SENTENSI NA MIUNDO YAKE

Wataalamu mbalimbali wamefasili dhana ya sentensi kama ifuatavyo Kapinga (1983), anafasili sentensi kuwa ni kipashio kikubwa kuliko vipashio vya kiisimu na huwa na wazo kamili. Anaendelea kueleza kuwa sentensi ni sehemu ya sarufi ambayo agharabu hujisimamia kimaana, mala nyingi sentensi huweza kuwa na maana anbazo huweza kuwa ni taarifa, ombi, mashariti, au hata amri.

 
Richard et all (1985), anasema sentensi ni dhana asilia ya lugha ambayo hufafanuliwa kudhihirisha sehemu ya sarufi yenye neno moja au zaidi inayosimamia wazo kamili nae Radford (1997), anasema sentensi ni sehemu ya sarufi ambayo hujisimamia kisintaksia na ambayo huwa na kiima na kiarifu ambacho kina kitenzi kimoja au zaidi. Kwaujumla sentensi ni tungo yenye muundo wa kiima na kiarifu na vilevile husimamia wazo kuu.
 
Sentensi huweza kuainishwa kwa mkabala wa kisemantiki (mapokeo) cha maana ambapo kuna sentensi swali, sentensi maelezo, sentensi mshangao na sentensi shurtia. 

Vilevile sentensi huainishwa kwa mkabala wa kisasa (kimuundo) ambapo kuna sentensi sahili, sentensi changamano, na sentensi ambatano. Sentensi ya Kiswahili huwa na muundo anuai kama inavyo fafanuliwa hapa
 
Sentensi huwa muundo wa kiima. TUKI (2004) wanaeleza kiima kuwa ni neno au kifungu cha maneno katika sentensi ambacho hutangulia kitennzi. Hivyo muundo wa kiima katika sentensi  ni sehemu ya sentensi ambayo inatawaliwa na nomino, vilevile kinaweza kushirikisha kikundi kivumishi au kishazi tegemezi, Mfano
          Matunda matamu huvutia
                         K
          Wanafunzi waliokuwa wametoka shuleni wameathibiwa
                              K
Muundo wa kiarifu. Kiaifu TUKI (2004), wanaeleza kuwa kiarifu ni sehemu ya sentensi yenye kitenzi, shamirisho na shagizo.hivyo muundo wa kiarifu katika sentensi ni sehemu ya sentensi yenye kitenzi ambayo hushirikisha kikundi kielezi au kikundi kivumishi, vilevile kinaweza kuwa na nomino kama shamilisho.
Mfano      Mvua inarutubisha vitu vyote
                                     A
                 Dunia huzunguka jua
                                     A    nzi kinaweza kuwa
Miundo ya Shamilisho ni miundo katika sentensi ambayo mtendwa au mtendewa katika sentensi ni sehemu ya sentensi inayowakilisha kitu kilichofanyiwa kitu. Aidha kirai kitenzi kinaweza kuwa na kirai nomino kama shamilisho.
Kwaujumla sentensi za Kiswahili huwa na dhima mahususi mahusiano yake ni tofauti na lugha ya ulaya vilevile sifa za lugha ya Kiswahili na lugha ya kibantu zinafanana, sifa hizo ni kama vile sentensi huwa na upatanishi wa kisarufi ambapo kiima hudhibiti virai vingine kwa kutumia viambishi vipatanishi. Mfano Mtu mrefu amekufa

Marejereo
Kapinga, M.C (1983), Sarufi Maumbo ya Kiswahili Sanifu:Dar es Salaam TUKI   

TUKI (2004) Kamusi ya Kiswahili Sanifu: Dar es saalama, TUKI

Massamba, D.P.B, Kihore, Y.M, na Hokororo J.I (1999), Sarufi Miundo ya Kiswahili Sarufi SAMIKISA Sekondari na Vyuo:Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili . Dar es Salaam
Powered by Blogger.