LUGHA-FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI NA KIAFRIKA

 

FASIHI   SIMULIZI  YA  KISWAHILI   NA KIAFRIKA

MODULE   1; UTANGULIZ


I

 FASIHINSIMULIZI   YA  KISWAHILI

 

Senkoro   (1988:10-11) Anasema Fasihi simulizi ni ile inayojitambulisha na kujihusisha na utamaduni wa waswahili popote pale walipo ulimwenguni.Utamaduni  wa waswahili ni ule unaohusu desturi na mila za waswahili sayansi,sanaa zao,uchumi wao na maisha yao kwa ujumla.

Hali kadhalika inawahusika ,maudhui,falsafa,mawazo,historia, n.k vinvyofanana na maisha ya waswahili. Kwa upande wa lugha ,Falsafa ya Kiswahili ni ile inayotumia lugha au lahaja ya Kiswahili.

    FASIHI SIMULIZI YA KIAFRIKA

  Ni ile inayojitambulisha na kujihusisha na utamaduni  wanaa zao ,siasa na  Afrika kupitia jamii na Lugha zao. Hivyo  utamaduni wa Waafrika ni ule unaohusu mila zao ,siasa na uchumi wao kwa ujumla.

   Hivyo Fasihi simulizi  ya kiafrika ina mawazo ,falsafa,wahusika,maudhui,na dhamira zinazoendana na maisha yao.Imetungwa kwa lugha za kiafrika au lahaja za lugha hizo.

   Maswali hapa ya kujiuliza ni;

Ø  Je fasihi simulizi ni ya kiafrika?

Ø  Je fasihi  simulizi  inayotumia lugha za nje zinazotumika nje ya  Afrika ni ya kiafrika pia?

Ø  Je   fasihi simulizi ya kiafrika inapaswa kuandikwa na nani? Mwafrika au hata mzungu?

 

FASIHI   SIMULIZI

  Mgullu  (2003 uk  16) anasema Fasihi simulizi ni sanaa itoayo maudhui yake kwa lugha ya maneno ambayo hutamkwa ama hutendwa.

Ni fasihi inayohusu mkusanyiko wa kazi za kisanaa za binadamu zinazowasilishwa kwa njia ya mazungumzo au utendaji.Siku hizi fasihi  simulizi  huhifadhiwa kwa kuandikwa vitabuni,kanda za video,Redio na santuri.

Mlacha  (1985:16)  Anasema Fasihi simulizi ni Nyanja ya maisha ya jamii ambayo huchangia sana katika kuendeleza na kudumisha historia ya jamii husika.

       Fasihi simulizi  huchangia katika kuelimisha jamii kuhusu asili  yake ,chanzo chake na maendeleo ya utamaduni wake na maisha  ya jamii hiyo tangu zamani .

Wamitila (2003:44) AnasemaFasihi simulizini dhana inayotumika kurejelea kazi ambazo kimsingi hudokeza na kwa njia ya masimulizi ya mdomo.Hutumika katika jamii kama njia ya kupashana maarifa yanayohusu utamaduni fulani,historia fulani ya jamii na matamanio yao.

OKPEWHO (1992:3) Anasema Fasihi simulizi ni matini bainifu ambazo huvutia fikra zetu au hisia zetu,kama vile hadithi,mashairi na michezo ya kuigiza  na sio kwa matini za kweli kama vile Ripoti za magazetini au rekodi za kihistoria,hata hivyo nazo zikiandikwa kwa kuvutia zinaweza kuwa fasihi.

Mlokozi (1996:24) Anasema Fasihi simulizini fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani  na kuwasilishwa  kwa hadhira kwa njia yam domo na vitendo bila kutumia maandishi.

Hivyo ni tukio linalofungamana na muktadha fulani wa kijamii na kutawaliwa na mwingiliano wa  mambo sita,ambayo ni;

Ø  Fanani (msanii)

Ø  Hadhira

Ø  Fani inayotendwa

Ø  Tukio

Ø  Mahali na wakati

Ø  Fasihi  simulizi inaendana na tukio

SWALI: ‘’Mbali na jitihada za wataalamu mbalimbali katika kufasili fasihi simulizi na fasihi simulizi ya kiafrika mpaka sasa hakuna fasihi  iliyotoshelevu.Jidili  dai hili na pendekeza fasili yako’’

KUFANANA NA KUTOFAUTIANA KWA FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI NA YA KIAFRIKA

v  Zote zinahifadhi mila ,desturi na historia pamoja na lugha za jamii husika

v  Zote zinahitaji utendaji  ambao unajumuisha vifaa mbali mbali kama vile maleba yaani mavazi maalumu

v  Vipera na tanzu vinaingiliana na kufanana

v  Muktadha na maudhui ya lugha maalum dhana hizi zinajitokeza kote

UTOFAUTI  KATI YAFASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI NA YA KIAFRIKA

Ø  Fasihi simulizi ya kiafrika ni pana sana  lakini fasihi ya Kiswahili ni finyu kwani fasihi  ya Kiswahili huchota vipengele fulani katika fasihi simulizi ya kiafrika.

Ø  Fasihi simulizi ya kiafrika ni kongwe

Ø  Utamaduni wa Fasihi simulizi ya kiafrika ni tofauti na ule wa kiafrika.

TANZU ZA FASIHI SIMULIZI NA UAINISHAJI WAKE

 Tanzu ni matawi.Uainishaji wa Tanzu za Fasihi simulizi  si jambo rahisi.Wataalamu mbali mbali wamejaribu kuainisha lakini wamepambana na matatizo kdha wa kadha  kwani;

v  Afrika ina utajiri mkubwa wa tanzu za fasihi simulizi.

v  Tanzu hizo zinafanana sana

v  Tanzu hizo zinaingiliana.

 

Wageni walipokuja kama vile Finegan (1970),Matteru (1977),Mlokozi (1996),Catheline, Kitula na king’ei  (2005),Wafula  na Ndungo (1993),Liongo (1972),Wafula na Njogu  (2007) na wengine wamefanya jitihada za kuainisha tanzu za Fasihi simulizi.Si rahisi kuainisha Tanzu kwani hakuna mipaka bayana kati ya Utanzu mmoja na mwingine.Hadithi,methali,Vitendawili na mafumbo vinaweza kuwekwa katika kundi moja.

Ø  Wapo wataalamu walioainisha Tanzu za watoto na tanzu za watu wazima.Mfano Methali ni tanzu za watu wazima.

Ø  Swali; Je ni upi utanzu bora kuliko mwingine?  Baadhi  ya wataalamu walisema methali ni uti wa mgongo wa  mazungumzo.

VIGEZO VYA UAINISHAJI WA TANZU ZA FASIHI SIMULIZI

Wafula na Njogu wanasema ili tuweze kuainisha tanzu za fasihi simulizi lazima tuwe na vigezo;

v  Majina ya tanzu

v  Miundo

v  Mitindo

v  Wahusika

v  Wakati na mahali pa utendaji

Wafula R. na Ndungo .C (1993) wametumia vigezo vifuatavyo katika uainishaji wao;

*      Majina ya tanzu

*      Miundo

*      Mitindo yake

*      Mianzo na miisho  yake

*      Maudhui

*      Kujipambanua kwake kitabaka

*      Jinsia (kuna tanzu za kike na za kiume)

*      Mahali na wakati

*      Wahusika

Materu (1983) ameainisha tanzu za Fasihi simulizi katika makundi makubwa matatu,ambayo ni;

1.       NATHARI

Ni masimulizi au mazungumzo

·         Ngano

·         Visasili

·         Misendu na n.k

2.      USHAIRI

Ø  Mashairi

Ø  Nyimbo

Ø  Tumbuizo

Ø  Utenzi

Ø  Maghani

Ø  Ghibu

3.      SEMI

·         Mafumbo

·         Misemo ya kilinge

·         Methali

·         Vitendawili

  Kitula king’ei na Catheline Kisovi wametaja makundi  4 ya tanzu ambayo ni;

1.      SEMI

Ø  Misemo

Ø  Methali

Ø  Mafumbo

Ø  Vitanza ndimi

Ø  Utani

2.       Hadithi

v  Ngano/Hekaya

v  Visasili

v  Maghani

v  Visakale

3.      MAIGIZO

*      Michezo ya kuigiza

*      Sarakasi

*      Majigambo

*      Ngomezi

*      Utani

*      Mawaidha

*      Mipasho/Michongoano

*      Ngonjera

*      Vichekesho

4.      USHAIRI

v  Nyimbo kama vile Rege,Chakacha,Nyimbo za harusi,Mbolezi,Wawe,Mkwaju ngoma,Nyimbo za Unyago,Bembelezi,Nyimbo za jandoni n.k

v  Ngonjera

v  Mashairi

v  Tenzi

v  Kirumbikizi

 Mlokozi M.M (1996) ameainisha tanzu kwa kutumia vigezo  vifuatavyo;

Ø  Umbile na tabia ya Utanzu

Ø  Muktadha wa uwasilishaji yaani wakati na mazingira

Ø  Namna ya uwasilishaji wake kwa hadhira  (Mtindo)

Ø  Dhima ya Fani na utanzu wake.

Mlokozi ameainisha Tanzu za Fasihi simulizi  katika makundi sita ambayo ni ;

1.       MAZUNGUMZO

Utanzu huu una vipera vine,ambavyo ni;

·         Hotuba

·         Malumbano ya watani

·         Mizaha

·         Sala

*      Dua

*      Maapizo

*      Tabano

2.      MASIMULIZI

Utanzu huu una vipera  vitatu,ambavyo ni

Ø  Hadithi za kubuni

*      Vigano

*      Istiara

*      Mbazi

*      Michapo

Ø  Salua

*      Visakale

*      Mapisi

*      Tarihi

*      Shajara

*      Kumbukumbu

Ø  Visasili

*      Visasili vya uzuri

*      Visasili vya ibada na dini

*      Visasili vya miungu na mizimu

3.      MAIGIZO

Utanzu huu unajumuisha maigizo ya watoto,misiba,Sherehe za kidini n.k

4.USHAIRI  SIMULIZI

  Vipera vyake ni;

·         Nyimbo

*      Tumbuizo

-Bembea

-Mbolezi

-Nyiso

*      Tukuzo

-Kongozi

-Nyimbo za dini

-Nyimbo za taifa

*      Chapuzo au kimai

-Nyimbo za kutwanga

-Nyimbo za watoto

-Nyimbo za vita

*      Tenzi na Tendi

·         Maghani

*      Ghani nafsi-kutamba

*      Ghani tumbuizi

*      Sifo-Vivugo (majigambo)

       -Tondozi

*      Maghani simulizi

-Tendi

-Rara

5.      SEMI

·         Methali

·         Vitendawili

·         Mafumbo

-Chemsha bongo

-Fumbo jina

·         Simo/misimo

·         Kauli kaulia

6.Ngomezi

 

FASILI YA DHANA MBALI MBALI ZA FASIHI

v  Mazungumzo

Ni mazungumzo yenye sanaa ndani yake yaliyosheheni mbinu za kifani (Fani na Maudhui).

Mfano Tamathali za semi  kama vile sitiari,Tashibiha n.k

v  Mbazi

Ni hadithi fupi zenye lengo la kuonya

v  Salua

Ni hadithi zinazosimulia matukio ya kihistoria / ya zamani .

v  Visakale

Ni visa vya kimapokeo vya mashujaa

v  Mapisi

Ni historia ya matukio ya kweli

v  Tarihi

Ni maelezo au jedwali la matukio muhimu na tarehe zake.

v  Visasili

Ni hadithi za kale zinazozungumzia asili ya kitu au imani ya mtu.mfano asili ya binadamu.

v  Mbolezi

Ni nyimbo za kuliwaza katika msiba.

v  Nyiso

Ni nyimbo  za jandoni na unyago.

v  Wawe

Ni nyimbo za kazi

v  Kongozi

  Ni  nyimbo za kuaga mwaka,mara nyingi zinaambatana na tambiko.

v  Tenzi

Ni utungo unaozungumzia tukio fulani.

v  Tendi

Ni utungo unaozungumzia tukio la kishujaa

v  Sifo

Ni nyimbo za kusifu

v  Tondozi

Ni tungo za kusifu wanyama n.k

v  Rara

Ni maghani ya kusimulia tukio fulani la kihistoria na huenda sambamba na ala za mziki.

v  Fumbo jina

Ni mafumbo ya yanayotaja majina .mfano  Mwamvua alizaliwa kipindi cha mvua

v  Lakabu

Kupewa jina kulingana na tabia mfano Mwl J.K Nyere-Baba wa Taifa

v  Kauli Taulia

Ni kauli zenye mfuatano wa sauti

 

 

 

 

 

 

 

 

UHUSIANO  WA FASIHI SIMULIZI NA TAALUMA NYINGINE

 Fasihi simulizi haipo katika upweke au Ombwe bali inahusiana na taaluma mbali mbali .Hii inatokana  na ukongwe  wake yaani dhima zake,sifa zake,utendaji wake, na n.k vinafranya ihusiane na taaluma nyingine.Miongoni mwa taaluma hizo ni Mziki,Sosholojia,Historia,Isimu ya Lugha,Etimolojia na hata Fasihi Andishi.

A.     UHUSIANO WA FASIHI SIMULIZI NA MUZIKI

Mziki ni nini? Au ni vitu gani vinafanya utambue kuwa huu ni mziki?

Ø  Ala za mziki kama vile zeze,marimba,ngoma,manyanga,n.k.Fasihi simulizi inahusiana na mziki katika utendaji kwani katika    Fasihi simulizi kwani vipera mbali mbali vya fasihi simulizi vinahusisha ala fulani za muziki,mfano Majigambo,Tenzi.

B.Historia

 ni taaluma  inayochunguza matukio kisayansi ya wakati uliopita na uliopo.Ni taaluma inayoshughulika na uchunguzi wa maisha ya binadamu ambayo yanatuwezesha kujua maendeleo na mabadiliko ya binadamu. Fasihi  ananafasi kubwa katika historia ya binadamu kwa kupitia baadhi ya vipera vya fasihi simulizi.Hivyo  Fasihi simulizi  inatusaidia kuelewa historia yetu (sayansi fulani) mfano Tenzi,baadhi ya tenzi za kiswahili zinazungumzia mashujaa wa Afrika,Mfano Fumo Liyongo.Hii inatusaidia  kujua mtzamo wa jamii husika katika kipindi fulani cha kihistoria.Wanahistoria  pia wamechota baadhi ya mambo yao kutoka katika Fasihi simulizi.Data za fasihi simulizi zinasaidia kujenga rekodi za kihistoria .Vipera mbali mbali kama Tendi,Visakale,Tarihi,Shajara n.k vinatusaidia kuelewa historia ya jamii japo kwa kiasi kidogo kuhusu matukio ya watu au mashujaa katika jamii hiyo.

Suala la utendaji/Utofauti wa vipera vya fasihi simulizi  zamani na sasa vinaweza  kutusaidia kuelewa historia ya jamii fulani.Fasihi simulizi inasaidia kuhifadhi na kuendeleza historia katika jamii mfano majigambo.

C.      SOSHOLOJIA (Elimu viumbe,Athropolojia)

Ni taaluma inayoichunguza jamii kisayansi ili kujua mienendo yake na nguzo mbali mbali zinazoongoza jamii hiyo.Mfano Matabaka,Dini,kijadi,.Vingele hivi  tunavipata  katika sosholojia na vinatusaidia kuelewa namna ambayo vinweza kuzuia  mienendo.

  Hivyo  Fasihi simulizi tangu hapo mwanzo inatusaidia kujua hiyo mienendo  au mifumo mbali mbali ya jamii,kipera kinaweza kuwa chombo cha kutetea utabaka au kuchochotea  utabaka.

 Fasihi simulizi kilikuwa chombo pekee cha kuwasilisha maadili ya jamii kupitia vipera  kama vile kitendawili au nyimbo.Kupitia Fasihi simulizi tunaweza kurithishwa utamaduni ,mila na desturi za jamii hiyo.Taarifa za kisosholojia pia zinapatikana katika kazi za kifasihi.Mienendo na mabadilikomifumo ya kiuchumi na kijamii inapatikana kwa kurejelea kazi za Fasihi simulizi.

 

D.     UTAMADUNI

Utamaduni unapatikana katika fasihi simulizi  kwani fasihi simulizi ni chombo kizuri cha kurithisha utamaduni wa jamii husika na utamaduni huo hurithishwa kupitia utendaji wake katika baadhi ya vipengele kama vil;Maleba (mavazi),Utendaji,Mazingira ya utendaji,Vifaa,Fani husika.

Hivyo uhusiano kati Fasihi simulizi na utamaduni pia upo katikaLugha kwani Fasihi simulizi hutumia lugha,na lugha ni nyenzo muhimu za fani husika  hivyo fasihi kama chombo na sehemu ya utamaduni inasaidia mambo kadha wa kadha kama vile;

Ø  Inakuuza utamaduni

Ø  Inahifadhi utamaduni

Ø  Inaeneza utamaduni

Ø  Kueleza utamaduni wa jamii hiyo.

  Kwa ujumla fasihi simulizi ipo katika kila hatua ya maisha yetu.

E.      ETHIOLOJIA

Fasihi simulizi inatumika  katika dini kama vile nyimbo na maandiko ya kidini ambayo yanaweza kuwa hadithi ,nyimbo ambazo zimo katika biblia na vitabu vya nyimbo za kidini.mfano Utenzi wa sundiata.

F.FASIHI ANDISHI

Uhusiano kati ya Fasihi simulizi na Fasihi andishi utafiti unaonyesha kuwa karibu tanzu zote za Fasihi   andishi zimetokana na Fasihi simulizi.

Ø  Maigizo yanazaa tamthiliya,pia uhusiano huu unajitokeza katika nafasi ya fasihi simulizi  katika  tanzu za fasihi andishi.Fasihi andishi inanufaika kwa kiwango kikubwa kutoka katika fasihi simulizi  kifani na kimaudhui kama vile vipera,matumizi ya lugha n.k vipengele hivi vya fasihi simulizi vinatumiwa katika fasihi andishi.Vitu hivi vinaleta athari kubwa katika fasihi simulizi.

Ø  Pia  kuna mianzo maalum katika tamthiliya kuna fomula za kihadithi mfano,Niendelee nisiendelee?

Ø  Vile vile matumizi ya wahusika wanyama,ndege,mazimwi,majitu n.k, pia matumizi ya wahusika bapa,matumizi y mbalimbali kama vile taswira,ucheshi n.k

Ø  Suala la kuingiliana kwa tanzu,katika fasihi  andishi kuna tanzu za fasihi simulizi kama vile hadithi,ngano,nyimbo n.k

Ø  Pia katika mashairi kuna utambaji ,malumbano na vipera vingine vya fasihi simulizi.

 

 

 

 

 

 

SUALA  LA UTENDAJI  KATIKA FASIHI SMULIZI

Katika  fasihi simulizi utendaji ni uti wa mgongo yaani ni suala la msingi.

     Mulokozi  (1996:24) Fasihi simulizi ni tukio na linafungamana na matukio ya kijamii na hutawaliwa na fanani (msanii au mtendaji)

Ø  Fanani ni mtendaji au mwasilishaji na mtunzi wa kipera,fani husika kwa hadhira katika muktadha wa tukio fulani ,kazi yake yaweza  kuwa kichwani au akatunga papo kwa papo.

Ø  Fani inayotendwa au kipera

Ø  Hadhira/wasikilizaji,washiriki,wachangiaji ,wahakiki,watazamaji hawa huangalia uzuri au ubaya.

Ø  Tukio-ni shughuli yoyote ya kijamii ambayo ndio muktadha wa utendaji.mfano msiba,ibada,harusi,sherehe,n.k

Ø  Mahali –eneo mahsusi ambapo sanaa hiyo inatendwa.

Ø  Wakati na muda maalum au majira maalum ya utendaji .Vipera vingi  vina wakati wake.mfano Sifo huimbwa wakati wa kuomba.Mwingiliano huu wa vipengele hivi ndiyo unaoamua fani hiyo iwasilishwe vipi.

OKPEWHO  (1992) Anasema Utendaji unaotofauta kutokana na sababu mbali mbali  kama vile;

Ø  Umri wa fanani

Ø  Umri wa hadhira

Ø  Nguvu ya fanani,baadhi ya vipera vinahitaji fanani awe na nguvu mfno majigambo

Ø  Tukio husika mfano Msiba hauwezi kufanana na sherehe

Ø  Aina ya mandhari  au  jukwaa maalum la kutendea yaani pale inapotendewa.

Ø  Vifaa ambatani vinavyotumika na fanani katika utendaji mfano maleba,mkuki

Ø  Idadi ya fanani

 

     Pia  utendaji unatokana au unatawaliwa  na;

Ø  Dhima ya kipera( tukio ),muktadha wa uwasilishaji na namna ya uwasilishaji hutegemea  dhima ya kipera katika jamii.

Ø  Muda na mahali,ni  muhimu kuzingatia kwa kipera chochote hutegemea au husukumwa na muda na mahali.mfano matambiko yanafanywa muda gani?

Ø  Mila na utamaduni ,kila jamii ina mila  na utamaduni wake na hivyo huathiri utendaji wa vipera husika.mfano Mavazi au maleba maalum ya kisanaa yaani kipera hiki kinahitaji aina ipi ya maleba?

Ø  Sifa za wahusika au watendaji wa kipera fulani wanapaswa wawe akina nani?

 SWALI; JE UTENDAJI NI NINI?

      Muluka (1999) anasema Utendaji ni uwasilishaji  wa hadithi  au ngano unaofanywa na msanii kwa hadhira kwa kutumia  mdomo na kuambatana na matendo ya viungo mbalimbali  vya mwili  na ishara uso.Hivyo kila kipera kipo  kwaajili ya kutendwa.

     UTENDAJI KATIKA VIPERA MBALI MBALI

 Finnegan  (1970) ‘’Oral  Literature in Africa’’ anasema  kuwa katika utendaji kuna kanuni maalum,jamii nyingi zina utamaduni wake.Hadithi ni utanzu muhimu katika jamii za kiafrika.Hadithi ni utanzu wa jioni na mtambaji  anazungukwa na hadhira.

    SWALI; Je kwanini hadithi inatambwa jioni?

Ø  Kwasababu  mchana mtambaji anakuwa katika utafutaji yaani katika shughuli zake za kila siku.

Ø  Hadithi ina fomula zake za kuanza na kumalizia yaani mianzo na miisho maalum ya kihadithi.

Ø  Katika kutamba hadithi fanani habanwi kutumia vipera vingine katika utendaji  wake.

Ø  Katika kutamba hadithi msimuliaji hatakiwi kukalili ila anapaswa kuleta upya fulani wa utendaji wa hadithi hiyo.

Ø   Mtambaji anapaswa kutumia sauti vizuri na iendane na utanzu wenyewe.

Ø  Kuna wasimuliaji wazuri na wabaya au wasiowazuri

Ø  Msimuliaji awe mbunifu ili kunogesha hadithi

Ø  Katika utendaji msimuliaji aoneshe hisia zake.

 

UFALAGUZI

Ni uwezo alionao fanani katika kuunda kutunga ,kugeuza na kuiwasilisha kazi ya fasihi simulizi papo kwa papo bila ya kujifunga na muundo asilia au na muundo uliozoeleka. Hivyo  katika utendaji wa kipera fulani kuna utungaji mpya kutokana na mbinu fulani unazotumia.

Ø  Hivyo  hadithi moja inaweza  simuliwa  tofauti na wasimuliaji tofauti.Utendaji wa kipera hurithishwa toka kizazi kimoja hadi kingine.

SIFA ZA FANANI BORA

Senkoro anasema Fanani bora anatakiwa afanye kazi ya ualimu ,awe mtoa maoni,msanii,mburudishaji,muigizaji

Ø  Fanani aifanye hadithi ionekane mpya  kila mara anaposimulia.

Ø  Fanani aifurahie  na kujivunia fani anayoitenda,kuisimulia ipasavyo.

Ø  Fanani awe mbunifu na awe na kumbukumbu.

Ø  Suala la utamaduni katika utendaji fanani azingatie utamaduni  wa kipera anachotamba.

Ø  Fanani awe tajiri wa lugha yaani ajue kutumia mbinu   mbalimbali za lugha kama  vile  nahau,semi,n.k.

Ø  Fanani asiwe na aibu katika utendaji atumie  vema lugha na viungo mbali mbali.

Ø  Kujua mambo ya kihistoria kwani Fasihi inapitia vipindi mbalimbali.

UTENDAJI WA KIPERA  CHA SEMI

1.      METHALI

Ni usemi  mfupi wa kimapokeo unaodokeza mafumbo mazito au fikra zinazotokana na uzoefu wa jamii husika.Katika utendaji  unaweza kutofautiana na vipera vingine kwani utendaji wa methali lazima unajitegemeza wakati wa kutenda fani nyingine mfano mkutano,maongezi ya kawaida,majadiliano,hadithi,wakati wa kukanya mtu n.k.

 Kimsingi watambaji wa methali ni watu wazima (wazee) kutokana na kuishi kwao katika jamii kwa muda mrefu.

 2.VITENDAWILI

Utendaji katika vitendawili si tegemezi kama methali bali kitendawili kinasimama  chenyewe kwa kufuata kanuni zilizowekwa na jamii husika.Mfano katika kabila la wajaluo  ukishindwa kutegua unaombwa mke au mme na katika jamii  nyingine unapewa mji.

 

2.      MAJIGAMBO

Katika Jamii ya wahaya ni jamii ambayo ni maarufu kwa majigambo.Huu ni utafiti wa kitaaluma uliofanywa na Rubanza (2004) na Method Samwel ,hawa wote wameangalia jamii ya wahaya.

    Katika jamii ya wahaya majigambo  yalikuwa na muktadha wake maalum walikuwa wanatamba mbele ya mtemi kabla ya kwenda vitani au baada ya kurudi toka vitani n.k

Ø  Kwa wahaya mjigambi hujigamba mbele ya watu ,sherehe ambayo inahudhuriwa na mtemi na kuna namna ya kuanza  na kumaliza.Mfano  wakati wa kuanza mjigambi anaweza kuanza kwa kujitambulisha kwa kujigamba na anaweza kumalizia kwa shukrani au heshima kwa mtemi au kiongozi aliyepo pale.

Ø  Katika majigambo ,mjigambi yupo huru kutumia lugha ya kujikweza akiwa amevaa maleba maalumu  mfano katika kujigamba  mjigambi anavaa kanzu ndefu au nguo za majani ya migomba na hushika silaha kama vile mkuki ,panga,n.k

Ø  Pia majigambo huambatana na ngoma yenye  mapigo ya pekee na maandamano fulani.

Ø  Katika majigambo kuna zawadi,shujaa aliyeshinda au aliyerudi toka kuwinda ,vitani n.k hupewa zawadi kama pombe.

Ø  Wale walioenda  vitani au kuwinda wakashindwa zawadi yao ilikuwa maji ya kunywa na kinyesi cha ng’ombe.Hii ilikuwa inaleta umakini kwani kurudi na kinyesi ilikuwa ni aibu.

     Miaka ya 1960 utendaji katika majigambo uliathiriwa sana kutokana na mabadiliko ya kijamii na kiutawala

 

 

 

 

 

Powered by Blogger.