Ngano Katika Fasihi Simulizi

Hadithi (ngano) ni utungo wenye visa vya kubuni unaosimuliwa kwa lugha nathari kwa kusudi la kuburudisha, kukuza maadili na kuunganisha jamii. Msimulizi wa hadithi huitwa Fanani au Mtambaji.

Vipera vya Ngano

Tunaweza kuainisha ngano kulingana na vipengele vifuatavyo:
  1. Wahusika => k.v khurafa, hekaya, mighani, mazimwi,
  2. Maudhui => k.v usuli, visasili, mtanziko
Utanzu huu wa fasihi simulizi umegawanyika katika vipera (aina) kadhaa:
AINAMAELEZO KWA UFUPI
Khurafahadithi ambazo wahusika ni wanyama.
Hekayamhusika mmoja (k.v sungura) huwa mjanja kuliko wenzake
Usuli (Visaviini)huelezea chanzo cha jambo au hali fulani
Visasilihuelezea asili au chimbuko la jamii au mambo ya kiada k.v mauti, ndoa, tohara n.k.
Maghani (Visakale)hadithi za mashujaa
Mazimwihuwa na wahusika majitu au mazimwi
Mtanzikohumwacha mhusika katika hali ya kutojua chaguo linalofaa. Kila achagualo lina matukio mabaya.

Sifa za Ngano

  1. Huwa na mianzo maalumu
    • Paukwa! Pakawa!
    • "Hadithi! Hadithi!" - "Hadithi Njoo!"
    • Hapo zamani za kale...
  2. Huwa na miishio maalum
    • Hadithi yangu yaishia papo!
    • ...wakaishi kwa raha mustarehe.
  3. Huwa na funzo fulani ambalo aghalabu hutajwa mwishoni mwa hadithi.
  4. Masimulizi yake huwa kwa wakati uliopita
  5. Husimuliwa kwa lugha ya natharia
  6. Huwa na wahusika ambao wanaweza kuwa binadamu, wanyama, miungu, mashetani au vitu visivyo hai
  7. Huhusisha mbinu nyingine za fasihi simulizi kama vile
    • Nyimbo - kuburudisha, kuamsha hadhira, kupitisha ujumbe
    • Methali - kutoa funzo
    • Misemo - kupamba lugha
    • Vitendawili na mafumbo - kushirikisha hadhira katika masimulizi
  8. Hutumia mbinu ya takriri ili kusisitiza ujumbe kwa kurudiarudia maneno, matukio au nyimbo
  9. Hutumia tamathali za lugha kama vile tashbihi, tashihisi, chuku, tanakali za sauti ili kupamba masimulizi n.k
  10. Huwa na muundo rahisi wenye mwanzo, kati na mwisho.
  11. Ufanisi wake hutegemea mbinu za mtambaji k.v ishara-uso na ubunifu wake jukwaani.
  12. Sehemu fulani zinaweza kubadilishwa kulingana na hadhira

Umuhimu wa Ngano

  1. Kuhifadhi au kurithisha mali ya jamii
  2. Kuunganisha na kukuza ushirikiano miongoni mwa jamii
  3. Kuelemisha au kutoa mafunzo kuhusu mambo fulani
  4. Kukuza maadili mema
  5. Kuonya, kuelekeza, kuhimiza na kunasihi
  6. Kuburudisha hadhira. Hadithi nyingi huwa na visa vya kusisimua na kuburudisha.
  7. Kupitisha muda haswa watoto wanaposubiri chakula kiive

Sifa za Mtambaji wa Hadithi

Msimulizi wa hadithi pia huitwa mtambajifanani au mganaji.
  • Huwa mchangamfu na mcheshi kwa hadhira yake ili kuwafanya wapendezwe na hadithi
  • Anafahamu utamaduni wa jamii yake.
  • Anaifahamu hadhira yake vizuri na kusimulia kulingana na mapendeleo yao. wasichana au wavulana? vijana au wazee?
  • Huwa na uwezo wa ufaraguni - uwezo wa kubadilisha sehemu fulani za sanaa bila kujifunga na muundo asilia.
  • Mwenye kumbukumbu nzuri - uwezo wa kukumbuka
  • Mwenye uwezo wa kuigiza kwa kutumia viungo vyake, uso (ishara-uso) na sauti(kiimbo)
  • Mwenye uwezo wa kujenga taharuki kwa kusita kidogo ili kuvuta nadhari ya hadhira yake.
  • Hushirikisha hadhira yake katika nyimbo n.k
  • Mlumbi hodari na mkwasi wa lugha.
Powered by Blogger.