MTIHANI WA KUJIPIMA KISWAHILI KIDATO CHA TATU

MTIHANI WA KUJIPIMA  KISWAHILI
KIDATO CHA TATU 
MUDA: Saa 2:30                                                                                                                                       
MAAGIZO:
·        Mtihani huu una sehemu A, B, C, D, na E.
·        Jibu maswali yote katika sehemu A, B na C. Jibu swali moja katika sehemu D na maswali mawili katika sehemu E.
·        Majibu yote yaandikwe kwenye karatasi ya majibu utakayopewa.
·        Zingatia maelekezo kwa makini.
SEHEMU A (ALAMA 10)
UFAHAMU
1.      Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha ujibu maswali.
Watoto wa baba Kapeto ni mfano wa kuigwa kwenye kijiji cha Sokomoko. Mama na baba Kapeto ni waajiriwa katika taasisi maarufu ya elimu ya juu iliyopo katikati ya mkoa wa Nyanda za juu nchini.
        Kapeto ni mtoto wa tatu kuzaliwa kwenye familia yao. Juhudi zake katika masomo zilimfanya kuwa kipenzi cha walimu pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Sokomoko. Ubunifu wake katika sanaa pamoja na umahiri wake kwenye riadha ulimpa umaarufu mkubwa hata katika shule za vijiji vya jirani.
        Hali ilikuwa tofauti kwa kitinda mimba wa familia hiyo. Licha ya kulelewa kwa kupewa huduma zote muhimu na kuengwa engwa kama mboni ya jicho, hapendeki hakusawiri kabisa tabia za watoto wa kaya hii. Kilichobainika kutoka kwa wakazi wengi wa kijiji hicho ni masikitiko, na wengine walidiriki kusema “….. ama kweli kwenye miti hakuna wajenzi.”
        Tabia ya kujishirikisha kwenye vikundi vya watoto watukutu, haikuacha kudhihirisha ile kawaida ya uozo wa tunda, kuambukiza mengine.
        Kwa manung’uniko na majonzi, mama Kapeto aliwahi kusikika akiukana mtazamo unaoamini kuwa baada ya dhiki faraja, kwa sababu ujauzito wa mvulana huyu ulimsumbua mama yake kupita kiasi ukilinganishwa na ule wa mwanzo uliokuwa wa watoto mapacha.
        Maendeleo ya kitaaluma yalimomonyoka taratibu wakati Hapendeki akiwa ukingoni mwa kuhitimu masomo yake. Hatimaye mwana huyu akawa ni mwanafunzi pekee aliyeshikilia mkia katika matokeo ya mtihani wa mwisho wa kumaliza elimu ya msingi. Tukio hili halikusita kuwakumbusha walimu waliokuwa wakiwakumbika vyema wakubwa wake waliopitia shule hiyo kutokana na historia njema waliyoiacha.
        Matumaini ya wazazi kupata muhandisi yalididimia. Walichoambulia ni madaktari ambao wanajiendeleza kimasomaso huko ughaibuni, huku kila mmoja akiwa na matarjio ya kubobea katika taaluma ya kutibu wagonjwa wa jinsia yake. Kapeto naye amefanikiwa kujiunga na masomo ya mchepuo wa biashara, ambayo nayo yanatoa ishara njema ya kumfanya awe mtaalamu wa uchumi hapo baadaye. Masikini wee! Nyota ya Hapendeki imezima.
MASWALI
(a)    Pendekeza kichwa cha habari kinachoshabihiana na mambo yaliyoelezwa kwenye kifungu.
(b)    Watoto wote wa familia hii ni wangapi?
(c)    Wataje watoto wote kwa majina yao.
(d)    Taja methali mbili zilizomo kwenye kifungu ulichosoma.
(e)    Eleza maana ya maneno yaliyopigiwa mstari kulingana na yalivyotumika kwenye kifungu.
2.      Fupisha aya ya tatu na ya nne katika kifungu kwa maneno yasiyozidi thelathini (30).
SEHEMU B (ALAMA 25)
SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA
Jibu maswali yote katika sehemu hii huku ukiwa makini katika kuyaelewa maswali
3.      Tungo sentensi huundwa kwa kuzingatia kanuni na vipashio vinavyohusika. Tunga sentensi yenye sifa zifuatazo:-
-        Yenye kishazi kimoja
-        Yenye kirai nomino na kirai kielezi
4.      Ichanganue sentensi uliyotunga hapo juu kwa njia ya kisanduku.
5.      Vitenzi vifuatavyo vikiambishwa vinaweza kuunda majina ya watu waliobobea kwenye kazi Fulani.
Mfano: Kagua            Mkaguzi
(i)        Ugua                  _______________________
(ii)       Chunguza          _______________________
(iii)      Andaa                 _______________________
(iv)      Pekua                 _______________________
(v)       Jenga                  _______________________
6.      (i) Toa fasili ya kielezi.
(ii) Toa mfano mmoja kwa kila kazi ya kielezi ili kuthibitisha ukamilifu wa fasili yako hapo juu.
7.      Taja aina ya ngeli inayowiana na kila nomino katika orodha ifuatayo.
NOMINO
AINA YA NGELI
(i) Kipofu
(ii) Kiti
(iii) Ngoma
(iv) Mtama
(v) Bata
SEHEMU C : (ALAMA 10)
UANDISHI
8.      Kwa kuzingatia muundo sahihi na mambo muhimu yanayohitajika mwandikie mzazi wako simu ili umfahamishe kuwa mumeshafunga shule.
SEHEMU D : (ALAMA 15)
MAENDELEO YA KISWAHILI
9.      “Waarabu hawana mchango wowote katika kukua na kuenea kwa lugha ya Kiswahili.” Jadili kwa mifano kauli hii.
SEHEMU E (ALAMA 40)
FASIHI
Jibu maswali mawili tu. Swali la 12 ni la lazima.
VITABU VYA REJEA
TAMTHILIYA
-        Kilio Chetu           -              Medical Aid Foundation (TPH)
-        Orodha                -              Steve Raymond (MA)
10.   Chagua wahusika wawili kutoka kila tamthiliya mbili ulizosoma kisha uoneshe jinsi mwandishi alivyowatumia katika kuifunza jamii maadili mema.
11.   Fani na maudhui huingiliana na kuathiriana. Jadili kauli hii kwa kutumia tamthiliya mbili ulizosoma.

12.   Fafanua njia mbali mbali zinazotumika katika ukusanyaji wa fasihi simulizi katika jamii.
Powered by Blogger.