VITABU MBALIMBALI

 





MAISHA YA UJANA,UTAKATIFU, CHANGAMOTO ZA KARNE YA 21 NA UTIMILIFU WA DALILI  ZA UJIO WA MASIHI

  UJANA

Ujana ni kipindi kati ya utoto na utu uzima.Unaanzia miaka 18 hadi miaka 40.Unaelezwa kama ni kipind cha maendeleo ya kimwili na kisaikolojia kuanzia mwanzo wa kubalehe kwa ukomavu na mwanzoni mwa utu uzima.Ukomavu wa mtu binafsi huenda unakosa kuwa sawa na umri wao kwani watu wasiokomaa hupatikana kwa umri wowote.

Kwa ujumla ujana unahusu wakati wa maisha ambao si utoto wala utu uzima lakini mahali fulani kati.Hiki ni kipindi  ambacho mtu anakuwa na nguvu ya kufanya jambo lolote.Kundi hili  ndilo linalotegemewa sana katika  kufanya kazi ya Mungu na ujenzi wa taifa kwa ujumla.

     1yohana 2:13-15 anasema ‘’Nawaandikia ninyi vijana kwasababu mmemshinda yule mwovu,Nimewaandikia ninyi vijana kwasababu mna nguvu na neno la Mungu linakaa ndani yenu nanyi mmemshinda yule mwovu’’.

            UTAKATIFU

Ni kuishi maisha mbali na dhambi au ni hali ya kujitenga na dhambi yaani ni hali ya kuwa mkamilifu.Hili ni agizo ambalo Mungu alitupatia kuwa tuishi maisha matakatifu kama yeye alivyo.

‘’Basi ninyi mtakuwa wakamilifukama baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”   [Mathayo 5:48]

    MAMBO YA KUFANYA ILI UWE MTAKATIFU

{1}Kuacha dhambi au kuzaliwa mara ya pili

Ili uwe mtakatifu ni lazima uache dhambi  kwani roho mtakatifu hakai mahali pachafu na Mungu hapendi michanganyo hivyo ni vyema kujitakasa na kuwa safi na bila hivyo huwezi kuuridhi  ufalme wa milele.

‘’…mtu asipozaliwa mara ya pili hawezi kuuona ufalme wa Mungu ………………..mtu asipozaliwa kwa maji  na kwa roho hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu [Yohana 3:1-6]

{2}Kusamehe ni hali ya kumhurumia au kumfutia makosa  mtu yeyote aliyekukosea bila kujali umri,kabila,rika,taifa wala ukubwa wa kosa alilokukosea kwani bila kusamehe na Mungu hawezi kukusamehe wewe pia.

‘’Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao na baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi,Bali msipo wasamehe watu makosa ya o wala baba yenu hatawasamehe  ninyi makosa yenu’’[ Mathayo 6:14]

{3}Kutoa sadaka

Ni hali ya kumtolea mungu kwa vile ulivyojaliwa Sadaka inaweza kuwa pesa,zao kama mahindi,maharage,kadri Mungu alivyokujalia.Tangu mwanzo kabisa watu walionyesha shukrani yao na kujitoa kwa Mungu kwa njia ya kumtolea sadaka.Katika sadaka nyingine za shukrani mtu alimtolea Mungu sehemu za nafaka zake au mifugo ile iliyo bora.’’Nuhu akamjengea BWANA madhabahu;akamtwaa katika kila mnyama aliye safi na katika kila ndege aliyesafi,akavitoa sadaka za kuteketezwa  juu ya madhabahu’’[mwanzo 8:20]

Wengine walionyesha ushirikiano mwema na Mungu na wanadamu wenzao,ambapo mtoaji alikula sehemu ya sadaka yake katika karamu pamoja na jamaa na marafiki.’’Yakobo akachinja sadaka katika mlima akawaita ndugu zake waje wale chakula,nao wakala chakula wakakaa usiku kucha mlimani’’[Mwanzo 31:54]

Sadaka nyingine ilikuwa kwaajili ya msamaha wa dhambi,ambapo mnyama aliyechinjwa alichukua adhabu ya mtoaji.’’Basi sasa,jitwalieni ng’ombe waume saba,na kondoo waume saba,mkamwendee mtumishi wangu ayubu,mjisingezee sadaka ya kuteketezwa;na huyo mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi;kwa kuwa nitamridhia yeye,nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu;kwani ninyi hamkunena maneno yaliyonyoka katika habari zangu kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu’’[Ayubu 42:8]

Lakini  Wakati wa agano la kale wapo watu ambao walimtolea Mungu sadaka bila kuhubiriwa bali walimsikiliza roho wa Mungu alipowaambia wafanye hivyo basi walifanya.mfano Kaini na habili[mwanzo 4:4-15] ,Ibrahim alimtoa mwanaye isaka kuwa sadaka bila kuteketezwa bila kuhubiriwa na mtu yeyote bali alimsikiliza roho wa Mungu alivyomwongoza[waebrania 11:17-18]

              Mipango ya sadaka za Israel ilikuwa ya aina kubwa tano  ingawa zilitofautiana lakini sadaka kuu zilikuwa ni zile za kuteketezwa.Sadaka hizi ziliitwa sadaka za kuteketezwa kwasababu wanyama wote waliteketezwa juu ya madhabahu,

Sadaka ya kuteketezwa ilitolewa kwaajili ya taifa zima na ilichochewa na kuteketea juu ya madhabahu  wakati wote pasipo kukoma ikiwa na maana ya kujitoa kwa Mungu bila kukoma’’Basi sadaka utakazozitoa juu ya madhabahu ni hizi;wanakondoo wa mwaka mmoja wawili siku baada ya siku daima,mwanakondoo mmoja utamchija asubuhi;na  mwanakondoo wa pili utamchinja jioni…………….’’[kutoka 29:38-42]

Sadaka ya unga pamoja na sadaka ya divai[au ya kinywaji]iliyounganika ilionyesha shukrani kwa Mungu kwaajili ya chakula cha kila siku kilichotoka kwake.Sadaka ya unga na divai haikutolewa peke yake bali siku zote ilitolewapamoja na sadaka za kuteketezwa au za amani.Divai ilimiminwa juu ya sadaka ya mnyama iliyokuwepo juu ya madhabahu,na mkono mmoja wa unga uliteketezwa pamoja nayo.’’Na sadaka ya unga itakuwa sehemu ya kumi na mbili za efa za unga mwembamba  uliochanganywa na mafuta,ni kafara ilisongezwa kwa BWANA kwa moto kuwa harufu ya kupendeza;na sadaka yake ya kinywaji itakuwa ni divai,robo ya hini’’[Lawi 23:13]

 Sadaka ya amani ilionyesha ushirika na uhusiano mwema,yaani jambo lilionyeshwa katika karamu iliyofuatana nayo.Baada ya sherehe ya damu mwanzoni,sherehe ya kuteketeza sehemu yake na  kutoa sehemu yake kwa kuhani,mtoaji alishirikiana na familia yake ,marafiki zake na watu wenye dhiki au maskini akla mabaki ya mnyama katika karamu ya furaha.’’……………….na hiyo nyama ya sadaka zake za amani zilizochinjwa kwaajili ya shukrani italiwa siku iyo hiyo ya matoleo yake ,asisaze yoyote hata asubuhi………….’’[Lawi 7:13-15]

 Sadaka ya dhambi,hii ni sadaka iliyokuwa inatolewa kwa mtu yeyote ambaye amejitambua kuwa amevunja sheria mojawapo ya Mungu.Kama kwa dhambi za makuhani walinyunyiza damu ya mnyama ndani ya mahali patakatifu,wakateketeza vipande vingine vya nyama katika madhabahu na mabaki wakachoma nje ya kambi na kama dhambi ilikuwa ya raia binafsi,makuhani walinyunyizadamu katika madhahabu wakateketeza vipande  vingine juu ya madhahabu hiyo na kula vipande vilivyobaki.’’Na mtu awaye yote katika watu wan chi akifanya dhambi pasipo kukusudia,kwa kufanya neno lolote katika hayo ambayo Bwana alizuilia yasifanywe,naye akapata hatia,atapojulishwa hiyo dhambi yake aliyoifanya ,ndipo atakapoleta mbuzi mke mkamilifu,awe matoleo yake  kwaajili ya dhambi yake aliyoifanya……..’’[Lawi 4:27-29]

 

AINA ZA SADAKA KATIKA KIPINDI HIKI CHA AGANO JIPYA HADI SASA

{A}Sadaka ya malimbuko

Sadaka hii ni zao la kwanza la kazi ya mikono yako mfano kama ni mazao basi mazao ya kwanza kabla ya kuanza kuyatumia,kazi ya sadaka hii ni  Kumheshimu Mungu kwa vile alivyokujalia.”Mheshimu BWANA kwa mali yako,na malimbuko ya mazao yako yote,Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi …………………….’’ [Mithali3:9-10 ]‘’ ‘’Atoaye dhabihu za kushukuru ndiye anayenitukuza’’ Katika kipindi hiki cha agano jipya kuna aina nyingi  za sadaka.’’ [Zaburi 50:23]

{B} Zaka{fungu la kumi}

Sadaka hii ni asilimia  10 au moja ya kumi au shemu moja ya Baraka aliyokupa Mungu.Zaka ilianza zamani sana kabla ya  MUNGU hajaweka sheria ya watu kutoa zaka,Wako watu waliompenda MUNGU kwa mioyo yao walimtolea zaka bila kulazimishwa wala kuhubiriwa ila walitoa kwa moyo.

‘’Leteni zaka kamili ghalani ili kiwemo chakula  katika nyumba yangu ,mkanijaribu kwa njia hiyo asema BWANA wa majeshi:mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni Baraka,hata isiwepo nafasi ya kutosha au la’’ [Malaki 3:10]

{C}Sadaka ya Nadhiri

Ni sadaka ya patano na MUNGU.Hii hutolewa kipindi mtu anapokuwa katika tatizo na anaahidi zawadi endapo atatekelezewa.

‘’Na mkaanani,mfalme wa  Aradi,aliyeketi upande wa Negebu,alisikia kuwa Israel amekuja kwa njia ya Atharim;bas akapigana na Israel na watu kadhaa wa kadhaa miongoni mwao akawateka ,Basi Israel akaweka Nadhiri kwa BWANA  Akasema;Kama wewe utawatia watu hawa mikononi mwangu kweli,ndipo mimi nitaiharibumiji yao kabisa,Basi bwana akasikiza sauti ya Israel……………’’[ Hesabu 21:1-3]

{D}Sadaka  ya Hiari au ya kawaida

Hutegemea mguso na msukumo wa ndani kutoka kwa MUNGU.Sadaka hii haina kiwango maalumu bali hutegemea mguso wa roho mtakatifu ndani ya mtu binafsi.

‘’Na hii itakuwa haki ya makuhani kwa watu hao wasongezao sadaka ikiwa ni ng’ombe  au kondoo wampe kuhani………………..’’[ Mwanzo 18:3-]

‘’Maana kama ipo hukubaliwa kwa kadri  ya alivyo navyo mtu si kwa kadri ya asivyo navyo’’[2Wakorintho 8:12]

{E}Sadaka ya shukrani

Hutolewa wakati wa ushindi,kubarikiwa na hata kuwa mzima.Mara nyingi Sadaka hii huambatana na Ushuhuda Fulani kutoka kwa mtoaji.

     ‘’Naye Haruni atawasongeza walawi mbele za BWANA  wawe sadaka ya kutakaswa,kwaajili ya wana wa Israel  ili wawe wenye kufanya utumishi wa BWANA……………………………umtoe mmoja kuwa sadaka ya dhambi kwa BWANA na huyo wa pili awe sadaka kuteketezwa ,ili kufanya upatanisho kwaajili ya walawi’’ [Hesabu 8:11]

NAFASI YA SADAKA MBELE ZA MUNGU

{A}Sadaka inafanya MUNGU atume malaika zake wakupiganie.

‘’Apandaye haba atavuna haba,maana utumishi wa huduma hiihauwatimizii wafatakatifu riziki walizopungukiwa tu bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani apewazo MUNGU’’[2Wakorintho 9:6-11]

{B}Sadaka zinatoa nafasi kwa MUNGU awe na sauti juu ya vitu.

 ‘’Kwa imani Habili alimtolea MUNGU dhabihu iliyo bora kuliko kaini kwa hiyo alishuhudiwa kuwa ana haki ;MUNGU akazishuhudia sadaka zake na kwa hiyo ijapokuwa amekufa angali akinena[ Waebrania 11:4].

{C}Sadaka inatoa nafasi ya kubarikiwa

 ‘’Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi tena nimejaa tele;nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vilivyotoka kwenu,harufu ya manukato ,sadaka yenye kibali,impendezayo MUNGU ,Na MUNGU wangu atawajazeni kila mnacho hitaji kwa kadri ya utajiri wake,katika utukufu,ndani ya kristo Yesu. [Wafilip 4:18-19]

{4}Uongozwe na roho mtakatifu

‘’Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu roho mtakatifu;nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalem na katika Uyahudi wote na samaria na hata mwisho wa nchi’’ [Matendo 1:8]

‘’……..kwasababu ya dhambi aliihukumu dhambi katika mwili ,ili maagizo ya torati  yatimizwe ndani yetu  sisi tusioenenda kwa kufuata mambo ya mwili bali mambo ya roho.’’[ Warumi 8:1-11]

                    UTANDAWAZI

Mtumizi ya neno UTANDAWAZI yalianzia miaka ya 1990.Neno utandawazi lina maana nyingi kutegemeananu matumizi yanayokusudiwa.                                                                                                                                                                                                           K wa maana ya kawaida utandawazi ni mfumo wa kuifanya dunia iwe kama kijiji kimoja kwa mfumo wa teknolojia ya mwasiliano,mtandao siasa,uchumi na utamaduni.

         KIBIBLIA UTANDAWAZI

Ni harakati za mfumo mpya wa kidunia ambao na Mpinga kristo unaowezesha watu wa dunia kuwa na uchumi mmoja,dini moja raisi mmoja na teknolojia moja.” Naye awanyaye wadogo kwa wakubwa na matajiri kwa maskini na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wa kuumeau katika vipaji vya nyuso zao, tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa ana chapa ile,yaani  jina la mnyama yuleau hesabu ya jina lak. Hapo ndipo penye hekim, yeye aliye na akili na aihesabu ya mnyama huyo, maana ni hesabu ya kibinadamu na hesabu yake ni mia sita sitini na sita”[ Ufunuo 13:16-18 ]  

Kulingana na maandiko utandawazi ulipo leo ni mandalizi tu ya mfumo wa wazi wa Mpinga kristo” Na  sasa lizuialo mwaliju, Yule apate kufunuliwa wakati wake maana ile siri ya kuasi hivi sasa  inatenda kaz,lakini yupo azuiaye sasa, hata atakapoondolewa, hapo ndipo atakapofunuliwa Yule asi ambaye Bwana Yesu atamua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo  kwake, Yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake shetani, kwa uwezo wote na ishara na ajabu za uongo na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea, kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli wapate kuokolewa”[2 Thesalonike 2:6-10]

Kuna dalili nyingi zinazojitokeza kudhibitisha ujio wa kumpinga kristo kea uwazi. Baadhi ya dalili hizo ni kuongezeka kwa maarifa ya utendaji isiyo ya kawaida ya binadamu” Lakini wewe ee Daniel yafunge maneno haya ukakitie mhuri kitabu, hata wakati wa mwisho , wengi wataenda mbio huko na hukon na maarifa yataongezeka” [ Daniel 12:4]

Karne ya mwishoni mwa karne ya 20 na mwanzoni mwa karne hii ya 21 (sasa) ni kipindi kumekuwepo na mnibuko mkubwa wa maendeleo ya teknolojia ya sayansi kama vile matumizi ya kitabu cha nyuso (facebook), Twitter,Ebuddy n.k. mabadiliko haya yameiathiri jamii hasa vijana kimwili na kiroho moja kwa moja

ATHARI ZA UTANDAWAZI KTK MAISHA YA KIROHO

1.      Kumzimisha roho mtakatifu au kupoteza nguvu ya kiroho                                                                                                                              Kuna mungu mmoja tu, na mungu huyo siku zote yupo katika utatu wa Baba, mwana na roho mtakatifu. Kwa hiyo ufahamu wa mwanadamu kuhusu roho mtakatifu umeunganishwa na ufahamu wake wa utata, na huo tena umeunganishwa na maisha na huduma ya yesu kristo. Na ufunuo wake ulifikia kilele chake katika yesu kristo.

 

ROHO MTAKATIFU WAKATI WA AGANO LA KALE                                                                                                                                                          Watu wa wakati wa agano la kale walipooana dalili maalumu za nguvu na uwezo wa mungu waliita nguvu hiyo wakitumia neno la kiebrania la “ruach”Neno hili liitumiwa katika lugha ya kila siku pasipo uhusiano wa pekee na “mungu” nalo liliweza kuwa na maana ya upepo                                                                                                                  Anasema “ Ikawa muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikanyesha mvua nyingi. Ahabu akapanda garini akaenda zake yazreeli” pia neno ( ruach) lilikuwa na maana ya” pumzi” au roho (katika maana ya maisha na hisia  za mtu                    [1Wafalme18:45)                                                                                                                             “Wakamwambia maneno yote ya yusufu  aliyowaambia na alipoona  magari aliyoyapeleka  yusufu, ilikumchukua, roho ya yakobo baba ikafufuka.[ Mwanzo 45:27].                                                                                                                      

          Katika kuhusianisha na mungu neno “ruach” liliweza kuwa na maana ya upepo ambaomungu aliutumumia ili kuongeza maendeleo ya hali ya ulimwengu

Anasema “Na mungu akamkumbuka Nuhu na kila kilicho hai na wanyama wote waliokuwa pamoja naye katika safana, Mungu akavumisha upepo juu ya nchi, maji yakapungua, chemichemi za vilindi zikafungwa [Mwanzo 8:1].                                 ‘’Bwana akageuza upepo wa magharibi wenye nguvu nyingi ambao uliwaondoa wale nzinge na kuwapeleka katika bahari ya sham, hakusalia hata nzinge hata mmoja ndani ya mipaka ya misri   Na vilevile “ruach” ilikuwa na maana ya “pumzi ya pua au kinywa” cha Mungu ambayo kwa njia yake alifanya mambo makuu au ya roho wake ambayekwa njia yake alikuwa na nguvu, matendo  na hisia za kiumbe hai.[ Kutoka  10:19]  

        “Kwa neno la Bwana mbingu zilifanyika, na jeshi lake lote kwa pumzi ya kuinywa chake” [Zaburi 33:6]

“Ndipo ilipoenekana mikondo ya maji, misingi ya ulimwengu  ikafichuliwa ee  Bwana, kwa kukemea kwako kwa mavuno ya pumzi ya puani  mwako”[ Zaburi 18:15]

       Katika matukio maalumu roho huyo wa mungu (au nguvu ya mungu ) alikuja juu ya watu walioteuliwa kwaajili ya makusudi maalumu

“Roho ya Bwana ikamjilia juu yake, nawe akawa mwamuzi wa Israel, akatoka kwenda vitani “[Waamuzi  3: 10]

“ Akajibu akaniambia akasema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, si kwa nguvu, bali ni kwa roho yenuasema Bwana wa majeshi” [Zakaria 4: 6 ]

Matokeo ya nguvu yanaweza kuwa uongozi wenye, ushindi, nguvu isiyo ya kawaida ya binadamu au uwezo wa ufundi maalumu.

“Nami nimemjaza roho ya Mungu,katika hekima na maarifa na ujuzi na mambo ya kazi ya kila aina” [Kutoka 31:3-5]

Mara nyingine matokeo yake yalikuwa matendo au tabia isiyo ya kawaida. Siku zote kazi yake ilikuwa upande wa haki na kupinga maovu.

 ” Lakini wakaasi wakamhuzunisha roho yake mtakatifu kwa hiyo akawageuzia akawa adui akapigana”

Nguvu  ya kiroho au roho mtakatifu hupokelewa na mtu yeyote pale anapookoka inaweza kuambatana na kunena kwa lugha na inaweza isiambatane hii inategemeana na mtu. Hii ni ahadi ambayo Yesu aliwaahidi wanafunzi wake kabla ya kupaa[ Isaya 63 : 10]

“ Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu roho mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika yerusalemu na katika  uyahudi  wote na samaria na hata mwisho wa nchi” [Matendo 1:7]

       Mtu aliyeokoka  anapokuwa na roho mtakatifu au nguvu ya roho kiwango cha kiroho hushuka pale anapokengeuka/anapotenda dhambi. Roho mtakati  alifanya kazi mbalimbali  wakati wa agano la kale kama ifuatavyo;

 

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA AGANO LA KALE

A.     Alihusika katika uumbaji

“ Hapo mwanzo Mungu aliimba mbingu na nchi,naye nchi ilikuwa ukiwa, tena   utupu na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji. Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji”[ Mwanzo 1:1-2]

Mungu alitumia roho mtakatifu (neno) katika uumbaji wala hakushika jembe,udongo,maji wala kifaa chochote

B.     Alihusika kutoa unabii tangu Isaya hadi Zakaria. Wakati wa agano la kale manabii waliotoa unabii walinena kwa roho mtakatifu.“ Alitazama juu akawaona waisraeli wamepiga  kambi kila kabila mahali pake, kisha  roho ya Mungu ikamjia naye akatamka kauli hii ya mwenyezi Mungu ………………….” [Hesabu 24:2-3]

“ Siku hizo Hezekia aliugua akawa katika hatari ya kufa na Isaya nabii, mwana wa Amosi akaenda kwa mfalme akamwambia Bwana akasema hivi, Tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa wala hutapona.[Isaya 38 :1-2]  

C.     Alihusika kuwapa watu maarifa,wakati wa agano la kale Roho mtakatifu aliwapa watu maarifa ya kufanya mambo mbalimbali.

“ Bwana akanena na Musa na akamwambia, Angalia nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwanawa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, nami nimemjaza roho ya Mungu katika hekima na maarifa na ujuzi wa mambo ya kazi ya kila aina”[ Kutoka 31: 1-2]

D.     Alitoa hekima ya kuongoza kwa viongozi. Yusufu alitoa tafsiri mbele ya Farao lilikuwa tendo jema likashamngaza Farao na wengine

“Farao akawambia watumwa wake, Tupate wapi mtu kama huyu mwenye roho ya Mungu ndani yake. Farao akamwambia Yusufu kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote hapana mwenye akili na hekima kama wewe. Basi wewe utakuwa juu ya nyumba yangu na kwa neno lako watu wangu watatawaliwa katika kiti cha enzi tu, itakuwa  mkuu kuliko wewe.[ Mwanzo 41: 38-40]”   “Nami nitashuka  niseme  nawe huko, nami nitatwaa sehemu ya roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao nao watachukua mzigo wa watu hawa pamoja na wewe, ili usiuchukue wewe peke yako” [Hesabu  11: 14-17]

Mungu aliahidi kuwa siku ingekuja ambapo siyo watu walioteuliwa tu bali watu  wa Mungu  bila kujali hali yao, kwa kuwa wanaume na wanawake  wangekuwa na roho wa mungu ambaye angemiminwa juu yao.

” Hata itakuwa baada ya hayo ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili, na wana wenu waume  kwa wake , wakatabiri wazee wenu wataota ndotona vijana wenu wataona maono”[ Joeli 2: 28-29]

 

ROHO MTAKATIFU  KATIKA AGANO JIPYA

Yesu kristo alipofika duniani watu walipokea ufunuo wazi zaidi kuhusu roho wa MUNGU .Watu  hawakutambua  jambo hili kila wakati lakini kila lilipotendeka mioyoni  mwa watu ilikuwa ni kwaaili ya kuwaleta watu kwa MUNGU kwa mara ya kwanza au kuumba tabia mpya ndani.Hii  ya ajabu ote ilifanywa na roho wa MUNGU asiyeonekana.

  Katika maonesho ya ajabu ya MUNGU, roho wa MUNGU alikuwa anakuja kwa watu  walioteuliwa kwaajili ya kazi maalumu.Yesu alikuwa na roho asiyekuwa na mipaka au kikomo.Yesu aliishi na kutimiza kazi yake kwa njia ya nguvu isiyo na kikomo yaani ya roho wa MUNGU aliyefanya kazi ndani yake kila wakati.

 ;Basi litatoka chipukizi katika shina la yese ,na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda,Na roho ya Bwana atakaa juu yake,roho ya hekima na ufahamu,roho ya shauri na uweza ,roho ya maarifa na ya kumcha’’.

   Watu walipata ufahamu kuhusiana na roho mtakatifu,Ufahamu huu ulianza kuonekana wakati wa ubatizo wa Yesu,Mungu baba,alikuwa Mbinguni,Mungu mwana alikuwa duniani  ambaye  ndiye YESU,Mungu roho alikuja kutoka  Mbinguni na kudhihirisha ukuu kwa kumkalia Mwana. [Isaya 11:1-2]

‘’Naye yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini,na tazama mbingu zikamfunukia,akamwona roho wa MUNGU akishuka kama hua akija juu yake,na tazama sauti kutoka  mbinguni ikisema Huyu ni mwanangu mpendwa wangu ninayependezwa naye’’  [  Mathayo 3:16-17]

 

ROHO MTAKATIFU NA KANISA LA KWANZAKwa njia ya Yesu kristo ,MUNGU  alitaka kuwapa waamini wote roho mtakatifu,Yesu alipaswa kutimiza kazi ambayo baba alimpa kabla waamini hawajampokea roho mtakatifu.

    Mungu alitaka kuonyesha ukuu na kuridhika kwake na kazi ya Yesu na alimfufua kutoka kwa wafu na kumpa utukufu.

         Baada ya utimizaji huo wa ushindi wa huduma ya Yesu kristo duniani Baba angewapa wengine Roho.Hivyo Yesu aliwaahidi wanafunzi wake wangoje Yerusalemu baada ya kupaa kwake nao wangempokea roho mtakatifu kama alivyowahidia.

‘’Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza,wasitoke Yerusalemu bali wangoje ahadi ya baba ambayo mlisikia habari zake kwangu,ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji,bali ninyi mtabatizwa kwa roho mtakatifu baada ya siku hizi chache’’[Matendo 1:4-5]

   Mungu alitimiza ahadi siku ya Pentekoste,Siku ambapo Mungu alimimina roho juu ya wanafunzi wa Yesu.

‘’Kukawatokea ndimi zilizogawanyika kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao,Wote wakajazwa roho mtakatifu,wakaanza kusema kwa lugha nyingine,kama roho alivyowajalia kutamka.’’[ Matendo 2:3-5]

   Hata sasa Mungu anamimina roho wake juu ya waamini bila kujali hali yao,umri wao,jinsia,wala kabila.Wanaookokaau wanomkiri Yesu wanajazwa roho mtakatifu katika mazingira tofauti na wakati tofauti kama vile wakati wanabatizwa,baada ya kufundisha somokuhusu roho mtakatifu n.k

 ILI KUMPOKEA ROHO MTAKATIFU

-lazima umpokee yesu kuwa Bwana kuwa mwokozi wamaisha yako

                        -Lazima uitake Baraka hii kwa bidii

                                   -Uwe na kiu ya kiroho

  ‘’ Hata siku ya mwisho,siku ile kubwa ya    sikukuu,yesu akasimama,akapaza sauti yake akisema,mtu akiona kiu na aje kwangu anywe,………………na neno hilo alilisema katika habari ya roho ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye’[ Yohana 7:37]

  -Tubu toba ya kweli

 ‘’Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu kristo,mpate ondoleo la dhambi zenu,nanyi mtapokea kipawa cha roho mtakatifu’’ [Matendo 2:38]

  -Tumia imani katika kumpokea roho mtakatifu

‘’ Basi ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vilivyo vyema,je baba aliye mbinguni hatazidi sana  kuwapa roho mtakatifu hao wamwombao?’’ [Luka 11:13]

  JINSI   YA KUJAZWA    ROHO   MTAKATIFU

1/Omba kwaajili ya kumpokea roho mtakatifu,omba kwa kumaanisha na kwa bidii.‘’.Basi ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema,jebaba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa roho  mtakatifu hao wamwombao?’’[ Luka 11:9-13]

2/Wasamehe waliokukosea na tubu dhambi zako,kwani dhambi ni hufanya mtu asipokee roho mtakatifu.‘’’……tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina la Yesu kristo,mpate ondoleo la dhambi zenu,nanyi mtapokea kipawa cha roho mtakatifu’’ [Matendo  2:38]

3/Onyesha kiu ya kumpokea na andaa moyo wako kwaajili ya kumpokea Roho mtakatifu ’’ Na neno hilo alilisema katika habari ya roho mtakatifu ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye’’ [Yohana  7:37-39]

4/Anza kumsifu MUNGU  mpaka unapokea upako wa roho mtakatifu

‘’Wakamwabudu;kisha wakarudi Yerusalemu wenye furaha kuu.Nao walikuwa daima ndani ya hekalu,wakimsifu Mungu’’[ Luka 24:52-53]

Wakati wa agano jipya  roho mtakatifu alikuwepo, na yupo lakini anafanya kazi  tofauti na kipindi cha agano la kale.Katika kipindi hiki cha agano jipya wanaomwamini Mungu wanampokea roho mtakatifu na huondoka pale muumuini anapokengeuka na si lazima ahusike katika kutabiri au kutoa unabii,lakini katika agano la kale alihusika zaidi katika kutoa unabii na kuongoza kwa ujumla.

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA  AGANO JIPYA

{A}Hutufundisha yote aliyoagiza kristo

Roho mtakatifu akikaa ndani ya mtu humfundisha yale tunayopaswa kutenda.

    ‘‘Lakini huyo msaidizi,huyo roho mtakatifu ambaye baba atampeleka kwa jina langu atawafundisha yote na kuwakumbusha yote niliyowaambia.’’[Yohana 14:26]

{B}Hutuongoza

Roho mtakatifu akikaa ndani mwamini humuongoza katika mambo mbali mbali ya kimwili na kiroho.Mfano mtu mwenye roho mtakatifu kuwahi ufika Ibadani si lazima agongewe kengele bali roho humuongoza na kumkumbusha.

‘’Lakini yeye atakapokuja huyo roho wa kweli,atawaongoza awatie kwenye kweli yote kwa maana hata nena kwa shauri lake mwenyewe ,lakini yote atakayo atayanena na mambo yajayo atawapasha habari yake.’’[ Yohana 16:13]

{C}Hutuombea

Katika kuomba muombaji anapoomba hadi kufikia kunena kwa lugha roho mtakatifu hutusaidia kwa kuugua kusikokuwa kwa kawaida.

‘’Kadhalika roho naye hutusaidia udhaifu wetu kwa maana hatujui kuomba jinsi ipasavyo,lakini roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkika.’’[ Warumi 8:26]

{D}Roho mtakatifu anakaa ndani ya muumini ,mwamini akiwa na roho mtakatifu atakuwa safi katika mwenendo na matendo yake kwani atamshuhudia juu uhusiano wake na MUNGU.                                                     ‘’Lakini ikiwa roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa  ndani yenu,yeye aliyemfufua kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa kwa Roho wake anayekaa ndani yenu’’. [Warumi 8:11]

 Mwamini anaweza kupoteza Nguvu ya kiroho au roho mtakatifu  kutegemeana na hali ya maisha au tabia mbali mbali mbaya ambazo hutawala maisha ya mtu kama vile kuangalia michezo ya luninga akili hutawaliwa na kufahamu wahusika wa michezo hiyo na n.k humpa ham mtazamaji ya kuangalia  kila wakati  na hivyo hupoteza hamu ya kusoma biblia.

  Kuangalia filamu chafu huvuta fikra za mtazamaji na kumfanya afikiri kila wakati kufanya tukio halisiau kufanya jaribio la kuiga mitindo mbali mbali mibaya  aliyoiona hivyo huteka fikra za mtazamaji na humfanya afunguwe milango ya kuingiwa  na pepo la uzinzi,mwisho huishia kuingia katika dhambi ya uzinzi.

{E}Hutapatia uhakika juu ya wokovu wetu

‘’Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu,ya kuwa sisi tu watoto wa MUNGU’’ [Warumi 8:16]

{F}Hutupatia nguvu ya kuishi maisha matakatifu

‘’Lakini yeye atakapokuja huyo roho wa kweli ,atawaongoza awatie kwenye kweli yote;kwa maana hata nena kwa shauri lake mwenyewe’’ [Yohana 16:13]

{G}Huleta uwezo na nguvu ya kumsifu MUNGU katika ibada na kuabudu katika roho na kweli.

‘’…..maana sisi tu tohara,tumwabuduo Mungu kwa roho,na kuona fahari juu ya kristo yesu,wala hatuutumainii mwili.’’            [Wafilip 3:3]

‘’Mungu ni roho,nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli’[ Yohana 4:24]

{H}Anaweza kuruhusu jambo Fulani lifanywe au lisifanywe kutegemeana na muktadha au mazingira au hali halisi  ya tukio hilo

‘’Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia,wakikatazwa na roho mtakatifu wasilihubiri lile neno katika Asia’’ [Matendo 16:6]

MADHARA  YA  KUMPOTEZA   ROHO  MTAKATIFU

{i}Kufa kiroho au Kuwa na imaniisiyona matendo

Mtu yeyote asipokuwa na roho mtakatifu hata katika imani atakuwa na imani haba sana.Imani yake huwa ni ya mdomoni na si matendo.Anaweza kuwa mhudhuriaji wa ibada kama picha lakini moyoni amepooza au amekufa kiroho.

‘’Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa ,vivyo                hivyo na imani pasipo matendo imekufa’’.[ Yakobo 2:26]

 ‘’Na kwa malaika wa kanisa lililoko  sardi andika,Haya ndiyo anenayo yeye aliyena hizo roho saba za Mungu na zile nyota saba,Nayajua matendo yako ya kuwa unajina la kuwa hai nawe umekufa’’.[ufunuo 3:1-3]

{ii}Kukosa au kutokuwa na maono au kutojua mambo yajayo katika ulimwengu wa roho.

Mtu yeyote aliyeokoka akimpoteza roho mtakatifu hawezi au nguvu ya kiroho  hawezi kujua mambo ya rohoni kwani  unakuwa umejiondoa katika ulimwengu wa roho.  Kuishi bila roho mtakatifu ni sawa na meli isiyo na nahodha baharini.Mara nyingi hukosa mambo mazuri na hupatwa na mabaya kwani hukosa taarifa katika rohoni kuwa aombe.

‘’…Lakini yote atakayo yasikia atayanena,na mambo yajayo atawapasha habari yake’’ [Yohana 16:13]

‘’Siku hizo Hezekia aliugua akawa katika hatari ya kufa ;na Isaya nabii,mwana wa Amozi akaenda kwa mfalme ,akamwambia Bwana asema hivi,Tengeneza mambo ya nyumba yako maana utakufa wala hutapona…………’’[Isaya 38;14]

{iii}Kuwa mropokaji,

Mtu yeyote aliyeokoka akimzimisha au asipokuwa na roho mtakatifu mara nyingi huwa mropokaji kwani hakuna roho inayomwongoza azungumze nini,wapi  na atumie maneno gani.

{iv}Kuenenda kwa mwili ,

Mtu yeyote akimpoteza roho mtakatifu kila anachoona anaweza kukifanya bila kufikiri kitu hicho kina madhara gani,au lip jema na lipi si jema hivyo hukengeuka moja kwa moja.

{2}Kuingiza mitindo mbali mbali ya uimbaji wa kidunia makanisani.

Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia waumini hasa vijana waliookoka wanachukua au wanaiga mitindo mbalimbali ya uimbaji wa kidunia na kuingiza kanisani kama vile mitindo ya dansi,rapu,lege, n.k wanaitumia moja kwa moja katika uimbaji makanisani.Uimbaji huu huambatana na uigaji wa mitindo ya kucheza,mavazi na n.

Mitindo hii inapotosha ua inaondoa ushuhuda kwa kanisa na uwepo wa Mungu pia.Hali hii imewafanya ambao hawajaokoka kutamka dhahiri kuwa walokole wa sasa wamechakachuliwa.

Mfano;Baadhi ya vijana huimba Hip Hop makanisani wakiwa na uvaaji unaosawili waimbaji wa hip hop wa kidunia kama vile kushika shika suruali,na kuvaa milegezo.Mitindo hii ya uimbaji inaigwa kutoka magharibi[ulaya].Kwa ujumla haifai Hip hop kuimbwa kanisani au eneo lolote la ibada hata kama nyimbo hizo zitamtaja Mungu kwani zinabadili maana halisi ya ibada na kanisa kwa ujumla.Ni vyema  tujue kuwa nyumba ya ibada inapaswa kuheshimiwa ili kurejesha heshima kwa Mungu wetu.

Mara nyingi watu wanaposikia nyimbo hizi wakiwa kanisani hukumbuka kipindi kabla hawajaokoka hivyo huangalia namna waimbaji wanavyocheza na sii kisikiliza ujumbe,Hatimaye huvutiwa kusikiliza na kucheza na mwisho wa yote huzifuata disco ambako zinaimbwa kwa wingi zaidi na baadaye kunogewa na starehe na kuacha wokovu.Ni wajibu wa kila mmoja kutafakari na kuangalia mienendo yake ya wokovu na si kuangalia mabadiliko ya dunia kwani Yesu au Mungu wetu habadilishwi na chochote.

[3]Kuoa na Kuolewa

           Katika karne ya 21 suala la ndoa au kuoa na kuolewa limekuwa na changamoto kubwa.Hii ni kutokana na uwepo wa njia tofauti wanazotumia watu kutafutana na kuombana uchumba kama vile kwa kutumia kitabu cha nyuso[Facebook],simu,twiter,skype na n.k

Kwa sasa vijana wanatamaniana hivyo wanatafutana si kwaajili ya kuoana au kuolewa au kwa kuzingatia vigezo kama vile umri na uhitaji wa kuwa na mwenza au familia n.k bali huoana kwaajili ya kuzitimiza tamaa zao za mwili na si kupendana kwa dhati.

Vijana  Wengi wanapofikia hatua hii hukengeuka na kumwacha Mungu kutokana na kupumbazwa na pressure ya mapenzi  na waliokwisha ingia huogopa kuchwa au kusitisha uhusiano wao.Mara nyingi mabinti hulazimishwa kufanya mambo mengi maovu na wapenzi wao,kwa woga huwa wanatii na kusahau kuwa wanamkosea Mungu.Mabinti wengi hulazimishwa kufanya uzinzi na matokeo yake huishia kuathirika na gonjwa hatari na kupata mimba zisizotarajiwa na waliowapa huwakataa.

             Hii ni kwasababu vijana wengi huliangalia suala la ndoa kwa wepesi zaidi bila kutambua kuwa katika ndoa ikiwa Mungu hatahusishwa huwa na matatizo.Ni vyema kujua kuwa mtu yeyote au mchumba huwa na muonekano huu;

Unapofikiri kuoa ni vyema utambue kuwa unayemchagua atakuwa mwenzi wa maisha milele hivyo haitoshi kuangali umbo la nje tu kwani linaweza kubadilika.Zingatia sana mahitaji ya nafsi na rohoni ndiko yanakotoka mambo mazuri na vigezo vingine ni ziada.

-Zingatia sana mapenzi ya Mungu katika maisha yako na kati ya wengi una chumbia mmoja,na katika kufanya maamuzi kabla ya kuanza kuchumbia mshirikishe Mungu.

    “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe’’[mithali 3:5]

-Imani moja kwani ndoa ni muunganiko wa watu wawili hadi kifo hivyo ili muunganiko uwe imara lazima uhusishe na masuala ya imani.

       ’’Msifungiwe nira pamoja na wasioamini,kwa jinsi isivyo sawasawa;kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi?Tena pana ushirika gani kati ya nuru na giza?Tena pana ulinganifu gani kati ya kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja nay eye asiyeamini?’’.[2wakorintho 6:14-15]

-Usiangalie sura,umbo au umbile,elimu n.k kwani Mungu ndiye muumbaji pia ndiye anayetoa hivyo hata akikupa mke au mume mwenye sura ya tofauti na matarajio pokea na ushukuru kwani yeye anamjua kila mtu kwa namna au jinsi alivyo.

‘’Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye,bali mke mwenye busara mtu hupewa na Bwana’’[Mithali 19:14]

       MTU/MCHUMBA

             -Jinsi ulivyomuona[muonekano wa nje]

            -Jinsi alivyo[moyoni]

            -Jinsi atakavyokuwa[baada ya kuoa au kuolewa]

Angalizo kwa vijana wa sasa ni kosa kuchumbia bila kumuomba Mungu kwani,unapoamua kwenda kutoa posa unakuwa umeridhika na muonekano wa nje bila kujua jinsi alivyo moyoni na jinsi atakavyokuwa baada ya kuolewa.Ni vyema kumuomba Mungu kwani yeye anajua akupe mke yupi atakayefanana na wewe kimwili na kiroho.

  Hata hivyo katika jamii,tumegawanyika katika makundi mawili ambayo ni;

   [A] INTROVERT

         Ni aina ya watu ambao ni watulivu wasiopenda kukaa na watu au ni aina ya watu wanaopenda kukaa peke yao kila wakati.

[A quite person who prefers to be alone than with other people]

SIFA    ZAO

  -Ni watulivu

 -Ni wataratibu

  -Hawapendi kujionyesha na si waongeaji bali wana maneno machache.

   -Ni watu wasiomkosea Mungu nani wepesi kuepuka dhambiya uongo,usengenyaji na n.k

 -Mara nyingi hupenda kujihusisha na  shughuli moja tu na si kuchanganya mfano kama ni mfanyakazi basi hawezi kujihusisha na biashara na n.k hivyo ni vigumu kwao kupata maendeleo.

 -Hata akiwa na wazo zuri anachelewa kufikiri na kufikia muafaka au kumweleza mtu mwingine ili amusaidie.

[B]EXTROVERT

   Ni aina ya watu wanaopenda kuchangamana na watu wengine.

[A person who is full confident, full of life  and who prefers being with other people]

SIFA  ZAO

-Ni wacheshi

-Ni wepesi kufikiri jambo kwa haraka na kulitafutia ufumbuzi

-Ni wepesi kumkosea Mungu na kuomba toba

-Ni waongeaji sana hivyo ni vigumu kuepuka dhambi kama vile udanganyifu,usengenyaji.

         Kutokana na uwepo wa makundi haya ni vigumu kujua ni yupi anayefaa kuwa mke mwema hivyo bila kumuomba Mungu unaweza kupata ubavu usio wako.Vijana tunapaswa kumuomba Mungu ili aseme na Yule unayemtaka lakini endapo Mungu atakujibu ni vyema kufuata utaratibu maalum uliowekwa na kanisa au jamii kwa ujumla ili kuepuka udanganyifu na ukengeufu kwani sii kila binti anafaa kuwa mke na sii kila kiajana anafaa kuwa mume wa mtu ‘’MUNGU ndiye anayejua kukuchagulia’’

’’Mfalme suleman akawapenda wanawake wengi wageni,pamoja na binti yake Farao,wanawake wa wamoabi na waamoni na waedomi nawasidoni na wahiti na wa mataifa Bwana aliyowaambia wana wa Israel,msiingie kwao wala wasiingie kwenu;kwa kuwa wataigeuza mioyo yenu kuifuata miungu yao’’     [  1Wafalme 11:1-3]

[4]Kushindwa kutambua karama uliyonayo.

Mungu  humuumba kila mmoja kwa makusudi maalum,humpa kila mtu karama au huduma yake na idadi ya karama hutofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine.Wengine wana karama ya kuimba,wengine kushuhudia,kuhubiri na n.k

     Changamoto kubwa kwa vijana wa leo wengi hawajui  karama zao na hawamuombi Mungu ili awafunulie karama hizo.Kutokana na kutojua karama hali inawafanya kutoshiriki au kutofanya kazi yeyote kanisani bali wanabaki kuabudu kama desturi.Kama Mungu ndiye muumba wa vyote ni vyema ujiulize maswali,kwanini asingekuumba kunguni,ng’ombe,bata au mnyama mwingine yeyote?Ni vyema mwanadamu ujue kuwa lipo kusudi la wewe kuumbwa kama mwanadam hivyo ni vyema umuombe Mungu ili akufunulie karama au huduma yako ili uifanyie kazi katika kuujenga ufalme wa mbinguni.

”Naye alitoa wengine kuwa mitume na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu,kwa kusudi la kukamilisha watakatifu hata kazi ya huduma itendeke hata mwili wa kristo ujengwe’’  [Waefeso 4:11-12]

    Wakati Fulani Mungu anaweza kumpamtu karama kwa mda maalum na kwa kusudi maalumu la wakati  huo,mfano karama ya unabii .Katika kanisa si lazima karama zifanane kwani Mungu humpa kila mtu kwa namna yake na kulingana na Mungu anavyotaka mtu awe au atumike katika kanisa.

‘’Basi pana tofauti za karama;bali roho ni yeye yule,tena pana tofauti za huduma na Bwana ni yeye yule,kisha pana tofauti za kutenda kazi bali Mungu ni yeye Yule azitendaye kazi katika wote.Lakini kila mmoja  hupewa ufunuo wa  roho kwa kufaidiana Maana mtu mmoja kwa roho apewa neno la hekima;na mwingine neon la maarifa,apendavyo roho yeye yule……………………’’        [1Wakorintho 12:4]

 Hivyo mnaweza kuokoka kwa siku moja,mkabatizwa kwa wakati mmoja,na mkajazwa roho mtakatifu wa wakati unaofanana lakini kila mmoja akawa na karama yake tofauti kadri Mungu atakavyo mjalia na hata katika kanisa karama mbali mbali hufanya kazi kwaajili ya kulijenga kanisa na kutimiza kazi ya Mungu.

  Mungu humuumba kila mtu kwa kusudi maalum,Hakuna mtu ambaye Mungu alimuumba awe mwizi,jambazi,mlevi,mzinzi na n.k bali shetani huwadanganya  watu ili apate wafuasi wa kwenda naye jehanamu.Ni vyema wanadamu tujiulize kama Mungu ndiye aliyeumba vitu vyote je kwa nini asingekuumba panya,paka,kuku,bata n.k hivyo lipo kusudi la kumuomba Mungu ili anene na wewe nini kusudi la kuumbwa kwako.

  KAZI ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTOA UNABII

Katika lugha ya kisasa maneno ‘’Unabii au Nabii’’ kwa kawaida yana maana ya kutabiri mambo yajayo.Maana hii haikuwa ya msingi katika huduma ya unabii wakati wa agano la kale.Wakati ule maana yake ilikuwa kujulisha mapenzi ya Mungu yaani nabii alikuwa msemaji wa Mungu.

{A}Kufundisha mafundisho ya kiroho ndani ya mtu

”Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji,bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu,watu wa nyumbani mwake Mungu,mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii,naye yesu kristo mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni’’   [Waefeso 2:19-20]

Mara nyingi unabii hulenga kufundisha mafundisho ya msingi katika kanisa ili kulipatia kanisa msingi ulio imara.

{B}Kubomoa na kuharibu kazi za shetani na kupanda roho ya Mungu ndani ya mtu.

     Yeremia 1:5-10 anasema ‘’Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua na kabla hujatoka tumboni nalikujua,nalikutakasa;nimekuweka kuwa nabii wa mataifa,Ndipo niliposema,aa Bwana Mungu,Tazama siwezi kusema;maana mimi ni mtoto,Lakini Bwana akaniambia ,Usiseme mimi ni mtoto mdogo;Maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekuamuru kwake,nawe utasema kila neno nitakalo kuamuru ……………………..Ndipo  Bwana akaunyosha mkono wake akanigusa kinywa changu,Bwana akaniambia,Tazama nimetia maneno yangu kinywani mwako angalia nimekwenda leo juu ya mataifa na juu ya falme ili kung’oa na kubomoa na kuharibu na kuangamiza ili kujenga na kupanda’’

{c}Kuonya

   ‘’Akaniambia mwanadamu nakutuma kwa wana wa Israel,kwa mataifa wanaoasi mimi;wao na baba zao wamekosa juu yangu,naam hata hivi leo,Na wana hao wana nyuso zisizo na haya na mioyo yao migumu.Mimi nakutuma kwa hao;nawe utawaambia Bwana Mungu asema hivi,Na kwamba watasikia {maana ndio nyumba ya kuasi hao) hata hivyo watajua yakuwa nabii amekuwako miongoni mwao “[Ezekiel  2:3-5]

{d}Kufariji, kutia moyo, nakuthibitisha kile ambacho Mungu amekwisha kusema na   wewe.

 “Bali yeye ahutubuye asema na watu maneno ya kuwajenga na kuwafariji na kuwatia moyo , yeye anenaye kwa lugha hujijenga nafsi yake; bali ahutubuye hulijnga kanisa ………..”[1Wakorintho 14:3]

Hata leo manabii wapo ila wanafanya kazi katika nafasi na kazi zao tofauti na za wale manabii wa agano la kale.

 “Naye alitoawengine kuwa mitume na wengine kuwa manabii na wengine kuwa wainjlisti na wengine kuwa wachungaji na walimu “[Efes 1 Yohana 4:1-4 anasema “wapenzi msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho kwamba zimetokana  na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani” [1Yohana 4:1-4]. Katika hili mwajua  roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatoka kwa Mungu; na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha  kuwako duniani.

SIFA ZA UNABII WA KWELI

I.Huambatana na upako au nguvu za Mungu(spiritual power).

 “Mkijua neno hili kwanza ya kwamba hakuna unabii katika maandalizi upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu Fulani tu, maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya binadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na roho mtakatifu”.[2 petro1;20-22]

II.Huambatana na matendo halisi

Mara nyingi unabii wa kweli huambatana na utokeaji au utendekaji wa tendo halisi

“ Basi tulipokuwa tukikaa huko siku nyingi, nabii mmoja jina lake Agabo akashuka kutoka uyahudi alipotufikia akautwaa mshipi wa Paulo, akajifunga miguu na mikono akasema roho mtakatifu asema hivi, Hivyo ndivyo wayahudi watakavyomfunga mtu mwenye mshipi huu nao watamtia katika mikono ya watu wa mataifa…….” [Matendo 21:9-14]

Haya yalitabiriwa juu ya Paulo na yalitokea wakati wake ulipofika(matendo 21;29-40) hivyo utabiri wa kweli ni ule unaotimia.

III.Hutimia kwa maombi

 “Elia alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi akiomba kwa bidii mvua isinyeshe na mvua haikunyesha juu ya nchi kwa muda wa miaka mitatu na miezi sita,akaomba mvua inyeshe tena na mbingu zikatoa mvua nayo nchi ikazaa matunda yake” [Yakobo 5:17-18]

5/ Mmomonyoko wa maadili

Kwa sasa suala la mapenzi linaonekana kama suala la msingi (current issue), kwaani vijana hat watu wazima wamekuwa wakijihusisha na  kwa namana moja ama nyingine, maendeleo ya sayansi na teknolojia  kama vile facebook,twitter pamoja na ofa mbali mbali zinazotolewa na mitandao ya simu za mikononi imefanya watu kuingia katika mahusiano yasiyo ya msingi. Mitandao hii imevunja ndoa kwa baadhi ya wanandoa, imewafanya waliookoka kutomtafakari Mungu na kusoma biblia bali sasa wameingia  kufanya mawasiliano(kuchati) na facebook, twitter kuangalia michezo ya luninga isiyo na maana picha chafu(pornography) na kuwasikiliza wasanii mbali mbali wanoima nyimbo za kidunia. Matokeo yake  wengi wameingiwa na pepo la uzinzi(ngono) na kufa kiroho. Wengi wamemsahau Mungu na kuyaenzi mapenzi.

“ Nawasihi enyi binti za yerusalem kwa paa na kwa ayala za porini,msiyachochee mapenzi wala kuyaamusha…..” [Wimbo uliobora 3:5]

6/  Kukosa msimamo

Watu wengi kwa sasa wamekosa msimamo kiimani wengi wanatamani mafanikio kuliko kwenda mbinguni. Hali hii imewafanya  waumini wengi hasa vijana  kutanga tanga huku na huko kiimani. Hawapendi watumishi wa hubiri kuhusiana na kuacha dhambi bali wanapenda mahubiri yahusuyo kubarikiwa au namna ya kupatafedha na mali.

Wakati kama hu vijana au waumini tunapaswa kuamka na kutambua  kuwa tumeokoka  ili twende mbinguni hivyo tuwe na msimamo dhabiti.

“Lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kuokoa roho zetu’’.[Waerania 10:39]

 

ATHARI ZA UTANDAWAZI KATIKA MAISHA YA KAWAIDA

1.Tamaduni za kigeni

Kwa sasa utamaduni wa kigeni umeanza kuenea sanaAfrika  na umewaathiri vijana katika mavazi. Vijana wameiga uvaaji mbaya kama vile kuvaa suruali mlegezo hata matumizi ya lugha  kwa vijana  yamekuwa ya kihuni sana. Vijana wameiga mambo mbali mbali yanayofanywa  na waimbaji wa hip hop,dansi blues n.k wa ulaya kama vile vijana wa kiume kusuka nywele kuva heleni  na mabinti kuvaa mavazi ya kiume kamavile suruali pamoja na mavazi yanayobana ambayo yanawavutia na kutoa ushawishi kwa vijana wa kiume. Mavazi haya ni chukizo kwa Mungu viongozi wa dini serikali wazazi na walezi wameshindwa kukemea na matokeo yake  mavazi yamechochea ubakaji n.k hadi sasa mavazi haya yanavaliwa hata kanisani

Watumishi wengi hushindwa kuwakemea waumini wao kwa kuhofia kuwapoteza au kuwakatisha tama katika maisha ya wokovu. Baadhi ya watumshi kuhofia kukosa waumini wanasahau kuwa kutokemea ni kuwapoteza kabisa kwani hali hii inaharibbu  ushuhuda  kwa kanisani kufanya wengine wasiokoke(wasimpokee Yesu).

” Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanaume wala mwanamume asivae mavazi yampasayo mwanamke kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa Bwana Mungu wako”.[Kumbu kumbu la tarati 22:5]

Hivyo viongozi wa dini naomba msimame kwenye nafasi zenu na kukemea uovu bila woga ili kulijengakanisa na kufanyawote tufike mbinguni, vinginevyo wokovu wetu utaishia hapa hapa duniani.

2.Mahusiano

Suala la mawasiliano kwa sasa limeshamiri sana katika jamii. Mika iliyopita masuala ya mahusiano yalitazamwa kwa jicho la tofauti kwani ilikuwa ni aibu wachumba (wapenzi), kutembea pamoja  ikiwa bado hawajawa wanandoa  na vijana wadogo hawakujihusisha katika mahusiano  wala hawakujua chochote kuhusiana na mapenzi.

Kwa sasa mahusiano kwa watoto wadogo  na vijana imekuwa changamoto kubwa. Kutokana  na utata wa vijana  kushindwa kujua n umri upi  binti  na kijana waingie katika mahusiano na ni umri upi binti achumbiwe na kijana  achumbie?

Changamoto hii imetokana na watoto wadogo wanaosoma shule za msingi  na sekondari wanaojiingiza katika mahusiano na kudanganyana  au kuahidiana kuoana  bila kujua ni kipi kifanyike kati ya kusubiri wakati wao ufike  au kuingia kwenye  mahusiano ndipo wamwombe Mungu. Vijana wanaanza kama marafiki na kuwa  wachumba kwa wakati mmoja ndipo wanamwomba Mungu, wanasahau kuwa Mungu ndiye mwenye kuianzisha safari  lakini wao wanamshirikisha  wakiwa wamesha patina. Kama kweli kijana amedhamilia  kupta mchumba  anapaswa kumwomba  Mungu kwani  ndiye mpaji nasi kuchagua  kwani  mke si  nguo wala sura, bali ni tabia  na ajuaye hayo ni Mungu pekee.

“ Je mmekuwa wajinga namana hii? Baada ya kuanza katika roho mnataka kukamilishwa sasa katika mwili?[Wagalatia 3:3]

Vijana wengi waamekuwa wakihusiha katikamapenzi wakiwa na umri mdogo  na matokeo yake wameishia  kuathirika  na ugonjwa wa ukimwi, magonjwa ya zinaa,kupata mimba zisizotarajiwa wanafunzi wengi wamefukuzwa shule,kupiga punyeto kwa vjana wa kiume na usagaji kwa mabinti. Hili ni chukizo kwa Mungu kwani  mwili wako ni hekalu la roho mtakatifu.

 “ ……lakini mwili si kwa znaa, bali ni kwa bwan, naye Bwana ni kwa mwili aye Mungu alimfufua Bwana  na tena atatufufua na sisikwa uwez wake. Je hamjui ya  kuwa miiliyenu ni  viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaa? Hasha! Au hamjui a kuwa yeyee aliyeungwa na  kahaba  ni mwili mmjoa naye? Maana asema  wale wawili watakuwamwili mmoja  lakini yeye aliyeungwa na Bwana  ni roho moja naye. Ikimbieni zinaa kila dhambi  aitendayo mwanadamu ni nje yamwili wake ila yeye  afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la roho mtakatifu? Aliyendani yenu mlipewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe maana  mlinunuliwa  kwa thamani …..”[1 wakorintho 6:13]

Wazazi wengi  na walezi wengi wamezembea kaatika suala  la malezi  na baadhi yao wamekengeuka  na kuonesha  mahusiano yao batili ( nje ya ndoa)  hadharani mbele ya watoto, jambo ambalo ni kinyume na  maadili yakidini  na kiAfrika pia. Wazazi wamekuwa  wakienda dico na kujihusisha katika mapenzi  na vijana  wadogo, wengi wakishaingiwa na pepo la uzinzi na uasherati ni vigumu kujinasua  hubaki  wanatapatapa namwishoni huambuliamauti.

“ Hamjui ya kuwa ninyi ni hekalu la Mungu nay a kuwa roho wa Mungu anakaa ndani yenu? Kama mtu akiliharibu hekalula Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu abalo ndilo ninyi”.[1wakorintho 3:16-1]

Wakati umefika vijana kujitambua , tuamke tujitambue tuache kufuata  mkumbokwani ukimwi na magonjwa ya zinaa vitatumaliza hivyo  ni bora kuoa kuliko kufanya zinaa

“Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanaume asimguse mwanamke lakini kwa sababu   ya zinaa kila mwanamume na awe na mke  wake  mwenyewe  na kila mwamanmke na awe na mme wake mwenyewe”.[1wakorintho 7:1-2]

 Kupiga punyeto, kuwa na girl friend au boy friend si njia ya kuepuka  kifo bali njia  pekee ni “kuacha dhambi”.

NI UPI WAKATI MZURI WA KIJANA(MTU)KUMPATA  MWENZA AU MCHUMBA?

Uchumba ni uhusiano  kati ya mume na mke  wenye lengo la kuishi pamoja  kama wanandoa.Hii ni kiwango cha juu sana cha urafiki kati ya msichana na mvulana ambao wameweka ahadi ya kuoana.Watu wengi huchumbia ovyo kutokana na kutomruhusu roho mtakatifu ahusike.Usimchumbie binti kwa kumdanganya ili ukubaliwe,ni vyema kumweleza dhahiri ili ajue hali halisi.

 ‘’Maana mtu mwenye kukubaliwa si yeye ajisifuye,bali yeye asifiwaye na Bwana’’[2wakorintho 10:18]Mara nyingi binti unayeletwa na Mungu hana maswali mengi.

Aina za uchumba

1.Uchumba wa siri (secret courtship)

Ni uchumba ambao wachumba wawili  wanakubaliana  kwa siri bila kushirikisha  jamii. Aina hii ya uchumba inafanywa kiholela, wachumba hao huchangamana na hutambuana vyema. Ila wachumba hao wasipokuwa makini  wataanguka katika dhambi ya uzinzi na kusalitiana. Aina hii ya uchumba mara nyingi  hutumiwa na vjana  ambao umri wao  haujafikia kuoa wala kuolewa.

2.Uchumba wa wazi(open courtship)

 Ni ule uchumba  ambao  unafahamika na kanisa au jamii kwa utaratibu wa  makanisa  mbali mabali uchumba huu huambatana na  kuvishana pete  rasmi inayoitwa pete ya uchumba  inayoshuhudiwa na mashahidi.

 Kilele cha hatua hiii ya uchumba nindoa. Ndoa ni makubaliano baina ya watu wawili  ya kuisi pamoja  kama mume na mke. Ndoa ni mpango wa Mungu toka  mwanzo na mwanzilishi  ni Mungu mwenyewe  lakini ili ndoa iwe ndoa  ni vyema  ipitie  hatua hii ya  uchumba .“ Kwa hiyo mwanaume  atamwacha  baba yake na mama yake naye  ataambatana  na mkewe, nao watakuwa  mwili mmoja” [Mwanzo 2:24-25]

Kipindi cha uchumba nikipindi kigumu wahusika wanapaswa kuwa makini kwani wanaweza kumkufuru Mungu na kuanguka katika  dhambi bila kujua  wakati mwingine  uchumba unaweza kuvunjika  bila kufikia kilele(ndoa).Changamoto kubwa kwa vijana  huwa ni  naye anayestahili  kuwa mwenza maana mabinti   ni wengi. Vijana wengine  hukosea katika  kufanya  maamuzi sahii kutokana na kushindwa kujua  Mungu kwao. Hii hutokana na wahusika  kutafutana bilia kumwomba Mungu na wengine huanza kuomba  wakiwa  wameshapatana, wakati mwingine kijana  anamwomba Mungu akiwa na sura ya binti au kijana  Fulani anayempenda, hili ni tatizo kubwa kwa vijana  wengi  vijana wanapaswa kutambua kuwa  ukiingia kwenye uchumba   ni vyema   kufiia kilele chake yaani ndoa  na ukiingia kwenye ndoa hupaswi kumwacha mkeo  au mumeo  hivyo ni vyema kumwomba Mungu vya kutosha  kabla ya  kuchumbia  au kuchumbiwa.

 

  “ Lakini wale waliokwisha  kuoana  nawaagiza; wala  hapo si mimi ila Bwana ; mke asiachane na mumewe  lakini ikiwa ameachana  naye  na akae asiolewe  au apatane na mumewe ; tena  mume asimwaache  mkewe”. [1 wakorintho 7:10-11]

Angalizo: si kila wakati unaweza kuchumbia  au kuchumbiwa  bali  kuna muda  maalumu

“Kwa kila jambo kuna wakati na majira  yake, na  wakati wa kila kusudi chini ya mbingu.[Mhubiri 3;1]

Hivyo ni dhahili kwamb kuna muda maalum ambao kijana anweza  kuchumbia au kuchumbiwa  kwa kawaida  baada ya  kutoa pos  hapo ndipo  uchumba  unapotambliwa  rasmi.

DONDOO

Kwa kijana wa kiume  kuanzia miaka  25 lakini  mazingira ya kiuchumindiyo yanayoamua

Kwa binti inategemea maumbile  anaweza kuchumbiwa  kuanzia miaka20

Kwa anayesoma bila kujali umri wake anashauriwa  kutojiingiza suala la kuoa au kuolewa  bila kumaliza   elimu ya awali yaani kidato cha nne na cha sita

Usiingize suala la kuoa au kuolewa kama unajua akili yako haijatuliwa  kwaniutaingia katika ndoa  bila kutarajia  hasa kwa kusukumwa na tama ya mwili.

Ujitazame kiwango chako cha elimu kazi n.k vinaweza kupelekea kuchumbia au kuchumbiwa.

SIFA ZA KIROHO KWA BINTI NA KIJANA  ANAYECHUMBIA AU KUCHUMBIWA

Lazima awe ameokoka na awe anaishi  maisha matakatifu

                           Zaburi 119:9 anasema “ Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? kwa kutii akilifuata neno lako.

Aliyejaa neno la Mungu,“Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, nisije nikakutenda dhambi’’ [Zaburi 119:11]

Anayejua nini maana ya ndoa kwa mtazamo wa kiMungu

“Hata wamekuwa si wawili tena, bali ni mwili mmoja,basi aliowaunganisha Mungu mwanadamu asiwatenganishi’’[Mathayo 19:3-6]

Anayejua kuwa ndoa ni agano la kufungamana na bila ya kuachana  hivyo lazima ufikiri kwanza kabla ya kuingia .

 “Kwa maana mwanamke aliyena mume amefungwa na sheria kwa Yule mume wakati anapokuwa  yu hai;bali akfa Yule mume , basi wakati awapo  hai mumewe ,kama akiwa  na mume mwingine huitwa mzinzi” [Warumi 7;2-3]

Ni vyema  anayechumbia  au kuchumbiwa ajue kuwa ndoa ni ya watu wawili na sio zaidi kwani bila kujua hayo matokeo ni mzozo na kuachana  au kupigana kila kukicha.

 

SIFA ZA KIMWILI  ZA KIJANA                                                 

Aliyetoka utotoni

Mwenye uwezo wa kuwa mume

Mwenye uwezo wa kuwa baba yaani kimajukumu  awe na uwezo kulisha familia.

Anayejua mkewe anapendelea vitu gani na je kinachomsukuma  kuoa ni nini? Pressure ya mwili, wakati au umri hasa anapaswa kuwa na hitaji toka moyoni

Anayejijua jinsi alivyo kitabia kama vile  mkimyautapata shida kwani hakuna hata anyeweza  kukaribisha mgeni.

Anayejitambua kitabia uwezo kielimu kwani si vyema mke akawa juu kielimu kuliko mume.

SIFA ZA KIMWILI ZA BINTI

Aliyetoka utotoni yaani aliyevunja ungo

Mwenye uwezo wa kuwa mke

Anayejitambua umri wake elimu yake tabia n.k

Mwenye mawazo yasiyo ya kitoto na  mwenyeuwezo wa kuwa mama

Aliyekomaa viuongo vyake

SIFA ZA KIJANA ANAYESTAHILI KUOA NA BINTI ANAYESTAHILI KUOLEWA.

Anayemcha Mungu

“kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa,bali wapumbavu hudharau hekima na adabu”.[Mithali1:7]

Unayemfahamu vizuri na kwa muda wa kutosha historia yake hali yake  ya kiimani n.k

“Nami nitakuapisha kwa Bwana Mungu wa mbingu na Mungu wan chi kwamba hutamtwalia mwanangu mke katika binti za wakaani ambao nakaa kati yao bali enenda hata nchi yangu na kwa jamaa zangu ukamtwalie mwanangu Isaka mke”[Mwanzo 24:3]

Kama kuna utofauti wa kiimani kati yenu ni vyema ukawa makini kujua hali halisi ya kifikra ni yupi atakayebadili  msimamo wake na kumfuata  mwenzie. Ni vyema sana mkifanana  kiimani kabla ya kuoana kwani usuluhishi wa matatizo ya wanandoa  wenye msimamo tofauti huwa ni mgumu kuisha na hata malezi kwa watoto  yanakuwa  magumu kwani baba atawapeleka huku na mama atawapeleka kwake mwisho watakosa msimamo.

Lakini kama hamjafahamiana  kwa muda wa kutosha (mrefu)hakikisha Mungu anahusika.

Ni vyema kufahamiana viwaango vya elimu uwezo wa kiuchumi hata viwango vya rohoni , kwani  kama viwango vyenuu vya kiroho wote mpo chini baada ya kuoana  mnaweza  kupoa kiroho na kuwa wakengeufu.

Anayejituma katika kazi ya Mungu mwenyewe ,mwenye  tabia njema  hata kama ana sura ya tofauti na ulivyotarajia.

Aliyemnyenyekevu, mkarimu au mtoaji.

Aliyeokoka vizuri na unayempenda kwa  dhati msionane  kwa kuoneana huruma kwani baadaye  huleta madhara  na majuto.

VITU MUHIMU KWA KIJANA KABLA YA KUCHUMBIA

-Hakikisha una shughuli yeyote yakuingiza kipato

-Hakikisha una mahali pa kuishi yaani umejenga nyumba au umepanga zaidi ya chumba kimoja.

-Hakikisha una kitanda godoro zuri na vyombo vya kupikia viti (kochi au sofa) n.k

-Uwe na mipango endelevu ya kimaisha na kiuchumi ambayo utamshirikisha  hata mwizi.

NINI KIJANA AFANYE  KABLA YA KUCHUMBIA

Fanya maombi ya kutosha, ni vyema yakawa maombi  ya kufunga  kwani yanakupa nguvu,kuvuta uwepo wa Mungu na kumtafakari Mungu zaidi. Usiombe kwa Mungu  ukiwa na sura ya mtu Fulani.

Anza kuomba kabla hujapata wala kufikiria  sura ya mtu fulani kwani Mungu ndiye kuchagulia na  kuidhihirisha.

Omba ushauri kwa  wachungaji au watu waliooa kabla ya kuchukua  hatua yeyote.

Endapo Mungu akisema  na wewe  juu ya mtu fulani usifanye haraka ili upate muda wa kujiridhisha

Mungu akikudhihirishia  kuwa ni yeye  tafuta muda  au fuata hatua zinazofaa ili mzungumze ikiwezekana  inaweza kuwa kanisani, nyumbani kwa mchungaji au mzee wa kanisa  na unapoongea naye epuka kushawishi au kumtongoza kwani mnaweza kuoana kwa kuoneana huruma kwani kuna  madhara makubwa  mbeleni.

NINI BINTI AFANYE ANAPOCHUMBIWA

Mwombe Mungu vya kutosha,ni vyema kufanya maombi ya kufunga ili kuvuta nguvu na uwep[o wa Mungu.

Usifanye haraka kujibu “ndiyo nimekubali”

Mshirikishe mama mchungaji au mzee wa kanisa atakushauri pia ataomba na wewe

Endapo Mungu atakupa kibali mpe majibu kwa heshima

Endapo hukupata kibali mjibu kwa heshima ili usimkwaze,kwani ukimjibu vibaya anaweza kuacha wokovu.

Kama limepata kibali anza  kufanya maandalizi mapema na jitahidi kuwa karibu na akina mama

MAMBO YA KUEPUKA WAKATI WA UCHUMBA

-Epuka mahusiano yenye lengo baya

-Anza mahusiano kwa  mawasiliano kwa  tahadhari na epuka zawadi fedha n.k huleta athari kubwa baadaye

-Ukaribu usiokuwa na kiasi kama vile  kukaa pamoja kuongea pamoja kila wakati na kuongozana  au kutembea pamoja  huleta anguko dhambini.

-Msionyeshane  matendo ya mapenzi wakati wa uchumba iwe kwa message au kwa maongezi.

 “……msiyachochee mapenzi wala kuyaamsha  hata yatakapoona vema yenyewe” [Wimbo uliobora 3;5]

-Epuka kukaa muda mrefu katika  uchumba ni vyema uchumba  wenu usizidi mwaka mmoja.

3.suala la elimu

   Vijana wengi wamejikita katika masuala mbali mbali kama vile uimbaji wa mziki  ya hip hop dansi wavipa kipaumbele. Hata katika shule mbali mbali za sekondari wanafunzi wengi hutumia daftari za darasani kuandika nyimbo za hip hop badala ya  kuandika masomowanayofundishwa. Hali ii imewafanya vijana wengi watakuwa waimbaji(wasanii)

Wamesahau kuwa hata kuwa msanii unapaswa uwe umesoma. Ili mwanafunzi afaulu ni vizuri darasani anapaswa kuwa  na utii heshima na adabu na anapaswa kumcha  Mungu kwani ndiye mpaji nani cha maarifa.

“ Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa bali wapumbavu hudharau hekima na adabu”.ni vyema vijana tujitambue  na tujue kuwa  Mungu anatuwazia mema hata katika mambo ya kitaalamuma tunasisitizwa kusoma kwa bidii.[Mithali 1:7]

 “Mkamate sana elimu wala usimwache aende zake maana yeye ni uzima wako”.[Mithali 4:13]

Vijana tuzingatie  elimu na tutumie muda vizuri kusoma na kupata elimu mbal mbali kama vile  kujifunza kuhusu ujasilia mali n.k hii itatusaidia  kujikwamua kiuchumi tuache uzurulaji na kukaa vijiweni bila kazi.

4.Matumizi ya muda

Ni changamoto kubwa na hasa kwa vijana wengi wa karne hii ya 21. Vijana wengi wanamwomba Mungu ili awafanikishe katika mambo mbali mbali laikini wakishafanikiwa  wanakuwa wazembe  kutekeleza maono  wanayopewa. Vijana wengi wanaendekeza usingizi na uzembe katika masomo na katika kazi. Wanafunzi wengi hawasomi wabidii  analala sana na matokeo yake anafeli mitiani inakuwa hasara kwake na kwa wengine na kuharibu ushuhuda. Vijana wakati umefika tuamke  tufanye shughuli za maendeleo tusome kwa bidii  tuache kuwa na fikira potofu ili kufikia malengo yetu.

“ Usipende usingizi usije ukawa maskini, fumbua macho yako nawe utashiba chakula”.[Mithali 20:13]

 

5/UGUMU WA MAISHA

Maendeleo ya sayansi na teknolojia  yamewaathiri vijana  moja kwa moja kwani yamepelekea vijana kukosa ajira kwani baadhi  ya kazi ambazo  zilikuwa  zinfanywa na watu  hapo awli kwa sasa zinafanywa na mashine . hali hii  inawasababshia  vijana wengi  kuwa na maisha  magumu  na matokeo yake wanaingia katika  vitendo viovu  kama wizzi uporaji ujambazi  utapeli na uvutaji wa madawwa ya kulevya na mabinti wanajiingiza kufanya ufuska(kujiuza) vitendo hivi vinahatarisha  maisha  pia ni dhambi.Hali ngumu  ya maisha hijaanza sasa  hata wakati wa Yesu ilikuwepo ilipelekea  hata yuda kupokea  vipande 30 vya pesa na hata vipande hivyo  hakuvitumia.

 “Akavitupa vile vipande  vya fedha  katika  hekalu  akaondoka; akaenda akjinyonga”.[Mathayo 27:5]

Suala la maisha magumu haliwezi kuisha  kwa vijana  kujihusisha  katika uzinzi(kujiuza) bali  ni kwakomba  kwani Mungu wetu anatuwazia mema.

“Unikumbushe  na tuhojian; eleza mambo yako, upate  kupewa haki yako”.[Isaya 43; 26]

  “Niite nami nitakuitikitia, nami nitakuonyesha mambo makubwa ,magumu usiyoyajua”.[Yeremia33:3]

Matokeo yake vijana  wengi wanajihusisha na vitendo  viovu wamefungwa  jera wengine wameuawa na wengine wameathirika kwa magonjwa.vijana tumwombe Mungu na tufanye kazi kwa bidii ili tujikwamue   kwani vijana wakipukutika nani atahubiri injili  nani atalijenga taifa?

T                                              u          f           u          n          g          u          k          e          sasa.

MBINU ZA KUZIKABILI CHANGAMOTO ZA KARNE YA 21ST C

A.KIMWILI

Vijana wanpaswa kujishughulisha na kufanya shughuli  Mbali mbali ili kujikwamua  na ugumu wa maisha 

Vijana wanapaswa  kuepuka kuangalia  picha  chafu kama vile  filamu chafu  na kujiingiza  kwenye  mahusiano  kabla ya wakti  na hata  wakati ukifika  ni vyema  kkumwomba  “Mungu” na si kuingia bila utaratibu.

“Lakini mambo yote na yatendeke  kwa uzuri na kwa utaratibu”.[1wakorintho 14;40]

Kuwa makini na marafiki  au kuacha kufuata mkumbo kwani baadhi  yaani marafiki wanakupotosha.

  “Enendeni pamoja na wenye hekima nawe utakuwa na hekima rafiki wa mpumbavu ataumia.[Mithali13:20]

 Kuachana tamaa ya pesa au mafankio kkutokana na tama vijana wengi wameingia kutafuta utajiri  kwa njia zisizohalali kama vile  njia za kishirikina  na wengine  wamejiingiza  katika wizi  ujambazi ubakaji, mauaji n.k bali wapaswa  kutulia na kutafakari kuhusu maendeleo  na vyema  kuridhika  na vile  ambavyo  Mungu  amekujalia.

 “Usiwe na tabia ya kupenda fedha mwe radhi na vitu mlivyonavyo kwa kuwa yeye mwenyewe amesema sitapungukiwa  kabisa wala sitakuacha kabisa”.[Waebrania 13: 5]

B.KIROHO

-Kumcha Mungu kwa bidii

“Kesheni basi kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu lakini fahamuni neon hili kama mwenye nyumba angalijua ile swala asingeliacha nyumba  yake kuvunjwa.[Mathayo 24:42-43]

“Dumuni sana katika kuomba mkikesha katika  kuomba huku  na kushukuru”.[Wakolosai 4:2]

-Ukiomba usipojibiwa  au Mungu akichelewa kujibu usimkasirikie  wala kumwazia  kwa upmbavu tene usiwaonee wivu wenzako wanaojibiwa  maombi yao  maana Mungu  humjibu kila mtu  kwa wakati wake kwani si kila  ombi hujibiwa  kama mwombaji anavyotaka.

-Ukiwa na shida usitoke rohoni na kuingiamwilini  na kuanza kutafuta  majibu ya tatizo lako

“ Basi sarai  mkewe Abrahamu hakumzalia mwana  naye alikuwa  na mjakazi mmisri jina lake  hajiri sarai akamwambia  Abram  basi sasa Bwana amenifunga tumbo nisizae,umwingilie  mjakazi wangu labda nitapata uzao kwa yeye .Abram akasikiliza  sauti ya srai  sarai mkewe Abramu akamtwaa hajiri mmisri mjakazi wake baada ya kukaa Abram katika nchi ya kanaani miaka kumi akampa Abram mumewe awe mkewe, asi akamwingilia hajiri naye akapata mimba  naye alipoona ya kwamba amepata mimba  bibi yake alikuwa duni machoni pake….. sarai akamtesa naye  akakimbia kutoka mbele yake”[Mwanzo 16:1-4]

-Kuzishinda tamaa za mwili na kuepuka maneno machafu. Vijana wanapaswa  kujizuia  na si kujiendekeza  lakini njia ya kuyashinda  ya dunia ni  kwa maombi  maana  shetani  amepandikiza  roho za uzinzi na uasherati  kwa vijana  na kuwafanya  vijana kuangamia  kwa magonjwa  kama vile  ukimwi, kaswende kisonono  pangusa n.k

“ Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja  na mawazo yake  mabaya na tama zake………”.[Wagalatia 5:24-25]

 “Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kutakaswa kwenu mwepuke na uasherati”[Wathelonike 4:3]

-kujipambanua nafsi 

vijana wanapaswa kujitambua wewe ni nani na wajibu wako ni nini? Na umeumbwa kwa kusudi gani/

“ lakini kama tumejipammbanua nafsi zetu  tusingehukumiwa,ila tuhukumiwapo tunarudiwa na Bwana isije ikatupasa adhabu”.[1wakorintho 11;31]

-Vijana hawana budi kutambua  hatima ya maisha yao hapa duniani

“ Kwa jasho la uso wako utakula chakula  hata utakapoirudia ardhi ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana  u mavumbi  wewe  nawe mavumbini utarudi”.[Mwanzo 3:19]

-Kuwa na msimamo thabiti na kusoma neno la Mungu na kulitendea kazi

-Vijana wanapaswa  kuwa na imani  thabiti isiyo na mashaka  kwani Mungu hapendezwi na watu wenye mashaka.

 ‘’Basi imani ni kuwa na hakka ya mmbo yatarajiwayo ,ni ayana ya mambo yasiyoonekana…… kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu  ulimbwa na Mungu  kwa neon  la Mungu hata  visivyoonekana”.[Waebrania 11:1]

kama umeamua kuokoka basi okoka  kweli hata ujaribiwe  usirudi  nyuma  bali mllie Mungu kwani yeye ndiye  muwez a wa yote. 

   ‘’Maana kama vile mwili pasipo na roho umekufa vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa”.[Yakobo 2:26]

MADHARA YA UTANDAWAZI KWA  KANISA LA LEO

-Mmomonyoko wa maadili

-Kanisa limekuwa la kisasa mno yaani roho mtakatifu haachiwi nafasi  ya kuongoza.

UTIMIILFU WA UNABII WA UJIO WA MASIHI

Ujio wa Masihi  ulitabiriwa  toka kipindi cha agano la kale. manabii wengi walitumiwa  na Mungu  kutabiri  dalli  na matukio  kadhaa wa kadhaa  yatakayotoke. kwa wakatii ule unabii uliilenga zaidi miji mbali mbali  ya Israel iliyokuwepo wakati ule lakini pia ulilengasiku za mwisho.

 KUZALIWA KWA YESU

Yesu alizaliwa Bethelehem ya uyahudi mji ambao mwanzoni ulikuwa mdogo kilometa chache kusini ya yerusalem. Ulikwisha kuwa mji wakati wa yakobo  jirani na mji huo kulikuwa na mahali ambapo yakobo alimzika  mke wake rahel.

“Akaja rahel akazikwa katika njia ya efrathi ndiyo bethelehem, yakobo akasimamisha nguzo  ya kaburi la raheli hata leo”.[Mwanzo 35:19-20]

Mji wa bethelehem ulikuwa katika eneo la kabila la yuda. Nchi yake ilikuwa ya milima  lakini ilifaa kwa kulima  nafaka  na kufuga kondoo 

  ‘’Ikiwa zamani za waamuzi walipoamua  kulikuwa na njaa katika nchi. Akaondoka mtu mmoja  akaenda mi wa bethelehem ya yuda akaenda kukaa nchi ya moabu, yeye na mkewe na wanawe wawili”.mfalme mkuu wa Israel Daudi alitoka bethelehem [Ruth 1:1]

“ Basi Daudi alikuwa  mwana wa yule mwefrathi wa bethelehem ya yuda aliyeitwa jina la yese; naye huyo alikuwa  na wana wanane; nay eye  mwenyewe alikuwa mzee siku za sauli na mkongwe miongoni mwa watu”.[1 samwel 17:12]

Hata Masihi aliyeahidiwa alizaliwa huko; manabii wengi walitabiri kuwa  Masihi yaani yes Kristo attazaliwa huko.

“Bali wewe bethelehem efrathi aliyemdogo kuwa miongoni mwa elfu za yuda; ktoka kwako wewe utanitolea  mmmoja atakayekuwa  mtawala katika Israel; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zama za kale tangu milele”.[Mika 5:2]

Wakati wa utimilifu wa unabii huu wa kuzaliwa  kwa Masihi “Mungu” aliwataarifu mamajusi pamoja na wachungaji wa makondeni na walikwenda kumsujudia Yesu bethelehem,hivyo basi Mungu akitaka akutumie haangalii sura mazingira wala kabila wala elimu bali  utayari wako. Kwa wakati ule  wachungaji waa makondeni walikuwa  ni watu wa hali ya chini. Walikuwepo wasomi kama  waandishi na mafarisayo lakini Mungu  hakuwa taarifu hao kwanza.

 

YESU KRISTO

Jina la Yesu lilikuwa ni jina la kwaida la kiyahudi nalo lilionekana katika  lugha ya kiyunani ya agano jipya likiwa sawa na jina la “Yoshua” la kebrania katika agano la kale. Maana ya jina la “Yesu” ni “Yahweh” (YEHOVA) ni mwokozi wetu na      hivyolilifaa kuwa jina kwa yeye ambaye aliokoa watu wake yaani wenye dhambi.

 “Naye atazaa mwana nawe utamwita jina lake Yesu, maana yeye ndiye atakayewa okoa watu  wake na dhambi zao”.[Mathayo 1:21]

 

Kristo lilikuwa neno la kiyunani lililokuwa sawa na neno kiebrania  Masihi

MASIHI

Neno Masihi linatokana na lugha ya kiebrania na maana yake ni mpakwa mafuta. Wana wa Israeli wakati wa agano la kale walifanya sherehe ya kukupakwa mafuta kwa mfaime. Makuhani na marunyinoine kwa manabii kwaajili ya kuwaweka raomi katika huduma zao. Katika sherehe za namna hiimafuta ya pekee ya kazi hiyo yalimiminwa kichwani pa mtu akiwa ishara ya kuwa  tumon wakati huo alikuwa na haki na madaraka  ya kutekeleza huduma iliyolingana na wito wake .

 “Mwite huyo  nduguyo  Haruni na wanawe nao mavazi hayo nawe watie mafuta na kuwaweka kwa kazi takatifu na kuwatakasa ili kunitumikia mimi katika kazi yaukuhani”.[Kutoka 28:41]

 “Na Yesu mwana wa Nimoihi mtie mafuta awe mfalme wa Israel. Na Elisha mwana shafati wa Abel mehola mtie mafuta awe nabii mahali pako”.[1Wafalme 19.16]

Wakati wa agano jipya nchi zilizokuwa zinatumia lugha ya kiyunani neno la kiebrania kreno nalo pia        lilikua na maana ya mpakwa mafuta 

WAKATI WA AGANO LA KALE

Wakati wa agano la kale neno mpakwa mafuta  lilitumiwa  zaidi kwa mfalme wa Israel ambaye ambaye mara nyingi aliitwa mpakwa mafuta

“Tazama leo hivi macho yako yanaona jinsi Bwana alivokutia mikononi mwangu pangoni na watu wengine wakaniambia   nikuue; lakini nikakuacha ; nikasema sitaki kunyoosha mkono wangu  juu ya Bwana  wangu; kwa  maana yeye ni “Masihi” wa “Bwana”.[1Samwel 24.10]

Katika kipindi cha kwanza taifa la Israel lilikuwa kama ukoo mkubwa tu. Mungu alionyesha  kwamba  uongozi wa taifa kwa wakati wa usoni ungekuwa katika  kabila la Yuda. Kutokana na kabila  hilo angepatikana ambaye  angetawala Taifa na kwa amani mafanikio na furaha tele.

“………………………………….fimbo ya enzi haitaondoka  katika  yuda wala mfanyashria  kati ya miguu yake, hata atakapo kuja yeye mwenye milki ambaye mataifa  watamtii atafunga punda wake katika mzabibu mzuri amefua nguo zake  kwa mvinyo  na mavazi yake  kwa damu a zabibu” karne kadhaa baadaye Mungu alikutekeleza  unabii huo kwa kumwahidi   mfalme Daudi (aliyekuwa mtu wa kabila la yuda) ufaalme wa ttofauti yake  ambao ungekuwa ufalme wa milele.[Mwanzo 49:10]

‘’Na nyumba yako na ufalme wako vinathibitishwa milele mbele yakonacho kiti chako kitafanywa  imara milele  kwa maeno hayo yote ndiyo na maneno hayo yote,ndiyo nathani alivyonena na Daudi”[2Samwel 7:16-17].

WaIsrael waliishi kwa kutazamia wakati ambapo maaui wote wangeangamizwa  na mfalme  bora angetawala kwa amani na haki ulimwenguni kote. Mfalme na mwokozi Yule angeitwa “MASIHI”

Mungu alipomwahidia Daudi ufalme wa pekee pia aliahidi kwamba  angemtendea mwana na mfuasi wa Duadi  kama mwanawe  yeye Mungu

“Mimi nitakuwa baba yake atakuwa mwanangu;akitenda  maovu nitamwadhibu kwa fimbo ya binadamu na kwa mapigo ya wanadamu”[2 samwel7;14]

Wa Israel waliona kuwa kila ushahidi juu ya maadui zao kama mfan wa ushindi  muu wa  ushindi  mkuu wa Masihi na uwekaji wa ufalme  wake. Waliwasifu  wafalme wao katika lugha  ilivyokuwa  ya hali  ya juu. Zaidi hata iwe  kweli kwa wafalme  waliohusika. WaIsrael waliyatazamia mambo makuu katika ufalme wao.lakini kwa  utimilifu wake  ulimhusu mfalme mkamilifu yaani “Masihi”.

 

TAFSIRI MBALI MBALI  ZILIZO MHUSU  MASIHI

Utabiri Uliotabiriwa na Manabii haukutimilizwi  katika ufalme  wowote  wa kipindi  cha mfalme  wa Daudi katika agano la kale  lakini jambo  hili haliku            wakatisha  tama siku zote walitazamia  Yule  ambaye  angekuwa  “ Daudi” mkuu wa wakati ujao

 “………maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,tumepewa  mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme  utakuwa begani mwake; naye ataitwa  jina lake mshauri wa ajabu, Mungu  mwenye  nguvu, baba wa milele mfalme wa amani  maongeo ya enzi yakena amanii  hayatakuwa na mwisho kamwe, katika kiti cha enzi  cha Daudi  na ufalme wake……”[Isaya 9: 2-7]Mfalme huyo alikuwa Yesu Kristo

“Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristomwana wa Daudi  mwana wa Ibrahimu”[Mathayo 1:1]

Wayahudi waliitafsiri zabuburi  ya 110 wakati wa Yesu kuwa zaburi hiyo ilimhusu  Masihi ingawa  waliukataa. ‘ Umasihi wa Yesu “ kwa kuwa mfalme  wa zaburi 110 pia alikuwa  kuani Yesu hakuwa mfalme  wa Umasihi  tu bali pia kuhani wa umasihi.   

‘’Bwana ameapa, wala hataghairi ndiwe kuhani hata milele, kwa mfano wa melkizedeki’’ [Zaburi 110:4]

Utawala wa Yesu wa muungano wa ukuhani na ufalme wa unabii uliotabiriwa katika kitabu cha nabii Zakaria.

 “Ukamwambie ukisema Bwana wa majeshi anasema hivi yakwamba tazama mtu huyu ndiye ambaye jina lake chipukizi naye atakuwa katika mahali pake  naye ataliinua hekalu la Bwana, naamu yeye atalinoa hekalu la Bwana. Naye atachukua huo utukufu ataketi akimiliki katika kiti chake cha enzi na kuta kuwa na kuhani katika kiti chake cha enzi na shauri la amani litakuwa kati ya hao wawili”.[Zakaria 6:12-13]

YESU NA WAYAHUDI

Yesu alikuwa Masihi kakini hatangaza uMasihi  wake hadharani   kwani wayahudi wakati ule  walikuwa na uelewa  kinyume kuhusu Masihi wayahudi hawa kujali sana kazi ya kiroho ya Masihi kwani wao hawa kutazamia kiongozi wa kiroho ambaye ange waokoa watu kutoka katika utumwa wa adui shetani na kuwaweka chini ya utawala wa Mungu. Badala yake walitazamia kiongozi wa siama ambaye angewaokoa kutoka katika malaka ya warumi na kuleta ufalme mpya na uhuru waa Israel ambao ungekuwa wa amani , uliuvu na mafanikio.

“ basi walipo kutanika wakamuuliza wakisema je’ Bwana wakati huu ndipo utakapo waludishi Israel ufalme akawaambia si kazi yenu kujua nyakati wa majira, baba aliyo yaweka katika mamlaka yake  mwenyewe’’[Matendo 1:6-7]

Aidha kama Yesu angetangaza hadharani kuwa ndiye Masihi kabla ya kuonyesha uMasihiwake angewavuta wafuasi wengi wa aina kinyume

Yesu haku kataa jina la Masihi lakini  alipendelea kulikwepa alipo sema habari ya nafsi yake alipendelea kujiita mwana wa adamu wayahudi wengi walifiri analitumia kumaanisha ni yeye tu kumbe jina hili lilikuwa na maana ya pekee tu kwa wale waliokolewa halihlisi ya ukweli wa Yesu Kristo pamoja na umasihi wake

Lengo la Yesu kujiita mwana wa adamu nikuwafanya watu wafkiri sana nafsi yake na ujumbe wake ulikuwa juu ya nini.

 “Basi makutano wakajibu sisi tumesikia katika toraiti  yakwamba Kristo adumu hata milele nawe wasemaje imempasa mwana wa adamu kuuliwa, huyu mwana wa adamu ni nani [Yohana 12: 34]

Jina mwana wa adamu,linatokana na unabii uliotolewa na nabii Danieli wakati wa agano la kale,“Nikaona katika njozi za usiku natazama mmoja aliye mfano mwanadamu akaja pamoja namawingu ya mbingu,akamkaribia huyo mzee wa siku wakamleta karibu naye akapewa mamlaka na utukufu na ufalme ili watu wa kabila zote na taifa zote na lugha zote wamtumikie,.mamlaka yake ni mamlaka ya milele ambayo hayata pita kamwe na ufalme wake ulio wezwa kuangamizwa [Danieli 7. 13:14] Maana ya mwana wa adamu uliunganishwa ni ile ya ufalme wa Mungu na jambo hili lilikuwa msingi wa maneno ya Bwana Yesu kujiita mwana wa adamu.Yesu alipofika duniani ufalme ulifika duniani. (Ulimwenguni) nakuonekana dhahiri kwa watu wakati huo ulimwengu ulikuwa chini ya nguvu za shetani.

“Ambao ndani yao Mungu wa dunia hii amepofusha fikra zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.[2Wakorintho 4:4]Lakini Yesu aliwaweka watu wote  waliokuwa wamefungwa  na shetani pamoja na wagonjwa  aliiwaweka huru. Hii  ilikuwa ishara ya  kuwa utawala na mamlaka  ya ufalme wa Mungu huweza  kuwaweka watu huru  kutoka katika mamlaka  ya shetani.

“ Naye alikuwa akizunguka  katika Galilaya yote akifundisha katika  masinagogi yao  na na kuihubiri habari njema  ya ufalme na kuponywa ugonjwa  na udhaifu  wa kila namana katika watu”.[Mathayo 4:23-24]

Pia mathayo 12: 28 anasema “ Lakini nikitoa pepo  kwa roho  wa Mungu , basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia”.Ufalme wa Mungu utadhihirishwa  dhahiri  na kupata  maana  halisi  kwa wasioamini wakati Yesu atkaporudi  ili ahukumu uovu  na waovu na kumwondoa  shetani ili  kusimika  utawala wa Mungu  uliyo  wa haki.

“ Basi kama vile magugu yakusanywapo  na kuchomwa motoni; ndvyo itakavyokuwa  katika wa dunia. Mwana wa Adamu  atawatuma malaika zake  nao watakusanya kutoka  katika ufalme  wake maachukizo yote  na hao watendao  maasi  na  kuwatupa  katika tanuru  ya moto  ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Ndipo  wenye haki watakapo ng’aa kama jua  katika ufalme  wa baba  yao mwenye masikio  na asikie”Mathayo 13:40-43]

Lakini maono ya Daniel yanaonyesha kuwa “ mwana wa Adamu “ atashiriki ufalme  wake  na watu wake.

 “ Na ufalme  na mamlaka  na uku wa  ufalme  chini ya mbingu zote watapewa  watu  watakatifu  wake  aliyejuu; ufalme wake ni ufalme  wa milele  na wote wenye  mamlaka  watamtumikia  na kumtii”.[Daniel 7:27]

Wakati mwana wa Adamu yupo duniani aliwaahidi  wale  waliomfuata  kwa kutenda  matendo mema kuwaatashrikiana nao katika ufalme  wake.

 “Yesu akawaambia  amini nawaambia ya kwamba  ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya atakkapoketi mwana wa Adamu   katikakiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi  katika viti  kumi na viwili  mkiwahukumu kabila  kumi na mbili za Israel”[Mathayo 19;28]

MAISHA YA YESU KRISTO

Waandishi wa injili  walitoa maelezo zaidi kuhusianana namna Yesu alivyoishi  na kufundisha lakini hawajaeleza   mfululizo  maalmu  wa maisha yake. Waandishi hao   waliandika katika  vipindi  tofauti  na sehemu  a miktadha(mazingira) mbali mbali.

 “Basi kuna ishara nyingi  alizozifanya  Yesu mbele  ya wanafunzi wake zisizoandikwa  katika  kitabu hiki, lakini  hizi zimeandikwa  ili mpate kuamini  ya kwamba Yesu ndiye  Kristo, mwana wa Mungu na kwa kuamini mwe na uzima  kwa jina lake”[Yohana 20:30-31].

Katika mandishi yao waandishi wote  hawajatofautiana  katika kueleza  nafsi  ya Yesu  kadri walivyotaka  kuionesha. Yesu  ni Mungu  pia ni bawana   na mwokozi wa  ulimwengu.

Masimulizi mbali mbali ya maisha  ya Yesu katika  injili  nne za mwanzo tunaweza kuyagawa katika  sehemu tatu kama ifuatavyo;-

1. Kuzaliwa kwake na utoto wake

2. Huduma yake ya hadharani kama vile  mafundisho yake uponyaji miujiza na mambo mengine    yaliyomhusu Yesu.

3.Matukio ya mateso kifo na kufufuka kwake.

Masimulizi kuhusu Yesu alivyozaliwa katika biblia takatifu yanachukua nafasi  kubwa. Wandishi wa injili hawajaeleza kuhusu  utoto wake mpaka alipopata  umri wa miaka 12. Lakini hata kipindi  akiwa na umri mdogo  Yesu alijua na kujitambua  dhahiri kuwa alikuwana uhusiano  wa pekee na Mungu kwa sababu  alikuwa mwana wa Mungu.

 “ Na alipata umri wake yapata  miaka kumi namiwili walipanda kama ilivyodesturi ya sikukuuna walipokwisha kuzitimiza  siku wakati wa kurudi kwao, Yule mmtoto Yesu alibaki nyuma  hhuko Yerusalemu, na wazee wake  walikuwa hawana  habari…….. nao wote waliomsikia  walistaajabu  fahamu zake na majibu yake ….”[Luka 2:42-49]

Pia waandishi wa injili hawajaeleza juu ya miaka 18 iliyofuata katika  maisha yake. Walianza  kueleza alipokuwa na miaka 30

“ Naye Yesu mwenyewe  alipoanza kufundisha  alikuwa amepata  umri wake  kama miaka 30 ….”[Luka 3:23].Pale mto Yordan Yesu alibatizwa naaliyembatiza alikuwa ni Yohana mbatizaji, Yesu alibatizwa na kuanza huduma yake hadharani. Ubatizo wa Yesu  ulionesha  mambo  makubwa  mawili;-

1.Alikuwa tayari kutekeleza makusudi aliyotumwa na Mungu.

2.Alikuwa na uhusiano na  alijiunganisha  dhahiri  na watu ambao alitaka kuchukua dhambi zao.

Ili kuthibitisha hayo Mungu alimtuma  roho mtakatifu kama njiwa (hua) juu yake

Hii ilikuwa ishara  ya wazi  kuwa alimpa uwezo  wa kuitenda(kuifanya) kazi aliyomtuma.

Mara baada ya Yesu kupokea uwezo wa pekee kutoka  kwa Mungu Yesu alijaribiwa na shetani  ili atumie uwezo wake  pasipokuunganishwa na baba yake lakini Yesu alishinda  jaribu hilo.

“ Kisha Yesu alipandishwa  na roho nyikani ili ajaribiwe  na ibilisi akafunga siku arobaini mchana na usiku mwisho akaona njaa……… ukiwa ndiwe mwana wa Mungu amuru kwamba mawe haya yawe mkate………..imeandikwa mtu hataishi kwa mkate tu ila kwa kila neon litokalo katika  kinywa  cha Mungu………ukiwa mwana wa Mungu jitupe chini kwa maana imeandikwa;atakuagiza malaika zake na mikononi mwao watakuchukua………….”[Mathayo 4:1-11]

Baada ya Yesu kushinda jaribu hilo alianza moja  kwa moja  kufanya kazi aliyokabidhiwa na baba yake.Huduma ya Yesu ilichukua  miaka mitatu na nusu. Yesu alifanya huduma  zake nyingi  galilaya kwa sasa ni sehemu za kaskazini mwa Palestina. Alikutana na upinzani mkubwa kutoka maeneo ya kusini mwa uyahudi(uyahudi kusini) hasa mjini yerusalem mji ambao  yalikuwa makao makuu ya mamlaka ya dini ya kiyahudi.Viongozi wa kiyahudi waliona kuwa Yesu  kuitwa mwana wa Mungu kama ni kufuru hivyo walipinga asiitwe masihi.

‘’mbona asema hivi?Anakufuru.Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmojandiye Mungu?”[Marko 2:7]

Yesu aliijua kuwa mwisho wa huduma  yake angeuawa na wayahudi  wa Yerusalemu; lakini alitambua kuwa alipaswa kumaliza  kazi aliyotumwa na Mungu(baba yake) na baada  ya kumaliza kazi ile  kwa wakati maalumu uliopangwa  na baba (Mungu) ulipofika aliacha wayahudi wamkamate  na kumsulubisha.

 “Basi wakatafuta kumkamata; lakini hakuna mtu aliyenyoosha  mkono wake ili kumshika kwani sababu saa yake ilikuwa haijaja bado”.‘[’Yohana 7: 30]

KUFA KWA MASIHI NA KUFUFUKAKWAKE

Wanafunzi wa Yesu hawakuelewa kuwa Yesu alipaswa  kufa na hata wayahudi wengi walijua unabii wa agano la kale kuhusu  mtumishi wa Mungu  aliyeteswa sawa sawa na walivyojua unabii kuhusu  Masihi wa Mungu  lakini hawakuunganisha  mambo yote  mawili yaani unabii wa mwana  wa Mungu  aliyeteswa na unabii wa Masihi.

“ Tazama mtumishi wangu alitenda  kwa busara, atatukuzwa na kuinuliwa juu naye atakuwa juu sana”.[Isaya 52: 13]. Yesu alidhihirisha dhahiri  “ kuwa yeye alikuwa yote yaani mtumishi aliyeteswa  na Masihi  wa Mungu. Aliwambia wanafunzi wake  kuwa alikuwa Masihi na alipaswa kufa.“ Ila nawaambia ya kwamba Elia alikwisha kuja, wasitambue lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao”[Mathayo  17:12]

Kusulubiwa kwa Masihi ilikuwa kinyume cha imani ya kawaida ya wayahudi kwani kwao  waliamini kuwa  “Masihi” ni mbarikiwa wa Mungu kuliko watu wote na mtu aliYesulubiwa  waliamini alilaaniwa na Mungu.“  Kristo alitukomboa katika laana ya torati  kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu;maana imeandikwa, amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti”.[Galatia 3:13]Hivyo imani ya wa kristo ya kumwamini  Yesu aliYesulubiwa  ikiwa ni mwokozi  na Masihi  ilikuwa kikwazo  kwa wayahudi.

Ufunuo wa YesuKristo  ulileta sura  mpya naya tofauti  kwani kitendo cha  kusulubiwa  lilionekana tatizo  kubwa. Hata wanafunzi wake  hawakuelewa  alipowatabiria  kuhusu ufunuo  wake. “ Kwa sababu alikuwa akiwafundisha  wanafunzi wake  mwanan wa Adamu  yuaenda  kutiwa katika  mikono ya watu  nao watamwua; hata akiisha kuuawa  baada  siku tatu atafufuka, lakini hawakulifahamu  neon lile wakaogopa kumwuliza”.[Marko 9:31-33].Alipofufuka alithibitisha tosha kuwa Yesu alikuwa “mwana wa Mungu” na “mpaka mafuta” wa kweli toka kwa Mungu.“Yeye mwenyewe alitangulia kuyaona haya alitaja habari za kufufuka kwake Kristo ya kwamba roho yake haikuachwa kuzima wala mwili wake haukuona iharibifu”.[Matendo 2:31]

 

 

UJIO WA MASIHI WALIVYO CHUKULIA WAKATI WA AGANO LA KALE

Wa Israel  wa wakati wa agano la  kale  walitazamia  siku ambbayo  Mungu  angechukua  hatua  katika mambo yote  ya wanadamu akitengeneza yaliyo kinyume na kuimarisha  utawala  wake  duniani waliita tukio  hilo  “ Siku ya ya Bwana”  ingawa siku ya Bwana kwa kawaida   ilifikiriwa kuwa jambo la kutisha   waIsrael  mara nyingi waliitazamia  kwa sababu maadui  zao na kuwaletea  waIsrael wakati wa  Baraka kubwa.

“ Hivyo siku ya Bwana ilivyo kuu i karibu, nayo inafanya  haraka sana; naam sauti ya siku ya Bwana  shujaa hulia kwa uchungu  mwingi  huko! Siku ile siku ya ghadhabu,siku ya fadhaa na dhiki, siku ya uharibifu na ukiwa, siku ya giza  na utusi tusi, siku ya mawingu  na giza  kuu”.[Sefania 3;14-15].Lakini walishindwa  kutambua  kuwa siku hiyo  Mungu angewaadhibu wenye dhambi wote pamoja na waIsrael na kuokoa wote walio waaminifu bila kujali taifa lao wala hali yao katika jamii.“Ole wenu ninyi  mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana; ni giza wala si nuru”.[Amosi 5:18]

Mambo mbali mabali ya kutisha kama  vile  mafiriko  ya naji njaa kali vita  waliita siku ya Bwana. Lakini maarifa  kama hayo yalikuwa ni utangulizi wa siku ile kubwa  na ya mwisho.‘’Nami nitaonyesha mambo ya ajabu  katika mbingu  na katika dunia,damu  na moto  na minara ya moshi. Jua litageuzwa kuwa giza  na mwezi kuwa damu kabla haijaja siku ya Bwana  iliyo kuu itishayo. Na itakuwa  kwamba  mtu awaye yeyote atakayeliita jina la Bwana ataponywa; kwa kuwa katika mlima sayuni na katika yerusalem watakuwako watu watakaookoa kama Bwana alivyosema; na katika mabaki hao awaitao Bwana”.[Yoel 2;30-32]

KURUDI KWAKE KRISTO KWA SHANGWE NA USHINDI

Kurudi au ujio wa Kristo mara ya pili  ni kilele cha mambo yote aliyoyafanya wakati yupo duniani na huo ndio utakuwa  utimilifu wa mambo yote  yaaani ushindi juu ya dhambi mauti na shetani wokovu wa wandamu kipawa cha uzima wa milele uponyaji wa ulimwengu wa viumbe vinvyoonekana na kusimamishwa kwa ufalme wa Mungu“ Na hao watakwenda zao kuingia katika Adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.[Mathayo 25;46]

Kurudi kwa Yesu (Masihi)mara ya pili “siku ile ya Bwana  ya mwisho” ambayo kilele cha historia  ya ulimwengu.“Naye Bwana  atakuwa mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja na jina lake moja. [Zakaria 14:9]

Wakati  wa agano la kale na agano  jipya manabii walitabiri kuharibiwa kwa miji tofauti ya wakati ule ambayo ilikuwa  imejaa uasi na dhambi kama vile kuangamizwa kwa Yerusalemu. Nji wayerusalem ulikuwepo tangu miaka mingi  na katika  kiindi hicho Yerusalemu ilibadilka mara nyingi mabonde yalijazwa  milima ilichonga  milima mingine  ilitokea kutokana mafungu ya kifusi  na takataka  na mipaka  ya Yerusalemu  ilibadilika kutoka kizazi kimoja  na kingine. Lakini sura ya mji uliojengwa  juu ya  mwinuko usio sawa uliendelea vile vile tangu wakati wa biblia.

Hapo mwanzo mji wa Yerusalemu ulijuulikana  kwa jina  lake fupi la  “Salemu” nao ulikuwa mji wa melekizedeki aliyekuwa mfalme  na kuhani wake.“ Na melkizedeki mfalme wa  salemu akaleta mkate  na divai, naye  alikuwa kuhani  wa Mungu aliyejuu sana”[Mwanzo 14:18]

WaIsrael wlipoingia kanaani  mji huo ulikuwa  na wayebusi  nao uliitwa  yebusi. Mara ya kwanza  waIsrael waliuteka  mji huo  pamoja  na maeneo yake, baada ya muda mfupi  wenyeji wa asili  waliuteka tena. Nji huu ulikuwa katika  eneo la urithi la Benyamini lakini wayebusi waliumiliki  mpaka wakati wa  enzi ya Daudi.“ Tena katika habari ya wayebusi, hao wenye kukaa Yerusalemu, wana wa yuda hawakuweza  kuwatoa; waliokaa pamoja  na wana wa yuda huko Yerusalemu hata hivi leo”.[Yoshua 15: 63]

Mfalme Daudi alikuwa na makusudi mbali mbali yaliyopelekea  kuuteka mji wa Yerusalemu na kuuweka uwe makao maku ya  ufalme wake. Na kwa wakati huo Yerusalemu ni nji ambao haukumilikiwa  na kabila  lolote la Israel.Wayebusi walidhani mji wa Yerusalemu  usingeweza kutekwa  lakini mashujaa wa  Daudi waliuteka  kwa mashambulizi  ya kushtusha. Waliingia Yerusalemu  kwa kuitia  kwenye pango  ambalo wayebusi  walilitumia  kwa kuleta maji  mjini kutoka  nje ya ukuta wa mji.“ Lakini Daudi aliipiga ngome  ya  sayuni; huu ndio mji wa  Daudi . naye Daudi alisema  siku hiyo yeyeatakatewapiga  wayebusi  na apande  kwenye mfereji  wamaji  na kuwapiga  na hao vipofu ambao roho yake Daudi inawachukia. Kwa sababu hii watu husema wapo vipofu  na viwete  hawawezi kuingia nyumbani. Basi Daudi akaa ndani ya ngome hiyo akaiita mji wa Daudi  kasha  Daudi  akajenga toka  milo na pande za ndani….”[2samwel 5: 7-10]

Malengo ya Daudi yalikuwa kufanya Yerusalemu kuwa  makao makuu ya serikali   na dini pia. Aliweka sanduku la Agano katika hema la pekee  alilokuwa  ameliweka  mjini kwajili  ya makusudi hayo.“Wa kaliingiza sanduku la Bwana  na kuliweka  mahali pake katikatiya hema,aliyoipiga Daudi kwa ajili yake, naye  Daudi akatoa sadaka  ya kuteketezwa  na sadaka za  amani  milele  mbele za Bwana”.[2Samwel 6:1-17].Daudi alifanya mpango kwa ajili ya mwanawe ambaye angerithi  kiti chake  cha enzi  ili ajengehekalu  la kudumu.

 Baada ya sulemani kurithi kiti cha enzi cha mfalme  Daudi aliufanya nji wa  Yerusalemu  uwe nji wa ufahari  uletao sifa kwa taifa lote na alijenga  jengo kubwa la kifalme  na majengo mengine yenye ufahari. Lakini  siasa yake  ya kunyanyasa watu  kuwalazimisha kufanya kazi bila malipo yeyote na walipe kodi nyingi   alijenga mawazi ya uasi miongoni mwao matokeo yake  makabila  mengi  ya Israel  yalijitenga na Yerusalemu  baada  kufa kwake  Sulemani.

 “Baba yako alifanya zito kongwa letu basi sasa utupunguzie utumwa mzito tuliotumikishwa na baba yako na lile kongwa zito alilotutwika nasi tutamtumikia……….”[1falme 12:1-19]

Makabilamawili tu yalisalia na uaminifu wao kutoka kwa mfalme Daudi  kwa pamoja  yaliitwa ufalme wa yuda na mji wao  mku ulikuwa Yerusalemu  kama ilivyokuwa  awali.Makabila menginekumi yalijiita Israel yakaimarisha utawala   wao kaskazini wakiwa na mji wao mkuu pamoja na  kanuni  na dini zao.

Mwaka 605 Kabla ya Kristo(KK) mji wa Yerusalemu  uliwekwa chini ya utawala  wa Babeli na baada  ya kufanya maasi mara kwa mara   mi wa Yerusalemu ulibomolewa na wababeli mnamo mwaka 587 Kabla Kristo.Ikawa katika mwaka wa kenda wa kutawala kwake, katika mwezi wa kumi na siku ya kumi ya mwezi huo, Nebu kadreza mfalme wa Babeli akaja yeye na jeshi lake  lote  kupigana na Yerusalemu akapanga hema zake kuukabiili…… basi nji huo ulihusuriwa hata mwaka wa kumi  na moja wa mfalme sedekia’’[2 Wafalme 25:1-12]

Mwaka wa 539 Kabla Kristo waajemi waliwashinda  na kuwapindua wababeli  wakawapa wafungwa wote uhuru. Wayahudi walirudi katika  nchi yao  wakaanza kujenga  Yerusalemu  kwa upya.“ Kisha nikawambia mnaona hali hii dhaifu tuliiyonayo jinsi Yerusalemu ulivyo hali ya ukiwa  na malango yake yalivyoteketezwa  kwa moto; haya na tuujenge tena  ukuta wa Yerusalemu  ili tusiwe shitumu tena”.[Nehemia 6:17]

Miaka michache baadaye(iliyofuata) wayahudi  walijenga hekalu upya pamoja na  mji wenyewe  na kuta  zake  kama  ilivyooneshwa  hapo juu. Nehemia alipomaliza kazi yake  historia  ya Yerusalemu  katika Agano la kale ilifikia  mwisho wake. Mwaka 333 Kabla Kristo Iskanda mkuu alishinda mfalme wawaajemi na  mwaka  uliofuata aliikuwa mtawala mkuu wa Yerusalemu  lakini baada ya miaka michache tu ufalme  wa uyunani uligawanyika. Upande wa mashariki kullikuwa nasehemu mbili yaani misri na shamu(syria) hivyo palestina ilitawaliwa na wamisri mpaka mwaka 198Kabla Kristo na baadaye Shamu.

Mwaka wa   168Kabla Kristo mapigano yalitokea miongoni mwa  makundi  mbali mbali ya wayahudi wa Yerusalemu mtawala   wa shamu  Antioko IV  Epifania  alitumia nafasi ile kushambulia Yerusalemu  na kuua wayahudi wengi lengo lake  ilikuwa aharibu dini ya kiyahudi. Baada ya kujenga madhabahu ya kiyunani katika hekalu la wayahudi  alichukua wanyama walikuwa najisi na haramu kwa wayahudi  na kuwatoa sadaka  kwa miungu ya kiyunani.Wayahudi walikuwa chini ya uongozi wa wamakadayo walikusanya jeshi la kumpinga Antioko. Baada ya miaka 3 ya vita  vya kupigania uhuru, wayahudi  walipata uhuru wakidini wakatakasa hekalu upya.

Mwaka  165 Kabla Kristo wamakabayo waliendelea kupigania uhuru  mpaka miaka 20 baadaye  wakapata uhuru kamili.Miaka 80  iliyofuata  Yerusalemu uliendelea kuwa  uhuru lakini  migongano ya wayahudi kwa wayahudi  mwishoni ilileta warumi ambao mwaka 63Kabla Kristo walibomoa hekalu na kuchukua  utwala  wa Yerusalemu.warumi walimweka mtawala juu ya Palestina  aliyeitwa Herode ambaye alisaidiwa  na serikali ya Rumi kufanya kazi ya kujenga  upya mji  wa Yerusalemu kwa muda  mfupi kabla ya wakati wa agano  la jipya.Kwa wayahudi  kazi yao kubwa  ilikuwa  ujenzi wa hekalu  jipya  baada  ya  kubomolewa  kwa hekalu  la zerubabeli na warumi  mwaka wa 63 KK lilijengwa  mahali pa mahekalu  yaliyotangulia  lakini lilikuwa  kubwa na zuri  zaidi. Kazi yake ya ujenzi  ilichukua zaidi ya miaka  40 muda mrefu  baada ya kufa HERODE.

“ Basi wayahudi wakasema , hekalu hili lilijengwa  katika  muda wa  miaka arobaini  na sita  nawe utalisimamisha  kaika siku tabu”.[Yohana 2:20]

HISTORIA FUPI YA YERUSALEMU  YA HIVI KARIBUNI

Mwaka 66 KK kulikuwa na maasi dhidi ya warumi yaliyoendeshwa na  kundi la wachokozi wa kiyahudi  matokeo yake warumi walishambulia Yerusalemu  kwali ukali wa kijeshi. Mwaka 70 Baada Kristo sehmu kubwa ya nji  pamoja na  hekalulibomolewa kama yeru alivyokuwa ametabiri.

 “Alipofika karibu  aliuona mji akaulilia akisema laiti ungelijua hatawewe katika siku hii  yapasayo amani!lakini sasa yamefichwa  machoni pako. Kwa kuwa siku zitakuja adui zako watakapokujengea boma.likuzunguke watakuzingirana kukuhusuru pande zote watakuangusha chini wewe na watoto wako  ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe  kwa sababu  hukutambua majira  ya kujiliwa kwako”.[Luka 19:41-44 ]

Warumi walijenga Yerusalemu upya mwaka 132 Baada ya Kristo  wakatangaza uwe mji wa kitaifa ambamo wayahudi  hawakuwa na ruhusa  ya kuingia.Kostantino alipokuwa kaisari wa warumi mwaka 313 Baada ya Kristoalitangaza Yerusalemu uwe uwe mji wa Kristo. Mwaka  wa 637 Baada Kristo waislamu waliuteka mji wa  Yerusalemu  na mwaka 691BK walijenga msikiti wao mahali  pale pale ambapo  kwanza palikuwa na hekalu la  kiyahudi.Mwaka 1542 Baada ya Kristo mtawala wa waislamu alijenga kuta za mji upya zilizopo mpaka leo. Mji wa Yerusalemu ulendelea kuwa chini ya  utwala  wa waislamu  mpaka mwaka 1967 BK  ambapo waIsrael walichukua mji wao tena. Msikiti juu yya kilima cha hekalu mpaka sasa upo.

Kurudi kwa Yesu  Kristo duniani  ni sehemu ya  mpango  wa Mungu  kuhusu  wokovu  wa wanadam.  Wakati wa Yesu  wanafunzi  wake  walidadisi  sana  na walitaka  kujua lini  hasa  atakaporudi  tena  mwana wa Adamu, Mafarisayo waliamini hasa juu ya  kiama  ya wafu  ila  walihitaji  mtu sahihi  ambaye  anaweza  kuelezea  zaidi au kutoa ufafanuzi  juu ya  kutokea kwake.Bwana Yesu alidokeza  juu ya dalili za kutokea  kwake na  kwa sababu  alikuwabado  yupo duniani  alitamka dhahili  au wazi kuwa  mipango tote ilikuwa  mikononi mwa  baba yake.“Si kazi yenu kujua nyakati wala majira baba aliyoweka katika mamlaka  yake mwenyewe”.[Matendo 1:7]

Wayahudi wengi  hawakuamini kuwa  Yesu ni Masihi  wengi waliogopa kushushwa  vyeo vyao hasa watawala kwani walifikiri utawala  wake  ni wa dunia  hii.‘’Basi walipokusanyika  wakamwuliza wakisema je! Bwana wakati huu ndipo unaporudishia Israel ufalme?”.[Matendo 1:6]Lakini Yesu alieleza kuwa  ufalme wake  si wa dunia hii,mapokeo ya yesu yalikuwa ya tofauti kwani wengi walijua anakuja kuwarudishia Israeli utawala toka kwa warumi.

 SABABU ZA KURUDI KWA YESU AU MASIHI

1.Kulichukua kanisa au kuwachukua  wateule wake

 “Kwa maana waitwao ni wengi bali wateule ni wachache”[Mathayo 22:14]

2.Kuamua vita

 “Basi hapo mtakapoliona chukizo  la uharibifu  lile lililonenwa  na nabii Daniel limesimama katika patakatifu asomaye na afahamu ndipo walio katika uyahudi na wakimbilie milimani”.[Mathayo 24:15]

Nabii Daniel unalenga kutekwa kwa mji wa  Yerusalemu hapo ndipo  vita itakapozuka  duniani na vita hiyoatakayekuja kuiamua ni Yesu pekee.

3.Kuwahukumu walio hai na wafu

     “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka na tzama farasi mweupe nay eye aliyempanda aitwaye mwaminifu na wa kweli naye kwa haki ahukumu………”[Ufunuo 19:11]WaKristo wa kipindi cha Agano la kale  hawakuwa na ujuzi wowote  kuhusu  uzima wa milele  ingawa mara nyingine  walionyesha  matumaini yao  ya ufufuo  ambao kwa njia yake wangeokolewa  kutoka mautini. Pia walitazamia ufufuo kwa ajili ya watu  waovu ambao wangehukumiwa  na kupata adhabu “Tena wengi wa hao walalao katika mavumbi ya chi  wataamuka  wengine  wapate uzima  wa milele  wengine aibu  na kudharauliwa milele”[Daniel 12:2]

Wakati wa agano la kale hawakuelewa kuhusu uzima wa milele   kwa sababu Yesu alikuwa bado  hajazaliwa.  Lakini kwa njia ya Yesu  Kristo  Mungu alivunja  nguvu za  mauti na  kudhihirisha  hali ya uzima wa ufufuo. “ Basi kwa kuwa watoto  wameshiriki damu na mwili yeye naye  vivyo  hivyo  alishiriki yayohayo  ili kw njia  ya mauti  amharibu  yeye aliyekuwa  na nguvu  za mauti yaani ibilisi awaache huru wale ambao kwamba maisha yao  yote kwa hofu ya mauti  walikuwa  katika hali ya  utumwa”.[Waebrania 2:14-15].Wayahudi wachache yaani masadukayo walikataa kuamini habari yeyote  kuhusiana na  ufufunuo.“Siku ile masadukayo  watu wasemao kwamba  hakuna kiyama ….”[Mathayo 22: 23]

Wokovu ni ufufuo wa kimwili kwa maisha   mapya Yesu  alishinda  dhambi  na mauti na kwa sababu  hii mtu  amwaminiye  Yesu  anaweza   kutazamia  wokovu  kutoka  katika  dhambi   na mauti. “Lakini tukiwa  tulikufa pamija  na Kristo  twaamini  ya kuwa  tutaishi pamoja  naye, tukijua  ya kuwa Kristo   akiisha  kufufuka  katika wafu  hafi tena, wala mauti   haimtawali tena  maana kwa  kule kwake , aliifia dhambi  mara mojatu, lakini kwa kule  kuishi kwake alimwishia Mungu”.[Warumi 6:8-10]

 Mungu alimwumba mwanadamu awe mkamilifu na hivyo anashughulika naye  katika  umoja  wa ukamiilifu wake Mungu  hadanganywi  na mwanadamu katika  sehemu ya  kimwili   na kiroho. Makusudi ya Mungu  kumwuumba mwanadamu   ni ya  milele wala  hayakuunganishwa  na kufa  bali na ufufuo wa kimwili pamoja na uzima wa milele.“Tena wengi wa hao walalao katika mavumbi ya chi  wataamuka  wengine  wapate uzima  wa milele  wengine aibu  na kudharauliwa milelena walio na hekima watang’aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang’aa kama nyota  milele na milele”.[Daniel 12:2]

DALILI ZA UJIO WA MASIHI

1. Chapa 666 au kuuza na kununua kwa kutumia namba 666

Unabii huu ulinenwa na  nabii yohanakuwa siku za mwisho kutakuwa na utaratibu  wa kufanya biashara  kwa kutumia electronic (eletroniki) badala ya pesa  taslimu kutakuwa na  mfumo huu kila  mtu atapewa  nmba itakayo mhusu yeye binafsi  na inayiendana  na  jina lake  na bila  namba hiyo hutaweza kununu kitu chochote.

13/3/2013 marekani walianza  kutumia kitu kiitwacho cheaply ambacho mtu anakivaa  kidoleni au sehemu yeyote  ya mwili  kazi yake ni  kupata  punguzo  kwenye  maduka  makubwa  pia  matumizi  ya ATM kadi  visa  kadi n.k ni utimilifu  wa unabii  huo.

 “ Naye awafanya wote wadogo  kwa wakubwa  na matajiri kwa maskini na walio huru kwa watumwa  watiwe chapa  katika mkono wao wa kuume au katika vipaji vya nyuso zao; tena  kwamba mtu awaye yeyote asiweze  kununua wala kuuza isipokuwa  ana chapa  ile yaani  jina la  mnyama  Yule au hesabu ya jina lake”.[Ufunuo 13: 16-17]

2. Kuanzishwa kwa taifa la Israel,Mnamo mwaka 597 KK Mungu alimpa nabii Ezekiel  ujumbe ufuatao;“ Ukawambie Bwana Mungu asema hivi; tazama nitawatwa wana wa Israel toka kati ya mataifa  walikookwenda  name  nitawakusanya  pande zote  na kuwaleta  katika nchi yaowenyewe”.[Ezekiel 37:21]

 Pia Ezekiel 38:8 anasema “ Na baada ya siku nyingi utawajiliwa;katika miaka ya mwisho  utaingia nchi uliyorudishiwa hali yake ya kwanza  baada ya kupigwa kwa upanga, iliyokusanywa toka kabila  nyingi za watu  wa milima ya Israel……”

Unabii huu ulitimia mwaka 1948 ambapo  kwa mara ya kwanza  wayahudi  kutoka katika pande zote  za dunia  walirudi  na kuingia  katika nchi yao  na kuanza  kudai kuwa  umoja wa mataifa   uwatambue kama taifa. Baada  ya  kuingia  katika nchi yao ilichukua miaka isiyozidi ishirini  kwa Israel  kuwa taifa mashuhuri  lenye nguvu katika  masuala ya kisiasa  kijeshi na kiuchumi katika mashariki ya kati. Hata sasa  ni taifa lenye nguvu.

3. Maarifa kuongezeka ,Mnamo miaka ya 605Kabla ya Kristo na 539 Kabla ya Kristo nabii Daniel alitabiri baada ya kuwa ametoka kifungoni ujumbe ufuatao; “Lakini wewe ee Daniel, yafunge maneno haya ukakitie mhuri kitabu hata wakatiwa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko na maarifa yataongezeka”.[Daniel 12:4]

Mungu alimtumia nabii Daniel kunena kuhusu kuongezeka Kwa marifa Kama dalili mojawapo ya siku za mwisho.katika karne hii ya 21 maarifa yameongezeka kwa kiwango kikubwa mno. Ongezeko la maarifa limefanya ulimwengu uchanganyikiwe Sana. Baadhi  ya vitu  ambavyo  vimeongeza maarifa ni pamoja  na kama vile computer luninga tovuti kittabu cha nyuso(facebook) hivi vyote  tunaviingiza katika  mfumo mzima  wa utandawazi . Lakini utabiri huu ni uthbitisho  kuwa  hizi ni siku za mwisho.

4.Vita kati ya taifa moja na jingine  

Kabla ya Yesu kuondoka duniani alinena ishara ya vita kali kati ya mataifa mbali mbali  kuwa itaibuka. Katika karne ya 20 yaani kuanzia mwaja 1900 hadi sasa vita na uhasama  ulimwenguni  umezidi  kuwa mkubwa  sana. Uhasama huo ndio uliosababisha  hata kutokea  kwa vita  ya kwanza  na  ya pili  ya dunia  mnamo 1914-1918 na 1939-1945. Hata sasa vita na uhasama  vinaendelea  kwa kasi mfano marekani  na korea  kaskazini piaa Israel na palestinahiyo ni dhahili  kuwa kurudi kwake  kumekaribia.

 “Ninyi  mtakaposikia  habarrir za vita na fitinamsitishwe maana hayo hayana budi kutukia kwanza lakini  ule  mwisho hauji upesi kisaha aliwaambia  taifa litaondoka  kupigana  na taifa nyingine na ufalme kupigana  na ufalme”.[Luka21:9-12].Utokeaji wa vita na uhasama ni ,maandalizi ya siku ya mwisho.

5.Ishara ya juu,anga na mwezi na nyota. Nabii Yoel alitabiri miaka ya 835-830 Kabla ya Kristo kuwa kutakuwana ishara  ya jua kabla ya ujio wa Masihi (Yesu) mara ya pili lakini  hata Yesu  alipokwepo  duniani aliwaeleza wanafunzi wake uwepo wa ishara  katika jua na mwezi na nyota; na katika chi dhidi ya mataifa wakishangaa kwa  uvumi wa bahari  na msukosuko  wake waatu wakivunjika  mioyo kw hofu na kwa kutazamia  mambo yatayoupata  ulimwengu. Kwa kuwa  nguvu za mbinguni zitatikisika.” Unabii huu ulianza kutimia kkuanzia karne ya 18 yaani kuanzia miakka ya 1700.

 19/5/1780 ni siku ya ajabu na yenye tukio la aina yake kwani “Anga” lote la kaskazini mashariki mwa amerika lilikuwa giza tupu.3rd Januari 1833 vimondo vilianguka marekani na anga lote  lilijaa vitu vya  kung’aa  kuanzia  saa nane usiku hadi mapambazuko anga  liling’ara na kuwaka.Mwanzoni mwa mwaka 1900 kimondo kilianguka nchini Tanzania katika mkoa wa Mbeya,kimondo hicho kipo hata sasa.Miaka ya 1990s jua na mwezi vilipatwa mchana  saa nane ,anga zima  lilijawa  mwanga mkali nchini Tanzania  watu wengi walihamaki mno.Mwaka 1999 dunia ilihamaki na watu wengi walitegemea  mwaka 2000 ni mwisho wa dunia wengine walijiua lakini haikuwa mwisho wa dunia ila Yesu  mwenyewe alisema japo matukio haya yalitokea ila mwisho hautakuja haraka,hivyo mfululizo wa matukio haya dalili tu za siku za mwisho.

.6.Utengenezaji wa mabom ya atom na silaha za nyuklia.Nabii petro alipewa ujumbe na Mungu  mnamo miaka 68 baada ya Kristo  petro alieleza  kuhussu kurudi  kwa Yesu ili kuwapa uhakika wale waliokuwa wanadharau  habari hizo  waaminio na kumgeukia Mungu.

“Lakini siku ya Bwana itakuja kama  mwivi; katika  siku hiyo mbingu zitatoweka  kwa mshindo mkuu  na viumbe  vya asili vitaunguzwa na kufumuliwa na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea”.[2Petro 3:10-12]

 Kuchelewa kurudi kwa Yesu Kristo ni kwa lengo la  kuwapa nafasi  wenye dhambi ili watubu na kuepuka  hukumu hiyo. Hivyo waKristo  ni vyema  tukaetayari kumlaki akirudi  kwa sababu kila mmoja akatoa hesabu yake mwenyewe . kwa sasa silaha  na mabomu yanatengenezwa  sana hivyo unabii unatumia kwani mwisho wa silaha hizo ni uharibifu. “ Bwana hakawii kutimiza ahadi yake  kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu maana hapendi mtu yeyote apotee bali wote wafikirie toba”.[Luka 3:9]

7.Kuanzishwa kwa umoja wam mataifa,Kitabu cha ufunuo kiliandikwa na yohana .alipofungwa  katika cha patmo si mbali na  pwani ya efeso magharibi ya asia ndogo yohana alipokea  maono  yake  katika  maandiko ya kiufunuo. Mungu  anatoa ufunuo wake kwa watu  kwa njia ya maono ya ajabu yanayoelezwa  na malaika . baada ya kuandika  yahana alituma  mjumbe  katika miji ya bara  ili akapeleke  kwa makanisa saba  ya asia ndogo.

      Katika kitabu cha funuo Mungu ameeleza kuhusiana na kuanzishwa kwa utawala  wa dunia nzima utakao tokea wakati wa siku za mwisho.ufunuo 13: 3-8 anasema “ nikaona kimoja cha vichwa  vyake kana kwamba kimetiwa jeraha la mauti na pigo  lake mauti  likapona. Dunia yote itastaajabia  mnyama  Yule  wakamsujudu Yule joka kwa sababu  alimpa huyo mnyama  uwezo wake ; nao wakamsujudu  Yule mnyama  wakisema  ni nani  afananaye na mnyama huyu? Tena ni nani awezaye kufanya vitu naye? Naye akapew kinywa  cha kunena  maneno  makuu ya makufuru  akapewa iwezo  wa kufanya  kazi yake  miezi arobaini na miwili. Akafunua na  na kulitukana jina  lake  na maskani yake  nao wakaao mbinguni”.Ukitazama kwa undani  umoja  wa mataifa  na miundo yake  ya kijeshi  kiuchumi mashirika  ya fedha  duniani  ulimwengu mzima  unausujudia  umoja wa mataifa  kiuchumi  haata kisiasa  pia hivyo hali hii inatu eleza kuwa na utawala  momoja  ni utimilifu wa dalili za ujio wa Masihi.

8.Kuhubriwa kwa injili kila mahali ulimwenguni,Kutokana na kukua au kuongezeka kwa maarifa (utandawazi) imepelekea  injili ya Kristo kufika kila mahali kwa njia mbali mbali kama redio, luninga, tovuti n.k,“Tena habari njema itahubiriwa katika ulimwengu  wote kuwa ushuhuda kwa mataifa  yote  hapo ndipo  ule mwisho utakapo kuja”[Mathayo  24:14].Hivyo uenezwaji wa neno la Mungu kila mahali  ni utimilifu wa  wa dalili za ujio wa  Masihi na hata atakuja Masihi hakuna atakayejitia kuwa siksia

9.Kupoa kwa upendo nawatu kupenda fedha kuliko kumpenda Mungu. “ Lakini ufahamu wa neon hili ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari maana watu watakuwa ni wenye kujipenda  wenyewe wenye kupenda fedha……………”.[2Timotheo 3:1-6],Watu wengi wana muasi Mungu kwa sababu ya fedha  na hata viongozi wa makanisa  wanagombana kwa ajili ya  fedha. Wengi wanafanya huduma kwa kuangalia fedha kuliko Mungu hivyo ni vyema  tujue kuwa ule  mwisho upo karibu.

Hadi sasa ishara iliyobaki ni moja  tu kutekwa kwa mji wa Israel kwaani  baada ya kutekwa kwa Israel mataifa mbali mbali yataingia kupigana na menginekulisaidia taifa hilo   vita itazuka ulimwengu mzima  na ndipo “mwana wa Adam atakaporejea kuamua vita ya ulimwengu mzima.“Lakinimtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi ndipo  jueni ya kwamba  uharibifu  wake umekaribia ……….wataanguka kwa makali ya upanga  na watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote na Yerusalemu utakanyagwa na mataifa hata majira ya mataifa yatakapotimia”.[Luka 21:20]

Ni wajibu wa kila mmoja  wetu  watoto vijana wazee  kufikiri namna ilivyotabiriwa  hapo awali na utimilifu wake. Ni vyema kila mmoja  ajiulize moyoni  mwake  je (Yesu)Masihi akirudi leo nitakwenda  mbinguni au nitakuwa upande gani?  Kuchelewa kurudi ni nafasi yetu  mimi na wewe kutubu na kutengeneza mambo yetu ili ajapo atukute tukiwa tayari hivyo tujiulize  na tuchukue hatua ya kutubu mapema.

MAMBO YATAKAYO TOKEA YESU (MASIHI) ATAKAPORUDI MARA YA PILI.

1.Kunyakuliwa kwa kanisa,Baada ya ishara zote kukamilika za siku za mwisho Yesu Kristo atarudi duniani  na kuja kwake  kutakuwa kwa awamu  kuu mbili;-

(a)Unyakuo wa kanisa

(b)Ufufuo wa wafu

“Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni  pamoja na mwaliko  na sauti ya malaika  mkuu na parapanda ya Mungu.nao waliokufa  katika Kristo  watafunguliwa  kwanza kasha  sisi tulio hai tuliosalia tutanyakuliwa  pamoja nao katika mawingu,ili tumlaki Bwana hewani na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi farijianeni kwa maneno hayo”.[1Wathesalonike 4:16-18]

Kunyakuliwa kwa kanisa litakuwa tukio  la mara moja yaani la haraka na si watu wote duniani watakaoliona na kuelewa kwa undani utokeaji wake. Unyakuo ndio utakao watenganisha  waamini na wasio amini na baada ya kuwatenganisha  yatatokea mateso ambayo hayajawahi kutokea ulimwenguni.Wale watakao kutwa duniani wakiwa hai watabadilishwa na kupaa kwenda mbinguni wakiungana na watu waliofufuliwa ambao walikufa katika Bwana. Baada ya unyakuo  watakao baki ni wale tu waliokataa  kumwamini Yesu Kristo.

2.Dhiki “ Kwa kuwa wakati huo kutakuwako dhiki kubwa ambayo haijatokea tangu mwanzo wa ulimwengu hata sa”.[Mathayo 24:2].Baada ya kunyakuliwa kwa waumini safi wasio na dhambi  kipindi  cha dhiki kuu kitaanza  na kitaambatana na uanzishwaji  wa wazi wa utwala  wa mfumo wa kifalme. Utawala  huu utjulikana kwa alama ya namba 666 na utaongozwa  na mpinga Kristo ataitawala dunia kwa ukatili  kwa kipindi cha miaka saba(7).

3. Ufufuo wa wasioamini, “Tena wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka wengine wapate uzima  wa milele wengine aibu  na kudharauliwa milele”[Daniel 12:2].Ufufuo wa watu ambao hawakumwamini Kristo wao hawatapewa miili ya kiroho isiyokuwa na uharibifu. Matokeo ya ufufuo wao siyo uzima   bali hukumu, kuadhibiwa na kuangamizwa milele.

 “Nikawaona wafu wakubwa kwa wadogo  wamesimama  mbele  ya hicho kiti cha enzi  na vitabu vikafunguliwa  na kitabu kingine  kikafunguliwa  ambacho ni cha uzima  na hao wafu wakahukumiwa  katika mambo hayo yaliyoandikwa katika  vile vitabu sawasawa na matendo  yao, bahari ikawatoa wafu  waliokuwamo ndani yake; na mauti  na kuzima zitawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo  yake.Ufunuo 20:12-15]

4.Utawala wa Kristo wa miaka elfu(1000) au millennia, Kwa lugha nyingine jina la ufalme huo ni  millennium na maana yake ni miaka elfu. Ingawa jina hili katika biblia halionekani sana lakini  linahusika sana na utwala wa miaka 1000 uliotajwa katika maono  ya kitabu cha ufunuo.“Hao wafu waliosalia hawatakuwa hai,hata itimie ile  miaka elfu. Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri na mtakatifu ni yeye  aliye wa kwanza; juu yah u mauti  ya pili haina nguvu bali watakuwa makuhani wa munngu na wa Kristo, nao watakatifu pamoja naye hiyo miaka elfu”.[Ufununo 20:4-6].Utawala huu utakuwa baada ya  ushindi wa Kristo katika  vita  kuu ya tatu  ya dunia ufalme wake utaanza hapa duniani.

5.Kubadilishwa kwa mbingu na dunia ,Baada ya kukamilika kwa matukio yote niliyotangulia kuyaeleza mbinguu na dunia zitapitishwa katika moto na kasha Mungu ataumba mbingu mpya na nchi mpya mahali ambapo kweli  na amani zitatawala milele.Mahali hapa palipo na raha isiyo na kikomo ndipo yatakapokuwa maskani ya milele ya wale wote watakaomkubali Yesu Kristo kuwa mwana waMungu na kumpokea maishani mwao kama Bwana na mwokozi wao.

 

 

 

 

 

 

 

                                               

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Powered by Blogger.