MITIHANI

 





WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

                SHULE YA SEKONDARI  EFFORTS

                    MTIHANI WA KUMALIZA MUHULA

                           KIDATO   CHA   SITA

                                  KISWAHILI-2                                                                   MUDA : SAA  3                                                               Novemba,2018                                               

                             MAELEKEZO

1. Karatasi hii  ina  jumla ya maswali  tisa ( 9 )

2. Jibu swali  moja kila sehemu na kila swali lina alama 20

3. Soma swli kwa mkini kabla ya kuanza kujibu

         4. Andika jina lako vizuri na mchepuo wako

                    

                    SEHEMU   A   (Alama  20)

                           FASIHI KWA UJUMLA

1.     “Usambazaji wa sanaa za maonesho nchini Tanzania unakabiliwa na changamoto lukuki’’.Kwa hoja sita na mifano thibitisha dai hili.

2.     “Tangu wakati wa uhuru hadi sasa Tamthiliya ya Kiswahili imetoa mchango mkubwa sana kwa jamii ya Tanzania”.Kwa hoja sita pamoja na mifano kutoka katika tamthiliya za Kiswahili thibitisha dai hili.

                         SEHEMU   B  ( Alama 20 )

                               USHAIRI

                          Kimbunga                  - Haji Gora

                     Fungate  ya Uhuru  -M.S.Khatibu

                     Mapenzi                     -S.Robert

                     Chungu  Tamu           -T.Mvungi

3.     “Matumizi ya Jazanda ni moja ya mbinu za mwandishi  katika kufikisha ujumbe kwa jamii lengwa’’.Jadili dai hili kwa kutoa Jazanda   nne  (4) kwa kila diwani kwa kutumia diwani mbili ulizosoma huku ukirejelea Tanzania ya leo.

4.     “Wasanii wa ushairi ni nguli wa kutumia tamathali za semi”.Kwa  kutumia  diwani mbili   thibitisha dai hili

                           SEHEMU   C  (Alama  20)

                                    RIWAYA

                           Usiku Utakapokwisha  -Mbunda Msokile

                           Mfadhili                          -Hussein  Tuwa

                            Kufikirika                        - Shaaban  Robert

                          Vuta n’kuvute                  -Shafi Adamu Shafi

5.     “Mara nyingi mandhari husaidia kuibua dhamira lengwa za msanii wa kazi ya fasihi’’.kwa kutoa hoja kwa kila riwaya toka katika riwaya mbili ulisoma thibisha dai hili

6.     Wasanii wa kazi ya fasihi hutumia mbinu za kifani ili kujenga ,kuzipa mvuto na kuleta radha tamu kwa wasomaji wa kazi zao.Fafanua mbinu tano ( 5 ) za kifani zilizotumika katika kila tamthiliya ,tumia tamthiliya mbili ulizosoma.

 

                          SEHEMU   D    (Alama   20)

                                            TAMTHILIYA

                   Kwenye  Ukingo wa Thim    - E.Hussein

                   Morani                                     -E.Mbogo

                   Kivuli Kinaishi                         -S.Mohamed

                   Nguzo  Mama                         -P.Mhando

7.     Jina la kitabu ni ishara tosha ya yote yanayojadiliwa na mwandishi”. Thibitisha  dai hili kwa hoja nne  (4) kwa kila Tamthiliya,Tumia tamthiliya mbili ulizosoma.

 

8.     Ubunifu wa kisanaa ni nguzo  muhimu sana katika kufikisha  ujumbe kwa jamii yeyote ile.Kwa kutumia  Tamthiliya mbili   ulizosoma jadili vipengele vya fani  vilivyotumiwa na mwandishi kufikisha ujumbe.

 

                   SEHEMU     E   (Alama  20 )

                        USANIFU  W MAANDISHI

9.     Soma habari ifuatayo kisha eleza mbinu za kisanaa zilizotumika;

Wakati wanakijiji wanazungumza na mgeni,mipango mingine ya utoro  ilikuwa inafanyika Samson na mkewe wakaona kuwa wamekabiliwa na jambo kubwa,hahahaha!!!!!,Mti na macho.Waliona vigumu kungoja hadi kesho yake mashauri yatakayofanyika.

       Waliposoma sura za wanakijiji  walihisi kuwa hakutakuwa na usalama wowote.Kwa hiyo  walikata shauri na kuondoka kisirisiri usiku wa manane  pamoja na watoto wao,watoto walianza kuchukua tabia za wazi wao.Amaa!!! kweli !!! mtoto wa nyoka  ni nyoka tu.Ilipofika usiku walianza kufunga funga vitu na visivyo vyao ambavyo walijua wataweza  kuvichukua,Amaah! Kweli!! Tabi haina dawa. Mnamo saa saba usiku,Samson alimtwaa punda mmoja na kumbebesha mzigo ile mizigo?. Maskini  ya MUNGU!!!!, Mnyonge  mnyongeni ……………..siku zote  kiumbe wa Mungu  huonewa sana!!,Hubebeshwa mizigo mizito.Usiku  ulikuwa wa nuru kama mchana na safari ikaanza.

    Walisafiri  usiku mzima lakini hawakuwa wamefika mbali sana kulipoanza kupambazuka kutokana  na mwendo mdogo wa  punda.Hata hivyo walipiga hatua kulipopambazuka watu walianza  kusalimiana.Kwa bahati mbaya mzee Hengaipinge aliamka mapema sana siku ile na kuamua kwenda kwa Samson.Alishangazwa na jinsi vitu vilivyokuwa vimetupwa hovyo hovyo kama nyumba ya kichaa,hivyo alihisi kuwa  jamaa wale wamekata mbuga.

      Wanakijiji walipata taarifa za kutoroka kwa Samson,watoto  na mkwewe.Watu walikwenda kushuhudia maajabu ya Mussa.

Ilipofika mchana mtu mmoja  mgeni  kutoka madongo kwinama aliwasili katika kijiji cha Magwale.Samaki mmoj akioza wote wameoza,kwani mgeni huyohuyo hakupokelewa kwa furaha.Kwa ufupi Samson na mkewe waliwatia wageni  katika mtego wa panya.

   Yule mgeni alipowasili walisalimiwa kama ilivyo kaida,lakini baada ya kumsalimia wanakijiji wakazidi kujadiliana juu ya lile lililotokea.Wengine waliwashauri kuwa lazima watu wale wasakwe na kukamatwa lakini  wengine waliona kuwa Mbio za sakafuni huishia ukingoni.

 Mgeni aliwaomba wamsindikize pia, ‘’Napenda kuwaeleza kuwa nilipoanza safari yngu,hao watu nilikutana nao” Ooooh!!!,Watu wote walishangaa.Aliendelea kwa kusema kuwa Punda wao  alitembea kama kinyonga kwa mizigo aliyobebeshwa.Tulishasikia habari za watu hawa  habari za watu awa kuwa walimtesa sana mtoto Lukemelye na kumdhulumu kupita kiasi,wana tama ya fisi.Watu hawa  watakuwa katika kijiji cha Ihang’ana hivi sasa.Mgeni aliahirisha safari yake na kurudi Ihang’ana kuyawahi mambo kabla hayajaenda mrama.

 

 

 

Powered by Blogger.