiswahili wanajadili vipengele mbalimbali kama tutakavyoona hapa chini. Mutembei (1993) katika utafiti wa shahada ya uzamili aliouita Phonological aspect of foreground in Kiswahili amejikita katika kuchunguza kipengele cha mchomozo katika ushairi wa Kiswahili, na jinsi kinavyosaidia katika kuibua maudhui. Mchomozo kama kipengele cha elimu mtindo, ndio unaoangaliwa katika kuchambua mtawanyiko wa kipengele cha kifonolojia cha takriri ya sauti, na kuona ni kwa jinsi gani kipengele hiki kinasaidia kuelewa maana ya shairi. Vipengele hivi vya kifonolojia vinavyoonesha mchomozo ni pamoja na irabu, konsonati, mkazo, kiimbo na shadda. Msambao wa vipengele hivi vya irabu na konsonanti 39 unachambuliwa na kujaribu kuonesha iwapo vina uhusiano wowote na maana inayobebwa na kazi ya fasihi. Ingawa kipengele hiki cha mchomozo kinachukuliwa kama mbinu ya kifani katika uchambuzi wa ushairi, bado hatuoneshwi dhima ya mwandishi katika ama kuteua au kutumia vipengele hivi. Kazi hii ingawa imeonesha uhusiano wa fani na maudhui kwa mipaka hiyo, bado inafanya uchambuzi wa ndani ya matini tu, bila kurejelea nje ya kazi au matini husika. Utafiti wa (Mutembei,1993) unapiga hatua moja zaidi kutoka katika elimu mtindo inayojikita katika fani pekee. Kazi ya uzamili ya (Mulokozi, 1996) inayoitwa A Styistic Comparison of Swahili Prose and Poetry: The case of Lexical Cohesion imejikita katika kuchambua kipengele cha ushikamani hasa wa kimsamiati kama kilivyojadiliwa na (Halliday na Hasan, 1976). Anakichambua kipengele hiki katika riwaya za Kiswahili pamoja na mashairi mbalimbali ya Kiswahili. Tofauti na ule wa Mutembei (kama ilivyoonwa hapa juu), utafiti huu unaongeza ujuzi wetu wa ulinganishi. Mulokozi analinganisha tanzu mbili za fasihi ya Kiswahili – ushairi na riwaya, kwa mkabala wa kielimu mitindo akikijadili kipengele cha ushikamani. Kahigi, (1998), anazama zaidi katika kipengele hiki cha ushikamani wa matini. Kwa kutumia dhana ya muundo alichambua kiushikamani kazi iliyofanywa na (Maw, 1974) na kuchambua mitindo mbalimbali katika kazi mbalimbali za Kiswahili. Katika kazi hiyo, Kulikoyela Kahigi anajadili aina tano za ushikamani kama zilivyopendekezwa na (Halliday na Hasan,1976). Aina hizi za ushikamani ni kama vile: ushikamani wa urejeo, udondoshaji, uunganishaji, ubadala na msamiati. Katika aina hizi za ushikamani, zile nne zilizotangulia ni za kiisimu 40 (urejeo, udondoshaji, uunganishaji, ubadala); wakati aina ya mwishoni ni ya kisemantiki (msamiati). Ingawa uchambuzi huu haukujikita sana katika fasihi, unaichambua lugha na kuonesha jinsi ilivyo. Bado hata hivyo, ni uchambuzi wa kielimu mtindo ambao hautoki nje ya lugha ya matini, na kuangalia uhusiano wowote wa lugha inayotumika na wale wanaoitumia. Aidha ni uchambuzi ambao haupigi hatua zaidi katika kuibua dhamira ya mwandishi wa matini au maudhui kwa ujumla. Kazi ya (Chambala, 2001) inatusogeza mbele katika kufahamu dhamira kupitia katika kipengele cha fani kwa mkabala wa kielimu mitindo. Katika kazi yake ya uzamili inayoitwa The Use of Parallelism in Mariama Ba’s Scarlet Song (Chambala,2001) amechambua kipengele cha usambamba na jinsi kilivyotumika katika riwaya hiyo. Makusudi yake yalikuwa kukiangalia kipengele cha usambamba kwa mkabala wa elimu mitindo na jinsi kipengele hicho kinavyomsaidia msomaji kuelewa au kuibua maudhui ya mwandishi. Mwanafasihi mwingine aliyeangalia uhusiano kati ya lugha na maana kwa mkabala wa kielimu mitindo ni (Lyimo, 2004). Katika tasnifu yake inayoitwa Reiteration in Kiswahili Poetry (Lyimo, 2004) amejikita katika kuchambua kipengele cha takriri katika ushairi wa Kiswahili; na jinsi kipengele hiki kinavyosaidia kumfanya msomaji aelewe maana ya shairi; na jinsi gani aina hizi za mashairi zinatofautiana na kufanana kimtindo. Ametumia tenzi, mashairi ya kimapokeo, na mashairi ya kimasivina ili kuchambua maudhui yanayoibuliwa kupitia matumizi ya takriri. Lyimo (2004) 41 kama ilivyokuwa kwa (Mutembei,1993) amejikita katika utanzu mmoja tu na hakuangalia mkabala wa elimu mitindo nje ya kazi husika. Ramadhani (2005) anatupatia ulinganishi unaohusisha kazi za fasihi zaidi ya moja. Katika tasnifu ya uzamili, aliyoiita The Use of Metaphor in Mbogo’s Ngoma ya Ng’wanamalundi and Hussein’s Mashetani: A Stylistic Comparison (Ramadhani, 2005) amejikita katika kulinganisha na kulinganua kipengele cha sitiari katika tamthilia mbili za Kiswahili ambazo ni Ngoma ya Ng’wanamalundi ya Emmanuel Mbogo; na Mashetani ya Ebrahim Hussein. Lengo lake lilikuwa ni kulinganisha na kulinganua matumizi ya sitiari kama kipengele cha kielimu mitindo katika tamthiliya hizo mbili. Kupitia katika ulinganishi huu, (Ramadhani, 2005) anaeleza namna matumizi ya sitiari yanavyosaidia kuelewa dhamira za waandishi. Hata hivyo, katika kazi hizi zote kilichozingatiwa ni lugha kama inavyojitokeza katika maandishi au matini husika. Kwa mfano, wachunguzi hao tuliowataja wameangalia vipengele kama vile mitindo mbalimbali ya uandishi wa fasihi, mchomozo katika uandishi wa ushairi wa Kiswahili, ushikamani wa msamiati na wa matini za Kiswahili, takriri katika ushairi wa Kiswahili, na sitiari katika tamthilia za Kiswahili. Wachambuzi hawa hawakuchunguza sababu zilizomsukuma mwandishi kuchagua au kutumia vipengele hivyo. Kwa maneno mengine, mkabala wa kielimu mitindo katika fasihi ya Kiswahili haukutoka nje ya matini inayochambuliwa. Kwa hiyo, kama ilivyobainishwa katika sehemu ya 1.4.2, utafiti huu una lengo la kuchambua kauli ya utendwa kama mbinu ya kielimu mitindo, na yale yaliyomwongoza mwandishi kuchagua kauli hiyo akiacha kauli ya utenda katika mazingira  ambamo matumizi ya kauli zote mbili yanawezekana. Aidha, ingawa utendwa ni kauli ambayo hujitokeza kwa wingi katika lugha ya Kiswahili (Mkude, 2005), hakuna utafiti ambao umeshafanywa kuhusu kipengele hiki cha kauli ya utendwa kama mbinu ya kielimu mitindo katika kazi za fasihi. Uchambuzi huu wa kielimu mitindo wa kauli ya utendwa katika Machozi ya Mwanamke utatuwezesha kubaini uhusiano wa dhamira na fani, lakini pia kufahamu matumizi ya utendwa huongozwa na nini, kwa watumiaji wa lugha na hasa fasihi ya Kiswahili.

2.5 Kiunzi cha Nadharia 

Kazi hii inachambua jinsi utendwa ulivyotumiwa katika tamthilia ya Machozi ya Mwanamke. Ingawa utendwa ni kauli ya kawaida katika sarufi ya Kiswahili, hapa kauli hiyo inaangaliwa kupitia nadharia ya elimu mtindo kama inavyofafanuliwa na (Halliday na Hasan, 1971) kwa upande mmoja; na (Leech na Short, 1981) kwa upande mwingine. Hoja inayochukuliwa kutoka kwa wataalamu hawa ni kuwa mtindo ni suala la uchaguzi (au uteuzi) na wakati huo huo, mtindo ni utofauti. Kama tutakavyoeleza hapa chini, dhana za uchaguzi na utofauti zinajichomoza kipekee hasa katika matumizi ya utendwa. Matumizi haya ya utendwa yanabainishwa kupitia kwa wahusika waliomo katika tamthilia hii. Wahusika hawa wanajengwa kutoa “sauti” fulani ambayo ni kiwakilishi tu. Kwasababu hiyo, kauli ya utendwa, kama “sauti”, inaangaliwa pia kwa kutumia nadharia ya usimulizi au naratolojia kama ilivyofafanulia na (Bal, 1985). Nadharia hii inamwangalia mwandishi wa kazi ya fasihi kama msimulizi akiwatumia 43 wahusika kutoa “sauti” wakisema yale anayokusudia yeye kama mwandishi au yeye kama kiwakilishi cha jamii. Nadharia hizi mbili kwa pamoja ndizo zinazounda kiunzi cha kinadharia ambacho tunakitumia katika kuchambua kauli ya utendwa katika tamthilia ya Machozi ya Mwanamke. Kabla hatujaingia kwa undani kufafanua kiunzi hiki, tuangalie mawazo makuu katika nadharia zote mbili. 2.5.1 Nadharia ya Elimu Mitindo Mtindo kama nadharia, umefafanuliwa na wataalamu mbalimbali kwa namna tofauti. Hata hivyo, kwa mtazamo wa wataalamu kama (Halliday na Hasan, 1971); (Enkvist, 1973); na (Leech na Short, 1981), mtindo unaonwa kuwa ni uchaguzi au ni utofauti. Katika kipengele kifuatacho, imejadiliwa maana ya mtindo kama uchaguzi na mtindo kama utofauti ili kuweka wazi mawazo yao.

2.5.1.1 Mtindo ni Uchaguzi au Uteuzi 

Wataalamu (Halliday &Hasan,1971) na (Leech & Short, 1981) wanaitetea hoja hii ya mtindo kama uchaguzi kwa kusisitiza kuwa, mtindo ni pale mwandishi anapoamua kuchagua matumizi ya kipengele fulani labda “x” badala ya kipengele kingine labda “y” kwenye kazi yake ya kisanaa, ambapo kimoja au kingine kingeliweza kutumiwa. Uchaguzi au uteuzi huu unamwezesha mwandishi atumie nini au asitumie nini bila kulazimishwa na sababu yoyote. Kwa hiyo, mahali ambapo hapana uchaguzi basi pana ulazima. Na mahali penye ulazima hapana mtindo. Hivyo uhiari wa lugha (uchaguzi) umewezesha kubainisha mtindo wa mwandishi tukiangalia kauli ya utendwa. 44 Kwa mantiki hiyo, kazi hii inaangalia madhumuni ya mwandishi katika kuchagua kauli ya utendwa na kuacha utenda katika mazingira yaleyale. Je katika kutimizi lengo la mwandishi ambalo ni ‘ukombozi wa wanawake,’ je, uchaguzi huu wa utendwa ni wa makusudi au unabeba mazingira ya kijamii na kihistoria? Baada ya kufasili mtindo kama uchaguzi, tuangalie sasa matumizi ya mtindo kama utofauti.

2.5.1.2 Mtindo ni Utofauti 

Enkvist (1973) anatafsiri mtindo kama kaida za utofauti katika kazi ya mwandishi fulani. Kuna utofauti kati ya kazi mbalimbali za kisanii kama ilivyo kwa ushairi, riwaya, na tamthilia. Kwa kufafanua hivi, Enkvist anatueleza kuwa hatuwezi kujua mtindo wa mwandishi kwa kuangalia kazi yake moja tu. Kwa kuangalia kazi mbalimbali za mwandishi mmoja tunaweza kuona jinsi uandishi wake unavyotofautiana toka kazi moja kwenda nyingine (au unavyofanana) na hivyo kugundua mtindo wa mwandishi huyo. Kutokana na tafsiri ya kiujumla, mtindo unaweza kutafsiriwa kuwa ni namna lugha inavyoweza kutumika kiutofauti kuendana na muktadha, hadhira, na lengo. Kwa mantiki hiyo, tafsiri ya mtindo kama “utofauti” inathibitisha kuwa “mtindo” ni sawa na “rejesta” kwani nayo hutofautisha matumizi ya lugha kwa sababu za kimuktadha, hadhira na lengo. Jambo hili pia linajidhihirisha wazi tukiichunguza fasili ya mtindo kwa mujibu wa (Crystal, 1966: 10) kwamba, “mtindo unaweza kufasiliwa kama tabia za matumizi ya lugha zinazojitokeza kwa wanajamiilugha husika. Tabia hizi za lugha hujibainisha katika kipindi fulani au kwa muda fulani”. Hapa ina maana ya tabia ya lugha kwa jamii nzima inayotumia 45 lugha hiyo na sio kwa mtu mmoja. Mawazo haya yanawekwa pamoja na waandishi kina (Leech na Short, 1981) wanaosema kuwa: Katika uwanja wa uandishi, kuna fasili mbalimbali kama vile upekee wa mwandishi kwa namna anavyoamua kuitumia lugha. Na kwa upande mwingine ni jinsi lugha inavyotumika kulingana na aina ya kazi, kipindi au wakati ilipotungwa, shule ya kitaaluma na mjumuiko wa yote kwa pamoja (1981: 38). Kwa mujibu wa maelezo haya kuhusu namna mbili za kuutazama mtindo, utafiti huu unajikita kuchambua matumizi ya kauli za utendwa kwa kuangalia kauli hiyo “mtindo kama uchaguzi (uteuzi)” wa mwandishi. Uchambuzi wa data utaendana na mawazo haya kuwa mwandishi alikuwa na hiari ya kuchagua. Kwa uhuru huo, mwandishi ameamua kutumia kauli zenye utendwa, badala ya kauli zenye utenda katika kuwasilisha mawazo yake. Uteuzi huu hata hivyo, unaweza kuwa umefanyika hivyo kutokana na kuwa mwandishi anayazungumza yale yaliyomo katika jamii yake; na kama hivi ndivyo, uhiari wake unakuwa katika kubanwa na matakwa au mwongozo wa jamii iliyomkuza. Jambo hili linatupeleka katika kuitumia nadharia ya usimulizi tukimwangalia mwandishi kama msimuliaji wa yale yanayotokea katika jamii yake. Ikiwa hivi ndivyo, nadharia ya naratolojia itatusaidia kuchunguza nafasi ya mwandishi na nafsi anazozitumia kupitia wahusika wake.

2.5.2 Nadharia ya Naratolojia 

Naratolojia ni nadharia inayofafanua namna usimulizi unavyofanywa na msimuliaji. Kwa mujibu wa (Bal, 1985), nadharia hii inatazama kila tendo la kisanaa, au fikra iliyowekwa katika maandishi, uchongaji vinyago, usanifu majumba, michoro, utalizi, ufinyanzi na kadhalika, kama matukio yenye kusimulia jambo mahususi. Katika kazi za kisanaa zilizo katika maandishi, masimulizi hayo hufanywa na wahusika - wasimuliaji au watendaji na kwa lengo maalumu. Mwandishi huwafanya wahusika wake waongee na kusimulia kwa niaba yake. Kupitia katika dhana ya fabula mwandishi hujitoa na kuwaacha wasimuliaji wajieleze kwa namna fulani. Fabula ni ule mtiririko wa kimantiki na kimfuatano unaosimulia kuhusu tukio linalosababishwa na wahusika katika matini; ni jinsi wahusika wanavyopangilia visa vya hadithi waitoayo tangu mwanzo hadi mwisho. Fabula sio lazima ihusiane na lugha moja kwa moja, bali ni mpangilio wa uigizaji, matukio, muda wa matukio na jinsi yalivyopangiliwa, na mahali yanapotokea. Hadithi inayosimuliwa inaweza kuwa ni: matini, picha, kionwa, tukio fulani, kazi ya sanaa, au jengo. Lengo kuu katika nadharia hii ni kuibua nafsi mbalimbali katika usimulizi na hivyo kuweza kubaini hasa msemaji wa tukio fulani ni nani, na ana nafasi gani katika jamii. Ni nadharia inayomwangalia msimulizi na kuona wasemaji au watendaji wengine nyuma yake ambao hao ndio hasa wenye kauli kuhusu lile lisemwalo na sio yeye mwenyewe. Nadharia hii ya naratolojia inasaidia kuelewa, kuchambua, na kutathmini kazi yoyote ya 47 kisanaa kama yenye usimulizi maalumu, au kwa maneno mengine kila kazi ya kisanaa ni matini simulizi (Bal, 1985: 3). Nadharia hii, hasa itatusaidia kufafanua jinsi mfuatano wa maonyesho na sehemu za tamthilia ulivyo na uhusiano wa lugha na dhamira kuu. Katika tamthilia tunayoichambua, maonesho na sehemu zake zitaangaliwa kama zinazotengeneza matini moja simulizi. Matini simulizi ni matini ambamo wakala anasimulia hadithi kwa kutumia njia mbalimbali kama vile: lugha, taswira, sauti, majengo, au mjumuiko wa yote kwa pamoja (Bal, 1985: 5). Msimuliaji wa simulizi si mwandishi bali ni wakala ambaye anatumiwa na mwandishi ili kuisimulia hadithi. Wakala huyu anaweza kujibainisha katika madarajia mawili: darajia la kwanza ni lile linalotumia nafsi ya kwanza au ya pili ambayo inaufanya usimuliaji ufungamane na nafsi ya mwandishi. Mathalani, matumizi ya viambishi vya nafsi ya kwanza na ya pili kama vile: “ni” (katika umoja), na “tu” (katika wingi); na “u” (katika umoja), na “m” (katika wingi) hutawala vitenzi. Darajia la pili ni lile linalotumia nafsi ya tatu katika usimuliaji, ikimaanisha msimuliaji ni mtu tofauti ambaye si mwandishi na si wakala wake. Katika darajia hili matumizi ya viambishi nafsi vya nafsi ya tatu hutawala. Mathalani, “a” (katika umoja), na “wa” (katika wingi) hutawala katika vitenzi. Nadharia hii ya usimulizi imekuwa ni muhimu katika uchambuzi wa data ya kazi hii kwakuwa imetusaidia kuelewa kauli ya utendwa zimeegemea wapi. Kwa maneno mengine tunaweza kufahamu msemaji wa kweli wa kauli ya utendwa ni nani hata kama mhusika fulani ndiye anayetoa kauli husika. Jambo muhimu zaidi, ni kuwa kupitia katika nadharia hii, tunaweza pia kufahamu sababu za uteuzi wa kauli moja na kuacha 48 nyingine katika mazingira ambamo zote mbili zingelifaa. Ili tujenge hoja yetu kwa mantiki, na kuonesha uhusika wa wahusika na nafsi zao, sasa tuangalie dhana ya wahusika katika kazi ya fasihi. Dhana hii tunaiangalia hali tukiwa na nadharia mbili katika uchambuzi wetu, kama tulivyozitaja. 2.6 Wahusika katika kazi ya fasihi Kwa mujibu wa Kamusi ya Fasihi, Istilahi, na Nadharia, mhusika ni: Kiumbe anayepatikana katika kazi ya kifasihi na ambaye anafanana na binadamu kwa kiasi fulani. Wasifu wa mhusika unategemea mkabala uliopo. Kazi zinazoegemezwa katika mitazamo ya kihalisia zinamsawiri mhusika kwa namna inayokaribiana sana na binadamu katika ulimwengu wa kawaida (Wamitila, 2003:123). Brockett (1964) kwa upande wake anaelezea kuwa mhusika ni kitu muhimu sana katika msuko wa matukio ya hadithi. Msuko huu huweza kuelezwa kupitia migogoro na matamanio tofauti tofauti ya wahusika, ambao kwa kutumia mazungumzo na tabia zao tofauti huwezesha kuukuza mgogoro. Brockett anaeleza sifa za aina nne za mhusika kuwa ni: za kimaumbile, za hali ya kisaiolojia, za nafasi yake katika jamii, na za kimaadili. Kimaumbile – tunaangalia: je, mhusika anaonekanaje kiumbo ? Je, ni mnene au mwembamba? Je, ni mweupe au mweusi ? Je, ni mfupi au mrefu. Kisaikolojia mhusika anatazamwa hali yake ya kiakili – je anapenda nini na hapendi nini? Kijamii mhusika anatazamwa kuwa anafanya kazi gani – je ni mkulima, mwalimu, mfanyabiashara, mchungaji na kadhalika. Kimaadili - mhusika anachunguzwa namna anavyoweza kufanya uchaguzi au uamuzi wa jambo moja kati ya mawili ambayo yako mbele yake (Brocckett, 1964 uk.30). 49 Kutokana na maelezo hayo hapo juu, inaonekana kuwa dhana ya uhusika na dhana ya uigizaji haitofautishwi. Wamitila (2003) na (Brockett, 1964) wanamjadili mhusika kuwa ni kiumbe (mtu) lakini hawaongelei lolote kuhusu mhusika kama mashini, mnyama, mawe, na viwakilishi vingine ambavyo si binadamu. Hata hivyo, dhana ya uhusika ni ya jumla na dhahania zaidi ikilinganishwa na dhana ya uigizaji ambayo ni mahususi. Mwigizaji ni lazima awe binadamu, lakini mhusika si lazima awe binadamu. Dhana hii, na utofauti uliopo ni mambo muhimu katika kuchambua wahusika wa tamthilia ya Machozi ya Mwanamke na kubaini kauli zao wanazozitumia. Maana na tofauti hizi za wahusika na waigizaji zimefafanuliwa wazi katika nadharia ya usimulizi (naratolojia). 2.7 Wahusika katika Nadharia ya Naratolojia Scholes na Kellogg (1966) wanaelezea dhana ya uhusika katika nadharia ya usimulizi kuwa haiwezi kutenganishwa na usimuliaji wa tukio katika hadithi. Mhusika ni nyenzo anayoitumia mwandishi ili kusimulia tukio au jambo fulani. Scholes na Kellogg (1966) wanasema : Mhusika ni kitu gani kama sio kiwakilishi cha tukio? Tukio ni kitu gani kama hakitafafanuliwa kupitia mhusika? Je picha ni kitu gani au novela (riwaya) ni nini pasipo kuwepo mhusika? Je ni kitu gani tutakuwa tunakitafuta kwenye riwaya au picha kama hatutatumia au kuwahusisha wahusika?... (Scholes na Kellogg, 1966: 160) Hoja inayowasilishwa na (Scholes na Kellogg, 1966) inadhihirisha kuwa si rahisi kuelezea 50 dhana ya uhusika pasipo kuelezea tukio linalotendwa; si rahisi kutenganisha tukio na mhusika katika simulizi, vitu hivi vinajengana na kutegemeana. Wahusika na tukio ni kama pande mbili za sarafu moja ambazo haviwezi kutenganishwa. Kwa mujibu wa (Bal, 1985), uhusika na uigizaji ni dhana mbili ambazo hazina budi kutofautishwa. Dhana moja inajikita katika kueleza ujumla wa mambo, ikihusishwa na matendo (au tukio); na nyingine ikieleza jambo mahsusi. Mhusika ni wakala ambaye anafanya matendo fulani. Mhusika si lazima awe binadamu, lakini lazima awe mtendaji (Bal, 1985: 5). Uhusika ni istilahi inayojumuisha wigo mpana (au wa jumla) kuliko ilivyo kwa istilahi finyu ya uigizaji. Kwa maneno mengine, mbwa, mashini, na kitu chochote kisicho binadamu kinaweza kuwa mhusika na sio kinyume chake. Kwa upande mwingine, mwigizaji anafafanuliwa katika nadharia hii kama kiumbe ambacho kinasimama badala ya kitu kingine katika usimulizi. Kiumbe hiki awe ni binadamu au la, hupewa sifa za binadamu ili kukamilisha usimulizi. Mwandishi anawezesha kumpa mwigizaji sifa (wasifu) kwa kutumia ufafanuzi ambao unamfanya mwigizaji aweze kuvaa sura ambayo inamfanya afanane na binadamu halisi kwa kuwa na haiba, saikolojia, na itikadi (Bal, 1985:115). Kwa hiyo, mhusika hupewa wasifu wa aina mbalimbali ili dhana ya uigizaji iweze kupatikana. Jambo hili linafanywa na mwandishi kwa uteuzi maalumu ili jambo analotaka  kuliongelea liweze kuiwakilisha jamii anayoisemea. Na kwahiyo hapa tunaona hatua tatu muhimu: mwandishi, wahusika wake na jamii, hatua hizi zinatokeza uigizaji anaoufanya mwandishi kupitia katika kazi yake. “Dhima za wahusika kinadharia si za mtunzi binafsi bali ni miundo inayopatikana katika jamii kwa ujumla” (Wafula na Njogu, 2007:16). Ukweli huu unadhihirisha mambo mawili katika nadharia ya naratolojia. Kwamba, mtunzi anajiondoa yeye na kuwafanya wahusika kusema kwa niaba yake; na pili, kuwa, wahusika wenyewe hawajisemei wao kama wao, bali pia wao kama wawakilishi wa jamii wanamotokea. Upekee wa lengo la mwandishi unajitokeza kwa jinsi anavyochagua mhusika wa kumsemea na kuisemea jamii na kumpa mhusika huyo lugha inayoendana na dhima yake. Wakiandika kuhusu “Freud, Ndoto, na Fasihi” Wafula na Njogu (kama ilivyotajwa hapo kabla) wanasema: “nao wahusika wanaopatikana katika fasihi ni wanadamu wanaoishi katika ndoto na njozi za mwandishi. Hawa ni kama vile wanadamu wa kweli wanaoshirikiana na mwandishi katika matatizo na matarajio yake” (2007: 79). Wahusika ni zana muhimu katika matini simulizi kwa kuwa, mwandishi huyafikisha maudhui na hasa dhamira kwa kupitia kwao. Mathalani, katika tamthilia ya Machozi ya Mwanamke - mwandishi amewasilisha dhamira ya unyanyaswaji wa wanawake unaofanywa kupitia kwa mhusika Madahiro. Vilevile, amejadili suala la ukombozi wa mwanamke kwa kuwapa hoja hiyo wahusika kama: Manila, Nzole, Wambali kwa upande mmoja; na wakeze Madahiro kama: Mauja, Mlahaka, Deka, na Nasaa kwa upande mwingine. 52 Kupitia katika nadharia za elimu mitindo kama uchaguzi, na naratolojia, tunawaangalia wahusika hawa na hasa yale wayasemayo tukiwa na mawazo kuwa wanayasema wayasemayo kutokana na jamii waliyomo na iliyowakuza. Wanayoyasema na kuyatenda ni msukumo wa mfumo ambao wao ni matokeo yake. Uchaguzi wa kauli za utendwa walizonazo wahusika hawa ukiangaliwa kupitia katika nadharia hizi, unaweza kutueleza mengi kuhusu mfumo na jamii husika; na hivyo, tukafahamu hasa msemaji katika wahusika hawa ni nani na kwanini anasema kwa kutumia utendwa na sio utenda. 2.8 Hitimisho Katika sura hii ya mapitio ya vitabu, zimechunguzwa kazi mbalimbali ambazo zimechambua kauli ya utendwa katika lugha ya Kiswahili na nyinginezo nje na lugha hii. Katika kazi hizo zote, tumeangalia dhana ya kauli ya utendwa na mabadiliko ya mpangilio, maumbo, na uelekezi, na jinsi mabadiliko hayo yanavyoathiri utolewaji wa kauli husika. Kauli hizi na uchaguzi wake zimejadiliwa kupitia katika kiunzi cha nadharia kilichoweka pamoja nadharia mbili. Nadharia zilizotumika ni zile za elimu mitindo na naratolojia. Katika nadharia ya elimu mitindo - mtindo ulifafanuliwa kwa mikabala miwili ya ‘uchaguzi’ na ‘utofauti’, huku tukijadili urazini wa dhana hizo mbili. Kutokea katika mikabala hii miwili, mtindo kama uchaguzi ilichukuliwa ikiangaliwa pamoja na nadharia ya naratolojia iliyofafanuliwa ikimwangalia mhusika na aina zake, akitofautishwa na muigizaji na uwakilishi wake kwa yale yasemwayo na mwandishi. Ilikuwa ni muhimu kuhusisha nadharia ya naratolojia na kazi hii kwa sababu ya kuchunguza muktadha wa nani, anasema nini, na kwa nini kauli za utendwa 53 zimechaguliwa badala ya utenda. Ili kupata data za kazi hii, mbinu mbalimbali zimetumika. Sura ifuatayo inafafanua mbinu za utafiti na ukusanyaji data.

SURA YA TATU MBINU ZA UTAFITI 

3.1 Utangulizi 

Sura hii imeshughulikia hatua mbalimbali zilizopitiwa katika kutafiti matumizi ya kauli za utendwa katika tamthilia ya Machozi ya Mwanamke. Hatua hizo ni pamoja na kuteua tamthilia inayochambuliwa, mbinu za kukusanya data kuhusiana na au kutoka katika tamthilia hiyo, na mbinu za uchambuzi wa data.

3.2 Uchaguzi wa tamthiliya hii 


Kigezo kikuu kilichochochea kuteuliwa kwa tamthilia hii, ni ukinzani. Mahali popote penye ukinzani kuna dalili za, au ni mwanzo wa maendeleo. Jina la tamthilia hii linatokeza mvuto wa kipekee kutokana na ukinzani wa kimuktadha na kihistoria. Ikiwa muktadha wa tamthilia hii unahusu ukombozi wa mwanamke, ni kwanini tamthilia hii inaitwa Machozi ya Mwanamke, kama kwamba ukombozi unaosemwa utasababisha au unasababisha kilio? Katika historia, mwaka na mazingira ilipoandikwa tamthilia hii, vilikuwa vinaashiria furaha na shangwe ya hatua muhimu katika maendeleo ya wanawake: mwaka wa kujadili ukombozi na kuondokana na unyanyaswaji wa mwanamke na kutiliwa maanani kwa haki za binadamu wote. Hata hivyo, msomaji anapata ukinzani kwakuwa, kichwa cha tamthilia kinaonesha kinyume cha mambo. Tena ukinzani unakuzwa zaidi baada ya kusoma ndani na kuona kuwa wahusika wengi wa kike wamepewa kauli za utendwa. Ikiwa wanawake wanataka kujikomboa, kwanini namna yao ya kuongea haiakisi utashi huo wa kujikomboa kwa kutoa kauli za utenda, bali wanayoyaongea yanaonesha kuwa mtendaji ni jinsia nyingine. Ukombozi utapatikanaje ikiwa, kila wakati wale wanaotaka ukombozi hawana sauti ambayo ni tendaji? Mwanamke akibakia katika kutendwa na kupewa kauli ya utendwa; hali mwanaume akiwa mtendaji. Je, ukombozi unaotarajiwa utapatikana? Hii inadhihirisha kuwa kazi ya Ngozi siyo ya kipropaganda. Katika ukinzani huu, ndimo mlimo na kichocheo cha kazi ya kitaaluma. Uteuzi na uchaguzi ulivutwa na ukinzani huu. 3.3 Ukusanyaji wa Data Data kuu iliyotumika katika utafiti wetu ni maneno yaliyochopolewa kutoka katika tamthilia. Data hiyo imekusanya vishazi vyote vyenye hali ya utendwa katika tamthilia ya Machozi ya Mwanamke. Ili kuvipata vishazi hivyo, tamthilia hii ilichapwa yote katika kompyuta na ilipangwa kama matini moja yenye mtiririko ambapo kila mstari ulichukuliwa kama sentensi. Mistari hiyo (au sentensi) ni maneno yaliyosemwa na wahusika. Kila sentensi ilipewa namba tangu onyesho la kwanza hadi la tatu. Baada ya hapo, vishazi vyote vilivyo katika utendwa vilikolezwa kwa wino, vikapigwa mstari, na kuandikwa kwa hati ya mlalo ili vijitokeze wazi kutoka katika maneno mengine ya mstari husika. Vishazi vya utendwa wa hiari na lazima vimeshughulikiwa. Vishazi vyenye utendwa wa hiari ni vile vinavyotoa uhuru kwa mzungumzaji kuweza kutumia kauli zote mbili – yaani kauli ya utenda na utendwa bila kujali jinsia yake. Vishazi vya utendwa wa ulazima ni vile vinavyohusiana hasa na matendo yanayoelezea mahusiano ya kingono kwa wanawake na wanaume. Matendo haya huwalazimisha wanawake kuyatumia katika hali ya kutendwa, na wanaume kuyatumia katika hali ya kutenda. Jambo hili litafafanuliwa katika sura nne inayohusu matokeo ya utafiti na mjadala; ili kuonesha jinsi lugha na utamaduni  vinavyokamilishana. Baada ya kuvibaini vishazi hivi, tuone sasa mbinu ya uchambuzi wa data tuliyoikusanya.

3.4 Mbinu za uchambuzi wa Data 

Mbinu za uchambuzi wa data zimeegemea katika mawazo ya wataalamu kama vile (Halliday na Hasan, 1976) na (Kahigi, 1997). Ingawa kumekuwa na mabadiliko madogo madogo, wazo la msingi lililoongoza mbinu hizi ni matumizi ya utendwa kama suala la uhiari. Baada ya kuzibainisha data tutakazotumia, (yaani kauli za utendwa) na kuzichopoa miongoni mwa maneno mengine, hatua kadhaa zilifuatwa katika mchakato wa uchambuzi wa data. Kwanza ilikuwa ni kuainisha kauli za utendwa. Katika hatua hii, matumizi ya utendwa yaligawanywa katika aina tatu ambazo ni: upekee wa lengo la mwandishi, mada, na mazingira. Kwa hiyo, kila data ambayo imechambuliwa imewekwa katika aina hizo. Kiambatisho namba 1, 2, na 3 kinatoa taarifa hii kwa kina (Taz. Uk. Wa 52 - 60). Hatua ya pili katika uchambuzi ni kubainisha kishazi gani kimetolewa na nani. Kwa maneno mengine kila mhusika aliwekwa pamoja na kauli za utendwa au utenda anazozitoa. Wahusika hawa waligawanywa sio tu katika jinsia zao, bali hata uhusika wao na nafasi zao (au umuhimu wao) katika kuiwakilisha dhamira ya mwandishi (Taz. Jedwali namba 5,6, na7 Uk. wa 80 – 85). Hatua ya tatu ilikuwa ni kubainisha dhamira kuu ya mwandishi. Ubainishaji huu ulikuwa ni wa kuangalia kazi nzima kwa ujumla na kuangalia kazi kwa kuigawa katika maonesho yake na sehemu zake. Utambuzi wa dhamira kuu ilikuwa ni hatua muhimu katika kuchambua data kwakuwa, baada ya hatua hii, hatua ya nne ilikuwa ni kuweka pamoja vishazi vyote vya utendwa vilivyokwisha bainishwa kwa kuvipanga kutokana na ukaribu wake katika kuiwakilisha dhamira hiyo kuu. Dhamira kuu iliyobainishwa ni ukombozi wa mwanamke. 57 Vifungu vyote vinavyowakilisha dhamira hii viliwekwa pamoja na kuangalia kiwango cha utendwa katika vifungu hivyo, nani anatoa kauli hiyo na katika mazingira gani. Hatua ya tano ilikuwa ni kupanga vifungu hivi katika majedwali yanayowakilisha aina za uchambuzi tulizozifanya. Hatua hizi (au mbinu hizi) tulizozitaja, zimefanyika kwa makini ili kuweza kutoa matokeo yasiyotetereka ambayo yanawasilishwa katika sura inayofuata. Sura hii ya nne pia itaonesha uchambuzi wenyewe, na kujenga mjadala unaolenga kujibu maswali ya utafiti. Ni katika mjadala huu tunapojizatiti kukamilisha malengo ya kazi nzima. 3.5 Hitimisho Katika sura hii, tumejadili sababu iliyotufanya tuteue tamthiliya ya Machozi ya Mwanamke katika utafiti wetu. Vilevile, tumejadili mbinu za ukusanyaji na uchambuzi wa data ambayo imeshughulikiwa. Mwisho, tumetoa hitimisho la sura ya tatu jambo linalotuwezesha kuiangalia sura ya nne.

SURA YA NNE UWASILISHAJI WA DATA, UCHAMBUZI, NA MJADALA

4.1 Utangulizi 

Sura hii inahusika na uwasilishaji wa data, uchambuzi, na mjadala. Katika kufanya hivi, sura ina sehemu nne ambazo ni: 4.0 utangulizi, 4.1 uwasilishaji na uchambuzi wa data, 4.2 mjadala na 4.3 hitimisho. 4.2 Uwasilishaji na Uchambuzi wa data Sehemu hii inawasilisha data zilizokusanywa kutoka katika tamthilia ya Machozi ya Mwanamke na uchambuzi wa data hizo. Uchambuzi huo wa data unalenga kupata majibu ya maswali ya utafiti huku ukiongozwa na malengo ya utafiti. Data inayowasilishwa hapa imewekwa katika majedwali. Kila baada ya jedwali kuna maelezo yanayolenga kufafanua yale yaliyosemwa katika jedwali husika. Uwasilishaji huu utafanywa kupitia katika hatua mbili muhimu: hatua ya kwanza ni kuainisha sababu za upekee, mada, na mazingira (Tazama jedwali la 1, 2 na 3). Hatua ya pili ni kuonesha ujengwaji wa maonesho na sehemu za tamthilia vinavyohusiana na yale ayaongeleayo mwandishi. (Tazama jedwali la 4). Baada ya kuwasilisha data na kufanya uchambuzi, tutaingia katika mjadala. Katika mjadala tutabainisha dhamira mbalimbali katika tamthilia hii huku tukiziangalia nadharia za elimu mtindo na hasa nadharia ya usimulizi. Katika kufanya hivi, tutakuwa tunajadili kuhusu kauli zinazotolewa na pia ni nani anayezitoa na tutathubutu kujadili kwanini zinatolewa.

 4.2.1 DATA NA UCHAMBUZI WAKE 4.2.

1.1 UPEKEE WA LENGO LA MWANDISHI
Muktadha wa Kauli ya Utendwa UPEKEE WA LENGO la Mwandishi Lakini mke wa mwenetu Kisanko, amewekewa boi wa kufagia nyumba na kufua (S.145)* Jinsia ya kiume inapozungumza na wanaume wenzake kuwahusu jinsia ya kike. Basi Bwana Kilakita, ameshindwa na mkewe hasa (S. 115)* Jinsia ya kiume inapowazungumzia jinsia ya kike kwa ujumla wao. Ujue umetawaliwa na mkeo Bwana wee (S.1234)* Jinsia ya kiume inapozungumza na wanaume wenzake kuwahusu jinsia ya kike. Wamepata nini hasa wanaume hawapendi kutawaliwa na wake zao (S. 1291)* Jinsia ya kiume inapowazungumzia jinsia ya kike kwa ujumla wao. Kule kuumbwa kwao na Mungu wawe hivyo, yaani kuchukua mimba, haina maana muwaonee na kuwatesa (S.1192)* Jinsia ya kiume inapozungumza na wanaume wenzake kuwahusu jinsia ya kike. Sisi leo tumefukuzwa, lakini mali aliyonayo huyu bwana tumeichuma wote (S.1079) *. Jinsia ya kike inapoongelea hali au mustakabali wake katika ndoa. Basi ndiyo tunawekwa humu ndani kama vimada (S.825) *. Jinsia ya kike inapoongelea hali au mustakabali wake katika ndoa. Jedwali Na. 1. Mwainisho wa kauli za utendwa na upekee wa lengo la mwandishi *. Namba ya sentensi kwenye tamthilia Upekee wa lengo la mwandishi unamaanisha uamuzi wake wa kuwapa wahusika kauli fulani mahususi. Upekee huu unatokea pale mwandishi anapoamua mhusika yupi atumie kauli ya aina gani na kwa nini. Katika utafiti huu, mazingira au muktadha wa ujitokezaji wa kauli ya utendwa unaoneshwa katia sura tatu muhimu: kwanza, mwandishi ametumia kauli ya utendwa pale jinsia ya kiume inapozungumza na wanaume wenzake kuwahusu jinsia ya kike; pili, ni pale jinsia ya kiume inapowazungumzia jinsia ya kike kwa ujumla wao; na tatu, ni pale jinsia ya kike inapoongelea hali au mustakabali wa wanawake katika ndoa. 60 Katika mazingira haya matatu, inadhihirika wazi kuwa mwanamke bado anaangaliwa kama kiumbe anayestahili kutendewa kazi na kuwa yeye hana uwezo wa kutenda. Hata pale mwanamke mwenyewe anapoongea kuhusu mustakabali wake katika ndoa, anaishia kusema tu: “tumefukuzwa” au “tumewekwa humu ndani”, ingawa anayesema hivyo anajua kuwa amefanya kazi kubwa ya kujenga familia na kuchuma mali kwa ajili ya familia, hatumii utenda katika kauli inayogusa mustakabali wake au kuishi kwake katika ndoa. Mfano mwingine, kutumika kwa utendwa “amewekewa boi,” kunaonesha kuwa, katika macho ya mwanaume (Madahiro), mwanamke bado ni wakufanyiwa kazi. Mwandishi angeliweza kumpa mwanamke kauli ya utenda na bado maana ya msingi ikabaki ni ile ile. Katika mazingira haya angeliweza kusema: “Mke wa mwanetu Kisanko ameweka boi wa kufagia nyumba na kufua” (S.145). Kwakuwa mjadala unamhusisha mwanamke kupitia katika jicho la, (na kwa hakika mdomo wa) mwanaume, ndio maana utendwa umetumika. Hoja hii ya ni nani hasa anayeongea tutaiangalia kwa undani katika sehemu ya mjadala kwa kuitumia nadharia ya usimulizi. Suala la mwonekano wa mwanamke mbele ya mwanaume tunalipata pia katika upekee wa mwandishi pale jinsia ya kiume inapoongelea jinsia ya kike kwa ujumla wao. Katika maongezi baina ya jinsia ya kiume tunaona sentensi ifuatayo: “Wamepata nini hasa wanaume hawapendi kutawaliwa na wake zao” (S.1291). Kutumika kwa utendwa kunaonesha kuwa, katika macho ya mwanaume (Madahiro), siku zote dhana ya kutendwa haikubaliki kwa mwanaume. Kwakuwa mwanaume anajiona yuko juu ya mwanamke mwandishi ametumia kitenzi cha ukanushi “hawapendi” kuonesha kuwa suala la kutendwa kwa mwanaume, na hasa inapotokea mtendaji ni mwanamke, ni suala lisilokubalika. 61 Mwanaume ndiye anayeweza kutawala na sio vinginevyo. Mwandishi amemnyima mwanamke kauli ya utenda hata pale ambapo maana ya msingi ingelibaki ni ile ile. Kwa mfano katika mazingira haya angeliweza kusema: “Wamepata nini hasa wanaume hawapendi wake zao wawatawale”. Suala la mwanamke kupewa dhana ya utenda, ni jambo ambalo mwandishi ameliepuka kabisa. Uteuzi na matumizi haya umekwenda sambamba, sio tu na upekee wa mwandishi, bali hata uchaguzi wa mada inayozungumziwa. Katika mifano ifuatayo tutaona, japo kwa uchache jinsi mwandishi alivyoumba mazungumzo ambayo yanadokeza mada inayoongelewa: 4.2.1.2 MADA INAYOZUNGUMZIWA Kauli ya Utendwa MADA inavyochochea matumizi ya utendwa Tangu utotoni, mtoto wa kike anawekwa katika hali ya uke hasa, na kufanywa amtumikie kaka yake (S. 1280)* Ujamiishaji: mwanamke ni wa kumtumikia mwanaume. Mama ameumbwa ili alee watoto na kufanya kazi za nyumbani na ndiyo maana hawezi kuwa na nguvu sawa na mwanaume (S. 1191)* Ujamiishaji: udhaifu wa mwanamke ni wa asili hauwezi kubadilishwa. Mradi tumeitwa ‘wanawake’ ndiyo hata tunapigwa hamna hata kujitetea! (S.788) * Mtazamo potofu unaoegemezwa katika mila. Mada ya uonevu kwa wanawake. Na kupigwa hasa. Mtu unatimbwa mpaka unakaribia kufa (803) * Uonevu kwa wanawake. Sisi leo tumefukuzwa, lakini mali aliyonayo huyu bwana tumeichuma wote (S.1079) *. Uonevu kwa wanawake. Ukiangalia kwa jicho la akili, bila ya kuupendelea upande wowote, utaona jinsi wanavyoonewa, wanavyogandamizwa, kunyanyaswa na kudharauliwa (S.1262) *. Uonevu na unyanyaswaji kwa wanawake. Umeolewa kwa fedha mama (S.316) * Mahari kama kisingizio cha kumnyanyasa mwanamke. Jedwali Na. 2. Mada inavyochochea matumizi ya kauli za utendwa. 62 Kwa hakika mada mbalimbali zilizozungumziwa na mwandishi zimelazimisha uteuzi kadhaa wa kauli za utendwa. Katika mifano hii michache katika jedwali namba 2, mwandishi anateua kauli za utendwa ambazo zitaendana na mada anayoizungumzia. Kwa mfano, ujamiishaji wa kijinsia1 unamfanya mwandishi atumie utendwa kama vile: “anawekwa, kufanywa, na ameumbwa,” wakati anapomzungumzia mwanamke. Swali la kujiuliza hapa ni nani ambaye “anaweka” au “anafanya”. Mtendaji ni nani; na kwanini mwanamke apewe kauli ya utendwa? Wakati wa kujadili data hizi tutaona ni jinsi gani uteuzi huu umefanywa kwa uangalifu mkubwa ili kutimiza lengo la mwandishi. Ni nani anaumba tofauti za kikazi kati ya msichana na mvulana kuhusiana ushiriki wao katika shughuli za kijamii? Jamii inafanywa iamini kuwa udhaifu wa mwanamke ni wa asili. Imani hii inajengwa kwa mbinu mbalimbali na mojawapo katika fasihi ni kuwafanya wahusika kupewa lugha itakayobeba maana na maudhui hayo; ni lugha kama hiyo ambayo pia imetumika kuonesha dhana ya uonevu. Dhamira ya uonevu, unyanyasaji, ukandamizaji, na dharau ndiyo imechukua nafasi kubwa katika tamthilia ya Machozi ya Mwanamke. Kuthibitisha hili, kauli za utendwa zinazohusiana na dhamira hii, au zinazodokeza dhamira hii, zimejitokeza mara nyingi zaidi kiidadi kuliko kauli za utendwa za mada nyingine. Katika jedwali la 2, kauli za utendwa zilizotumika ni kama vile: kupigwa, kutimbwa, kufukuzwa, kunyanyaswa na kadhalika. Katika mazingira haya, mwandishi angeliweza kutumia maneno hayo hayo katika kauli za utenda na bado 1 Ujamiishaji wa kijinsia ni hatua na michakato yote ambayo jamii hupitia katika kumfanya mtoto wa kiume au wa kike akue akijua kuwa yeye ni wa jinsia fulani na hapaswi kufanya kazi, au kuishi maisha kama jinsia nyingine. Katika kufanya hivi, jamii humuaminisha mhusika hata afikiri kuwa ndivyo anavyotakiwa kuwa na si vinginevyo. 63 maana ya msingi ikabaki ni ile ile. Hata hivyo, kauli ya utendwa inapotoka mdomoni mwa mtendewa, basi inaonesha dhahiri hali yake ya kuukubali udhaifu na kujiona kuwa yuko chini ya mamlaka au nguvu fulani ambazo hana uwezo wa kuzipinga na kuziondosha. Matumizi ya kauli ya utendwa yanafungamana na matendo ya ukandamizwaji; ambapo, lugha inamchomoza mhanga wa ukandamizwaji ambaye katika Machozi ya Mwanamke ni mwanamke. Mwanamke mwenyewe tunaona anatumia lugha ya utendwa akijiweka katika hali ya kunyanyasika, kuonewa na kukandamizwa. Matumizi haya ya lugha yanatupeleka kwenye madai ya Lakoff (1975) aliyoyatoa kuhusiana na matumizi ya lugha na wanawake. Lakoff, (kama ilivyotajwa) anadai kuwa, wanawake hunyanyaswa mara mbili: kwanza kwa jinsi lugha inavyotumika kuwazungumzia wao; na pili, jinsi wanavyokuzwa na kufundishwa namna ya kutumia lugha hiyo. Mbali na lugha kama hii kuna hata matendo au taratibu za mila ambazo jamii huziegemea katika kumtofautisha mwanamke na mwanaume. Mojawapo ya nguvu ya kijamii ambayo inatumiwa vibaya kumnyanyasa mwanamke ni suala la mahari. Wataalamu kadhaa wameandika kuhusu uhusiano wa mahari na unyanyaswaji wa mwanamke. Baadhi yao ni kama vile: (Brewer, hakuna mwaka, http://links.org.au/node/159); (Amatullah, 2005), (Habati, 2005) na sura ya tatu ya jarida la (Permanent Revolution, 2006). Katika makala hizi tafiti zimefanyika katika jamii mbalimbali na kuonesha utumiwaji mbaya wa mila ya mahari, na jinsi baadhi ya wanaume katika jamii wanavyomnyanyasa mwanamke wakiegemea katika mahari. Katika tamthilia ya Machozi ya Mwanamke, mwandishi analiongelea hili akimtumia mhusika mkuu Madahiro, anayetoa kauli ya utenda akisema: “... mke niliyemwoa kwa pesa za jasho langu...umeolewa kwa fedha mama...Fedha...” (uk. 9-10). 64 Kwa kusema hivi, jinsia ya kiume kupitia kwa Madahiro inatumia vibaya mila ya kutoa mahari, na kuibadili kuwa kigezo cha mateso, kunyanyasa na kumkandamiza mwanamke. Kwakuwa katika mahusiano hakuna jinsia inayosimama peke yake na kujitosheleza kwa kutumia vitenzi kama vile “penda,” au “oa,”, basi maneno yaliyotumika hapa, kama vile: “kuolewa” au “kupendwa” yangaliweza kuwa ya utendana na maana ikabaki ni ile ile. Kwa hakika maana ingelikuwa wazi zaidi na sahihi kutumia kauli ya kutendana kuliko utendwa. Kwa hiyo, uteuzi wa msamiati ambalo ni suala la mtindo, unatuonesha kuwa mwandishi alikuwa makini kumpa kila mhusika wake lugha inayoendana na jambo ambalo anataka kuliwasilisha. Suala hili la kumpa mhusika lugha maalumu linaendana pia na sababu za mazingira. Sababu za mazingira tutaziangalia hapa chini ili kuona ni katika muktadha gani mhusika anatumia neno analolichagua kulitumia. Mazingira yatatuongezea ufahamu wetu wa ni nini humuongoza msemaji wakati anachagua neno moja na kuacha jingine katika kuwa na mawasiliano miongoni mwa wahusika. 65 4.2.1.3 MAZINGIRA YANAYOZUNGUKA KAULI ZA WAHUSIKA Kauli (utenda au utendwa) inayotolewa Mazingira yake Ndiyo maana akili zao ndogo huwa hawafikiri chochote wakikutwa na matatizo isipokuwa kulia (1182) * Mazingira yanayoendekeza mawazo ya ukasuku kuhusu wanawake. (mimi) nilimpa siku tatu...akirudi atanieleza vizuri (18 )* Mazingira ambapo utenda unatumika kuonesha mamlaka ya mwanaume. Shauri yake tena. Atanunuliwa na bwana aliyemkawiza huko (22)* Mazingira yanayoonesha mwanamke kutokuwa na uwezo wa kutenda yeye mwenyewe. Mwanamke bila kumpa amri yako sio mkeo tena (99)* Mazingira ambapo utenda unatumika kuonesha mamlaka ya mwanaume. Na usilogwe kutawaliwa na mkeo-ujue umekwisha…(105)* Mazingira abapo mwanaume anakataa kuchukuwa utendwa. Ati nini? Unanitukana…!(235)* Kauli ya utenda, amewekewa mwanamke ili kuandaa mazingira ya uonevu. “…sikiliza wewe unafikiri mimi bila ya kutoa pesa ungalikuwa hapa? Umeolewa kwa fedha mama (316)* Mazingira yanayoonesha mamlaka na nguvu ya pesa. Mazingira ambapo mwanaume anatumia pesa kumnyanyasa mwanamke. Aaa! Babu, lazima niseme ati! (576)* Mazingira ya kujikomboa. Mwanzo ni kujipa kauli ya utenda. Basi nasi tunajilegeza mno...hamna hata kujitetea... bora kujitetea(787)* Mazingira ambapo mwanamke anajiandaa kujitetea na kuanza kutumia utenda. Mazingira ambapo maneno yanaanza kujenga fikra za ukombozi. Mbona kazi gumu ngumu tunazifanya? Jamani leo tujaribuni. Akimpiga mmoja wetu tuingilie kati na kumvamia (866)* Mazingira ambapo fikra za ukombozi zinazaa mpango mkakati wa namna ya kutenda. Fikra zinazaa matendo. Haiwezekani, hivi ni nani kweli awezae kupokonywa wanae mwenyewe? (1145)* Sauti ya mwanaume ikitumia utendwa kuonesha mazingira ya kushindwa na hoja. Jedwali Na. 3. Kauli za utendwa na utenda zinavyojengwa na Mazingira Mazingira mbalimbali yanaibua kauli za utenda na utendwa zinazotolewa na wahusika. Katika kufanya hivi, wahusika huzingatia sana nafasi walizonazo: nafasi zao katika jamii, nafasi ikilinganishwa na wale wanaoongea nao, nafasi wakati wa kuongea na kadhalika. 66 Muktadha wa maongezi na uchaguzi wa msamiati hujali sana mila na tamaduni za jamii husika. Kwa mfano, wahusika ambao wamekuzwa katika mfumo na mila ambapo wanaume na wanawake huangaliana kwa namna tofauti, maongezi yao pia yataakisi namna hii ya kuangaliana. Mfano halisi ni namna mwandishi alivyochora mawazo ya wanaume kuhusu wanawake akisema: wanawake wakikutwa na matatizo wanalia tu. Katika kusema hivi, mwanamke anaondolewa uwezo wake wa kujimudu. Kutokujimudu kunaongozwa na namna anavyopewa kauli ya utendwa: “wanakutwa”. Mwanamke anaonekana ni muhanga na hana uwezo wa kujiondolea tatizo hilo. Maneno kama: “anajikuta katika matatizo”, au “akikutana na matatizo” yangeliweza kutumika bila kubadili lengo la msingi katika kuwasilisha wazo linalosemwa. Mazingira yanayoongoza uteuzi huu ni yale ambayo, katika jamii mwanamke huonwa kuwa hawezi kujimudu, ni muhanga na yeye mwenyewe hana njia nyingine ya kupambana na yanayomsibu isipokuwa kulia. Mazingira haya ndiyo huzaa misemo kama vile: “Machozi ya Mwanamke yako karibu.” Au utasikia mwanaume akiambiwa: “usilie kama mwanamke.” Hizi ni mojawapo ya kauli zinazotengeneza mazingira ambamo mwanamke huonekana mnyonge. Kauli nyingine zinazomjenga mwanamke aonekane muhanga na hivyo hawezi kujimudu ni kama vile: kununuliwa, kutawaliwa na kuolewa. Kauli hizi zinajichomoza katika mazingira ambamo mwanaume anaonekana ni mwenye madaraka na mamlaka katika jamii ilihali mwanamke anakuwa ni mtu asiye na uwezo, mamlaka, na madaraka. Mazingira ya uonevu, kutawaliwa na kunyanyaswa yanaonekana mwanzoni mwa tamthilia 67 hii. Na kadri mwandishi anavyoandika kuhusu muktadha huu wa uonevu, ndivyo wahusika wake wa kike wanavyopewa kauli za utendwa. Kwa upande wake, mwanaume anapewa kauli za utenda. Yeye ndiye mtendaji, akionesha mamlaka, nguvu na uwezo. Kwa mfano katika jedwali kauli tunazoziona ni kama vile: kumpa, na kutoa. Kauli hizi na nyingine nyingi zinazoonesha utenda, zinapatikana sana mwanzoni mwa tamthilia hadi kati kabla ya mabadiliko ambayo yanalengwa na mwandishi. Mazingira ya mwanzo na kati mwa tamthilia yaliandaliwa na mwandishi kutoa sura ya wanajamii kuhusiana na suala la ukombozi wa mwanamke. Ni mazingira ambamo mwandishi anampa mwanamke utendwa, na kutokea pale anaonesha jinsi jamii isivyo tayari kumwona mwanamke akijikomboa. Ni mazingira ambamo mwanaume anapewa kauli ya utenda na kuoneshwa jinsi anavyojifanya ni mwenye uwezo wa kutenda na kuendesha familia: kuoa wake wengi, kuwanunulia nguo, na kuleta mahitaji kwa jinsi anavyoona yeye; lakini wakati huohuo, kusimamia kazi ambazo zote zinaonekana zikifanywa na wanawake. Mazingira haya yamechorwa ndani ya msuko wa matukio yakiambatana na kauli za utendwa na utenda zinazotolewa na wahusika. Mwandishi ameipanga vema tamthilia hii ili maonesho yote na hata sehemu zake ziendane na yale yanayolengwa kusemwa. Katika sehemu inayofuata, tutaona msuko huu na mpangilio wa maonesho jinsi unavyoendana na yale yasemwayo na dhamira nzima ya tamthilia hii ambayo ni ukombozi wa mwanamke. 68 4.2.1.4 MSUKO WA MAONESHO NA UHUSIANO WAKE NA YASEMWAYO Muundo wa tamthilia Yale yasemwayo Onyesho la Kwanza “Pazia linapofunguka tunauona ukumbi wa Bwana Madahiro...” Ingawa hii ni nyumba yenye wake wengi na mume mmoja, mwandishi anatujulisha kuhusu umiliki wa mali na nyumba kupitia katika kumwonesha zaidi mwanaume. Maelezo na taswira zinajenga kuonesha mamlaka ya mwanaume Onyesho la Pili Sehemu ya Kwanza “Pazia linapofunguliwa tunamwona Madahiro amelewa chakari...” Kutokuwajibika kwa mwanaume kunaoneshwa tangu mwanzo kupitia katika taswira ya ulevi kwa upande mmoja na taswira ya kazi kwa wake zake kwa upande mwingine. Mwanaume anaoneshwa “...akila, akinywa, na kuoa wake...” Sehemu ya Pili Katika sehemu hii, tunaoneshwa utendaji wa kazi wa akina mama. Mwandishi anatuonesha maisha ya wake wa mume mmoja na nafasi ya mume wao katika maisha yao. Taratibu wasomaji wanaelekezwa kulinganisha maisha ya wanawake-wachapa kazi, na maisha ya mume-mvivu, mlevi, mgomvi. Onyesho la tatu Taswira ya mabadiliko na ya ukombozi inaoneshwa tangu mwanzo kwa wanawake kutoka “nyuma ya nyumba” na kufanyia kazi zao “nje ya nyumba.” Wanawake wanaanza kuonekana Wanawake wamepewa lugha yenye kauli za utenda katika onyesho la tatu kuliko katika maonyesho mawili yaliyotangulia Ukombozi wa mwanamke unaanzia katika ukombozi wa fikra: elimu na hatua ya utekelezaji inafuata. Jedwali Na. 4 Mwingiliano kati ya muundo, maudhui na dhamira za tamthilia Tamthilia ya Machozi ya Mwanamke ina maonesho matatu yenye jumla ya kurasa 39. Tamthilia hii imeundwa hivi kwamba, onesho linalobeba dhamira kuu limepewa nafasi zaidi. Katika kuhakikisha hili, onesho la kwanza lina kurasa nane tu. Ni onesho linaloeleza mamlaka na nafasi ya mwanaume katika ndoa, uwezo wake, na utashi wa kuoa wake wengi; 69 maongezi ya wanaume kuhusu nafasi yao kama wanaume katika jamii ikilinganishwa na wanawake, na ugomvi na mapigano ambapo mwanaume anagombana na kuwapiga wake zake. Katika onesho hili pia tunaona kuwa wanawake ambao wanapigwa na kutukanwa wamepewa kauli za utendwa zaidi kuliko utenda; wakati wanaume wana kauli za utenda na wanaonekana wakitenda kwa kupiga na kutukana. Nafasi ya mwanaume ikilinganishwa na mwanamke, inaonekana tangu mwanzo mwa onesho. Pazia linapofunguliwa tunaambiwa kuhusu Madahiro. Tunaambiwa kuwa ni (“ukumbi wa Bwana Madahiro)”. Tunaandaliwa kumwona Madahiro na sio wake zake. Sura ya wake zake tunayooneshwa na (“mke mwenye mimba kubwa akiingia akiwa amechukua mzigo wa kuni kichwani, akimbembeleza mtoto mgongoni...”) Mara moja msomaji wa tamthilia hii anatazamishwa kuona mume anayetawala na mke anayetawaliwa. Ni onesho linaloanza na kutokufanya kazi kwa mwanaume (“anajitupa katika kiti cha uvivu akivuta mtemba...”) na kumalizika na mume akiazimia kuoa mke mwingine na akitaka kumpiga Mlahaka mkewe aliye naye. Huo ndio msuko katika onesho la kwanza. Masuala ya familia yanafafanuliwa zaidi katika Onesho la pili. Onesho la pili lina kurasa zaidi ya onesho la kwanza-zimo kurasa 12. Ikimaanisha kuonesha visa na vituko zaidi katika kumwandaa msomaji kufahamu upana wa tatizo la unyanyaswaji wa wanawake, na hitaji la lazima na umuhimu wa ukombozi wa wanawake. Onesho hili lina sehemu mbili zinazolingana, kila moja ikiwa na kurasa sita. Onesho linafunguliwa kwa kuoneshwa ulevi wa mwanaume Madahiro – mhusika mkuu. Maneno ya kilevi ya Madahiro yanaakisi nafasi yake katika ndoa na katika jamii ya mfumo dume: utamu wa maisha 70 unaonekana katika kula, kunywa na kuoa wake ambao wataendelea kumfanyia kazi mwanaume (uk.9). Sura hii tunaipata katika sehemu ya kwanza ya onesho la pili. Kiburi anachopata mwanaume na mamlaka anayojitwalia katika familia vinachipuka kutokana na mahari. Mhusika mkuu Madahiro anasema: “Ohooo...naona sasa unataka kuingilia uhuru wangu. Tena wataka kunitukana. Sitaki kutawaliwa na mke wangu mimi. Mke niliyemwoa kwa pesa za jasho langu...sikiliza wewe unafikiri mimi bila ya kutoa pesa ungalikuwa hapa? Umeolewa kwa fedha mama...Fedha...” (uk9-10). Suala hili ndilo linalojenga nguzo ya mazungumzo katika sehemu hii na hata ubabe anaouonesha Madahiro kwa mkewe Mauja. Sehemu hii inaanza kwa ulevi na kuisha kwa ulevi ikionesha na kusisitiza uvivu wa mwanaume katika familia na utendaji kazi wa mwanamke. Ni sehemu inayoonesha kuwa ingawa mwanaume anapewa kauli ya utenda, ikishadidiwa na tendo la utoaji mahari, kazi za nyumbani zinafanywa na mwanamke. Kazi za nyumbani ndio taswira tunayoipata tunapoanza sehemu ya pili ya onesho la pili. Sehemu hii inaonesha kinyume na mwisho wa sehemu ya kwanza. Hii ya pili tunaoneshwa kuwa mtendaji halisi ni mwanamke. Hata kabla ya pazia kufunguliwa tunasikia vishindo vya kutwanga. Linapogunguliwa: (“tunawaona Mlakaha na Deka wakitwanga katika kinu kimoja na Mauja ambaye amembeba mwanae mgongoni akipepeta kando yao”) Mwandishi anatuonesha maisha ya kawaida katika nyumba ya wake wengi; na kisha tunamwona mume akiingia. Mwandishi anatuonesha dhana kuwa “mambo ya kugombana ni ya wanawake” na kuwa wanawake ni viumbe wasio na akili (ukurasa wa 17). Mwamuzi (na hivyo asiyependa ugomvi na mwenye akili) ni mwanaume. Katika hali kama hii, bado mwanaume anapewa 71 kauli za utenda, na mwanamke anapewa kauli za utendwa. Kutokana na muundo huu, mwanaume: Madahiro anawanyanyasa wake zake, akiwaonea na kuwasimanga, na lugha yake ikisheheni kauli za utenda. Onesho la pili sehemu ya pili inamalizika kwa mume kumfukuza mkewe mmoja mbele ya wake zake wengine ambao hawana jambo la kufanya zaidi ya kushangaa na kulia. Msomaji anajengewa mazingira ya kitaharuki kutaka kujua ni nini kitafuata na mustakabali wa wake za Madahiro utakuwaje. Taharuki hii imejengwa kwa kutumia mbinu ya kidrama ya usababisho na matokeo ambapo tendo B linatokana moja kwa moja na tendo A. Hali hii ndiyo inayotuingiza katika Onesho la tatu na la mwisho. Onesho la tatu lina jumla ya kurasa kumi na tisa. Ndilo onesho refu kuliko mengine yaliyotangulia. Limepewa urefu huu ili kujenga na kusisitiza umuhimu wa suala la ukombozi kwa mwanamke. Ukombozi dhidi ya matendo na matukio yaliyoonwa katika maonesho mawili yaliyotangulia. Tangu mwanzo tunaandaliwa kumwona mwanamke zaidi kuliko mwanaume. (“Pazia linapofunguliwa, anaonekana Deka akiwa amekaa kitini akimsuka nywele Nasaa na karibu yake kitini amekaa Mlahaka”). Taswira ya kumwona mwanamke akiwa amekaa kitini na akifanya shughuli nyepesi, ni kinyume kabisa cha maonesho yaliyotangulia. Kwa hiyo, taswira tunayoiona mwanzoni kabisa ni ya mabadiliko na ya ukombozi. Mabadiliko yanaletwa na mwonekano wa wazi wa wanawake tangu mwanzo. Mabadiliko haya yanaendana na lugha wanayoipata katika onesho hili. Tofauti na maonesho yaliyotangulia, hapa mwanamke anaonekana kuwa na kauli za utenda zaidi kuliko utendwa. Suala hili sio tu linaendana na msuko wa onesho bali pia nafasi za uhusika wanazopewa. Kwa 72 mfano, Mlahaka anaonekana akisuka. Kwanza tunaona kuwa hii ni “elimu mpya” ya kumfanya ajikomboe na pili, tunaona kuwa ni kupitia katika Umoja na kazi ndipo mwanamke atakapoweza kupata ukombozi wa kweli. Nasaa anamwambia hivi Mlahaka: “Tena ungalikuwa umekwisha kujua toka siku nyingi kama ungelisikia maneno yetu ya kujiunga na Umoja wa akina Mama. Wenzio tunejifunza mengi...” Jambo hili linatupa mwangaza wa nini kinachoelekea kutokea - ukombozi wa mwanamke. Jambo la msingi katika ukombozi wa kweli ni elimu-kupitia katika elimu: kupata ufahamu na kuchukua hatua ndimo mlimo na nguzo za ukombozi. Onesho hili linatawaliwa na maandalizi ya kifikra ya dhana ya kujikomboa, kabla ya kutiana moyo na kuchukua hatua ya ujasiri na ya mapinduzi. Ujasiri huu unaonekana tangu mwanzo ambapo nafasi ya mwanamke inatoka kuwa ya nyuma, uani, mahali pa kufichwa; na kutokuonekana hadi kuwa mahali pa mbele, pa wazi, panapomfanya aonekane. Muundo huu na mazingira ya ukaaji au uonekanaji unakwenda sambamba na mhusika kuwa na kauli ya utenda. Kauli inayompa msemaji ujasiri wa kuonekana kuwa anaweza kufanya jambo. Hapa tunaona kauli kama vile: lazima niseme, tunajilegeza, kujitetea, tunazifanya, tujaribuni, tuingilie na kumvamia. Tangu mwanzo tunaona kuwa kufunguka mdomo na kutoa kauli ni hatua ya inayoonesha kukomaa kwa fikra. Katika maonesho ya mwanzo kunyamazishwa kwa mwanamke sio tu kunaonekana katika kupigwa na kutukanwa, bali hata katika kusema: MADAHIRO: “He! Shika adabu yako. Kama mimi ninasema wewe siyo kunichongelea hilo domo lako...” (Onesho la pili, sehemu ya kwanza, Uk. 12). Madahiro anaendelea akijitahidi kuwanyamazisha: “Kelele! Sitaki kusikia tena sauti zenu...He! Funga bakuli lako... Nimesema sitaki kelele hukusikia... Na sasa sitaki tena kusikia maneno yako...” (uk. 17). 73 Katika onesho la tatu, nguvu ya mwanamke katika kujikomboa inajichomoza katika kudai na kutaka kusema na sio kunyamazishwa: NASAA: “...Bora kujitetea. Lakini tukimwacha, ataendelea kutuonea sana. Mpaka lini? ...tunawatukuza sana wanaume na kukubali unyonge wetu. Lazima tuuondowe unyonge huu kama tunataka mabadiliko... hebu leo tujaribuni kujikaza jama...” (uk. 24-26). Taratibu tunaona jinsi hali ya kujikomboa ilivyoanzia katika elimu. Wanawake wanaelezwa mahali walipokosea na panapotakiwa kurekebisha. Wanaelezana mbinu za kufikia marekebisho hayo na umuhimu wa kuwa na umoja katika kufikia malengo. Hatua kubwa inayofuata ni vitendo. Vitendo vya kujikomboa kwa wake dhidi ya mume wao, kitendo cha kukataa kunyanyaswa, kuonewa na kupigwa, vyote hivi vinatanguliwa na wanawake kupata kauli ya utenda. Uhusika wao mara unabadilika, kutoka katika utendwa, pale wanapokuwa wanakaa tu na kusubiri kutendewa (kuonewa na kupigwa); hadi wanapoanza kwa kauli ya utenda wakiongea na kukataa kunyamazishwa na kisha hatua ya mapambano: NASAA: “Unamwonea tu, leo zamu yako kututambua nasi...” (uk. 27). Mbali na kauli hiyo inayofuatwa na kitendo cha wanawake kumvamia mume wao Madahiro na kuanza kumpiga na kumzidi nguvu, kunafuata pia sababu ya kuchukua hatua hiyo: DEKA: “Kwa ufupi ni kwamba baba Tama amezidi mno kutupiga, kututukana, kutusimanga, na kutunyanyasa utadhani tu watumwa...” (uk. 29). Wanawake wanatambua nafasi yao, na wanachukua hatua: NASAA: “...Unafikiri tunaweza tena kuishi nawe baada ya mambo haya yaliyotokea? Unafikiri nani atakaa tena aonewe?...” (uk. 31). Kauli ya utenda inatuonesha hatua muhimu inayostahili kuwapo katika jamii ikiwa suala la ukombozi litakuwa la kudumu:NASAA: “....Tena nakuahidi Baba Tama, mimi nitokapo 74 hapa, kazi yangu kubwa itakuwa kuwaelimisha watu juu ya suala hili zima la uhusiano kati ya mwanaume na mwanamke...” (uk. 32). Mwanamke anajipa kauli ya utenda na kuonesha azma yake ya kuikomboa jamii kupitia katika elimu. Elimu itakayoleta usawa: NASAA: “...sasa hivi tunachotaka ni haki yetu tu, tujiondokee. Mali iliyopo hapa hukuichuma peke yako (uk. 32). Kutoka katika tamko hili, mwandishi anatuonesha dhamira muhimu ya ukombozi. Maudhui ya tamthilia hii ikiwa ni pamoja na ujumbe, na dhamira vinatuelekeza katika ukombozi. Ili tuiangalie vema kauli hii ya ukombozi katika mapana yake na jinsi wahusika walivyopewa lugha inayoendana na uhusika wao, hatuna budi sasa kuingia katika mjadala wa kina utakaounganisha mawazo yatokanayo na uchambuzi wetu wa tamthilia hii na nadharia za mtindo na hasa ile ya usimulizi ambayo tumeitumia katika uchambuzi na tutaitumia katika kujenga mjadala. Ili mjadala wetu utiririke vizuri hatuna budi kuiweka tamthilia hii katika mukadha wa kihistoria. 4.3 Mjadala Katikati ya miaka ya sabini, harakati za ukombozi wa mwanamke ziliingia katika msukumo wa kipekee, na hasa baada ya kujulikana kuwa mwaka 1975 ulikuwa ni mwaka wa kujikomboa kwa wanawake, kama ulivyotangazwa na Umoja wa Mataifa. Kwa muktadha huu, inaweza kuonekana kuwa tamthilia ya Machozi wa Mwanamke ilikuwa inaungana na harakati hizi katika kuwaelimisha wanawake na jamii kwa ujumla kuhusu harakati hizi. Kwa kutumia nadharia ya naratolojia tunaweza kugundua ikiwa mwandishi anabakia kuwa sehemu ya mfumo au anajitoa na kuwa nje ya mfumo ili kuweza kuubadilisha kiuyakinifu. 75 Tunaweza kujua ikiwa mwandishi naye ni mhanga wa mfumo huo huo ambao anadhani anaupinga, au ni shujaa anayeugeuza mfumo, hali yeye mwenyewe akiwa sehemu yake. Katika utangulizi wa tamthilia ya Machozi ya Mwanamke, tunaambiwa kuwa mwandishi anakusudia kuwazindua wanawake, ili wajitambue na kujijua nafasi yao katika kutetea haki zao. Lakini, kwa nini kuzinduliwa huku kupitie katika machozi? Kwa vyovyote vile, lugha ya mwandishi imebeba ujumbe zaidi ya ule unaoonekana katika maandishi. Je ni jinsi gani mhakiki anaweza kuubaini ujumbe huo ambao hauko wazi? Mhakiki atumie mbinu gani kuangalia nje ya lugha ya maandishi na kuyaona yale yanayotokea katika jamii yakiwakilishwa kwa njia ya kisanaa kupitia katika tamthilia hii? Mawazo haya ndiyo yanajitokeza katika uchambuzi wa data. Kwa upande mmoja, mtafiti alitaka kujua ikiwa mwandishi alikuwa akiunga harakati za kujikomboa wanawake; kwanini alitumia mwanamke anayelia na kushadidia lugha ya “Machozi ya Mwanamke?” Je, kuna jambo lipi analotendwa mwanamke hata akalia? Kwa upande wa pili mtafiti alitaka kujua, je, mwandishi alitaka kutuonesha hayo anayotendwa mwanamke? Au aliyokuwa akitendwa na sasa amejikomboa nayo? Ili kufahamu haya, uchambuzi unalazimika kuangalia dhamira ya mwandishi. Katika sehemu iliyopita ya uwasilishaji wa data na uchambuzi wake tulijadili data hizo kwa kuzungukia maswali mawili kwa mujibu wa mkabala wa kiusimulizi. Swali la kwanza ni: “nani anaongea”. Swali la pili ni: “anaongea nini”. Katika maswali haya mawili tuliona waongeaji wanawake kwa wanaume, na kile kilichoongelewa kiliangaliwa kwa kutazama 76 kauli za utenda na utendwa. Swali jingine muhimu tutakalolitumia katika mjadala unaochambua dhamira ni: “nani anaona.” Katika nadharia ya naratolojia, swali hili ni sawa na kuuliza: “ni nani anatazamisha?” Maswali haya matatu yanayochipuka kutoka nadharia ya naratolojia, ndiyo yatakayoongoza mjadala katika sehemu hii. Kwa mujibu wa nadharia ya naratolojia, matini yoyote ile huangaliwa kama yenye kusimulia jambo. Swali linalouliza kuhusu mwongeaji ni nani, husaidia kutambua sauti inayosimulia, mbali na mhusika atoaye sauti hiyo. Hii ina maana kuwa, mhusika anayeongea anaweza kuwa ni mwakilishi tu wa kikundi fulani katika jamii, na hivyo sauti yake inachukuliwa kuwa ya kikundi hicho anachokiwakilisha na sio lazima hayo yawe ni mawazo yake. Anaweza kuwa ni mfanyakazi, pale anapoongea na wafanyakazi wenzake, akatoa sauti kumwakilisha mwajiri wake; akifanya hivyo anaweza kutokueleweka mbele ya wafanyakazi wenzake ambao wanamwona kama mwenzao, lakini wanasikia kinachowafanya wamwangalie kama si mwenzao. Anaweza kuwa ni mhusika mwanamke akatoa sauti kuwakilisha wanaume katika jamii, kwa kuwa wanaume ndio wanaotawala katika mfumo wa jamii husika. Na mhusika huyo kama mwanajamii asingependa kwenda kinyume na matakwa na uzoefu wa jamii aliyomo. Suala hili ndilo tunaloliona katika usimulizi wa tamthilia ya Machozi ya Mwanamke, tunapowaangalia baadhi ya wahusika wanawake Kabla ya mabadiliko, hasa katika Onesho la kwanza na la pili, ingawa Mlahaka ni mwanamke-sauti tunayoisikia kutoka kwake ni sauti ya kiume. Inawakilisha mawazo ya mfumo wa kiume. Ili mwandishi ajenge dhamira kuu ambayo ni ukombozi wa mwanamke, ametujengea maongezi ambayo yanakinzana yakionesha wazi mgogoro kati ya jinsia ya 77 kiume dhidi ya jinsia ya kike. Maneno asemayo MLAHAKA: “Unatuonea tu kwa kuwa sisi wanawake. Hebu pigana na hao wanaume wenzako...” (uk. 8) ni sauti inayosisitiza kuonekana kwa wanawake kama walio wanyonge, ilihali wanaume wakionekana kuwa ni wenye nguvu. Katika tamthilia inayotetea wanyonge na inayodhamiria kuleta ukombozi, sauti kama hii haitarajiwi. Sauti kama hii kwa hakika haina tofauti na sauti aitoayo Madahiro anaposema: “Wewe ni mwanamke tu. Unajua nini wewe?...” (uk.9). Mawazo haya ndiyo hutawala katika mfumo unaotawaliwa na wanaume. Sauti yoyote katika mfumo huu, ni lazima ifuate mawazo kama haya hata kama anayeitoa sauti hiyo si wa kiume. Ngozi anaendana na kiwango cha elimu na urazini wa mhusika. Anakwepa sanaa ya kipropaganda. Inapotokea hivyo, mhusika huwa anamtazamisha msomaji aione jamii kupitia katika mfumo dume. Jamii ionwe kama anavyoiona anayeongea. Kwa mujibu wa nadharia hii, kilicho muhimu ni pamoja na yule asemaye, kile kisemwacho, na namna kinavyosemwa. Kile kisemwacho kinaweza kutupatia maana ya ndani ya yule asemaye. Kwa mfano, Madahiro anarudia usemi wa mkewe, Mama Tama (Mauja) anasema: “Jamani nilikuwa bado ninaichoma... Uwongo mtupu...” (uk.11). Kwa kuyarudia maneno yaliyosemwa na mkewe, Madahiro anatutazamisha wasomaji sio tu tuone kebehi, bali zaidi tuone dhamira ya ndani aliyonayo msemaji. Maneno yaliyofuata: “...uwongo mtupu...” ni maneno yaliyonyuma ya sauti hiyo ya kebehi. Madahiro anatufanya tuisikie sauti ya Mauja kupitia kwa jinsi anavyoiona na kuihukumu yeye. Anatutazamisha wasomaji au wasikilizaji tuione dharau, na kebehi. Hii ni namna moja ya kumtazamisha msomaji au msikilizaji wa kazi ya sanaa. 78 Kwahiyo, kumtazamisha mtu ni kumfanya atazame kama ambavyo anatakiwa na mtu mwingine, sio kama ambavyo anataka yeye; ni kumfanya aone kupitia kwa mwonaji mwingine, sio kama anavyotaka kuona yeye. Katika kukabiliana na kuona au kutazamisha huku, mwandishi ametupatia wahusika katika makundi yanayo”tazama” kwa namna mbili tofauti kutokana na jinsi sauti zao zilivyo na uwakilishi tafauti. Wahusika wanaume amewagawa katika uwakilishi wa sauti mbili. Kwanza, ni wale wanaume ambao wamepewa sauti kuwakilisha utetezi wa wanawake. Wanaume hawa wanakosoa tabia za wanaume wenzao kuhusiana na matendo na uhusiano wao na wanawake. Kwa mfano, Kajela, Bongo, Nzole na Wambali, sauti zao zinaeleza msimamo huo. Tangu mwanzo mhusika Kajela anasema: “Lakini Madahiro, hivi wewe husikii inasemwa sana siku hizi kwamba kuoa wake wengi kunakufanya wewe kuwa 'Bwana' wao?” (uk.3). Hapa sauti ya Kajela inajitahidi kumfanya Madahiro aende na wakati. Inataka Madahiro abadilike, na aache tabia ya kutumikisha na kunyanyasa wake zake. Sauti kama hii tunaisikia pia kwa Nzole akitaka mabadiliko: “...Hawa wakeze wamekwisha tambua kuwa walikuwa wanaonewa, na hakuna apendae kuonewa...na Bwana Madahiro kama wanaume tulivyo, au binadamu wote kwa ujumla, inatuwia vigumu kubadili mienendo kubadili mienendo, tabia au fikra zetu zilizokuwa zikitawala mawazo yetu kwa miaka mingi kwa mara moja” (uk.32). Nzole sawa na Kajela wanawakilisha sauti ambazo zina nia ya kutaka mabadiliko. Hata hivyo, ugumu wa kubadilika unaoneshwa wazi na kauli ya Nzole. Kauli hii ni sauti inayowakilisha wanajamii ambao, wanatambua tatizo lakini wanashindwa kupiga hatua. Sauti inayoonesha ujasiri kwa kuchukua hatua tunaisikia kupitia kwa Wambali. Yeye anasema 79 wazi: “Mimi nashindwa kukubaliana nanyi jama ... kuna wanaume wengi wazururaji tu, wavivu kupindukia, na wazembe kushinda wanawake maradufu. Hiyo mwanamke asipobeba gogo, sio kwamba usawa wake kati yake na mwanaume umetoweka...” (uk 34). Katika kuchambua sauti hii, tunaona kuwa lile alisemalo Wambali ni sauti ya utetezi, inayoangalia mambo kiuyakinifu. Sauti ya Wambali ni kama inawaeleza wale wote wenye msimamo pingamizi: “nashindwa kukubaliana nanyi...”. Ni sauti inayowaeleza na wale wengine kuwa ugumu wa kubadilika hauna budi kuyeyuka. Sauti ya Wambali inajiweka katika umbo la mtu aliye kwenye tatizo haswa. Yaye mwenyewe anatambua tatizo, na zaidi ya hapo, anatambua kuwa yeye pia ni sehemu ya tatizo hilo na sasa yeye anapiga hatua: WAMBALI: “...hivyo tuukubali ukweli kwamba sisi wanaume, tunawaonea wanawake...Ndiyo. Au niseme tunawanyima haki zao, na hatuwapi nafsi hata kidogo ya kuonyesha uwezo wao, hivyo tunawagandamiza...” (uk 35). Utambuzi huu ni wa msingi katika mchakato wa kutaka mabadiliko ya kweli. Mabadiliko ya kweli huanza kwa mtu mwenyewe anayetaka kuona mabadiliko. Na hivi ndivyo Wambali na sauti anazoziwakilisha wanavyoona. Sauti hizi ni tofauti na sauti za Madahiro, Manila, au Tuli. Wanaume kama hawa wanautazama ukombozi wa mwanamke kama tangazo la vita dhidi yao na wako tayari kupambana ili kuzuia mabadiliko. Tukimwachilia mbali Madahiro ambaye tumekwisha kuona msimamo wake, sauti za Manila na Tuli ni sauti za jamii inayoshikilia hali ya kutokubadilika. Tuli, akipingana na Wambali na Nzole anasema: “Bwana Nzole, acha habari za usawa kati ya mume na mke. Hivi wewe hujasikia kuwa imethibitishwa na wataalamu kuwa Ubongo wa 80 mwanaume ni mzito kupita wa mwanamke. Ndio maana akili zao ndogo...” (uk.35). Sauti kama hii inasikika tena kutoka kwa Manila: Bwana Nzole, acha habari za usawa kati ya mwanaume na mwanamke. Haiwezekani hata kidogo. Tazama Bwana, Mwenyezi Mungu mwenyewe amewaumba watu tofauti tofauti...Mama ameumbwa ili alee watoto na kufanya kazi za nyumbani...” (uk.35). Katika jamii ipo mihimili inayoshikilia mila na kuithibitisha. Mhimili mmojawapo ni dini. Hapa Manila anauwakilisha mhimili huu na kuutumia ili kuthibitisha imani potofu kuhusu mwanamke. Sauti za wanaume hawa ni viwakilishi vya mfumo unaozuia mabadiliko. Mabadiliko yanayolenga kuleta usawa kati ya wanaume na wanawake katika jamii. Baada ya kuzisikia sauti tofauti za wanaume, na za wanawake kama tulivyoona hapo kabla, sasa tugeukie kuangalia uhusiano kati ya lugha ya wahusika – na hasa uteuzi wao wa vitenzi vya kauli ya utenda na utendwa, na dhamira mbalimbali za tamthilia hii, na jinsi vipengele hivi vinavyohusiana na ujenzi wa maonesho au muundo wa tamthilia. Suala hili litatusaidia kujua uhusiano uliopo miongoni mwa malengo matatu ambayo tumekuwa tukiyajadili. Hoja tunayoiangalia ni kuona ikiwa tunaweza kuwa na ushikamano maalumu wa kimaudhui ambao unaweza kufuatwa katika uchanganuzi wa tamthilia kama hizi kwa kutumia mikabala miwili ya uchambuzi. 4.3.1. Ushikamano wa Vijenzi vya Tamthilia Kimaudhui Ushikamno wa vijenzi kimaudhui, ni mbinu ya uhakiki ambapo dhamira inachambuliwa kutokana na sauti zinazowakilishwa na wahusika; na msuko wa maonesho na sehemu zake. Tangu mwanzo katika sura hii, tumeona kuwa sauti za wahusika – na hapa tunazingatia sauti 81 za utenda na utendwa tu, zimeshikamana katika kujenga dhamira inayotarajiwa na mwandishi. Katika kuchambua kauli hii, tunawaangalia wanaume na wanawake na jinsi mwenendo wa utolewaji wa kauli za utenda na utendwa unavyokuwa. Mwendo wa utolewaji wa kauli hizi katika dialojia za wahusika unadokeza ujenzi wa dhamira kuu. Tamthilia hii ina dhamira kadhaa ambazo wahusika wanaziwasilisha kwa wasomaji au wasikilizaji. Mbinu ya kujulikana kwa dhamira hizi ndiyo tunaijadili hapa kupitia katika dhana ya ushikamano wa vijenzi kimaudhui. Ziko dhamira kuu na dhamira nyingine ndogo ndogo. Mwendo wa ujenzi wa dhamira hizo unaonesha ushikamano unaotokeza muunganiko wa kitu kizima. Tuangalie modeli ya ujenzi wa mwendo wa kauli ya utenda kutoka kwa wahusika wa kiume na wa kike katika kujenga dhamira kuu ambayo ni ukombozi wa mwanamke. 82 ONYESHO LA KWANZA ONYESHO LA PILI ONYESHO LA TATU SEHEMU YA KWANZA SEHEMU YA PILI 20 15 10 05 00 Kauli ya utenda ya mwanaume inapokutana na ya mwanamke, inatokeza mabadiliko, na hapo ndipo uhalisia wa dhamira ya ukombozi unapoanzia. Ufunguo: Hali ya kauli ua utenda (mwanamke) Hali ya kauli ya utenda (mwanaume) Modeli ya ujenzi wa mwendo wa kauli ya utenda Kwa mujibu wa modeli hii hapa juu, katika Onesho la kwanza kauli ya utenda haisikiki sana kutoka kwa wahusika wanawake. Kauli ya utenda inasikika zaidi kutoka kwa wahusika wa kiume na hasa mhusika mkuu Madahiro. Hata hivyo, kadri ya ujenzi wa maonesho na sehemu zake unavyozidi kusogeza mbele matukio, kauli ya utenda inashuka kwa mhusika wa kiume na kupanda kwa mhusika wa kike, (Tazama, mwendo katika Onyesho la pili). Katika onesho la pili, kuna mabadiliko ya kufikirisha katika msuko wa matukio. Kauli ya utenda inashuka Ж 83 kwa mhusika wa kiume na imepanda kwa mhusika wa kike. Hali hii inapatikana katika sehemu ya kwanza ambapo hasa tunawasikia wahusika wa kike tu wakiongea mambo mbalimbali na wamekaa katika mahali pa kuonekana. Sehemu hii inakuwa ni kama matayarisho, ueleweshaji, na uwezeshaji kifikra kwa wanawake-urazini. Katika sehemu ya pili kauli ya utenda kwa mwanaume inajitahidi kurudishwa; na kwa mwanamke kuna hali ya uwiano, hii inaendana na kutokuwa na uelewa wa kutosha wa harakati za ukombozi na maana yake kwa jamii nzima. Kwa ujumla kauli za utenda na utendwa zinapohusishwa na dhamira ya ukombozi wa mwanamke kwa upande mmoja na wahusika wanaozitoa na utokeaji wake katika maonesho, kwa upande mwingine, tunapata ushikamano kimaudhui. Katika ushikamano huu inaonesha kuwa kilele cha dhamira kusudiwa kinatokea pale kauli ya utenda ya kiume inapogongana na kauli ya utenda ya kike. Modeli inaonyesha kuwa ikiwa jinsia mbili zina mawazo yanayotofautiana kimsingi, basi itafikia wakati mawazo hayo yatagongana, na hili litakapotokea hapo ndipo kutakuwa na kilele cha kusudio la mwandishi katika dhamira kuu aliyopanga kuielezea. Katika modeli yetu, mgongano huu unatokea pale palipo na alama hii “ Ж”, alama inayoonesha kupanda kwa matumizi ya utenda kwa mwanamke (na hivyo kuashiria kutokutumia sana utendwa), na kushuka kwa kauli ya utenda kwa mwanaume (na hivyo kuashiria mwanzo wa kukoma kutumia utenda katika uhusiano wake na mwanamke). Jambo hili linapotokea tunaweza kusema kuwa dhamira ya ukombozi imeanza kutekelezwa. Dhamira hii inaweza kuangalia pia kutumia jedwali katika jedwali lifuatalo, (taz. Jedwali na. 84 5), dhamira ya ukombozi inajieleza kupitia katika sauti mbalimbali za utenda na utendwa kama hivi: Dhamira Vitenzi vinavyoashiria dhamira hizo Maonesho/Sehemu Wahusika wawakilishi wa dhamira hizo 1).Ukombozi wa mwanamke ... Unatuonea tu kwa kuwa sisi wanawake (S.260)*. Hebu pigana na hao wanaume wenzio…(S.261 )* Onyesho la kwanza Mlahaka ... Kwani hizo pesa za mahari ulizotoa ndio nini( S.310)*? Onyesho la pili : sehemu ya kwanza Mauja … Fedha za mahari ni zawadi tu, siyo kama vile ununuavyo kitu dukani (S.320)*. Onyesho la pili: sehemu ya kwanza Mauja …Unafikiri nani atakaa tena aonewe(S.1068)*? onyesho la tatu Nasaa …wanawake wanaanza kutambua kuwa wanaonewa, na kudhulumiwa (S.1153)* onyesho la tatu Nzole …kutambua hali hiyo na kudai UKOMBOZI.(S.1283)* onyesho la tatu Nzole … Hawarudi nakwambia WAMEJIKOMBOA (S.1300)*. onyesho la tatu Nzole Jedwali Na. 5. Dhamira ya Ukombozi wa Mwanamke na vijenzi kutoka katika utendwa na utenda Kutokana na data yetu tunaona kuwa vitendo anavyofanyiwa mwanamke katika onyesho la kwanza, na kumfanya ajisikie anakandamizwa, ananyanyaswa, anaonewa, na anadharauliwa vinapata mwangwi wake hasa katika onyesho la tatu ambapo sauti ya kiume inayotaka mabadiliko inavisemea (Sauti ya Nzole katika onesho la tatu). Vitendo hivi kwa ujumla wake 85 vinafanyika hasa katika onyesho la kwanza. Hapo ndipo tunaona uhusiano wa mwanamke anajipanga kuviondosha katika onyesho la pili, na hatua ya kuviondosha inafanyika katika onyesho la tatu. Mwanamke katika hayo maonesho mawili ya mwanzoni, hasikiki sana akitumia utenda bali utendwa. Suala la ukombozi wa mwanamke linalojadiliwa hapa kupitia uwezo wake wa kupata kauli ya utenda, linajichomoza kutokana na dhamira nyingine muhimu inayoongelewa katika tamthilia hii. Hii ni dhamira inayozungumzia suala la ndoa. Ndoa inaangaliwa kama taasisi inayosimamiwa na mila, huku zikijadiliwa pia dhana za mitala na ukewenza. Huku wahusika wakipewa kauli mbalimbali. Utenda na utendwa unaojitokeza hapa unahusu zaidi dhana ya kuoa na kuolewa. Kuhusu ukewenza–kipengele hiki kimejadiliwa kwa kuwaonesha wahusika wanawake na wanaume vilevile; japo kwa kiasi kikubwa inawahusu wanawake. Mwandishi anayaonesha maisha ya ukewenza kama yanavyojitokeza katika maisha halisi ya wanawake wakiwa ni wake wa mtu mmoja. Kwa mfano, tunamwona Madahiro na rafiki zake wakiongelea kuhusu kuongeza idadi ya wake; huku wakeze Madahiro wakilalamikia tabia ya mume wao ya kuoa wake wapya kila kukicha. Sauti inayowakilisha wanawake, ingawa inatolewa na mwanaume, inapinga suala hili ingawa bila ya mafanikio makubwa. Kauli zinazotolewa zinajitokeza kama ifuatvyo: 86 2).Utamaduni katika ndoa, Kuoa (S.93)*; Kuoa (S.296) *, Kuoa (S.415)* Kuoa (S.418)*, Kuoa (S.420)*, Kuoa (S.422)* kuolewa (S.1086)*, kutoolewa (S.1086)* waolewao (S.354 )* onyesho la kwanza, la Pili, na la tatu Madahiro Nasaa Manila Ndoa za mitala, na Nenda ukaoe hata wanawake kumi (S.277)*. Nitaoa mke mwingine (S.275)*, Nioe mke mwingine (S.44)*, Kuoa mke mwingine (S.125)*, Umeoa mke mwingine (S.358)* … Bwana gani huyu tuliyenaye Anamfukuza mtu, kama mbwa asiyetakiwa! (778)* … Na kuoa wake wengi wengi na wengine kuwafukuza ( 821)* onyesho la kwanza, la pili, na la tatu Mlahaka Madahiro Madahiro Deka Nasaa Ukewenza … Huo ni wivu tu unaomsumbua kwa kuwa umeoa mke mwingine… (358)*. … Maana anaturingia (S.490)*. … Hamwishi kuniteta! (S.494)* … Nikijikalia kimya, ohoo anaringa! (S.498)* … Tuache kusema kama unaringa (S.502)*? … Hata kama ninawaringia wewe kinakuuma nini hasa (S.503)*? … Leo hii nataka anieleze kinachomkereketa (S.510)* … Babu usiniteme au unataka mengine tena (S.520)*. … Kama ulikuwa na chuki na mama yake, siyo kuwafanyia watoto (S.762 )*. Onyesho la pili:sehemu ya kwanza Onyesho la pili, sehemu ya pili Onyesho la pili, sehemu ya pili Onyesho la tatu Manila Mlahaka Deka Deka Mlahaka Deka Deka Mlahaka Deka Jedwali Na. 6. Dhamira ya Ndoa na sura zake katika utamaduni Kama tulivyoonesha mahali pengine (taz. 4.1.1.2), kauli za kuoa (kuolewa) na kupenda (kupendwa) zingaliwekwa katika hali ya kutendana. Ingawa hali hii ndivyo inayotokea katika hali halisi, mila inayoichonga lugha haikubaliani na hali hii. Mwandishi, ambaye ni zao la 87 jamii yenye mila hii, naye anafuta kaida hii hata pale ambapo angelipenda kuipiga vita na kuikomesha. Suala hili la mila kuiumba lugha haina budi kuangaliwa katika mukadha mpana wa utamaduni. Utamaduni unawaweka wanawake katika matumizi ya lugha kama jamii inavyotaka. Kwa mfano tunawasikia wanawake katika maongezi yao wakisema: MLAHAKA: “Kha! Mwenzetu ndiyo anajua kupendeka hasa. Ameolewa juzi juzi tu, jana tena amenunuliwa nguo mpya!” (uk.15). Mahusiano ya wake wawili au watatu wa mume mmoja yanaleta hali ya wivu na kukwaruzana kusiko kwa lazima kutokana na kuoneana kijicho. Hata katika hali hii, bado lugha wanayopewa wahusika inaakisi mfumo unaotawala maisha ya kila siku ya jamii. Mfumo ambao unambana mwanamke atumie utendwa na sio utenda. Wahusika wanawake wanapewa lugha inayotokana na utamaduni na mfumo uliowazunguka. Wanalazimishwa na utamaduni wa lugha kusema “nimeolewa”, “nimetongozwa”, “nimetolewa mahari”, “nimeposwa”, “nimechumbiwa” na kadhalika. Katika mfumo huu, inaonekana kuwa ni kitu cha kawaida wanawake kutumia utendwa huo. Jamii inakubaliana na mfumo huo, na mwandishi hawezi kwenda nje yake na kukiuka kawaida. Kwa mfano, katika lugha ya Kiingereza, kutokana na utamaduni wao, mwanamke hutumia utenda: “I will marry him” (nitamuoa). Na mwanaume, akiwaeleza wenzake kuhusu harusi yake na mchumba wake wa kike, huweza kusema: “I am getting married tomorrow” (Nitaolewa kesho). Jamii ya Wanalugha hii duniani inakubaliana na utamaduni unaobebwa na lugha, na ambao unajinasua katika mfumo dume kwa maana hii. Hali hii, ni tofauti na lugha katika ulimwengu wa “Machozi ya Mwanamke.” 88 Katika jamii iliyoibua tamthilia ya Machozi ya Mwanamke – jamii ya Watanzania, lugha ambayo ni kiwakilishi cha mfumo, ni ile ya wanaume kuwa watenda na wanawake watendwa. Katika uhakiki na mjadala wa sura hii, lugha hii ya kuwa “watenda” na sio “watendwa” tunaiangalia kupitia katika kauli ya utenda na utendwa. Hakuna namna inayompa uhiari mwanamke kutoa kauli ya utenda katika masuala ya ngono. Kwa upande mwingine, wanaume nao wanalazimishwa na utamaduni wa lugha ya Kiswahili, kutumia kauli ya utenda tu (ukiwaondoa wanaume mashoga) katika kuelezea matendo ya kingono. Kwa mfano, wanaume hawa huruhusiwa kusema “nimeoa,” “nimetongoza,” “nimetoa mahari,” “nimeposa,” na “nimechumbia” na kadhalika. Hakuna namna inayomruhusu mwanaume kutumia utendwa katika kueleza mahusiano hayo. Matumizi haya ya lugha yanalazimishwa na utamaduni zaidi kuliko mfumo wa lugha ulivyo. Jambo hili linatuonyesha kuwa lugha kama chombo cha mawasiliano inaweza kuwa na uhuru lakini hakuna uhuru katika utamaduni; na kwakuwa utamaduni ndio unaoongoza lugha, mabadiliko yoyote yale kuhusu lugha hayana budi kuanzia katika utamaduni. Ni mfumo wa utamaduni kama huu, ndio unaoangalia kazi na kuzigawa kijinsia. Katika mfumo huu, kazi za nyumbani zinajulikana kama kazi za mwanamke. Katika Machozi ya Mwanamke, suala la kazi na uhusiano wake na jinsia limejadiliwa kuonesha kuwa linaongeza mizigo kwa mwanamke. Katika maonyesho tunasikia sauti mbalimbali zikiongea kama ionyeshavyo katika jedwali la 7 hapa chini: 3). Kazi na mgawanyo wake ... Ninapika (S. 57). ... Jamani bado tu hayo mahindi tuyapete(S.476 )? Onyesho la kwanza Onyesho la pili Mauja Mauja 89 …kufanya kazi za nyumbani (S.1191) …amefanya nao karibuni kazi zote (S.1178) …kazi hizi za tumbaku mnafanya wote (S.1171) kuna kazi za kiume na kazi za kike (1263) onyesho la tatu onyesho la tatu onyesho la tatu onyesho la tatu Manila Nzole Wambali Wambali Jedwali la 7. Kazi kama suala la kijinsia Katika kulijadili suala la kazi kama suala la kijinsia, sauti mbalimbali zinasikika. Sauti zinazowakilisha jamii na utamaduni wake, zinashikilia kuwa kazi za nyumbani hufanywa, na hazina budi zifanywe na ama mwanamke au ikiwa ni mtoto, basi ni mtoto wa kike. Kwa mfano, tunaisikia sauti ya Madahiro ikisema wazi: “Mtoto wa kike huwezi kujikaza... mtoto asiyeweza kuwasaidia wazazi wake?” (uk. 1) “....Mkeo lazima akusaidie kazi...” “Sasa unafikiri asipofanya hivyo tutakula nini? Mimi ninataka kuoa mke mwingine ili waweze kunisaidia kazi, maana hizi kazi za matumbaku ni ngumu ati!” (uk.4). “Eee Mama Tama ... Hivi chakula bado tu? Ah! Fanya upesi chakula kinapikwa mwezi mzima? Na ukimaliza kupika, nifulie zile nguo zangu nilizovaa jana, kisha ukaazime pasi uzinyooshe...”(uk. 5-6). Sauti hii inatolewa na mwanaume kuwakilisha mawazo ya mfumo unaotawala. Sauti kama hii inapata mwangwi wake kupitia katika mdomo wa mhusika mwanamke akisema: “Unatuonea tu kwa kuwa sisi wanawake.” (uk 8). Sauti hizi mbili zinakubaliana ingawa kwa viwango tofauti. Mwanamke anaposema hivi, anakuwa ni mdomo tu wa kupitishia mawazo ya kiume hata kama yeye mwenyewe hakubaliani nayo; wakati mwanaume anaposema anakuwa ni sauti inayokubaliana na kile anachokisema. Sauti hizi mbili zimo katika mjadala na sauti nyingine zinazoonekana zinapingana na utamaduni huu. Mhusika Nasaa anasema kwa kukataa hali hii: “Mradi tumeitwa wanawake ndiyo hata 90 tunapigwa hamna hata kujitetea!” “...bora kujitetea...”.“…mtu hupumziki hata dakika moja. Utoke shamba, uvunje vunje kuni za kupikia, haya uende kisimani, ukirudi unapitiliza moja kwa moja jikoni. Yeye wakati anavuta tu mtemba, akihimiza, chakula bado tu?” (uk.24). Mhusika Wambali, ingawa ni mwanaume, anaikataa sauti inayomhusisha na jinsi yake, na anashikilia sauti ya mabadiliko. Anasema: “Ndiyo, au niseme tunawanyima haki zao, na hatuwapi nafasi hata kidogo ya kuonyesha uwezo wao hivyo tunawakandamiza…” (uk.35). Mbali na wazo la kufanya kazi, Mhusika mwingine ambaye pia ni mwanaume, sauti anayoitoa inapingana na mfumo uliopo ikidai mabadiliko. Sauti ya Nzole inasikika wazi wazi kuhusu kazi na ndoa: “Utaona Bwana analewa mpaka pesa zote zinakwisha. Au ataoa mke mwingine akiwasahau kabisa watoto na wakeze ambao amefanya nao karibuni kazi zote...” (uk 35). Kutofautiana kwa sauti hizi ni kiwakilishi kinachoonesha hali halisi katika jamii kuhusiana na suala na maana ya ukombozi kwa mwanamke. Sehemu nyingine ya jamii inajadili nafasi ya mume katika nyumba na kazi anazofanya. Kwa mfano, suala hili la mume kutumia pesa zote ambazo kwa asilimia kubwa huko vijijini, zinazalishwa zaidi na mwanamke linajadiliwa katika Machozi ya Mwanamke, kupitia katika taswira ya ulevi. Taswira hii inawakilisha dhamira nyingine ndogo ya mwandishi ambayo ni ulevi. Dhamira ya ulevi inaangaliwa tofauti na pande mbili. Upande wa wale wanywaji wanaizungumza kama suala la fahari. Madahiro ambaye ni sauti ya mlevi anasema kwa ufahari kabisa: “Leo [pesa] nimezipata. Nikisha kula tu, niende Igoko nikaonje. Kesho kukicha niende mjini Isevya. Pombe ya Isevya safi kabisa...” kwa mtu kama Madahiro haoni 91 aibu kulinganisha unywaji wa pombe, na ama kununua baiskeli mpya au kuoa mke mwingine. Katika maisha yake ya kupokea pesa anafikiria hayo mambo matatu: kulewa, kununua baisikeli au kuoa. Na katika hayo, suala la kunywa ndilo linapata kipaumbele. Mawazo haya Madahiro anayapata katika onesho la kwanza. Tunapoanza onyesho la pili sehemu ya kwanza, tunaambiwa: (“...Pazia linapofunguliwa tunamwona Madahiro akiwa amelewa chakari akiwa na bakuli la pombe akirandaranda...” uk. 9), na mwishoni mwa sehemu hii ya kwanza tunaambiwa. (“... anakohoa na ghafla anaanza kutapika sana” uk. 14). Katika maisha Madahiro mwenyewe anasema: “Oh maisha matamu sana haya. Ninakula ninashiba na pombe ninakunywa! Sitaki shida na mtu mimi...wake ninao watatu...” Ingawa hii ni sauti ya kiwakilishi cha ulevi na kuoa wake wengi, kuna sauti nyingine inapingana na hali hii. Mlahaka anasema: “Na fedha zote anazimaliza yeye kwenye ulevi.” Nasaa anaongezea: “Na kuoa wake wengi na wengine kuwafukuza...” (uk. 25). Sauti za wake wa Madahiro sawa na wake wengine katika jamii zinapinga vikali suala la kulewa chakari na hasa kulewa na mlevi akasahau hata familia yake. Sauti hizi zinatoa kauli ya utenda wakati zikikataa hali hii. Sauti ya ukanushi inaonesha wazi hali ya kukataa: “Hatukuteka!”... Baada ya sauti hii kauli ya utenda inafuata ikiwa wazi ikitoka kwa NASAA: “Unamwonea tu, leo zamu yako kututambua nasi...tumechoshwa na uonevu wa huyu Bwana wetu. Hivyo ndiyo maana tukaamua leo nasi kujitetea...” Sauti ya Nasaa ni kiwakilishi cha sauti inayodai haki na kuchukua uamuzi. Ni sauti inayotekeleza hatua za ukombozi kwa mapinduzi ya nguvu. Ni uamuzi wa watu waliokata tamaa ya kupata usawa kwa namna nyingine iwayo. Ni sauti inayotokana na kuchoshwa na kutukanwa, kupigwa na kusimangwa ambayo ni dhamira nyingine ndogo katika tamthilia hii. Wanawake hali wakitumia utendwa wanaanza kwa 92 kunung’unika kuwa wanapigwa, wanatukanwa, wanatapikiwa na kadhalika. Lakini katika hali ya kuchukua hatua, wanapata sauti ya utenda na kuanza kujihami kama ilivyooneshwa hapa juu. Zile sauti za “yalaa ananiuwa” (uk. 7) ambazo zinatolewa na mwanamke, zinabadilika katika onyesho la tatu na sasa zinatolewa na mwanaume: “Yalaa...Yalaa wananiua” (uk 27). Baada ya “kujikomboa” maneno yale yale sasa yanasemwa kwa sauti ya utenda: DEKA: “... Baba Tama amezidi mno kutupiga, kututukana, kutusimanga na kutunyanyasa...” (uk29). Yale maneno ya “kupigwa, kutukanwa, kunyanyaswa...” sasa yamebadilika kuingia katika utenda; na sababu ya kubadilika huku iko wazi. Sauti ya mwanamke inasema: “...sisi sio watumwa...” (uk 29). Sauti na mpangilio wake vimewekwa katika kiunzi mahususi kinachotokeza ukinzani hasa baada ya sauti ya utendwa inapobadilishana nafasi na ile ya utenda. Hiki ndicho kiunzi au modeli ambayo tunaiita ushikamano wa vijenzi kimaudhui. 4.4 Hitimisho Katika sura hii, mbali ya kuwasilisha data tulizozikusanya katika utafiti wetu, tumechambua data hizo na kujenga mjadala tukiegemeza hoja zetu katika nadharia ya naratolojia. Katika nadharia hii, wahusika katika kazi ya kifasihi wanaangalia sio tu kama wawakilishi wa watu katika jamii, bali hasa sauti zao zimechambuliwa kuwa zinaweza kuwakilisha nafsi mbalimbali. Hii ina maana kwamba, ingawa mhusika anaweza kuwa mmoja, uhusika wake unaweza kuangaliwa kwa namna mbalimbali kutokana na yale anayoyasema. Mhusika mmoja anaweza kuwa anaongea akiwa ni kiwakilishi cha zaidi ya mtu mmoja. Aidha, kupitia katika nadharia hii, mhusika haangaliwi uhusika wake kwa kuegemea kwenye 93 jinsia yake. Anaweza kuwa ni mhusika mwanamke kwa kuonekana, lakini mawazo na sauti yake ikawa ya kiume. Hali kadhalika, anaweza kuwa ni mhusika wa kiume lakini sauti na uhusika wake ukawa ni wa kuwawakilisha wanawake. Hali hii inatusaidia kuona yale ayasemayo mwandishi kwa kuangalia si maandishi, bali zaidi sauti ambazo ni zaidi ya kile kilichoandikwa. Kwa kuangalia sauti mbali na maandishi yanayowasilishwa na wahusika, tumeangalia kauli mbili ile ya utenda na ile ya utendwa. Sauti hizi mbili tumeziangalia kama zenye kujenga na kusimamia dhamira mbalimbali za mwandishi. Katika mjadala huu tumependekeza kiunzi cha uhakiki ambacho tumekiita ushikamano wa vijenzi kimaudhui. Vijenzi hivi ni zile sauti ambazo kwa kuziangalia katika ujumla wake, zinajenga ushikamano fulani ambao ukiufuatilia unaweza kuchora aina fulani ya ruwaza katika kutafiti na kugundua dhamira za kazi ya fasihi. 94 SURA YA TANO HITIMISHO NA MAPENDEKEZO 5.1 Utangulizi Dhamira ya ukombozi wa mwanamke imejadiliwa kwa namna mbalimbali na kwa kutumia mikabala mbalimbali. Katika tasnifu hii, tumeijadili dhamira hii kwa kutumia mkabala wa kielimu mtindo na nadharia ya naratolojia. Malengo ya tasnifu hii, pamoja na maswali tuliyojiuliza katika sura ya kwanza yamejadiliwa hasa katika sura ya nne. Katika sura hii ya tano, tunahitimisha mjadala wetu kwanza, kwa kuonesha kwa ujumla yale yaliyojadiliwa katika sura ya mjadala. Kisha, sura hii itahusu hitimisho na hasa ambayo yanaweza kufanyiwa utafiti mwingine kwa kina zaidi na wanazuoni wengine, ama kwa hatua ya masomo ya umahiri au masomo ya uzamivu, au hata kwa kuandika tu makala inayotokana na utafiti. 5.2 Hitimisho Katika kazi hii, tumetumia mkabala wa kielimu mtindo kuzichunguza kauli za utenda na utendwa katika kuchambua na kuhakiki dhamira za Machozi ya Mwanamke. Ndani ya kazi hii tumefafanua elimu mtindo kumaanisha suala la uchaguzi (au uteuzi) na wakati huo huo, ikimaanisha mtindo ni utofauti. Kauli za utenda na utendwa zimetumiwa na mwandishi ama kwa kuchaguliwa huku akiwa amedhamiria kufanya hivyo, au pengine kwa kutokudhamiria. Ikiwa tutamchukua mwandishi kama zao la jamii, inawezekana kusema, sio lazima uchaguzi wake uwe wa kiurazini. Inawezekana kuwa uchaguzi wake ni kiakisi cha mfumo na utamaduni wa jamii iliyomkuza na alimokulia mwandishi. Hata hivyo, inawezekana kuwa aliteua na kisha kupambanisha kauli za utenda na utendwa kwa kudhamiria ili wahusika wake wapate kuyasema hayo waliyoyasema kuhusiana na dhamira ya ukombozi. 95 Kwa vyovyote vile, lugha aliyotumia mwandishi inaweza kuangaliwa kielimu mtindo kuwa ni uchaguzi. Kwamba, mwandishi amechagua kuwapa wahusika wake lugha fulani ambayo ni muafaka kwa matendo na uhusika wao. Aidha, kwa kutumia nadharia ya naratolojia tumeangalia uwasilishi wa dhamira mbalimbali za mwandishi kama kazi ya usimulizi. Tumewajadili wahusika kama wenye kusimulia jambo linalotokea katika jamii. Kwa njia hii tumezijadili sauti za wahusika na sio wahusika wenyewe. Sauti zinazojitokeza katika tamthiliya hii, zimeweza kubainika kwa kutumia nadharia ya naratolojia. Katika nadharia hii, mwandishi anamtumia wakala ili amsemee mawazo yake. Matumizi ya nafsi ya kwanza yanaonesha kuwa anayesimulia ni mwandishi. Matumizi haya yako karibu na nafsi ya mwandishi na jambo hili linatufanya tumwone mwandishi. Inapotokea mwandishi akatumia nafsi ya pili, anatudokezea kuwa sasa ameacha kuongea kama yeye, na amemtafuta wakala wake. Wakala anaweza kueleza yale aliyotumwa na ujumbe ukaishia hapo. Hata hivyo, hazuiwi na taratibu za naratolojia kuongeza yale ya kwake kama wakala. Inapotokea hivyo, sauti zinakuwa zenye kupishana na kupandana. Uchambuzi wa aina hii pia unatusaidia kuona nje ya maandishi ya kawaida na kuangalia lugha na mtoaji au msemaji. Kwa upande mwingine, matumizi ya nafsi ya tatu yanaonesha kuwa anayesimulia sio mwandishi wala wakala wake; bali ni mhusika au mtendaji tofauti. Mara nyingi, mawazo yasiyo na taasubi ni yale yanayowasilishwa kwa kutumia nafsi ya tatu kwa kuwa nafsi hii inakuwa haijafungamana na nafsi ya mwandishi. Sauti hizi za wahusika akiwa kama wakala au vinginevyo, hazimaanishi kuwa anayesema ni mwandishi, Ni sauti ambazo wahusika na 96 wakala wanaoishi kwenye akili ya mwandishi huitoa ili kumwakilisha mwandishi. Aidha, sauti ya wahusika au mhusika maalumu imechukuliwa kuwa ni sauti inayowakilisha kundi au makundi fulani katika jamii. Mhusika anaweza kuwa ni mwanamke, lakini sauti yake tunayoisikia ikawa inawakilisha mawazo na tabia za wanaume. Hali kadhalika, mhusika anaweza kuwa ni wa kiume, lakini sauti anayoitoa hadhira ya wasomaji ikisikia kuwa ni sauti ya wanawake. Uchambuzi kwa kutumia nadharia ya naratolojia umejengwa kutoka katika mapitio ya marejeo mbalimbali yaliyorejelewa katika sura ya pili. Katika sura ya tatu, kazi hii imehusika zaidi na mbinu za utafiti ikiwa ni pamoja na njia za ukusanyaji data, data zilizotumiwa, mahali zilipopatikana data hizo, na mbinu za uchambuzi wa data husika. Data tuliyoitumia ni maneno yanayounda kauli za utenda na utendwa kutoka katika tamthilia ya Machozi ya Mwanamke. Ni kutokana na ukusanyaji na mpangilio wa kauli hizo ndipo tukaingia katika sura ya nne na kuwasilisha data. Ni katika sura ya nne hasa, ambapo tunajenga mjadala ambao ni nguzo ya tasnifu hii. Huu ni mjadala ambao kwa kutumie elimu mtindo, unalenga kujibu maswali ya jumla yaliyoulizwa katika utafiti huu, na hasa majibu ya maswali matatu mahususi. Ni sura iliyowasilisha matokeo, ikayafafanua, na kuyachambua ikijenga mjadala kuhusu matumizi ya utendwa kama suala la mtindo na utofauti wake na ujitokezaji wa utendwa miongoni mwa watumiaji wa lugha katika kazi ya Machozi ya Mwanamke. Kwa kutumia elimu mtindo, imefahamika kuwa, matumizi ya kauli ya utendwa au utenda yana uhiari kisintaksia; kwamba, unaweza kuamua kulisema wazo lako ama kwa kutumia 97 kauli ya utendwa au ya utenda kuelezea maana ambayo inakusudiwa. Katika mjadala wetu kwa mfano, tumeona kuwa wanaume au wanawake wanaweza kutumia kauli za utendwa au utenda wakati wakiwa katika hali fulani na wanapotaka kueleza nia au hitaji fulani mahususi. Hata hivyo, tumeona kuwa sio miktadha yote huruhusu matumizi ya kauli moja na kuacha nyingine kwa uhuru. Yale matendo yasiyotoa uhuru kwa mwanamke au mwanaume kutumia kauli zote mbili (yaani utendwa wa ulazima) yametuwezesha hadhira kutambua nafasi ya utamaduni katika kuiumba na kuielekeza lugha. Hii inatufanya tuone jambo moja muhimu kwamba, kuna uhuru katika lugha lakini hakuna uhuru katika utamaduni. Na ili kupata uhuru wa kweli, jamii haina budi kuondokana na “utumwa” wa utamaduni, pale ambapo utamaduni husika unaonekana kuwa kandamizi. Mwandishi wa Machozi ya Mwanamke anajitahidi kutetea uhuru dhidi ya utamaduni kandamizi - hata kama ndio uliomkuza yeye kama mwandishi hata akafikia uwezo wa kuusemea na kuukemea. Ingawa mwandishi anatuingiza katika mjadala muhimu wa uhuru na maana ya ukombozi wa mwanamke, anatuacha tunajiuliza maana ya uhuru huo na njia za kuupigania. Tamthilia yake inaishia na maswali na mjadala ambao haujamalizika unaoendelezwa na wahusika. Suala hili linatuingiza katika dhana nyingine inayoelezwa na nadharia ya naratolojia, dhana ya utazamishwaji. Kutazamishwa ni kumfanya msomaji au mtazamaji wa kazi fulani ya sanaa alione jambo kama anavyoliona mhusika wa kazi ya fasihi. Mhusika huyu anapoangalia kama anayefanya kazi za kutazamisha hadhira yake anaitwa: mtazamishaji. Katika kutazamishwa huku, kuupata ukweli wa jambo hutegemea ushawishi wa mtazamishaji kwa upande mmoja; na uhalisia wa 98 taarifa zinazotolewa. Hii inatokana na matokeo kuwa, mhusika mtazamishaji huchuja taarifa au usimulizi akachagua ni lipi lisemwe katika hadhira na lisemwe au lifikishwe vipi/namna gani. Utazamishwaji uko wa aina mbili: kuna utazamishwaji wa nje na ule wa ndani. Utazamishwaji wa nje hufanywa na msimulizi pale anapotumia nafsi ya tatu kusimulia matini ya hadithi. Yeye anatutazamisha ili tuone yanayotendwa na wahusika watendaji katika hadithi lakini yeye sio sehemu ya hadithi au simulio Kwa upande mwingine, utazamishwaji wa ndani hufanywa na wahusika pale wanapotumia nafsi ya kwanza na ya pili katika kueleza maoni na mitazamo yao, hapa inaonesha mwandishi au wakala wake yuko karibu na simulio – yaani anakubaliana na yale yanayowasilishwa na mhusika aliyemwumba. Kutokana na utazamishwaji huu unaofanywa na wahusika, ndipo tunaziona sauti mbalimbali ambazo tumezijadili hapo kabla. Kwa mfano, mwandishi kwa upande mmoja anajaribu kupingana na mfumo wa kiukandamizaji uliopo katika jamii na anatoa sauti yake kupitia kwa mhusika. Kwa mfano, tunamwona Nzole akijaribu kueleza utaratibu wa kisheria ambao unaweza kutumika ili wanawake wapate haki zao. Kutokana na ukinzani katika jamii, tunamwona mwandishi akiushadidia ukandamizwaji unaofanywa dhidi ya wanawake kwa kupitia mhusika wake mkuu Madahiro. Mhusika huyu ni mtendaji katika simulio analolitoa mwandishi, ambaye tunaona matendo na msimamo wake; tunaona itikadi na imani yake kuhusu mila na utamaduni uliomlea. Hadi mwisho, tunamsikia akilalama kuwa jambo hili kamwe halitawezekana na wake zake watamrudia na yeye atabakia na ubwana, ilihali wake zake wataendelea kuwa watwana. Katika sura hii pia tumejaribu kubuni kile tulichokiita “ushikamano wa vijenzi vya tamthilia 99 kimaudhui” (Taz. 4.2.1). Hoja inayojengwa hapa ni kuwa katika kuchambua maudhui, mhakiki anaweza kuona kwa ujumla wake, vijenzi ambavyo vinaweza kufuatiliwa na kutokeza picha ya ushikamano. Vijenzi hivi ni yale maneno ambayo yanatamkwa na wahusika na yanaonekana kuwa ni muhimu katika kujenga dhamira fulani mahususi. Maneno hayo yanajenga ruwaza maalumu na pale kunapotokea kugongana kwa mawazo (kupitia katika maneno hayo), au kupishana, basi huo unachukuliwa kuwa mwanzo wa, au kiini cha dhamira fulani mahususi. Kwahiyo, hii inaweza kuwa ni njia mojawapo ya kutambua dhamira ya matini iwe ni andishi au simulizi. 5.3 Mapendekezo Utafiti huu ulitumia nadharia ya naratolojia kwa upande mmoja, na elimu mtindo kwa upande wa pili katika kujenga mjadala kuhusu dhamira za mwandishi na uhusiano wale na vipengele vya lugha ambavyo ni utenda na utendwa. Kazi ya mwandishi iliyoangaliwa ni moja tu, miongoni mwa kazi nyingi za fasihi ya Kiswahili. Litakuwa ni jambo la muhimu kitaaluma ikiwa watafiti wengine wataangalia ujitokezaji wa vipengele hivi katika kazi zaidi ya moja ili katika mjadala wa juu zaidi iweze kujulikana ikiwa kauli mbalimbali na ujitokezaji wake huwa na uhusiano wa moja kwa moja na dhamira au la. Aidha, katika kazi hii, tumependekeza kiunzi cha “ushikamano wa vijenzi vya tamthilia kimaudhui.” Pendekezo hili linaweza kuangaliwa katika utafiti mkubwa zaidi na kutupatia matokea ya kufikirisha kitaaluma. Ingalifaa kama kutafanyika utafiti linganifu wa kazi zaidi ya moja za utanzu ule ule, na mtafiti akaamua kuangalia ujitokezaji wa kauli ya utendwa katika kazi hizo; na kuweza kubainisha ikiwa matokea ya uhakiki wa dhamira yatakuwa yale 100 yale au la. Pengine, hata mchambuzi kukusanya kazi za tanzu mbalimbali za fasihi na akaangalia kipengele kimoja cha lugha, na uhusiano wake na dhamira; au ujumbe anaotaka kuutoa mwandishi wa fasihi kupitia katika kazi yake. Vile vile, uchunguzi wa utendwa na utenda umeleta changamoto za udadisi zaidi kitaaluma. Kuna nyanja ambazo bado zinaweza kufanyiwa kazi na matokeo yake kupimwa ili kujua kama yatakuwa ni yale yale au yanatofautiana. Kwa mfano, mchunguzi anaweza kutaka kujua ikiwa matumizi ya kauli za utenda na utendwa katika hadithi za magazetini yanauhusiano wowote na yale yasemwayo au na namna yanavyosemwa. 101 MAREJEO Abdulla, A (2005), The Bride Price: Dowry Abuse, Islam Online http://www.islamonline.net/servlet/Satellite?c=Article_C&pagename=Zone-EnglishFamily/FYELayout&cid=1157365818651 imesomwa Jumatano, 28 Agosti, 2005 Alfred, G. J, Brusaw, C. T, na Oliu, W. E (2006). Handbook of Technical Writing. http://www.books.google.co.tz imesomwa Jumatano, 20 Agosti, 2008 Bal, M (1985). Narratology: Introduction to the Theory of Narrative, (2ndedition), London: University of Torronto Press Bearth, T (2003), “Syntax”, in Derek, N and Gerard, P The Bantu Languages. Rout ledge London, pp 121-142 Brewer, P (h.t). On the origins of women's oppression Online article http://links.org.au/node/159 imesomwa Jumatano, 20 Agosti, 2008 Brockett, O (1964) The Theatre: An Introduction, United States of America: Holt, Rinehart, and Winston Inc Chambala, M (2005), The use of parallelism in Mariama’s Ba Scarlet Song, (Unpublished M.A. Dissertation), University of Dar es Salaam Crystal, D. na Davy, D (1969), Investigating English Style, London: Longmans Eagleton, T (1978), Criticism and Ideology, New York: Schocken Enkvist, N. E (1973), Linguistic Stylistics, Mouton: The Hague & Paris Erichsen, G (2008), Passive Voice, http://www.spanish.about.com imesomwa Alhamis, 11 Disemba, 2008 Habati, M. A (2005), “Brides pay price of being bought”? in The Independent, http://www.independent.co.ug/index.php/society/society/37-society/1067- brides-pay-price-of-being-bought, imesomwa Alhamis, 11 Disemba, 2008 102 Habwe, J. na Karanja, P (2004), Misingi ya Sarufi ya Kiswahili, Nairobi: Phonix Publishers Halliday, M.A.K. & Hasan, R (1976), Cohesion in English, London: Longman Hansard, M (1995), Active and Passive Voice, http://www.owl.english.purdue.edu imesomwa Jumatano, 20 Agosti, 2008 Jameson, F (1971), Marxism and Form: Twentieth-Century Dialectical Theories of Literature, Princeton: Princeton University Press, imesomwa Alhamis, 11 Disemba, 2008 Kabugi, C. M (1974), Jifunze Kiswahili, Singapore: McGraw-Hill For Eastern Publishers Limited Kahigi, K. K (1997), “Structural and Cohesion Dimensions of Style: A Consideration of some Swahili text in Maw (1974)”, Journal of Linguistics and Language in Education (New Series), Dar es Salaam: University of Dar es Salaam, Volume 3 Khamisi, A. M (1988), “Kitenzi msingi wa mundo”, Juzuu la Kiswahili. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Toleo la 55, Na.1 Kihore, Y. M., Massamba, D. P. B., na Hokororo, J.I (2001), Sarufi Maumbo ya Kiswahili Sanifu, Dar es Salaam: Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili Kolln, M (1994), Understanding English Grammar, (4 th Edition), New York: Mac Millan Publishing Company, http://www.grammar.ccc.commnet.edu imesomwa Jumatano, 20 Agosti, 2008 Lakoff, R (1975), Language and Women’s Place, New York: Herper and Row Lyimo, E. B (2004), Reitaration in Kiswahili Poetry, (Unpublished M.A. Dissertation), University of Dar es Salaam Martin, W (1986), Recent Theories of Narrative, Cornell University Press: United States of America 103 Massamba, D. P. B., Kihore, Y.M., Msanjila, Y.P (1999), Sarufi Miundo ya Kiswahili Sanifu, Dar es Salaam: Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili Maw, J (1974), Swahili Style, London: University of London School of Oriental and African Studies Mazrui, M (1983), “The Passive Transformations in Swahili”, Juzuu la Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Toleo la 55, Na.1 Mkude, J.D (2005), The Passive Construction in Swahili, Tokyo University of Foreign Studies: Research Institute for Languages and Cultures of Asia and Africa (ILCAA) Mohamed, A. M (1986), Sarufi Mpya New Kiswahili Grammar, Dar es Salaam: Press and Publicity Centre Mulokozi, A. M. K (1996), A Stylistic Comparison of Swahili Prose and Poetry: The case of Lexical Cohesion, (Unpublished M.A. Dissertation), University of Dar es Salaam Mutembei, A. K (1994), Phonological Aspects of Foreground in Kiswahili, (Unpublished M.A. Dissertation), University of Dar es Salaam Ngozi, I (1977), Machozi ya Mwanamke, Dar es Salaam: Tanzania Publishing House Picarazzi, T. L (2006), Italian Verbs for Dummies, United States of America: Wiley Publishing Inc. http://www. wiley. com imesomwa Jumatano, 20 Agosti, 2008 Ramadhani, D (2005), The use of metaphor in Mbogo’s Ngoma ya Ng’wanamalundi and Hussein’s Mashetani: A stylistic comparison. (Unpublished M.A. Dissertation), University of Dar es Salaam Russian Language Centre, (2008), Reflexive verbs, http://www.rlcentr.com imesomwa Ijumaa, 14th Novemba, 2008 104 Scholes, R. & Kellogg, R (1966), The Nature of Narrative, Oxford University Press: United States of America Senkoro, F.E.M.K (1987), Fasihi na Jamii (Toleo la 2), KAUTTU Ltd: Dar es Salaam Spivak, G (1990), The Post-Colonial Critic: Interviews, Strategies, Dialogues, Routledge: London Stein, G (2004), The complete idiot’s guide to French verbs, United States of America: Marie Batler Kight, http://www.books.google.co.tz imesomwa Jumatano, 20 Agosti, 2008 Talib, I.S (1995), Transitivity 1, http://www.courses.nus.edu imesomwa Jumatano, 20 Agosti, 2008 The Writing Center University of North Carolina at Chapel Hill, (1998), North American Academic Writing, http://www.unc.edu imesomwa Jumatano, 20 Agosti, 2008 The Writing Centre Princeton Writing Program, (1999), On UsingPassive Voice, http://www.princeton.edu imesomwa Jumatano, 20 Agosti, 2008 TUKI, (1981), Kamusi ya Kiswahili Sanifu, Oxford University Press: Nairobi Verhuist, H., Sanders, M., na Tingloo, A (2005), Advanced Writing in Germany: A Guide for Dutch Authors. http://www.books.google.co.tz imesomwa Ijumaa, 14 Novemba, 2008 Wamitila, K. W (2003), Kamusi ya Fasihi, Istilahi, na Nadharia, English Press: Nairobi Wamitila, K.W (2001), Uhakiki wa Fasihi, Misingi na Vipengele Vyake, Standard Textbooks Graphics and Publishing: Nairobi Williams, R (1977), Marxism and Literature, OUP: Oxford 105 Namba ya sentensi Sentensi zenye utendwa wa uhiari katika Machozi ya Mwanamke (Ngozi, 1977) Upekee Mada Mazingira 22 Atanunuliwa na bwana aliyemkawiza huko X 35 Siyo mapombe ya huku kwenu yanayowekwa sukari kidogo kabisa X 83 Maana unahimizwa sana juu ya jambo hili X 93 Hivi wewe husikii inasemwa sana siku hizi kwamba kuoa wake wengi kunawafanya wewe kuwa ‘Bwana’ wao X 105 Na usilogwe kutawaliwa na mkeo ujue umekwisha yakhe! X 115 Basi Bwana Kilakita, ameshindwa na mkewe hasa X 138 Nasema wale wanaoolewa na kukaa tu, mighairi ya kazi X 145 Lakini mke wa mwenetu Kisanko, amewekewa boi wa kufagia nyumba na kufua X 182 Fanya upesi chakula kinapikwa mwezi mzima X 198 Mwanamke gani huyu... akipewa ruhusa kwenda kwao basi ndiyo tena amepewa nafasi ya kwenda kwa hawara zake X X 307 Sitaki kutawaliwa na mke wangu mimiX 316 Umeolewa kwa fedha mama X 345 Au anataka usawa unaosemwa semwa kila mara maradioni X 354 Na kama ni zawadi kwa nini wapewe tu wanawake na sisi wasitupe au kwa kuwa wao ndio waolewao X X 390 Kila ukitumwa unaenda jumla! X 447 Usikae unanisumbua...nikae nakuita wee kama mtu aliyepungukiwa na akili X 482 Ameolewa juzijuzi tu, jana tena amenunuliwa nguo mpya! X X 508 Mimi leo nataka anieleze maana tangu nimeolewa humu, kila situ maneno hayaishi X 514 Si mwenzetu anapendwa na Bwana X 106 524 Haya makama ya vitenge niliyonunuliwa wewe ndiyo unafikiri nguo hizi X 528 Kila kitu akileta bwana, unafikishiwa wewe X 529 Akileta nyama unafikishiwa wewe X 531 Sasa tena wewe tu, ndiyo unakuwa unanunuliwa nguo mpya X 563 Mbona umeshindwa (kauli ya utendwa) X 577 Wagombane watu wengine mie tena ndio nirudiwe X 698 Akiambiwa jiunge na wenzio mara ooh! X 712 Mtoto aache kutumwa X 741 Mbona yeye hatujasikia hata siku moja akitumwa X 767 Hata mimi niliyeolewa hivi karibuni tu, ninaviona visa vyake X 772 Maana aliadhiriwa kupita mpaka tena X 774 Mimi alipokuwa akiondoka hali ana mtoto mchanga mgongoni, moyo wangu uliingiwa na uchungu sana, ingawa sijazaa.......... X 778 Anamfukuza mtu, kama mbwa asiyetakiwa! X 788 Mradi tumeitwa 'wanawake' ndiyo hata tunapigwa hamna hata kujitetea! X 798 Mpaka mtu unaghadhabishwa X 802 Nakupigwa hasa X 803 Mtu unatimbwa mpaka unakaribia kufaX 817 Tunakaa tukinukiwa na harufu mbaya ya matapishi ya pombe X 822 Mimi nilipokuwa nikiolewa, sikujua kwamba mwingine ndiyo kwanza ameachwa X X 825 Basi ndiyo tunawekwa humu ndani kama vimada X 950 Lazima itafutwe sheria X 988 Kwa ufupi Mzee Nyole ni kwamba tumechoshwa na uonevu wa huyu Bwana wetu X 1003 Tunaambiwa kila mara maradioni kuwa binadamu wote ni sawa, na kwa Watanzania kila mtu anastahili heshima X 107 1068 Unafikiri nani atakaa tena aonewe X 1071 Hawa wakeze wamekwisha tambua kuwa walikuwa wakionewa, na hakuna apendae kuonewa X 1079 Sisi leo tumefukuzwa, lakini mali aliyonayo huyu bwana tumeichuma wote X 1086 Hayo ya kuolewa au kutoolewa ni mengine tena X 1091 Itakapoondolewa, tutaona kama wanaume mtaendelea kuwagandamiza wanawake! X 1122 Hivyo basi ninyi akina mama mtaenda kulala kwa Balozi ndugu, Bongo Mwaikusa, na kesho wataitwa wazee na wazazi wenu wote X 1123 Vitu vilivyomo humu ndani vyote, pamoja na mashamba na kila mali iliyomo mtagawanyishwa kwani pia mmefanya kazi) X 1128 Usipokubali hapa, mambo haya yatafikishwa mahakamani X 1129 Na huko, haki itachunguzwa X 1145 Hivi ni nani kweli awezae kupokonywa wanae mwenyewe X 1147 Umetoka kuelezwa hapa sasa hivi kuwa watoto ni wenu wote… X 1153 Sasa wanawake wanaanza kutambua kuwa wanaonewa, na kudhulumiwa na wanaume, hivyo wanataka usawa X 1181 Hivi wewe hujasikia kuwa imethibitishwa na wataalamu kuwa ubongo wa mwanaume ni mzito kupita wa mwanamke utenda) X 1182 Ndiyo maana akili zao ndogo huwa hawafikiri chochote wakikutwa na matatizo isipokuwa kulia X 1183 Hata kama imethibitishwa kuwa ubongo wa mwanamke hauna uzito sawa na mwanaume, haimaanishi kuwa hawawezi kufikiri sawa na mwanaume X 1191 Mama ameumbwa ili alee watoto na kufanya kazi za nyumbani na ndiyo maana hawezi kuwa na ngumu sawa na mwanaume X 1192 Kule kuumbwa kwao na Mungu wawe hivyo, yaani kuchukua _amba, haina maana muwaonee na kuwatesa X 1210 Na ukiolewa na mwanamke ujue ndiyo umekuwa mtumwa wake X 1216 Hivyo iwapo, itaamuliwa mahari itolewe baadhi yao hawata lifanya hili liwe tatizo? X 1217 Isitoshe ile kawaida ya mwanamke asiyetolewa mahari, 108 basi si mke ila kimada, inawafanya wanaume wengi na hata wanawake wenzao wawaone wenzao duni 1220 Ingawa mimi sijafikia uamuzi akilini mwangu juu ya suala hili, nionavyo ni kuwa wakati umeshapita wa kumwita, ati malaya, mwanamke ambaye amewekwa kimada X 1221 Kwa nini asitambuliwe kama mke na kupewa heshima anayostahili X 1222 Tatizo la mahari ndilo linatufanya wengi wetu tusioe mapema au tushindwe kuoa kabisa X 1234 Ujue umetawaliwa na mkeo Bwana wee X 1247 Na kuanza kutumwa tumwa na mkewe X X 1262 Ukiangalia kwa jicho la akili, bila ya kuupendelea upande wowote, utaona jinsi wanavyoonewa, wanavyogandamizwa, kunyanyaswa na kudharauliwa X X X X 1280 Tangu utotoni, mtoto wa kike anawekwa katika hali ya uke hasa, na kufanywa amtumikie kaka yake X 1282 Hivyo wakikua wanakua na kasumba hiyo, inakuwa vigumu sana kubadili mienendo hii waliyozoweshwa na wahenga X 1284 Mimi najuta sana kwa kuadhiriwa kiasi hiki na wake zangu X 1291 Wamepata nini hasa wanaume hawapendi kutawaliwa na wake zao X 1292 Hivyo hawataolewa na mwisho wataanza kutufuata tena waume zao X 109 MADAHIRO: Tazama!(1) Mshenzi mkubwa wee!mikono yako imelegea kama ya mama yako.(2 ) Mtoto wa kike huwezi kujikaza! (3 ) Haya simama! ( 4)Inuka uende!watoto wa siku hizi balaa tupu! (5 ) Ati kuzaa! (6 ) Kuzaa gani huku! (7 )Motto asiyeweza kuwasaidia wazazi wake? ( 8)Mama Tama! ( 9) Hivi huwezi kumbembeleza mtoto akanyamaza? ( 10)Sijui una kazi gani huko? (11 ) MAUJA: Namkorogea uji! ( 12) MADAHIRO: Tangu umefika unamkorogea uji tu?huwezi kumbembeleza? (13)Inakuwa kelele moja kwa moja utafikiri kilabuni hapa! ( 14)Una ila wewe mama! (15 )Aaah!(16 ) Na huyo mke mwenzio naye, ndio amekwenda jii. (17 ) Nilimpa siku tatu kwenda kuwatizama nduguze, basi tena imekuwa jumla………(18 )Ngoja akirudi atanieleza vizuri alikokuwa(19 ). Tena leo nimepata fedha za tumbaku, kesho nataka kwenda kuwanunulia nguo madukani halafu tena mwenzio hayupo! (20 ) Shauri yake tena( 21). Atanunuliwa na bwana aliyemkawiza huko( 22). Er……… (23 )Mama Tama…….. ( 24)Mama Tamaa! ( 25) MADAHIRO: Hebu niletee moto( 26). Mtemba wangu umezimika………(27 )Ah! (28 )Kazi za matumbaku nazo hela zake za shida(29 ). Mtu unazisubiri miezi na miezi(30 ). Leo hii nimezipata( 31). Nikisha kula tu niende Igoko nikaonje(32). Kesho kukicha niende mjini Isevya( 33). Pombe ya Isevya safi kabisa(34). Siyo mapombe ya huku kwetu yanayowekwa sukari kidogo kabisa(35 ). Tena hata ukali haina(36 ). Mtu unakunywa utafikiri unakunywa togwa( 37). Au nikanunue baiskeli mpya(38 )? Maana baiskeli yangu hii inakuwa kila wakati inaleta gogoro( 39). Hebu nione( 40). Ah! (41 ) Ndiyo(42 ). Pesa nyingi kiasi( 43). Je nioe mke mwingine (44 )? Maana hawa wake zangu ghasia tupu( 45). Mtu huna raha hata kidogo……(46) utaona…… (47).Mama Tama………( 48) Mama Tama……(49 ) MAUJA: Bee……………..( 50) MADAHIRO: Chakula bado hakijawa tayari tu( 51)? MAUJA: Aa! (52 )Mume wangu wangu, mbona ndio tumerudi ( 53)? MADAHIRO: Ndiyo majibu yako hayo(54 )? Huna hata chembe ya adabu ( 55)? Mimi nakuuliza unajibu Ah! (56 ) MAUJA: Ninapika ( 57). MADAHIRO: Fanya upesi, nataka kwenda Igoko kumwona Bwana Mwakyembe ( 58). Leo tunataka kuonja kidogo…………( 59)Oh! (60 )Karibu ………..(61 )Ingia ………( 62).Ohoo…………( 63)Bwana Wambali, karibu ndugu yangu ……..( 64)Er……….(65 )Tama leta kiti( 66). KAJELA : Asante sana………….nimeshakaribia………..( 67) TAMA : Shikamoo………….( 68) KAJELA : Marahaba (69 ). Oh! ( 70) Bi Tama unakua sana……..tena kwa haraka kweli………( 71) MADAHORO: Habari za siku nyingi Mtanzania mwenzangu ( 72)? KAJELA: Nzuri sana mzalishaji mwenzangu (73 ). KAJELA : Mh! (74 ) Leo mmezikunja noti kweli Bwana Madahiro( 75). MADAHIRO: Ah! (76 )Wapi Bwana (77 ). Kiasi tu(78). 110 KAJELA: Basi ninyi wakulima wa tumbaku ndivyo mlivyo ( 79). Hata ukipata elfu ishirini unasema ah kiasi tu…….(80) Sijui kwa nini( 81)? Sasa ndio vipi utajenga nyumba kubwa ya kudumu( 82)? Maana unahimizwa sana juu ya jambo hili( 83). MADAHIRO: Oh! ( 84)Nyumba hii yatosha bwana wee! (85 ) Mtu utajitakia makuu ya nini( 86)? Tena huenda zikabomolewa maana mambo ya siku hizi hayaishi kubadilika(87 ). Mimi nionavyo ni kwamba huenda nikao……….( 88) KAJELA: Mke mwingine tena si unao wawili hivi sasa( 89)? MADAHIRO: Wamenichosha(90). Nataka kubadili upepo kidogo( 91). KAJELA: Lakini Madahiro( 92). Hivi wewe husikii inasemwa sana siku hizi kwamba kuoa wake wengi kunakufanya wewe kuwa ‘Bwana’ wao( 93)? MADAHIRO: Tena basi; hivi wewe unadhani mkeo akuiteje( 94)? Akuite ‘Bibi’ au ‘Mke’ mwenzangu( 95). KAJELA: Isitoshe, utakuwa unawapa amri kalikali na kuwamenyesha na kazi……….( 96) MADAHIRO: Nisikukate kauli Ndugu Wambali (97 ). Mtu asikudanganye Bwana (98 ). Mwanamke bila kumpa amri yako siyo mkeo tena ( 99). Sasa unafikiri kutakuwa na Mabwana wangapi nyumbani (100 )? Mimi nitoe amri yangu nay eye atoe yake………( 101)Ebo! ( 102) Haiwezekani! (103 ) Ujue mwanamke huyo kakutawala( 104). Na usilogwe kutawaliwa na mkeoujue umekwisha yakhe! (105 ) KAJELA: Lakini…………( 106) MADAHIRO: Subiri nikueleeweshe kijana, maana wewe hujaoa bado( 107). Sisi tuliooa tunavifahamu visa vyao ( 108). Kuna rafiki yangu huko Rufita……..( 109) KAJELA: Nani huyo ……….( 110) Sosela(111 )? MADAHIRO: Hapana(112 ). Sosela na Frank Malini wako Mpanda(113 ). Bwana………eee…….Kilakatta( 114). Basi Bwana Kilakitta, ameshindwa na mkewe hasa(115 ). Yeye anafanya kazi ya ukarani kwenye chama chetu cha tumbaku (116). Basi mshahara anaoupata, wote anaenda mpa mkewe (117 ). Halafu mke ndiye anayeanza kupanga vitu vya kununua ( 118). Basi utamkuta huyu Bwana, hata ile shilingi moja ya kwenda kunywea, anambembeleza kweli mkewe ampe…………nusu ya kumlamba miguu(119 ). Kha! (120 ) Maisha gain hayo(121)? KAJELA: Basi tena ndiyo unawamenyesha na kazi( 122). MADAHIRO: Mkeo lazima akusaidie kazi Bwana( 123). Sasa unafikiri asipofanya hivyo mtakula nini( 124)? Mimi ninataka kuona mke mwingine ili waweze kunisaidia kazi, maana hizi kazi za matumbaku ni ngumu ati! (125) Hivyo, ukiwa na wake wengi wa kukusaidia kazi ndiyo nafuu yako( 126). Ingawa hawawezi kazi za kiume kama vile kuangusha miti, kazi nyingine watakusaidia bwana-kupalilia………….kulima………….kuchuma tumbaku…………kuimbua………..(127 ) KAJELA: Aaa…….yaani wakezo unawafanya kama vile plau…………(128 ) MADAHIRO: Vipi( 129)? Naona Bwana Wambali unataka kunitukana sasa……….( 130)Hivi mkeo utamweka tu nyumbani kama picha ukutani ya kuangalia, asifanye kazi yoyote ile( 131)? Huku ni shamba bwana sio mjini(132 ). KAJELA: Kwani wake wa mijini wana nini(133 )? 111 MADAHIRO: Ho! (134 )Wake wa mijini kwani huwaoni wafanyavyo( 135)? KAJELA: Wako wanaofanya kazi maofisini kama wanaume(136 ). MADAHIRO: Wacha hao………( 137)Nasema wale wanaoolewa na kukaa tu, mighairi ya kazi(138). Wenyewe wanawaita magolikipa(139 ). Basi jamaa yangu mmoja wa Bukene…….( )140.Bwana Kisanko….mkewe hafanyi lolote lile( 141). Bwana anaenda kibaruani, mkewe anadorora tu, hafanyi lolote lile ( 142). KAJELA: Kwani hapiki chakula na kuwaangalia watoto( 143)? MADAHIRO: Afadhali anagalifanya angalau hayo, kama wafanyavyo wake wengine(144 ). Lakini mke wa mwenetu Kisanko, amewekewa boi wa kufagia nyumba na kufua(145 ). Halafu kuna mpishi na yaya wa kuangalia watoto(146). KAJELA: Lo! (147 )Halafu mkewe anafanya nini( 148)? MADAHIRO: Afanye nini tena( 149)? Basi ndiyo kastarehe tena kama malkia wa nyuki! (150 ) KAJELA: Loh! (151 )Balaa tena hilo…..( 152) MADAHIRO: Si ndivyo utakavyo wewe(153 )? KAJELA: La hasha! ( 154) Si mke tena(155 ). Huyo amevuka mpaka……….( 156)Eh! nilipita kukujulieni hali tu mara mara moja na sasa narejea nyumbani(157). MADAHIRO: Oh! (158 ) Mboa shemejio hujamwona(159 )? Subiri kidogo anapika chakula( 160). KAJELA: Hapana nina haraka kidogo, maana nina kijisafiri cha kwenda Igoko(161 ). Utanisalimia akina shemeji…..(162)Eh! ( 163) Kweli mama Ojunju amekwisha rudi( 164)? MADAHIRO: Laana yule…………bado hajarudi ( 165). Akirudi, atanieleza vizuri kile kilichomkawiza huko( 166) KAJELA: Oh! ( 167) Tutaongea siku nyingine……nina haraka ya kwenda Igoko(168 ). MADAHIRO: Haya….(169 )Karibu tena( 170). Oh! (171 )Na ukimwona Bwana Mwakyembe huko Igoko, mwambie nitawapitia pamoja na Kanuya, Mgassa, na Mndeme tukaonje kidogo (172 ). KAJELA: Loh! ( 173) Kikundi chenu kimekamilika(174 ). Haya nitamfahamisha nikimwona (175 ). MADAHIRO: Eee…….(176 )Mama Tama……( 177) MAUJA: Beee…………(178 ) MADAHIRO: Hivi chakula bado tu? (179 ) MAUJA : Ndi kwanza nimetia unga, ninasonga ( 180). MADAHIRO: Ah! ( 181)Fanya upesi chakula kinapikwa mwezi mzima(182 )? Na ukimaliza kupika, nifulie zile nguo zangu nilizovaa jana( 183). Kisha ukaazime pasi uzinyooshe(184 ). Maana kesho nitazivaa kwenda Isevya(185 ). Umesikia( 186)? MAUJA : Ndiyo(187 ). MADAHIRO: Loh! ( 188) Sijui tutakula saa ngapi leo hii( 189)? LETISIA na OJUNJU : Shikamoo baba….( 190) MADAHIRO: Marahaba, hamjambo, enh ( 191)? LETISIA na OJUNJU: Hatujambo(192 ). 112 MLAHAKA: Habari za hapa, baba Tama……..(193 ) MADAHIRO: Kaweke mzigo wako ndani (194 ). Umwambie mke mwenzio awape chakula watoto kwanza………(195) Wewe urudi hapa(196). Leo hii atanieleza vizuri kilichomkawiza huko (197). Mwanamke gani huyu….akipewa ruhusa kwenda kwao basi ndiyo tena anakuwa amepewa nafasi ya kwenda kwa hawara zake(198 ). Leo hii….( 199) MLAHAKA: Mbona uko wima(200 )? MLAHAKA: Jamani, kuna nini(201 )? MADAHIRO: Ati anauliza………(202 ) “Jamani kuna nini( 203)?” Malaya mkubwa wewe…..(204 )Umepata shahada ya ufasiki………hebu eleza( 205). Ulikuwa wapi siku zote hizi (206 )? MLAHAKA: He! ( 207)Baba watoto, hata hatujaulizana habari unaanza matusi (208 )? MADAHIRO: Nimekuuliza, ulikuwa wapi kwa siku zote hizi(209 )? MLAHAKA: Kwani wewe unadhani nilikuwa wapi( 210)? MADAHIRO: Ati nini( 211)? Hebu sema nisikie…( 212) MADAHIRO: Yaani hutaki kunijibu, sio enh( 213)? Nakuuliza , ULIKUWA WAPI( 214)? MLAHAKA: Ah! ( 215) Jamani …mtu ukirudi tu hapa, basi magomvi hayaishi(216 ). Mimi sitaki ugomvi…….(217 ) MADAHIRO: Nimekuuliza ‘ULIKUWA WAPI( 218)?’ MLAHAKA: Nyumbani( 219). MADAHIRO: Nilikupa siku ngapi za kukaa huko( 220)? MLAHAKA: Siku tatu( 221). MADAHIRO: Sasa….( 222)? Yamekuwaje tena( 223)? MLAHAKA: Nimewakuta akina Paskalia, Omari na Haule wagonjwa wa macho(224 ). Na baba hakuwepo(225 ). MADAHIRO: Sasa hao ndiyo walikuambia ukae huko kwa mwaka mzima( 226)? MLAHAKA: Ah! (227)Jamani, siku sita tu ndio umekuwa mwaka! (228) MADAHIRO: Ndiyo majibu yako hayo, enh( 229)? MADAHIRO: Nakuuliza ndiyo majibu yako hayo( 230)? Huna adabu(231 ). Mshenzi wewe…..( 232) MLAHAKA: Mshenzi mwenyewe……….(233 ) MADAHIRO: Ati nini( 234)? Unanitukana…….!( 235) MLAHAKA: Yalaa…..ananiuwa…(236)Nakufaa mie….( 237)Yalaa….(238 ) MADAHIRO: Nanga mkubwa wewe…(239 )Sasa wewe ndiyo utakayenitambua leo hii….chakula kiko wapi( 240)? MADAHIRO: Mpumbavu wewe.…..wewe na mwenzio wote washenzi….( 241)Tangu saa ile nauliza chakula bado tu hujapika(242). Mwanamke gani mvivu hivyo……( 243) MAUJA : Yalaa….nakufaa….(244 ) MADAHIRO: Nyokoo….leo utanikoma…(245 ) MAUJA: Basi nimekoma mme wangu……( 246) MADAHIRO: Hujakoma bado…( 247)Utakoma hasa! (248 ) MADAHIRO: Niacheni…( 249) NZOLE: Bwana Madahiro…hebu acha ugomvi! (250 ) MADAHIRO: Ninyi niacheni tu niwakomeshe wanaharamu hawa…(251 ) 113 MAUJA: Yalaa…ananiuwa….( 252) MADAHIRO: Kufa…huna adabu…(253 ) NZOLE : Bwana Madahiro utamuua mkeo bwana…( 254) MADAHIRO: Mke gani mbwa huyu…..( )Mwache afe tutamzika! ( 255) TULI: Tulizana kwanza Bwana Madahiro( 256). MANILA: Hebu acha ugomvi kwanza…….(257 ) MADAHIRO: Na wewe…na wewe….utanikoma nikikukamata( 258). Wewe ndio umemponza mwenzio huyu…(259 ) MLAHAKA: Unatuonea tu kwa kuwa sisi wanawake( 260). Hebu pigana na hao wanaume wenzio…(261 ) MADAHIRO: Nini( 262)? MADAHIRO: Mnasikia anavyonijibu( 263)? Wanawake gani hawa…..(264 ) TULI: Mlaani shetani bwana Madahiro(265 ). MADAHIRO: Shetani gani tena kuzidi mashetani hawa nilionao humu ndani(266 )? NZOLE: Madahiro(267 ). Si vizuri kugombagomba na wakezo kila wakati…(268 )Hebu tulia kwanza…( 269) MADAHIRO: Basi yamekwisha…(270 ).Niachieni….( 271) MANILA: Lakini usiwapige tena….(272 ) MADAHIRO: Ah! Ya kazi gani(273 ). Naifahamu sana dawa yao( 274). Nitaoa mke mwingine tu, lazima( 275). NITAOA! (276 ) MLAHAKA: Nenda ukaoe hata wanawake kumi(277). Nani anayekukataza(278 )? MADAHIRO: Unasemaje(279 )? Hebu niacheni…(280 )Niacheni….( 281) Onyesho la pili. Sehemu ya kwanza. MADAHIRO: Oh! (282 ) Maisha matamu hasa haya(283 ). Ninakula ninashiba na pombe ninakunywa! ( 284) Sitaki shida na mtu mimi…(285 )Akaa….! (286 )Wake ninao watatu(287 ). Mwingine ndio nimemwoa juzi juzi tu( 288). Mtoto mbichi kabisa…(289 )Wanaonionea wivu nao wakaoe…( 290)Lakini kama wanazo…(291 )Mimi kwangu ziko chungu nzima, kama vile utitiri…(292 )Ha! ha! ha! (293 ) Ndiyo zipo(294). Noti chungu nzima….(295 )Nikitaka kuoa mke mwingine tena, sasa hivi ninaweza( 296). Hata waseme mahari kiasi gani, saa hiyo hiyo…dakika hiyo hiyo…ninatoa…( 297)Wangapi wanaweza hivyo hapa Isikizya(298 )? MAUJA: Ah! (299) Baba Tama huachi kujisifu juu ya fedha…( 300)? MADAHIRO: Aaaa, Jagashi huko bwana( 301). Wewe ni mwanamke tu( 302). Unajua nini wewe(303)? MAUJA: Basi tena ndio hatusikii lolote lile isipokuwa maneno yako ya kujisifu ( 304)? MADAHIRO: Ohooo…naona sasa unataka kuingilia uhuru wangu( 305). Tena wataka kunitukana(306). Sitaki kutawaliwa na mke wangu mimi(307 ). Mke niliyemwoa kwa pesa za jasho langu ( 308). MAUJA: Ah! (309 ) Kwani hizo pesa za mahari ulizotoa ndio nini( 310)? MADAHIRO: Jamani…ati anauliza ndiyo nini( 311)? Ndiyo nini…(312 )Hajui jamani…( 313)Ha! ha!ha! (314)Sikiliza……wewe unafikiri mimi bila ya 114 kutoa pesa ungalikuwa hapa(315 )? Umeolewa kwa fedha mama….( 316)Fedha…( 317) MAUJA: Kwani wanaume wenzio waoao hawatoi fedha(318 )? Wanatoa fedha na hata mifugo kama vile ng’ombe lakini hatuwasikii kujisifusifu(319 ). Fedha za mahari ni zawadi tu, siyo kama vile ununuavyo kitu dukani( 320). MADAHIRO: Kwanini basi wazee wenu wanadai fedha au ng’ombe wengi wengi tunapowaoeni(321 )? MAUJA: Sasa hiyo inatokea kutokana na utamaduni wa makabila tofauti tofauti(322 ). Kuna wengine wanaotaka kufikiri kwamba watoto wao wa kike ni utajiri(323 ). Pia tamaa za wazee Fulani Fulani za kutaka kujipatia mali hata kwa njia zisizofaa( 324). MADAHIRO: Ah! ( 325)Ha! ( 326) Ha! (327 )Ha! ( 328)Mke wangu, naona siku hizi siasa inakuingia kwelikweli….( 329) MAUJA: Siyo siasa…( 330) MANILA: Hodi! hodi! hodi! Wenye nyumba hii…( 331)Hodi! hodi…hodiiii…( 332) MADAHIRO: Aaa wewe pita tu; umekwisha ingia ndani bado tu unapiga hodi ! hodi hodiiii…( 333) MAUJA: Karibu tuketi…(334 ) MADAHIRO: Eh! (335 )Mama Tama …hebu katuletee asusa kidogo……(336 ) MAUJA: Na leo hiyo nyama wengine hatuili isipokuwa imekuwa asusa ya walevi tu…(337 ) MADAHIRO: Wacha maneno ya kiburi hivi…(338 )Unaanza…(339 ) MADAHIRO: Loh! ( 340)Nikuambie nini Bwana Manila(341 ). Siku hizi mke wangu huyu kawa mkali na mkaidi kupindukia…(342 )Sijui kwa nini(343 )? MANILA: Labda kwa kuwa umeoa mke mwingine…(344 )Au anataka usawa unaosemwa semwa kila mara maradioni………( 345) MADAHIRO: Labda…( 346)Maana naona maneno hayamwishi(347 ). Tena anajifanya siku hizi anajua kila kitu(348 ). Eh! ( (349 Kabla hujaingia ati ananiambia kuwa fedha za mahari tutoazo ni zawadi tu……….(350 ) MANILA: Zawadi gani(351 )? MADAHIRO: Sijui …labda zawadi ya Bwana kwa Bibi katika ndoa( 352). MANILA: Ha!ha!ha!ha!hoh! ( 353)Na kama ni zawadi kwa nini wapewe tu wanawake na sisi wasitupe: au kwa kuwa wao ndio waolewao(354 )? MADAHIRO: Naona ni hivyo basi. Lakini ajabu ni kwamba, wazazi wake ndio wanaozila! (355 )Basi bwana, ndiyo ananichongolea mdomo hasa…..(356 ) MANILA: Ah! (357 )Huo ni wivu tu unaomsumbua kwa kuwa umeoa mke mwingine….( 358) MADAHIRO: Na kama ni wivu, hautamfikisha mbali kwani mara moja ninaweza kumwacha yeye niakoa tena mke mwingine….(359 )Pesa ziko bwana……( 360) MANILA: Na mtu asikudanganye bwana…(361 )Waswahili husema, ‘Tupa Sululu’(362 ). Kinachosema ni pesa tu(363) Wewe unakaa kimya …(364). Unaangalia mambo yanavyokwenda(365 ). MADAHIRO: Basi mama Tama anasema kuwa fedha si kitu…(366 ) 115 MANILA: Si kitu(367 )? Ha!ha!ha! (368 )Mgonjwa huyo(369 ). Wapi bwana; ni mahali gani ambapo fedha si kitu(370)? MADAHIRO: Labda mijini….(371 ) MANILA: Loh! ( 372)Tafadhali bwana wewe…ni kama kusema kuwa paka anakula nyama kumshinda simba! (373) Huko mijini ndiyo pesa imaetawala kabisa fikra za watu(374 ). Kila kitu pesa tu(375 ). Tena utaona siku hizi, wanawake wengi wanakimbilia mijini kwenda kujiuza tu( 376). Si aibu hii! ( 377)Halafu tena wao ndiyo wa kwanza wanaotaka usawa na wanaume! ( 378) MADAHIRO: Ah!ha!ha!ha! (379 ) Ati usawa! (380 ) Si kichekesho hiki jamani…( 381)Eh! ( 382)Hivi mama Tama bado hajarudi tu( 383)? Mwanamke kawa na kiburi huyu …(384 )Mama Tamaa…( 385)Mama Tamaa…(386 ) MAUJA: Bee… ( 387)Ninakujaa…( 388) MADAHIRO: Mpumbavu wewe …(389 )Kila ukitumwa unaenda jumla! ( 390) MAUJA: Jamani nilikuwa bado naichoma! (391 ) MADAHIRO: Jamani nilikuwa bado naichoma…(392 )Uwongo mtupu( 393). Unaichoma kwa mwaka mzima! ( 394)Shetani mkubwa wewe! ( 395) Sasa hivi mimi ninaweza kukuvurugavuruga vibaya kabisa…(396 ) MAUJA: Sasa jamani…( 397) MADAHIRO: He! (398 )Shika adabu yako(399 ). Kama mimi ninasema wewe siyo kunichongolea hilo domo lako…(400 ) MANILA: Basi yaishe hayo Bwana Madahiro( 401). Wacha tunywe pombe na asusa…(402 ) Asante saana shemeeeeeji! (403 ) Bwana Madahiro karibu tule nyama…(404 ) MADAHIRO: Basi kawa kichwa ngumu kweli huyu….(405 ) MANILA: Ah! (405 )Achana naye huyo(406 ). Wewe usimwendekeze…(406 ) MADAHIRO: Sifahamu kwanini lakini…( 407)Au labda kwasababu anaona wivu kwa kuwa wako wengi…(408 ) MANILA: Wapi bwana(409 ). Mbona mimi ninae mmoja tu, lakini ndiyo ghasia na zogo sawa kabisa na humu mwako(410 ). Hivi sasa nimeondoka huko nahisi nafuu( 411). Maana mke wangu naye ana kiburi kweli kweli (412 ). Kila mara ninampiga kwa kiburi chake, lakini wapi(413 ). Hasikii hata kidogo…(414 ) MADAHIRO: Dawa yao ni kuwaacha tu na kuoa mke mwingine….(415) MANILA: Loh! ( 416)Huwezi kujua bwana…( 417)labda ndiyo unaweza kwenda kuoa mwendawazimu kabisaa….(418) MADAHIRO: Ah! (419 ) Kwangu si shida kuoa au kumwacha mke wangu(420 ). Kama hafuati amri yangu, huyo si mke tena…bora kumwacha…..( 421) MANILA: Naweza kuoa tena mwingine kama nikimfukuza huyu…maana masika inakaribia….( 422) MANILA: Ah! (423 ) Mimi naenda zangu bwana…( 424)Na watoto wote wako wapi( 425)? MADAHIRO: Wameenda kuwaangalia bibi zao huko Mabatini tangu juzi(426 ). MANILA: Ndiyo maana siwaoni(427 ). Basi mimi sikai tena(428 ). Utaniagia akina shemeji(429 ). MADAHIRO: Huwaagi mwenyewe(430 )? 116 MANILA: Siku nyingine bwana wee(431 ). Naenda Igoko(432 ). MADAHIRO: Igoko( 433)? MANILA: Ndiyo(434 ). MADAHIRO: Basi pitia kwa bwana Mwakyembe, mweleze kuwa kesho nitampitia tuende Isevya kwa bwana Jitenge, akatunyweshe kidogo( 435). Pia nisalimie sana akina Unono, Marande, Kitwana na Msomple(436). MANILA: Sawa( 437). Nitawafahamisha( 438). MADAHIRO: Eeee…(439 )Mama Tamaa… ( 440)Mama Tamaa… ( 441)Mama Tamaa(442 ). MAUJA: Beee…( 443) MADAHIRO: Sikia mama Tama( 444). Mimi sipendi kabisa wewe niwe nakuita mara hamsini(445 ). Nataka nikuite mara moja tu, unatokea(446 ). Usikae unanisumbua… nikae nakuita wee kama mtu aliyepungukiwa na akili(447 ). Umesikia( 448)? Mimi sijawa bado mafuu…(449 )Natumaini tumeelewana(450 ). Hebu niletee mtemba wangu…(451 )Na uuwashe kabisa( 452). Hapo zamani mimi sikuwa hivi…(453 ) Nimekuwa hivi shauri ya pombe( 454). MADAHIRO: Tandambele! (455 )Nimekuambia UUWASHE…(456 )Mbwa wewe(457 ). Nyama huyu…wanawake sijui akili zao huwa wanaziweka wapi! (458 ) Unapomwambia unafikiri anasikia kumbe hana hata moja! ( 459) Eee…(460 )Hebu niongeze na nyama…(461 )Huyu mama Tama anajifanya kichwa ngumu sana(462 ). Eee… ( 463)Hebu niletee na kiporo cha wali wa jana maana nasikia njaa(464 ). MAUJA: Wacha nikuletee maji ya kunawa…( 465) MADAHIRO: Ah! (466 )Wacha tu. Maji ya kazi gani(467 )? Niletee pilipili na chumvi uongeze(468 ). Eh! ( 469)Mama Tama… (470 )Mama Tama…(471 ).Hebu niletee na maji ya kunywa…(472 )Eee …unasikia mama Tama…mimi(473 ). Mh! ( 474)Eee…mimi( 475) PAZIA. SEHEMU YA PILI MAUJA: Jamani bado tu hayo mahindi tuyapete(476 )? DEKA: Hebu tuyaangalie( 477). Naona tayari… (478 )Wacha nikachukue mengine ndani(479 ). MLAHAKA: Kha! ( 480) Mwenzetu ndiyo anajua kupendeka hasa(481 ). Ameolewa juzi juzi tu, jana tena amenunuliwa nguo mpya! ( 482) MAUJA: Ah! Yatakwisha tu hayo mama( 483). Unafikiri tunae mume mama (484 )? si wazimu tu(485 ). Jana tu ametapika nusu ya kufa, lakini matusi ndiyo haachi( 486). Mwenzio bado anapendeka(487 ). Kipya kinyemi( 488). MLAHAKA: Basi ndiyo Deka hasa(489 ). Maana anaturingia( 490). DEKA: Nimesikia! (491 ) Nimesikia! ( 492)Loh! (493 ) Hamwishi kuniteta! (494 )Nikifanya hivi, oho mvivu( 495). Nikisema, oho mvivu ( 496). Nikisema, ohooo ana mdomo(497 ). Nikijikalia kimya, ohoo anaringa! (498) Hivi, hebu niambieni hasa hasa wewe mama Ojunju(499 ). Unachokitaka kwangu ni nini hasa(500 )? 117 MLAHAKA: Aaa( 501). Tuache kusema kama unaringa( 502)? DEKA: Hata kama ninawaringia wewe kinakuuma nini hasa(503 )? Si uniache tu na wendawazimu wangu(504 ). MAUJA: Jamani hebu yaacheni hayo mwishowe yatafika mbali tena( 505). Hivi mmeanza(506). DEKA: Hapana…(507 )Mimi leo nataka anieleze maana tangu niolewe humu, kila siku maneno maneno hayaishi (508 ). Tena basi habari anazivumisha hata kwa majirani( 509). Leo hii nataka anieleze kinachomkereketa ( 510). Pilipili ziko shamba, wewe zakuwashiani( 511)? MAUJA: Bi Deka hebu nyamaza(512 ). MLAHAKA: Wewe mwache tu apayuke(513 ). Si mwenzetu anapendwa na Bwana(514 )? DEKA: Hata kama ananipenda na wewe hakupendi, hasa ndiyo iwe kunitangaza kwenye majumba( 515)? MLAHAKA: Kwani nimekutangaza wapi(516 )? DEKA: Loh! ( 517)Mwanamke mwongo huyu! (518 )Phtuu! (519 ) MLAHAKA: Babu usiniteme au unataka mengine tena(520). DEKA: Utanifanya nini(521 )? Utanifanya nini kijana kama mimi(522 ). Loh! (523 )Haya makama ya vitenge niliyonunuliwa wewe ndiyo unafikiri nguo hizi( 524)? Tumevaa nguo ngapi sisi, itakuwa haya makama(525 )? Kama unataka nikuachie wewe ni kuniambia tu, siyo kuenda kunitangaza kwenye majumba ya watu…(526 ) MLAHAKA: Aaaa babu; kwa nini tufiche(527 )? Kila kitu akileta bwana, unafikishiwa wewe(528 ). Akileta nyama unafikishiwa wewe( 529). Akileta sukari, kwako tu( 530). Sasa tena wewe tu, ndiyo unakuwa unanunuliwa nguo mpya(531). Kwani unafikiri sisi tunapenda(532 )? DEKA: Kama hampendi, kwa nini hamumwambii bwana wenu, ili awanunulie(533 )? Ndiyo iwe kunitangaza mimi kila nyumba( 534)? Sasa, ukifanya hivyo ndiyo itakusaidia nini(535 )? Hao majirani watakununulia nguo(536 )? Mwanamke huachi maneno-neno ya uwongo(537)? Mwanamke mzima na watoti unao….(538) Eeh! Hawa akina Ojunju na Letisia, lakini mambo ya kijinga ndiyo huachi( 539)? MLAHAKA: Mambo ya kijinga( 540)? DEKA: Unajifanya hujui enh? Na huku unakoenda mara kwa mara kuomba madawa, unadhani hawana midomo (541 )? MAUJA: Anatafuta madawa! (542 ) DEKA: Tena basi; ( 543)Ndiyo kazi yake kila akitoka hapa- kwenda kwa Waganga kutafuta dawa eti apendeke! (544)Mwanamke umeshakua, huachi ushirikina(545 )? MLAHAKA: Babu usinisingizie(546 ). DEKA: Nakupa ukweli wako, nikusingizie nina shida gani kwako mimi unafikiri mimi nina unafiki, unazibaziba na owongo kama wako(547 )? Mwanamke mbaya kupindukia! (548 )Phtuu! ( 549) MLAHAKA: Nimekuonya usiniteme………(550 ) 118 DEKA: Phtuuuu………….!( 551) MADAHIRO: Eh! ( 552) Kuna nini tena hapa( 553)? MAUJA: Ah! (554 ) Baba Tama unauliza na hali unaona ugomvi(555 ). Waamue wataumizana(556 ). MADAHIRO: Ah!( 557)Mambo ya wanawake! (558 )Hawana akili hata kidogo! (559) Haya wacheni ugomvi……wacheni(560 ). Mwachie mwenzio(561 ). DEKA: Mngeniacha nikamkomesha tu…hana adabu baradhuli huyu! (562 ) MLAHAKA: Mbona umeshindwa! ( 563) MADAHIRO: Kelele! (564 )Sitaki kusikia tena sauti zenu, nyama ninyi(565 ). Mnataka kunisumbua akili, sivyo enh( 566)? Nitawatwangeni nyote wawili, halafu niwafukuzieni mbali nguruwe ninyi( 567). Mistaki kunibughuzi kama mwehu mwenzenu huyu jana( 568). MAUJA: Ah! (569 ) Baba Tama, mie tena nimekukosa nini(570 )? MADAHIRO: He! (571 ) Funga bakuli lako( 572). MAUJA: Ah! (573 )Yarabi, mimi tena ndiyo…( 574) MADAHIRO: Nimesema sitaki kelele hukusikia( 575)? MAUJA: Aaa! ( 576)Babu, lazima niseme ati! ( 576) Wagombane watu wengine mie tena ndio nirudiwe……..( 577) MADAHIRO: Ohooo! ( 578)Naona bado hujanielewa wewe( 579). MAUJA: Kama umenichoka sikuniambia tu(580 ). MADAHIRO: Hilo tu(581 ). Sio kubwa kwangu(582 ). Saa yeyote ile unaweza kurudi kwenu( 583). MAUJA: Eee……… babu afadhali………..( 584) MADAHIRO: Na sasa sitaki tena kusikia maneno yako. Haya toeni hizi ghasia zenu(585 ). Katwangieni nyuma ya nyumba(586 ). Na tangu leo hamna ruhusa ya kukaa hapa(587 ). MADAHIRO: Sijui wanawake wana mawazo gani(588 )? Yamekaa tu, utafikiri makondoo( 589). Hayawezi kufikiri hata kidogo( 590). Sasa tena haya mengine yaliyokuwa yakigombana, sijui yalikuwa yakigombeani! ( 591) Na huyu mama Tama naye anachingolea mdomo sana siku hizi(592 ). Sijui nini kinachomvimbisha kichwa(593). Tutaona habari yake(594 ). Eee……….(595 )Mama Tama(598 ). Mama Tama! (599 )Mama Tama! (600 )Wee Mama Tama! (601 )Mauja! (602 ) MAUJA: Bee( 603). MADAHIRO: Fisi wewe! (604 )Mbwa kasoro mkia! ( 605)Hivi nikuite mara ngapi ndiyo uitike( 606)? MAUJA: Sasa jamani, mbona tulikuwa nyuma ya nyumba (607 )? MADAHIRO: Yaani mkiwa nyuma ya nyumba ndio usiitike, enh (608 )? MAUJA: Sikusikia(609 ). MADAHIRO: Sikusikia! (610 )Yaani kiziwi wewe siku hizi, au sivyo(611 )? MAUJA: Si nilikuwa mbali! ( 612) MADAHIRO: Si nilikuwa mbali! (613 )Ulikuwa mbali, mbinguni( 614)? Mwone uso wake(615 ). Huna hata haya kusema uwongo kama huo(616)? MADAHIRO: Enhe, hebu nieleze; na hao mahayawani wenzio walikuwa wanagombea 119 nini(617 )? MAUJA: Walikuwa hapa hapa, kwanini usiwaulize(618 )? MADAHIRO: Nini(619 )? Hebu rudia tena( 620). Mimi nakuuliza wewe sio hao majuha wenzio(621 ). Walikuwa wanagombea nini( 622)? MADAHIRO: Mama Tama, utanijibu au hutanijibu( 623)? MAUJA: Baba Tama, naona siku hizi unanisakama sana(624 ). Chochote nikifanya wewe kwako kibaya tu(625 ). Mwanangu huyu Majuto(626 ). Mwanangu huyu Majuto, angalikuwa amekuwa, wallahi, baba yangu mmoja, nisingalikaa hapa(627 ). MADAHIRO: Ah! (628 )Hayo maneno yako tu( 629). Kwani mwanao huwezi kwenda nae( 630)? MAUJA: Na Tama na Masumbuko nao je(631 )? Nikiondoka hapa watapata taabu kweli(632 ). ‘Mtoto na mama yake’ ndio maana unaniona navumilia( 633). Ama sivyo…!( 634) MADAHIRO: Niachie maneno yako ya upuuzi(635 ). Dhiki tu ndiyo inakuweka hapa(636 ). Ukiondoka hapa unafikiri utaacha kwenda kufa na njaa kwenu( 637)? MAUJA: Ah! ( 638) Baba Tama ndiyo unanijibu hivyo kweli…………(639 ) MADAHIRO: Ah! ( 640) Kwa nini tufiche ukweli( 641)? Baba yako maskini atakulisha nini( 642)? Tuachie uchuro hapa mama( 643). MAUJA: Baba Tama, mimi nitakwenda( 644). MADAHIRO: Utakwenda wapi(645 )? MAUJA: Kwani ulinitoa pangoni au kwenye zizi la ng’ombe( 646). Au uliniokota jalalani(647 )? Nitakwenda kwetu(648 ). Tena unasema baba yangu masikini……..(649 )Hata kama ni masikini, wewe ndiyo tajiri(650 )? MADAHIRO: Mimi angalau ninacho chakula cha kuwalisha( 651). Unafikiri kama mngalikuwa hamli chakula, ungalivumilia wewe kukaa hapa( 652)? MAUJA: Kwani nyumbani wanakula nini( 653)? Mbona wanaishi(654 )? Au wewe ulipokuja kuniposa mimi ulinikuta ninakula nini( 655)? MADAHIRO: Siku hizi unajifanya kusema na wewe( 656). MAUJA: Ah! (657 )Baba! ( 658)Kama mtu umemchoka ni kumweleza tu, sio kuniletea masimango(659 ). MADAHIRO: Huo mdomo wako mchafu ndio unaokuponza(660 ). MAUJA: Wewe wako ndio safi( 661)? MADAHIRO: Nini( 662)? Ati nini( 663)? Mshenzi wewe nikusikie tena…..( 664) MAUJA: Mshenzi mwenyewe ( 665) MADAHIRO: Huna adabu! (666 ) MAUJA: Nakwenda kwetu sasa hivi………………(667 ).Nakwenda……….(668 ) MADAHIRO: Ndio nilikuwa nataka useme hivyo(669 ). Kwenda! (670 )Nyani wee……..(671 )Nani anakutaka hapa(672 )? Nitaoa mke mwingine mimi(673 ). Hunipi shida yeyote baradhuli mkubwa wewe……( 674) MAUJA: Ah! ( 675)Nimechoka nakwenda……….(676 ) MADAHIRO: Nenda(677 ). Nenda………….(678 )Na wala hutaniona nikija kwenu kudai mahari(679 ). Kwenda(680 ). Kwenda……( 681) MAUJA: Usinisukume( 682). Nitaenda mwenyewe………….( 683) 120 MADAHIRO: Unangoja nini( 684)? Kwenda! ( 685) DEKA: Jamani Baba Tama(686). Fanya subira! ( 687) MADAHIRO: Sitaki bugudha( 688). Mwache aende( 689). ONYESHO LA TATU. MLAHAKA: He! (690 )Karibuni nami nitakuwa fundi wa kufuma vitambaa( 691). DEKA: Wewe kazana tu……….(692 ) MLAHAKA: Zamani nilikuwa sifahamu hata kusika ile sindano(693 ). NASAA: Tena ungalikuwa umekwisha kujua toka siku nyingi kama ungesikia maneno yetu ya kujiunga na Umoja wa akina mama(694 ). Wenzio hapa kijijini wamejifunza mambo mengi kweli(695 ). Kufuma, kushona, kufuga kuku wa kisasa, uzazi wa majira, malezi bora, afya, na mambo mengi mengine ya manufaa………….(696 ) DEKA: Yeye tena mwenzetu aliendekeza sana ujumba(697 ). Akimbiwa jiunge na ewnzio mara ooh! ( 698) Bwana mkali……mara naona aibu sijui kusoma………….(699 ) MLAHAKA: Hata kama sijui kusoma wewe kinakuuma nini(700)? DEKA: Usiambiwe hata kama hujui( 701)? Utajificha mpaka lini(702 )? NASAA: Anaona aibu kuonekana mama mzima hajui kusoma……..(703 ) DEKA: Sasa akijificha, basi ndiyo atabakia nyuma tu, wakati wenzio wanaendelea( 704). Kama anaona aibu kujitokeza, wanae kina Letisia, ambao wamekwisha fahamu kusoma, kwanini asiwaambie wamfunze(705)? MLAHAKA: Mimi nasema sitaki(706 ). Kama ni ujinga kwani wenu(707). Ninyi niacheni tu na ujinga wangu(708 ). Kawekeni vitabu vyenu ndani, halafu wewe Tama, katenge chungu cha ugali jikoni(709 ). Mbona mnanitumbulia mboni( 710)? DEKA: Tunastaajabu, unavyomtumamtuma huyu mtoto Tama kila siku…………..(711 ) MLAHAKA: Mtoto aache kutumwa! ( 712)Tama wee……….we Tama! (713 ) TAMA: Bee…………..(714 ) MLAHAKA: Hebu chukua kwanza kibuyu ukalete maji kisimani( 715). Halafu ukirudi, utwange ile mihogo uliyoiacha jana(716 ). NASAA: Kha! (717 ) Mama Letisia, hata mtoto hajapumzika( 718)? MLAHAKA: Niache kumtuma kwanini( 719)? NASAA: Msubiri kwanza apumzike(720 ). Basi ndiyo kwanza tu anatoka shuleni, aende kisimani, aje tena atwange! ( 721) DEKA: Anamtesa kwa kuwa siyo mwanae(722). Kwanini asimtume mwanae Letisia( 723)? MLAHAKA: Hamwezi kunichagulia mtoto wa kutuma(724 ). Wote ni wanangu(725 ). DEKA: Wote ni wanao ndiyo, lakini ndiyo usifanye ubaguzi kwa kuwa wengine ni watoto wako wa kambo tu( 726). MLAHAKA: Ah! (727 )Hivi mmenianza(728 ). Tama usisikilize huu upuuzi, nenda kisimani( 729). 121 DEKA: Usiende Tama(730 ). Kama maji, tumia yaliyomo ndani( 731). MLAHAKA: Mimi ninamtuma wewe unamzuia! (732 )Tama hebu nenda kisimani( 733). Kachukue kibuyu uende( 734). Nenda. Husikii(735 )? DEKA: Usiende Tama( 736). Tena hata kupika leo hii usipike, wala kutwanga(737). Mwachie na Letisia naye apike leo(738 ). Kwani wewe unamzidi nini yeye( 739)? Kama kimo, mko sawa(740 ). Mbona yeye hatujasikia hata siku moja akitumwa(741 )? MLAHAKA: Tama unaanza ukaidi- siyo enh( 742)? Nenda kisimani nakuambia ( 743). Usisikilize maneno ya mtu! (744) DEKA: Usiende! (745 ) MLAHAKA: Nakuambia Tama nenda(746 ). DEKA: Usiende popote! ( 747) MLAHAKA: Tama, uende ama sivyo utanikoma leo hii…………….umenisahau( 748)? DEKA: Hakuna lolote(749 ). Umezoea sana kumpigapiga(750 ). Leo hii humpigi! ( 751) MLAHAKA: Tama nakwambia uende(752 ). Ama sivyo utalia, nitakuchapa hasa! (753 ) DEKA: Nyamaza………(754 )Usilie……(755)Hakuna mtu wa kukuchapa leo(756 ). MLAHAKA: Nakwambia Tama( 757). DEKA: Haya mwanangu Tama. Nenda kacheze na wenzio(758 ). Chakula tutapika mtakula, hakuna wasiwasi. MLAHAKA: Lakini mnamfunza uvivu hivyo! (759) DEKA: Wacha maneno yako(760 ). Mtoto wa mwenzio unataka kumkondesha nini( 761)? Kama ulikuwa na chuki na mama yake, siyo kuwafanyia watoto(762 ). Hivi wewe utafurahi kweli, kama ukiondoka hapa, halafu sisi tuwe tunawatesa wanao(763 )? MLAHAKA: Niondoke niende wapi( 764)? DEKA: Uende kwenu, kwani humuoni huyu bwana wetu kuwa ni mtu mwenye ndimi mbili( 765)? NASAA: Hata mimi niliyeolewa hivi karibuni tu, ninaviona visa vyake(766 ). Yu kigeugeu ajabu! ( 767) DEKA: Basi nikuambie nini, mwenzangu! ( 768) Mama Tama hakupenda hata kidogo kuondoka hapa( 769). Alifahamu kuwa, akiondoka, huku nyuma wanae watapata taabu( 770). Lakini mwishowe aliondoka mama(771 ). Maana aliadhiriwa kupita mpaka tena(772 ). Loh! ( 773) Mimi, alipokuwa akiondoka hali ana mtoto mchanga mgongoni, moyo wangu uliingiwa na uchungu sana, ingawa sijazaa………..(774 )Machozi yakawa yakinitiririka tu, bila ya kujifahamu( 775). Mh! ( 776)Bwana gani huyu tuliyenaye( 777)? Anamfukuza mtu, kama mbwa asiyetakiwa! (778 ) NASAA: Tena isitoshe, mtu mkeo mwenyewe mmekaa naye kwa wema miaka mingi, mpaka mmepata na watoto( 779). Leo kuenda kumfanya hivyo(780 )? DEKA: Basi hukuwapo mama…………(781)Wallahi, ungeshangaa visa vya huyu Bwana(782 ). NASAA: Kwani sivioni anavyotufanyia sasa(783 )? Juzi tu amempiga mama Ojunju bila ya kisa chochote kile(784 ). MLAHAKA: Anatuonea tu, kwa kuwa sisi ni wanawake(785 ). Hata mimi najikalia hapa 122 basi tu(786 ). NASAA: Basi nasi tunajilegeza mno(787). Mradi tumeitwa ‘wanawake’ ndiyo hata tunapigwa hamna hata kujitetea! (788 ) MLAHAKA: Kujitetea! (789 ) Loh! ( 790)Babu huyo ni mwanaume(791 ). NASAA: Ndiyo, kila mtu anajua kuwa yeye ni mwanaume(792 ). Tena dume hasa, lakini na sisi hapa tuko wanawake watatu…..( 793)Bora kujitetea(794 ). Lakini tukimwacha, ataendelea kutuonea sana( 795). Mpaka lini(796 )? MLAHAKA: Tena siku hizi ndiyo amefungulia matusi ajabu(797 ). Mpaka mtu unaghadhabishwa(798 ). Ukitaka kumbishia anakutishia kukufukuza(799 ). DEKA : Siyo matusi tu(800 ). Matusi na masimango(801 ). NASAA: Nakupigwa hasa(802). Mtu unatimbwa mpaka unakaribia kufa( 803). Loh! ( 804)Bwana huyu, atakuja kutuua mwishoni(805 ). DEKA: Na maneno ndiyo hayaishi( 806). Kutwa nzima anajisifia pesa( 807). NASAA: Isitoshe hizo pesa bila ya sisi kwani angalizipata(808 )? Kwani ni akina nani wanaoshinda shambani kutwa nzima kama siyo sisi(809 )? Tena mtu hupumziki hata dakika moja( 810). Utoke shamba, uvunje vunje kuni za kupikia, haya uende kisimani, ukirudi unapitilizia moja kwa moja jikoni( 811). Yeye wakati wenyewe anavuta tu mtemba, akihimiza, ‘chakula bado tu’(812 )? DEKA: Afadhali hata akiwa amekaa tu bila maneno maneno(813 ). MLAHAKA: Lakini akilewa………..( 814) DEKA: Akilewa tena, ndiyo inakuwa matusi na masimango moja kwa moja( 815). NASAA: Halafu mara atapike humu ndani( 816). Tunakaa tukinukiwa na harufu mbaya ya matapishi ya pombe ( 817). MLAHAKA: Na hata siku moja huwezi kumwona akiyamwagia mchanga matapishi yake( 818). NASAA: Na mshahara ndiyo matusi, masimango na vipigo! ( 819) MLAHAKA: Fedha zote anazimaliza yeye kwenye ulevi(820 ). NASAA: Na kuoa wake wengi wengi na wengine kuwafukuza( 821). Mimi nilipokuwa nikiolewa, sikujua kwamba mwingine ndiyo kwanza ameachwa(822 ). Amekuwa popo bwana huyu( 823). MLAHAKA: Yeye anasema kila mara kuwa kuoa, au kumwacha mke, kwake si shida! (824 ) DEKA: Basi ndiyo tunawekwa humu ndani kama vimada(825 ). Maana wanaume wawekao vimada ndiyo kazi yao (826 ). Mara akae na huyu, mara yule; amfukuze huyu……mara tena akaokote mwingine( 827). Anakuwa anawabadili kama nguo(828 ). Basi ili mradi ghasia tupu( 829). Kwake ndiyo starehe! ( 830) NASAA: Labda ingalikuwa nafuu na sisi kama tungalikuwa vimada, maana hapo unahiari ya kuondoka wakati wowote ule ukichoka(831 ) . DEKA: Na yeye angalikuwa na wasaa wa kukufukuza wakati wowote ule aupendao(832 ). Anakuwa amekuchezea na kukuchakaza na kazi, kama hizi kazi za matumbaku, halafu anakupiga teke(833 ). Nani tena atafikiria 123 kukuoa umeshazeeka(834 )? Wewe unakuwa umemnufaisha tu, kwa jasho lako(835). Umemlimia mashamba na mashamba(836 ). NASAA: Kama hivi alivyo bwana wetu(837 ). Kazi tunafanya wote(838 ). Isitoshe kama kazi za mashamba tunazifanya kumshinda hata yeye, lakini pesa zinazopatikana zote ni zake( 839). Wewe anakununulia gauni moja tu, la kuchumia tumbaku, msimu ukifika(840 ). Halafu fedha zote anaenda kulewea na kuwahonga wanawake wake wa nje! (841 ) Wewe unakuwa umefanya kazi bila ujira( 842). MLAHAKA: Ujira wako matusi! ( 843) DEKA: Tena hana hata ile chembe ya huruma baba huyu(844). Ukiugua wala hakujali, anajionea udhia tu(845 ). Isitoshe hana imani hata kidogo(846 ). Nakumbuka jinsi alivyomwadhiri mama Tama, wakati akimfukuza (847 ). Kwanza alimpiga kweli, ndipo akamfukuza (848). Sasa kila akiwaomba wanae wakamtembelee, Madahiro hataki! (849 )Mimi nikamshauri amwone Mwenyekiti wa kijiji akasema ataenda sijui yalikuwaje! ( 850) Kha! ( 851)Mme gani huyu! ( 852) MLAHAKA: Naye amezoea kweli kutupigapiga kila siku(853 ). Lakini hivyo ndivyo wanaume wote; hatuna la kuwafanya( 854). NASAA: Basi hilo ndiyo tatizo letu kubwa wanawake(855 ). Tunawatukuza sana wanaume na kukubali unyonge( 856). Lazima tuuondowe unyonge huu kama tunataka mabadiliko( 857). Mimi namwambia tumezidi kujilegeza mno( 858). Hebu leo tujaribuni kujikaza kidogo, jama( 859). MLAHAKA: Hivi kweli tutamweza( 860)? NASAA: Basi wanawake ndivyo tulivyo( 861). Huo unyonge tunajipa wenyewe, kwasababu ya kujiendekeza sana( 862). Kwa nini tusimuweze(863 )? Mbona kazi ngumu ngumu tunazifanya( 864)? Jamani, leo tujaribuni(865 ). Akimpiga mmoja wetu, tuingilie kati na kumvamia(866 ). Amezidi mno uonevu, loh! ( 867) DEKA: Sawa(868 ). Akifika, lazima atatafuta ugomvi! (869 )Ampige mmoja wetu, kama kawaida yake, basi nasi tumvamie( 870). Mama Ojunju wewe unaonaje?(871) MLAHAKA: Sawa sawa, mpango mzuri, naona atanifikia mimi kwanza(872 ). Lakini naogopa kweli kweli(873 ). Kwanza akitukuta hapa……….( 874) DEKA: Usiogope, sisi tupo….(875 )Shss…(876 )Nasikia sauti…naona ndiye yeye( 877). MLAHAKA: Mie naogopa……( 878) DEKA: Shsh…(879 )Nyamaza! (880 ) MLAHAKA: Mimi…mimi…nita…nita…( 881) MADAHIRO:He! (882 ) Hivi ni kweli au macho yangu(883 )? Yaani mnataka kuniambia leo ndiyo mmeamua kusukaniana hapa( 884)? Yaani mnajifanya mabubu siyo enh(885 )? NASAA: Kabla hatujaulizana habari, baba Tama(886 )? 124 MADAHIRO: Haya, habari za hapa(887 )? Hebu nipe kiti(888 ). Nitasimama mpaka saa ngapi( 889)? Mtu umeniona hivi hivi, mpaka nikuambie kunipa kiti(890 )? Huna adabu( 891). Eee…(892 )Nenda kaniletee na mtemba wangu ndani(893 ). Uniwashie kabisa(894 ). Na hebu sasa nielezeni imekuwaje leo mmejiamulia kukaa na kusukiana hapa(895 )? Kila siku nawaeleza kuwa mahali pa wanawake ni jikoni ndani na uani- huko nyuma ya nyumba( 896). Sasa tena leo mbona mmekaa hapa(897 )? DEKA: Baba Tama, kukaa si kukaa tu, tuko hapahapa nyumbani kwani kuna ubaya gani(898 )? MADAHIRO: Nini( 899)? Hebu nieleze nisikie(900 ). Sasa hivi nataka muondoke hapa(901 ). Wanawake hukaa ndani siyo nje; nje ni mahali pa wanaume( 902). Je, chakula tayari?(903) MLAHAKA: Bado…..(904)Na tena mbona ndiyo…..kwanza unafika(905 )? MADAHIRO: Oh! (906 ) Nina kijisafari kidogo( 907). Vipi je maji ya kuoga yako tayari niende nikajimwagie kabisa( 908)? MADAHIRO: Kuna nini( 909)? Mbona mnaangaliana tu( 910). Hukusikia(911 )?nimekuuliza maji ya kuoga tayari(912 )? DEKA: Ah! (913 ) Hakuna( 914). Mbona….( 915) MADAHIRO: Ati nini(916 )? MLAHAKA: Hatukuteka(917). MADAHIRO: Hamkunini( 918)? MLAHAKA: Hatu…hatu..hatukuteka! ( 919) MADAHIRO: Nyama wee( 920). NASAA: Unamwonea tu, leo zamu yako kututambua nasi…( 921) MADAHIRO: Mnanichangia(922 )? Nitawavuruga wote….(923 )Nita…(924 )Nita… ( 925) MADAHIRO: Yalaaaa…yalaaa( 926).Njooni mtuamue jama…(927 )Tuamueni jama, NITAWAUA WAKE ZANGU( 928). Yalaa…(929 )Yalaa... (930 )Ah! (931 )Ninakufaa…( 932)NINAKUFA…( 933)Wananiua…(934 ) Yalaa…( 935) MANILA: Loh! (936)Wanawake balaa hawa; mnanipiga Mwanaume! (937 ) DEKA: Kha! ( 938)Amezidi babu! ( 939) MADAHIRO: Shenzi hawa…watanikoma…(940 ) NZOLE: Hebu tulizana kwanza Bwana Madahiro…( 941) MADAHIRO: Hapana…( 942)Hapana…(943 )Sitaki kusikia chochote(944 ). Nimekwisha waacha(945 ). Siyo wake zangu asilani(946). Waende makwao wanipishe hapa(947). NASAA: Subiri kwanza…( 948)Hapa sisi hatuondoki bila ya mpango…(949 )Lazima itafutwe sheria…(950 ) MADAHIRO: Sheria nyumbani kwangu(951 )? Sitaki lolote mie( 951). Ninyi siwataki katakata…wote watatu(952 ). Nitaoa mke mwingine mimi( 953). NASAA: Unalia nini wewe mpumbavu( 954)? Acha kulia…(955 ) TULI: Hivi yamekuwaje hasa(956 )? MADAHIRO: Yamekuwaje! (957 )? Huoni kama…kama…wamenichangia( 958)? Siwataki tena(959 ). Ondokeni sasa hivi! (960 ) 125 NASAA: Hatuondoki hapa bila ya mpango(961 ). MADAHIRO: Mpango wenyewe; NIMEWAFUKUZA! ( 962) NASAA: Siyo hivyo kienyeji tu, mambo yamebadilika siku hizi, ulikuwa wapi( 963)? Waulize wenzio…(964 ) NZOLE: Bi Nasaa sasa tuseme mnataka nini hasa( 965)? NASAA: Aitwe Balozi, Bwana Shamba, na Mwenyekiti wa Kijiji ili tuyazungumze…(966 ) NZOLE: Vizuri.(967)Tama, nenda kawaite, Balozi, Mwenyekiti wa Kijiji na Bwana Shamba(968 ). Waeleze kuwa, waje mara moja kumetokea tatizo huku(969 ). MADAHIRO: Na hao mnawaita wa kazi gani( 970)? Mimi nimekwisha toa uamuzi wangu basi, sitaki jingine tena(971). NZOLE: Hapana( 972).Hapa kuna mgogoro mkubwa( 973). Wewe umetoa uamuzi wako ndiyo, lakini wakezo hawataki kuondoka kienyeji bila ya kuyazungumza( 974). TULI: Hasa(975 ). Tujue yamekuwaje hasa(976 ). Maana sisi tumekuta ugomvi tu…(977 )Nanyi watoto hebu ongezeni viti tuketi na halafu ninyi muende mkachezee nje( 978). MANILA: Mimi naona miujiza kabisa( 979). Wanawake hawa laana kabisa…(980) NZOLE: Bwana Manila, tafadhali tulieni kwanza, tusikie hasa mkasa uliopo hapa( 981). NZOLE: Akina mama hebu tulizaneni kwanza tujue mambo yalivyo hapa…( 982) MADAHIRO: Waende tu. (983)Nani anawataka hapa( 984)? NZOLE: Bwana Madahiro tulizana kwanza, hebu nyote ketini kwanza…( 985) NZOLE: Enhe! (986 )Yamekuwaje hapa(987 )? NASAA: Kwa ufupi Mzee Nzole ni kwamba tumechoshwa na uonevu wa huyu Bwana wetu( 988). Hivyo ndivyo maana tukaamua leo nasi kujitetea( 989). TULI: Yaani mkaamua kumchangia Bwana wenu na kumpiga( 990)? DEKA: Kama mlivyoshuhudia wenyewe( 991). MANILA: Hebu kwanza. Ninyi mnasema kuwa mmechoka na uonevu(992 ). Ni uonevu gani(993 )? DEKA: Bwana wetu huyu(994 ). MADAHIRO: Akaa! (995 )Usiniite Bwana( 996). Ninyi siyo wake zangu tena( 997). NASAA: Hayo tutayajua baadaye vizuri( 998). Tunaeleza tu hali ilivyokuwa(999 ). DEKA: Kwa ufupi ni kwamba Baba Tama amezidi mno kutupiga, kututukana, kutusimanga, na kutunyanyasa utadhani tu watumwa! (1000 ) MANILA: Kwani ninyi hamjui kuwa yeye ni mme wenu hivyo mnapaswa kumheshimu(1001)? NASAA: Heshima gani anayostahili iwapo yeye hatuheshimu(1002)? Tunaambiwa kila mara maradioni kuwa binadamu wote ni sawa, na kwa Watanzania kila mtu anastahili heshima(1003). MANILA: Kumbe nanyi mnasikiliza upuuzi wa radioni kuhusu usawa wa wanawake(1004)? Usawa gani mnaoutaka(1005)? DEKA: Usawa kati ya mwanaume na mwanamke(1006 )! TULI: Ndiyo usawa gani huo(1007)? MANILA: Wapuuzi hawa Bwana(1008). Usawa gani zaidi wautakao zaidi ya ule 126 aliowapa Mwenyezi Mungu mwenyewe(1009)? TULI: Au ndiyo njama zao tena, za kuwatawala wanaume(1010). MANILA: Na hawawezi katu! (100)Mwanaume ni mwanaume tu siku zote(1011 ). Hata siku moja hatageuka kuwa mwanamke(1012). MADAHIRO: Na wewe! (1013) Umerudia nini tena humu ndani hali tumeachana siku nyingi(1014)? Kimekuleta nini humu(1015)? MAUJA: Nimekuja wachukua watoto wangu mbele ya Mwenyekiti(1016). MADAHIRO: Nani kasema(1017)? KIADA: Bwana Madahiro…tumekuja hapa kwa usuluhishi(1018). Nasi vile vile tunashughuli zetu, hivyo nakuomba utulizane…(1019 )Huyu mama Tama alikuja kangu na malalamiko kuwa…wacha tuketi kwanza. Basi unasikia bwana, Mama Tama ametulalamikia siku nyingi sana kuwa wewe, Madahiro, huwaruhusu wanae wakamwone mama yao huyu Bi Mauja tangu pale mlipoachana (1020 ). Sisi tumechunguza madai yake na kuona kuwa ni sawa kabisa(1021 ). Eee…kwa kuwa tunaamini kabisa kuwa mwanamke ana haki sawa na mwanaume juu ya wanae, leo hii tumeongozana naye aje awachukue wanae(1022). MADAHIRO: Nini(1023)? Watoto wangu hawatoki humu katu! (1024) MBOGO: Bwana Madahiro, keti usikilize(1025). Kujifanya mkali hakutakusaidia kitu(1026 ). Hebu keti kwanza(1027 ). KIADA: Eeee…( 1028)Sasa imetokea tu kuwa tulipokuwa njiani kuelekea huku…tumekutana na Bi. Tama njiani na ametueleza kuwa kulikuwa na ugomvi humu ndani…….( 1029) BONGO: Na hata hali yenyewe yaonyesha(1030 ). MANILA: Bwana Mwenyekiti, wacha nami niseme(1031). Hawa wanawake wabaya sana(1032). Tena wauwaji wakubwa! (1033)Sisi tulipokuja kuamua, tumekuta wanampiga Madahiro nusura ya kumwua…( 1034) KIADA, MAUJA, WAMBALI, BONGO: WAMEMPIGA(1035)? TULI: Nusu ya kumuua(1036 ). Kama tungalichelewa…(1037 ) MANILA: Wamemchangia wote watatu(1038). Wanawake wauaji hawa…( 1039) KIADA: Bwana Manila, tafadhali sana unaposema usiseme kwa hasira(1040). Hivyo hatuwezi kujenga kitu. Hebu keti kwanza(1041). KIADA: Bwana tunasikia kulikuwa kuna ugomvi hapa au sivyo(1042)? MADAHIRO: Wamenichangia na kunipiga vibaya sana(1043). Hivyo mimi siwataki tena wote watatu! (1044 ) Na sasa hivi nataka watoke nyumbani mwangu…sasa hivi…Sitaki kuwaona tena! (1045) NZOLE: Na ndiyo maana tumewaiteni ili mje kuwaamua, maana wakeze nao hawakutaka kuondoka tu bila ‘mipango’(1046). MANILA: Mipango gani waitakayo nao wamekwisha kuachika(1047 )? KIADA: Mmmmm... (1048 )Hebu na tuwasikilize nao wanasemaje(1049). Akina mama(1050 ); Je, ni kweli kwamba kumetokea ugomvi na mmempiga mme wenu(1051)? NASAA: Wazee wangu…( 1052)Ni kwamba mme wetu alizidi mno 127 kutuonea(1053). BONGO: Kuwaonea(1054 )? Uonevu wa aina gani(1055)? NASAA: Kututukana, kutunyanyasa, kutusumbua, masimango na kutupiga(1056 ). MAUJA: Ndiyo kazi yake huyu…( 1057)Eh! (1058) Tuliondoka hapa kwa sababu ya adha kubwa(1059). Kuna mengi hapa(1060). NASAA: Basi nasi leo tukaamua kujitetea(1061 ). Alipomwonea mmoja wetu, nasi tukajitetea(1062). BONGO: Ndiyo mkampiga au sivyo(1063 )? NASAA: Ndipo ulipotokea ugomvi, nasi tukajihami(1064). MADAHIRO: Na tangu sasa siwataki wote(1065 ). NASAA: Kwani nani nawe anakutaka (1066)? Unafikiri tunaweza tena kuishi nawe baada ya mambo haya Yaliyotokea (1067 )? Unafikiri nani atakaa tena aonewe(1068)? NZOLE: Ukweli wenyewe ni kwamba, itakuwa vigumu sana(1069). Kwani Bwana alikwisha zoea kuwaonea wakeze na sasa mambo yamebadilika watawezaje tena kuishi pamoja(1070)? Hawa wakeze wamekwisha tambua kuwa walikuwa wakionewa, na hakuna apendae kuonewa(1071). Na Bwana Madahiro kama wanaume tulivyo au binadamu wote kwa ujumla, inatuwia vigumu sana kubadili mienendo, tabia, au fikra zetu zilizokuwa zikitawala mawazo yetu kwa miaka mingi kwa mara moja tu(1072). Hivyo, ni vigumu kwa kweli wao kuendelea kuishi humu kama wake wa Bwana Madahiro, na kuelewana kwa urahisi(1073). DEKA: Kabisaa mimi nakwenda kwetu(1074 ). Labda Mlahaka ndiye atakayebakia hapa(1075). MLAHAKA: Hata na mimi……siwezi…kubaki…( 1076)Nakwenda kwetu(1077 ). NASAA: Na ndiyo maana tumewaiteni wazee maana tunataka haki zetu(1078 ). Sisi leo tumefukuzwa, lakini mali aliyonayo huyu bwana tumeichuma wote(1079). Hivyo tunataka haki tu-tuondoke hapa(1080). MADAHIRO: Muondoke hapa! (1081 )Mnafikiri nani atawaoweni tena(1082 )? Ninyi mkiondoka, mimi nitampata wa kuoa mara moja na ninyi mtampata wapi(1083 )? Mimi kwangu si kazi! (1084)Ninazo fedha za mahari za kutosha kuolea wake hata wawili! (1085) NASAA: Hayo ya kuolewa au kutoolewa ni mengine tena(1086). Mh! (1087)Huko kutoa kwenu mahari kunawafanya wanaume wengi sana mjione ninyi ni sawa zaidi kuliko wanawake(1088). Hivyo, kuna haja ya kulizungumza suala hili la mahari(1089 ). Kwa kupitia chama chetu cha wanawake, tutalijadili jambo hili na iwapo itabidi, tutapendekeza mahari isiwepo(1090). Itakapoondolewa, tutaona kama wanaume mtaandelea kuwagandamiza wanawake! (1091)Tena nakuaahidi Baba Tama, mimi nitokapo hapa, kazi yangu kubwa itakuwa kuwaelimisha watu juu ya suala hili zima la uhusiano kati ya mwanaume na mwanamke(1092 ). Tangu nilipokuwa shuile, tumeliongelea sana jambo hili- kuwa lazima tuwe sawa(1093). Lakini hayo ya baadaye (1094). Sasa hivi tunachotaka ni haki yetu tu, tujiondokee(1095). Mali iliyopo hapa hukuchuma peke yako(1096). KIADA: Wayaonaje mambo haya bwana Mwaikusa (1097)? 128 BONGO: Eee….(1098)Hali ilivyo ni kwamba, hawawezi kupatana(1099 ). Hivyo ni kufuata tu kanuni za kuachana(1100). KIADA: Vizuri (1101 ). Hivyo basi, akina mama, tumesikia mawazo yenu na kuyazingatia…( 1102)Eee…ni kwamba madai yenu ni sawa kabisa, nasi tumeyakubali(1103). Ninamuuliza Bwana Madahiro (1104); Je, unataka kuendelea kuishi na wakezo(1105)? Kwani kutengana si jambo zuri; isitoshe mtawachia taabu watoto wenu(1106 ). Je, unaonaje Bwana Madahiro (1107)? MADAHIRO: Nimekwisha sema kuwa mimi SIWATAKI TENA! (1108) Hivi mnataka niseme mara ngapi(1109)? SIWATAKI.(1110) Nimewaacha(1111 ). Nime…( 1112) KIADA: Je, nanyi akina mama (1113). Kumbukeni kuwa kuachana kunaleta uhasama mkubwa, ambao si jambo zuri(1114 ). Je, tuwapatanishe na mume wenu, muishi pamoja(1115)? NASAA: Haitawezekana (1116 ). DEKA: Yeye mwenyewe pia hatutaki (1117). Tutakalia hapa nini(1118)? MLAHAKA: Hata na mimi nakwenda kwetu tu(1119). Nimechoka(1120 ). KIADA: Vyema(1121 ). Hivyo basi ninyi akina mama mtaeende kulala kwa Balozi Ndugu, Bongo Mwaikusa, na kesho wataitwa wazee na wazazi wenu wote(1122 ). Vit vilivyomo humu ndani vyote, pamoja na mashamba na kila mali iliyopo mtagawanyishwa kwani nanyi pia mmefanya kazi(1123). MADAHIRO: Nini(1124)? Wachukue mashamba yangu(1125 )? Jamani! (1126 ) Si wizi huu wa mchana kabisa(1127 ). KIADA: Usipokubali hapa, mambo haya yatafikishwa mahakamani(1128). Na huko, haki itachunguzwa(1129 ). MLAHAKA: Na wanangu je(1130)? Naomba niende nao…baadaye watarudi(1131 ). KIADA: Sawa, utawachukua(1132). Mama watoto si wa mtu mmoja tu, ni watoto wenu wote sawasawa(1133). Pia Mauja, nawe umewajia wanao, pia utawachukua(1134). Nasi hatuna muda, mambo yote yatakwisha kesho(1135). Hivyo fanyeni twende(1136). MADAHIRO: Haiwezekani…(1137 )Haiweze…(1138) BONGO: Bwana Madahiro, hatuwezi kukaa hapa muda wote tukiusikiliza upumbavu wako(1139). Kama ndiyo hasira ya kupigwa na wakezo bora uitulize…( 1140) KIADA: Bwana Madahiro(1141 ). Tuachie kisirani(1142). Hebu keti kwanza(1143 ). MADAHIRO: Haiwezekani…haiwezekani…( 1144)Hivi ni nani kweli awezae kupokonywa wanae mwenyewe(1145)? NZOLE: Hakuna mtu wala mnyama, aliyepokonya(1146). Umetoka kuelezwa hapa sasa hivi kuwa watoto ni wenu wote…(1147) TULI: Ndiyo usawa wenyewe huu, wautakao wanawake wa kutunyang’anya watoto na mali zetu(1148)? MANILA: Bwana, hakuna cha usawa kati ya mume na mke(100). Hayo yote yatakwisha tu(1149 ). Unafikiri yatawafikisha (1150)… Wapi(1151)? 129 NZOLE: Jama, lazima tukubali kwamba mambo yanabadilika(1152). Sasa wanawake wanaanza kutambua kuwa wanaonewa, na kudhulumiwa na wanaume, hivyo wanataka usawa(1153). MANILA: Kama wanataka usawa hasa, basi nao washike mashoka waanze kukata miti kama wanaume, kubeba magogo, na kuchimba migodi(1154 ). TULI: Ndiyo(1155). Na wale wakaao mijini, wafanye kazi zote(1156). Kuwe na makuli wa kike, wavunja mawe, na wachimba barabara wa kike…( 1157)Kwa nini wasiyafanye hayo iwapo wanautaka usawa hasa(1158)? WAMBALI: Mimi nashindwa kukubaliana nanyi jama(1159 ). Kwanza, siyo wanaume wote wakaao mijini ni makuli au wachimba barabara(1160 ). Au kuwa wote wakaao shamba huchimba barabara (1161). kuna wanaume wengi wazururaji tu, wavivu kupindukia, na wazembe kushinda wanawake maradufu(1162). Hivyo mwanamke asipobeba gogo, sio kwamba usawa wake kati yake na mwanaume umetoweka (1163). Pili, kuna wanawake wengi siku hizi duniani wanaozifanya kazi hizo ulizitaja(1164 ). Hata humu mwetu’ huwaoni wanawake waliko katika Jeshi la Kujenga Taifa wakishika mashoka na kufanya kazi zote wafanyazo wanaume(1165)? Hivyo, kilicho wazi ni kwamba, tuukubali ukweli kwamba sisi wanaume, tunawaonea wanawake(1166). MADAHIRO: Tunawaonea(1167)? WAMBALI: Ndiyo(1168 ). Au niseme tunawanyima haki zao, na hatuwapi nafasi hata kidogo ya kuonyesha uwezo wao hivyo tunawagandamiza(1169 ). Hebu fikiri kidogo(1170). Kazi hizi za tumbaku mnafanya wote, lakini ni nani anayekwenda kuchukua fedha(1171 )? MANILA: Lazima awe ni Bwana(1172). WAMBALI: Kuna ulazima gani(1173)? Kwa nini asichukue mkeo(1174 )? Tena, isitoshe, kuna baadhi ya wanaume ambao wakishazipata tu pesa zenyewe hawaonekani nyumbani mpaka ziishe(1175). NZOLE: Kabisa(1176). Utaona Bwana analewa mpaka pesa zote zinakwisha(1177). Au ataoa mke mwingine akiwasahau kabisa watoto na wakeze ambao amefanya nao karibuni kazi zote(1178). Ndiyo usawa huu jamani(1179)? TULI: Bwana Nzole, acha habari za usawa kati ya mume na mke(1180). Hivi wewe hujasikia kuwa imethibitishwa na wataaalamu kuwa Ubongo wa mwanaume ni mzito kupita wa mwanamke(1181). Ndiyo maana akili zao ndogo huwa hawafikiri chochote wakikutwa na matatizo isipokuwa kulia(1182). NZOLE: Hata kama imethibitishwa kuwa ubongo wa mwanamke hauna uzito sawa na mwanaume, haimaanishi kuwa hawaweza kufikiri sawa na wanaume (1183). Wala haina maana kuwa mwanaume apate fursa ya kumwonea mwanamke(1185). Usawa unatakiwa…………… (1186 ) MANILA: Bwana Nzole, acha habari ya usawa kati ya mwanaume na mwanamke (1187). Haiwezekani hata kidogo(1188). Tazama Bwana, Mwenyezi Mungu mwenyewe, ameumba watu tofauti tofauti (1189 ). Ndiyo maana utaona mwanamke anachukua mimba na kuzaa(1190). Mama ameumbwa ili alee watoto na kufanya kazi za nyumbani na ndiyo maana hawezi kuwa na nguvu sawa na mwanaume(1191). 130 NZOLE: Kule kuumbwa kwao na Mungu wawe hivyo, yaani kuchukua mimba, haina maana muwaonee na kuwatesa(1192). Eh, tena nguvu wanazo Bwana wee(1193). Hamkuona jinsi walivyomdunda sasa hivi Bwana Madahiro(1194)? TULI: Wamemchangia(1195 ). MADAHIRO: Ndiyo(1196). Wamenichangia(1197). Wanawake watatu, mwanaume mmoja! (1198)Wao si sawa na mwanaume Bwana(1199). WAMBALI: Na sasa ndiyo wanautaka(1200). Waondoe unyonge walio nao wawe sawa na mume! (1201) MANILA: Hawawezi katu! (1202 ) Wao wenyewe wanajifahamu kuwa wako chini ya mwanaume(1203). Ndiyo maana sisi huwatongoza wanawake(1204). Kwa nini mwanamke asimtongoze mwanaume na kumhonga (1205)? TULI: Au kumuoa kabisa(1206). Sijasikia hata siku moja, mwanamke akimtolea mahari mwanaume na kumwoa(1207 ). Kama wanautaka usawa, basi watuchumbie na kutuoa(1208). MADAHIRO: Loh! (1209 ) Na ukiolewa na mwanamke ujue ndiyo umekuwa mtumwa wake(1210). WAMBALI: Ahaa……….( 1211).Ndiyo unataka kusema kuwa mahari watoayo wanaume ndiyo inakuwa chanzo cha kuwatawala nyumbani na kuwaonea! (1212) Unakuwa kama vile umenunua shati au sivyo(1213)? Hata hivyo, mimi mwenyewe jambo hili linanikanganya(1214). Hivi sasa hakuna dini zinazosisitiza utoaji wa mahari katika sheria ya ndoa zao(1215). Hivyo, iwapo itaamuliwa mahari itolewe, baadhi yao hawatalifanya hili liwe tatizo(1216)? Isitoshe, ile kawaida ya kuwa mwanamke asiyetolewa mahari, basi si mke bali kimada, inawafanya wanaume wengi na hata wanawake wenzao wawaone wenzao duni(1217 ). Lakini kawaida hii tukiibadili iwe na sura mpya na watu waikubali, basi mambo yatajirekebisha (1218). Heshima ambalo ni jambo muhimu, itakuwepo kama kawaida(1219). Ingawa mimi sijafikia uamuzi akilini mwangu juu ya suala hili, nionavyo ni kuwa wakati umeshapita wa kumwita, ati Malaya, mwanamke ambaye amewekwa kimada (1220). Kwa nini asitambuliwe kama mke na kupewa heshima anayostahili(1221)? Tatizo la mahari ndilo linatufanya wengi wetu tusione mapema au tushindwe kuoa kabisa(1222 ). Maana mahari imekuwa juu sana kupita kiasi kutokana na tama za wazazi wetu za kutaka kujipatia fedha(1223). Hali hii inawafanya baadhi ya wale wanaomudu wajione kuwa wao wana haki zaidi kwa wake waliowatolea mahari hiyo(1224). Hivyo, huwaonea wake zao na kuwafanya watakavyo(1225). TULI: Siyo uonevu(1226). Kuoneana kunategemea na mtu mwenyewe alivyo(1227 ). Siyo kwa sababu ya mahari(1228). Mimi, nimemwoa mke wangu sikumnunua; yeye siyo mtumwa! (1229) Ni uongozi tu ndani ya nyumba(1230). Lazima awepo nyumbani mwenye neno la mwisho ingawa mtafanya majadiliano wewe na mkeo(1231). Mkikalia ubishi tu, hamtajenga lolote lile! (1232 ) WAMBALI: Kwa nini yeye asitoe neno la mwisho(1233)? MANILA: Ujue umetawaliwa na mkeo Bwana wee(1234). Ataenda anajitapa kila 131 nyumba kuwa ‘Bwana wangu hafui dafu………………..!’ (1235) Hivyo mume kwa vyovyote vile, lazima atoe uamuzi wa mwisho(1236). TULI: Kama vile vile unaona mawazo yake yanafaa, basi huna budi kuyafuata(1237). Na wakati mwingine wowote, unaweza kumsikiliza na kumfuata(1238). Maana mkiwa ndani mambo ni kushauriana, lakini siyo ubishi usiokuwa na msingi wowote! (1239) NZOLE: Basi ndiyo tuwape usawa jama, kwani walikuwa wamelala, sasa wanaanza kuamka(1240). Tusipowapa haki kwa hiari, wataipata kutoka kwetu kwa nguvu(1241). Hivyo, majumbani mwenu muwe na usawa jama(1242). TULI: Usawa gani zaidi Sheikh Nzole(1243 )? Unataka mwanaume naye awe anapika chakula(1244)? MANILA: Na kuwaosha watoto na kuwabeba(1245)? MADAHIRO: Au kufagia na kutandika kitanda(1246)? MANILA: Na kuanza kutumwatumwa na mkewe(1247)? TULI: Mwishowe basi wake zetu watatupangia ratiba ya kupika kwa zamu, kuwatawaza watoto wakienda haja na kuwanyonyesha wakilia(1248)? MANILA: Ha! (1249) Ha! (1250)Ha! (1251)Kitakuwa kichekesho kweli Bwana Wambali nije nyumbani kwako, nakukuta umeshughulika jikoni unapika ugali na mkeo hali siyo mgonjwa wala kuwa na udhuru wowote ule, amekaa juu ya kochi anatingisha mguu, anasikiliza radio au santuri na gazeti mkononi anasubiri ugali unaompikia! (1252) NZOLE: Kwani kuna ubaya gani(1253 )? WAMBALI: Siyo hivyo tena Bwana wee. Kuna kazi za kiume na kike(1254 ). Yatakuwa mambo yamekithiri tena, loh! (1255) TULI: Si ndivyo unavyotaka wewe? Kufuru wafanyazo wanawake wa siku hizi za kuvaa nguo za mabwana zao kama mke wa Manga Mbagha- kwako sawa! (1256) NZOLE: Hayo tena msemayo ni mengine(1257 ). Nayo yanategemea mazingira yanavyobadilika, kutokana na nyakati tofautitofauti(1258 ). Mimi nimesikiliza sana radioni juu ya mjadala wa suala hili na nimeongea na watu wengi(1259). Na katika kubadilishana mawazo huko, nimepata ukweli mmoja kwamba ingawa wengi wetu hatukubali, lakini ukweli unabaki pale pale kwamba kwa mtu yeyote anayethamini na kuamini usawa wa binadamu kikweli, atakubaliana nami kwamba, wanawake hawana usawa huo(1260 ). Ukiangalia kwa jicho la akili, bila ya kuupendelea upande wowote, utaona jinsi wanavyoonewa, wanavyogandamizwa, kunyanyaswa na kudharauliwa(1262 ). Tuchukulie mfano kidogo-kazi za nyumbani ambazo Ndugu Manila amezitaja(1261). Kwa nini tuseme kama aliyosema hapa mwenzangu Wambali kuwa kuna kazi za kiume na kazi za kike(1263)? Kwa nini uwepo mbaguano huo(1264)? Kwa nini tusifanye kazi kutokana na uwezo wa mtu binafsi(1265)? Kwani si ukweli kwamba sote kazi hizo tunaweza kuzifanya(1266)? Kwa nini mtokapo shamba au kazini popote wewe na mkeo hali wote mkiwa mmechoka, umuachie yeye tu kazi za kuteka maji, kuwaosha watoto, kuwabeba, kupika, kuosha vyombo na usafi mwingine 132 wa nyumbani(1267 )? Kwa nini msisaidiane(1268)? Kwa nini wawe waandalizi wetu wa chakula, kutuchemshia maji ya kuoga na kuwatumatuma vitu vidogovidogo wao tu(1269)? Kwa nini tuseme mahali pao ni jikoni(1270 )? Msicheke, nayowaambiaeni siyo utani, na hilo ni jambo moja tu miongoni mwa mengi tuyatendayo tukiwafanya wawe duni kwetu, wasiwe na usawa(1271 ). La muhimu ni kwamba, wanawake ni binadamu(1272). Hivyo basi wanahitaji usawa kama binadamu wengine, siyo kuwagandamiza na kuwafanya wanyonge(1273). MANILA: Unyonge huo wajipa wenyewe kwani hawawezi kazi za kiume(1274). NZOLE: Kweli kabisa kwamba wanawake walio wengi hawajiamini kuwa wao wana uwezo wa kufanya lolote lile; kutokana na mazoezi ya unyonge(1275). Hili ni tatizo kubwa katika kuleta ‘usawa’ ila watakapojiamini, mambo yatabadilika kwa haraka sana(1276). Mfano; zamani mwanamke alikuwa haendeshi gari au kuwa askari. Walipoanza kujiamini tu, sasa tunao madereva na askari wa kike chungu nzima(1277 ). Hivyo kama wakijiamini, na kupata nafasi, waweza kujiendeleza sana(1278). WAMBALI: Tatizo jingine ni tabia kijamii(1279 ). Tangu utotoni, mtoto wa kike anawekwa katika hali ya uke hasa, na kufanywa amtumikie kaka yake(1280). Na mtoto wa kiume naye anaiga mfano wa baba yake(1281). Hivyo wakikua wanakua na kasumba hiyo, inakuwa vigumu sana kubadili mienendo hii waliyozoweshwa na wahenga(1282). NZOLE: Hata hiyo, wanawake wanaanza kutambua hali hiyo na kudai UKOMBOZI. Tutake au tusitake, itatubidi tuyakubali mabadiliko, na kuwapa usawa wautakao, au sivyo zitakuwa hadithi za akina Madahiro(1283). MADAHIRO: Mimi najuta sana kwa kuadhiriwa kiasi hiki na wake zangu(1284). Isitoshe wamewachukua na watoto! (1285 ) Bado sijaridhika(1286). Kesho tutayaongea(1287). Sasa, hivi wameniacha(1288). Ndiyo WAMEJIKOMBOA (1289) hivyo(1290 )? Wamepata nini hasa wanaume hawapendi kutawaliwa na wake zao(1291). Hivyo hawataolewa na mwisho wataanza kutufuata tena waume zao(1292 ). Hakuna lolote la usawa au kujikomboa! (1293) NZOLE: Hawatarudi kamwe…………………………….( 1294) MANILA: Watarudu tu hao…………………(1295) WAMBALI: Hawarudi! (1296 ) MADAHIRO: Watarudi tu! (1297 )Tena kesho ananirudia Mlahaka(1298). Mimi najua jinsi ya kuwaendesha wanawake! (1299) NZOLE: Hawarudi nakwambia WAMEJIKOMBOA(1300). Lazima tubadili mawazo na mienendo yetu(1301). MADAHIRO: Ukombozi gani(1302)? WATARUDI TU!(1303) Utaona………. (1304 ) 133
Powered by Blogger.