MJENGO WA TUNGO

SURA YA PILI 
MJENGO WA TUNGO
MAANA YA TUNGO:
            Neno tungo ni kipashio ambacho ni matokeo ya kupanga au kuweka pamoja vipashio sahili ili kupata kipashio kikubwa zaidi. Tungo ni neno au mpangilio wa maneno unaodokeza taarifa fulani ambayo yaweza kuwa kamili au isiwe kamili.   
Mfano:
 1. wana cheza
 2. mwezi uliopita
 3. kijana atakayeondoka
 4. mara kwa mara
 5. shangazi yake
 6. mchezaji
Mifano yote hiyo hapo juu ni tungo lakini viwango vya kukamilika kwa taarifa zake vinatofautiana.
 
MJENGO WA TUNGO
 Tungo za Kiswahili zinajibainisha katika makundi matatu yaani
 a)  virai
b) vishazi
c) sentensi
1. Virai
   kirai  ni.  neno au mpangilio wa maneno ambao una neno kuu moja na unatoa taarifa fulani. Kimsingi neno kuu ndiyo hutupatia aina ya kirai. Mfano kama neno kuu ni nomino tunapata kirai nomino.
Mfano:
 a)  mara kwa mara
b)  mtu mweusi mweusi hivi
c)  yule mwerevu
d)  chakula kilichopikwa
e)  jana jioni
f)  mpungufu wa busara
AINA ZA VIRAI
1.  Virai nomino
 Virai hivi vimekitwa katika mahusiano ya nomino na maneno mengine.
Miundo ya virai nomino
 (i) Muundo wenye nomino moja peke yake
     Mfano:
     (a)  Mtoto anacheza
     (b) Shangazi   amewasili
     (c)   Vijana   walisoma
(ii) Muundo wenye nomino mbili
     (a)Mwalimu na wanafunzi ni wavumilivu
     (b)  Mwenyekiti na wajumbe walikutana
     (c)  Juma na Asha wamepigana
    
ZOEZI
   
Pigia mstari virai nomino katika sentensi zifuatazo.
1. Mlima unapendeza sana
2. Juma amenunua kitabu
3. Mvua imenyesha usiku kucha
4. Mwalimu amefundisha vizuri
5. Dada anaimba wimbo
2.  VIRAI VIWAKILISHI
 Ni virai vinvyoundwa na viwakilishi badala ya nomino
Mfano:
a)  Huyu anacheza vizuri
b)  Mimi ninapenda ubwabwa
c)  Lile si mali yake
d)  Mkali amepigwa
e)  Warefu wakae mbele
Kumbuka :
Maneno yaliyopigiwa mstari ndio virai viwakilishi
  
3.  VIRAI VIVUMISHI
Ni neno au mpangilio wa maneno yanayo fanyakazi ya kuvumisha nomino ama viwakilishi .
Mfano
a) Lile la kijani linauzwa
b) Maandazi ishirini yanauzwa
c) Chakula kilicholetwa hapa hakifai
d) Mtu wa siasa amewasili
e) Mfano mwingine ni huu
  4.     VIRAI VIELEZI
Hivi hudokeza namna au jinsi, mahali, wakati na kiasi cha utendekaji wa jambo.
Mfano:
a) Vijana wameimba usiku kucha
b) Wametembea harakaharaka
c) Amepanda juu ya mti
d) Tutawasiliana badae
e) Anaishi Dar es saalam
A.        ZOEZI
Ainisha virai katika sentensi zifuatazo.
1.  Tuliyopewa na kiranja yanafaa
2. Watoto walioandikishwa wameanza masomo
3.  Wa mlango upo
4.  Dada anampenda mdogo wake
5.  Majani yameota kila mahali.
 B.      Kwa kutumia mifano iliyopo hapa chini Eleza sifa na tabia za virai.
(b)        Msichana yule mzuri
(c)        Mwalimu wetu
(d)       Askari hodari
(e)        Mwanafunzi na mwalimu
        SIFA ZA KIRAI
 1. Kirai hakina muundo wa kiima- kiarifu ambao unahusisha mtendaji wa tendo na tendo                        linalotendwa.           
2. Chaweza kuwa na hadhi ya kishazi (kishazi tegemezi vumishi kinaposhushwa hadhi) 
3.  Kirai kina dhima nyingi
4. Chaweza kuwa neno moja au zaidi
5. Chaweza kutokea upande wa kiima au kiarifu.
6. Hutambulika kwa kuwa na neno kuu moja
KISHAZI
Kishazi ni tungo yenye kitenzi ambacho chaweza kujitosheleza na kukamilisha ujumbe uliokusudiwa na mzungumzaji au kuwa na kitenzi kisichoweza kujitegemea chenyewe.
            Mfano
            (i)         Mzee analima
            (ii)        Mzee aliyekuja jana
Tofauti za vishazi (i) na (ii) hapo juu ni kwamba, kishazi (i) kina kitenzi kinachojitosheleza chenyewe kwani kinakamilisha ujumbe ulio dhamiriwa na mzungumzaji. Kwa upande mwingine kitenzi cha kishazi (ii) hakimtoshelezi msikilizaji kwa sababu hakimkamilishii ujumbe na kwa hali hiyo humfanya atake maelezo zaidi kutoka kwa mzungumzaji.  Mzee aliyekuja jana amefanya nini? Au  anataka nini?
            Kutokana na maelezo hayo hapo juu hufanya kuwe na aina mbili za vishazi ambazo ni vishazi huru na vishazi tegemezi .
AINA ZA VISHAZI
1.         KISHAZI HURU
            Ni kishazi kinachotawaliwa na kitenzi kikuu ama kitenzi kishirikishi ambacho kwa kawaida hutoa ujumbe kamili usiohitaji maelezo zaidi ya kuikamilisha maana
            Mfano:
(i)Mzee analima
(ii)Watoto wanaimba vizuri
(iii) Bibi anasuka mkeka
 (iv ) Wembamba si hoja
  (v) Juma alikuwa anaimba.
Kila kishazi huru kina hadhi ya sentensi sahili kwa hiyo tungo hizi twaweza kuziita pia sentensi kwani kila moja inajitosheleza kimaana.
ZOEZI
1.Tunga sentensi 5 ukionesha vishazi huru (kwa kupigia mstari)
2.Tungo kuwa na kitenzi kikuu, na kutoa taarifa kamili je, huweza kufanya
tungo hiyo kuwa kishazi huru?
3 .Tunga sentensi tatu kila sentensi ioneshe muundo wa kishazi huru(onesha (i) t, (ii) Ts na (iii) T)
2. KISHAZI TEGEMEZI
            Ni kishazi ambacho hakitoi taarifa kamili na hujibainisha  na kiambishi cha  -O-Rekeshi kilichomo katika kitenzi na maneno mengine yanayodokeza utegemezi.
.
            Mfano:
(i)Mzee uliyemwona jana
(ii)Nyumbu aliyepigwa risasi
(iii)Mbwa aliyepata kichaa
             (iv) Kwakuwa huna  pesa
 (v)  Kama hatachelewa
            Tungo hizi hapo juu hazijakamilisha maana, zinahitaji kishazi huru ili zikamilishe maana iliyokusudiwa na mzungumzaji.
Angalia mifano ifuatayo:
(i)Mzee uliyemwona jana ni babu yangu
(ii)Nyumbu aliyepigwa risasi amekufa
(iii)Mbwa aliyepata kichaa mwogope
 (iv)Kwa kuwa huna pesa nitakununulia chakula
 (v) Kama hatachelewa hataadhibiwa
            Tungo hizi zimetoa taarifa kamili baada ya kuambatanisha vishazi viwili, kishazi tegemezi na huru. Kishazi tegemezi na kishazi huru vinapoambatana hujenga sentensi changamano.
SIFA ZA KISHAZI TEGEMEZI
1.         Kishazi tegemezi hakiwezi kutoa maana kamili ikiwa hakijaambatana na kishazi     huru.
Mfano:
            (i)Yule kijana tuliyekuwa naye jana
            (ii)Ndama aliyezaliwa
            (iii)Mbuzi aliyenunuliwa juzi
2.Kishazi tegemezi kinaweza kutambulika kwa kuwa na viambishi rejeshi vinavyoambatanishwa kwenye kitenzi na maneno yanayodokeza utegemezi.
            Mfano:
(i)Mzee uliyemwona ni babu yangu
(ii)Nyumba iliyoungua juzi imebomoka
(iii)Vyombo vilivyopotea vimepatikana
(iv) Kama atakuja tutamuona
(v)Ngoma hailii vizuri kwakuwa imepasuka
3.Kishazi tegemezi kinaweza kufutwa katika sentensi bila kuharibu maana ya sentensi nzima
Mfano:
(i) –Nyumba iliyoungua juzi imebomoka
 -Nyumba imebomoka
(ii) –Vyombo vilivyopotea vimepatikana
 -Vyombo vimepatikana
(iii) -Ndama aliyezaliwa amekufa
 -Ndama amekufa
4.Kishazi tegemezi vilevile kinaweza kutambulika kwa kuwepo vishazi, kama vile  :- ‘ingawa’, ‘kwamba’, ‘ili’, ‘kwasababu au mzizi wa ‘AMBA-’
            mfano:
(i)Mwalimu amesema kwamba wanafunzi wengi ni watoto
(ii)Mwanafunzi ambaye hayupo ataadhibiwa
5.Kishazi tegemezi kinaweza kutanguliwa au kufuatiwa na kishazi huru.
            Mfano:
(i)Nilimwona Rehema nilipokwenda mjini
(ii)Nilipokwenda mjini nilimwona Rehema
DHIMA NA HADHI YA VISHAZI
            Kishazi huru kina hadhi ya sentensi (sahili ) lakini kishazi tegemezi hakina hadhi hii. Vishazi tegemezi ambavyo hutegemea vishazi vingine katika  tungo hushuka daraja na kuchukua dhima ya kikundi.
            Baadhi ya vishazi tegemezi huchukua dhima ya vivumishi katika tungo ambayo kwa kawaida ni dhima ya kikundi au neno . Vishazi hivi huvumisha nomino iliyo katika tungo hiyo. Vishazi hivi huitwa “vishazi tegemezi vivumishi”.
Mfano:
(i)Ng’ombe aliyezaa amekufa
(ii)Kalamu       iyopoteaimepatikana
            Baadhi ya vishazi tegemezi hufanya kazi ya vielezi viwapo katika tungo sawa na vikundi vielezi. Kutokana na hali hii vishazi hivi navyo, huwa pia vimeshushwa hadhi kwani vimeteremshwa daraja kutoka kishazi kuwa sawa na kikundi ambacho kwa kawaida kina hadhi ndogo kuliko kishazi. Hivi huitwa “vishazi tegemezi”
AINA ZA VISHAZI TEGEMEZI
1.Kishazi tegemezi vumishi ( βv)
Hivi huvumisha jina lililo katika tungo
mfano:
(i)Chakula kilichopikwa leo kimeliwa chote
(ii)Wimbo unaoimbwa ni mzuri
(iii) Samaki aliyeoza ananuka
2.Kishazi tegemezi kielezi ( βE)
Hiki hutoa maelezo zaidi kwa kitendo kilicho katika tungo.
mfano:
(i)Mama alichukia aliposengenywa
(ii)Sisi tulimhurumia alivyolia
(iii)Walimu walitufukuza walipotuona
 (iv) Gari lilipinduka lilipo gonga mti.
ZOEZI
1.Andika vishazi tegemezi sita kisha onesha viangama vya utegemezi
2.Kamilisha vishazi tegemezi vya swali la kwanza kwa kuongezea vishazi huru.
3.Ainisha vishazi katika tungo zifuatazo kwa kupigia mstari na kuweka alama          “ Ktg”kama ni kishazi tegemezi na” Khr” kwa vishazi huru.
                 
(a)Hizi ndizo kalamu ulizoagiza
(b)Viti vilivyovunjika vipelekwe kwa fundi
(c)Watu wanaofanya kazi kwa bidii watapata maendeleo haraka.
(d)Leo nitakiona kilichomtoa kanga manyoya.
SENTENSI
            Sentensi ni kifungu cha maneno kuanzia neno moja na kuendelea chenye  kiima na kiarifu na kinaleta  maana kamili. Sentensi ndio kipashio cha juu kabisa katika daraja ya vipashio katika lugha
MUUNDO WA SENTENSI
            Sentensi ina sehemu kuu mbili, yaani kiima na kiarifu
1.KIIMA (K)
Kiima ni sehemu ya sentensi inayotaja nomino ambayo inahusika na            utendaji au utendekaji wa jambo. Nomino hiyo inaweza kutajwa bayana au        isitajwe kwa kuwa inaeleweka kulingana na muktadha au mazungumzo ya awali. Kiima hutokea kushoto mwa kitenzi
mfano:
          K
(i)Mwalimu / anafundisha vizuri
                        K        
(ii)Deo / alikuwa anacheza
                  K              
            (iii)  / Anaimba.
VIPASHIO VYA KIIMA
            Kiima huundwa na
            (i)Jina (N) moja
                  K
            -Juliana/ anafua nguo
                                   
            (ii)Jina na Jina (N+N)
                            K
            - Sahani na vijiko / vimo kabatini
                                               
            (iii)Jina na kivumishi (N+V)
                             K
            - Kijana mwerevu / amefaulu
                                               
            (iv)Kiwakilishi peke yake
            - Wachache / watazawadiwa
                                                k
(v)Kitenzi – jina na kivumishi
                 K
- Kuimba kwa vijana / kunafurahisha
                                               
(vi)       Kitenzi jina
              K
-Kucheza kwake / kunapendeza
                                   
(vii)      Jina na kishazi tegemezi vumishi
                        K
-Mwanafunzi aliyeshindwa mtihani / amejinyonga   
                                   
(viii)     Kiwakilishi na kivumishi
         K
-Sisi sote / tunapenda kuimba
                       
2.KIARIFU (A)
Ni sehemu ya sentensi inayojazwa na maneno yanayoarifu tendo     lililofanywa, linalofanywa au litakalofanywa. Kiarifu ndio sehemu muhimu zaidi     katika sentensi ambayo wakati mwingine huweza kusimama pekee bila kiima             kwani  wakati mwingine huchukua viwakilishi  vya kiima.
            VIPASHIO VYA KIARIFU
            (i)Kitenzi kikuu ( prediketa)
                        Mfano
:
                         A
            -Juma / anacheza
                        A               
            -Maria / anakula
                        A        
            -Juma / alikuwa anacheza
                           A                 
            -Mtoto / alitaka kwenda kusoma
                                               
                          A
            -Kuku  / ni ndege
                        A            
            -Popo / si ndege
                                     
            (ii)        Shamirisho
Ni jina au kikundi jina kinachojaza nafasi ya mtendwa. katika          sentensi.Shamirisho hutokea baada ya kitenzi kikuu au baada ya kitenzi kishirikishi.Shamirisho hujibu swali Fulani (mtenda) ametenda             nini?   
           
Mfano:
            -Mwahija amembeba / mtoto
                                       sh
-Babu amefuga / ng’ombe wengi
                                    sh
(iii)       CHAGIZO(ch)         
Ni neno au kikundi cha maneno kinachojaza nafasi ya  kielezi katika tungo. Chagizo huweza kutokea mara baada ya kitenzi kikuu au       baada ya shamirisho.
Mfano:
-Mama anasoma kitabu pole pole
                        ch           -Binti anaimba vizuri sana
                              ch      
ZOEZI
Tenga kiima na kiarifu katika sentensi zifuatazo.
1.Watachezea kwenye chumba kilicho safishwa
2.   Magari ya megongana
3.   Hawa ndio wazazi wangu
4.   Chakula kilicholetwa hakifai
5.   Nia yetu ni kuoana
AINA ZA SENTENSI
1.Sentensi sahili
            Hii ni sentensi yenye kishazi huru kimoja tu. kishazi hicho kinaweza kuwa na kifungu tenzi kimoja kifungu tenzi hicho kinaweza kuwa kitenzi kikuu       na kitenzi kisaidizi au kitenzi kishirikishi.
            Mfano:
(i)Yule ni mwalimu wetu
             t
(ii)        Twiga wanaishi porini
                           T
(iii)Vipofu walikuwa wanaomba msaada
            Ts            T                             
Muundo wa sentensi sahili
(i)muundo wa kitenzi kikuu peke yake(T)
            Mfano:
            -Anaimba
            -Wanacheza
            -Tutalima
Katika muundo huu vitenzi husimama peke yake kama sentensi sahili.Vitenzi hivi ndivyo huwa kiini cha sentensi sahili.
(ii)Muundo wa kitenzi kisaidizi na kitenzi kikuu.
            Mfano:
-Alikuwa anasoma
      Ts              T
-Alikuwa anataka kukimbia
      Ts         Ts           T
-Tulikuwa tunataka kwenda kuimba
      Ts              Ts        Ts        T
(iii)Muundo wa kitenzi kishirikishi.
            Mfano:
-Mama ni mwalimu
              t
- Huu sio mti wa dawa
            t
   - Yeye angali masomoni
                  t
 -  Ana alikuwa mwizi.
     t
SIFA ZA SENTENSI SAHILI
(i)Ina kiima ambacho kimetajwa wazi au kimeacha kutajwa kwa kuwa                    kinaeleweka wazi.
(ii)Ina kiarifu kilichoundwa na kitenzi kikuu kimoja au kitenzi kikuu nakitenzi kisaidizi au kishirikishi.
(iii)Haifungamani na sentensi nyingine na hivi inajitosheleza kimuundo na kimaana
2.SENTENSI CHANGAMANO
            Hii ni sentensi iliyojengwa kwa kutumia kishazi huru kimoja na kishazi tegemezi kimoja au zaidi
            mfano:
Sherehe iliyotangazwa imeahirishwa
Kishazi tegemezi (k/tg) – sherehe iliyotangazwa
Kishazi huru (k/hr) – sherehe imeahirishwa
            Sifa ya sentensi changamano
Sentensi changamano ina kishazi tegemezi ambacho hutegemea kishazi       kingine huru ndani ya sentensi hiyo. Hivyo msingi muhimu wa uhusiano ndani ya sentensi hizi ni ule wa kishazi kimoja kutegemea kingine
Miundo ya sentensi changamano
Miundo ya sentensi changamano hutofautiana kutegemea jinsi vishazi         tegemezi vilivyoundwa ndani yake. Kutokana na hayo kuna miundo ifuatayo ya sentensi changamano.
(i)miundo yenye vishazi – virejeshi
Miundo hii ni ile ambamo kirai – nomino hubeba kishazi – kirejeshi
            Mfano:
-Mtoto aliyekuja jana anaumwa
-Mbuzi aliyenunuliwa juzi jioni amechinjwa leo asubuhi
Katika sentensi hizi uchangamano unaingizwa na vishazi tegemezi rejeshi vilivyopigiwa mstari. Vishazi hivi vimebebwa na virai nomino kiima katika sentensi husika.
(ii)Miundo – yenye vishazi vielezi.
Vishazi hivi ni vishazi vinavyoeleza hali ya vitenzi katika vishazi huruvinavyoandamana navyo ndani ya sentensi
            Mfano:
-Mimi niliwaona walipoiba mahindi
-Mimi sikuvutiwa alivyosoma
-Maria alikimba aliponiona
Maneno yaliyopigiwa mstari ni vishazi vielezi katika kila sentensi kila kishazi kama hicho hueleza hali katika kishazi kilichoandamana nacho.
ZOEZI
1.                  “Si kila tungo ni sentensi “ Fafanua kauli hii kwa hoja za kutosha ili kubainisha tofauti zake.
2.     Kwa kutumia mifano eleza maana ya istilahi zifuatazo
(a)  Kiima
(b)  Kiarifu
(c)  Sentensi
(d) Shamirisho
(e)  Chagizo
(f)  Sentensi sahili
  3.     Nini tofauti kati ya
(a)    Sentensi sahili na sentensi shurutia
(b)   Sentensi ambatano na sentensi shangamano
   4. Kwa kutumia mifano eleza wazi muundo wa sentensi sahili, changamano na ambatano.
3.         SENTENSI AMBATANO
            Ni aina ya sentensi ambayo hujengwa na sentensi mbili au zaidi zilizounganishwa kwa kutumia viunganishi kama vile na, lakini, wala, au, tena wakati mwingine alama ya mkato (,) hutumiwa badala ya viunganishi
            Mfano:
-Mwalimu anafundisha na wanafunzi wanasikiliza
-Juma ni mrefu lakini Hamisi ni mfupi
-Ni mkatili tena hana huruma.
Miundo ya sentensi Ambatano
(i)Miundo yenye sentensi sahili tu
            mfano:
-Baba analima na mama anapika
-Siogopi wala sitishiki
(ii)Miundo yenye sentensi sahili na changamano
            Mfano:
-Wanafunzi waliofika jana wamekwenda darasani lakinimwalimu wao hakufundisha.
(iii)Miundo yenye sentensi changamano tu
-Mzee aliyefika asubuhi ameondoka na mzigo aliokuja nao ameuacha
(iv)       Miundo yenye vishazi visivyounganishwa kwa viunganishi
vishazi vyote vinavyohusika katika miundo ya aina hii vina virai–                vitenzi vyenye kiambishi tamati. Kiambishi hiki kinaeleza hali ya nia ya kutenda jambo. Kila kishazi katika miundo kama hii kikiondolewa katika muktadha wa sentensi kubwa kinakuwa sentensi inayojitegemea. Isitoshe, miundo kama hii haihusishi njeo.
Mfano:
-Mwambie, aondoke,
-Mwombe, akupe
-Mfundishe, aelewe
miundo hii mara nyingi huwa imeelekezwa kwa nafsi ya pili umoja na wingi.
4.         Sentensi shurutia.
            Hizi ni sentensi zinazoonesha kutegemeana na matukio mawili. Sentensi shurutia zimejengwa kwa vishazi tegemezi viwili vinavyoonesha kuwa tukio moja lilitazamiwa litokee au lisitokee ili la pili litokee au lisitokee. Utegemezi huo huoneshwa kwa mofimu za masharti: ‘nge’, ‘ngali’, ‘ngeli’ na ‘ki’
            Mfano:
-Angewahi kuja tungekwenda kufua
-Angelisoma kwa bidii angelifaulu mtihani
-Akija nitakuita
Sentensi shurutia zenye viangama ngeli, ngali, nge daima huwa katika         wakati uliopita. Pia kiangama kimoja kama vile ‘nge’ kikitumika katika kishazi cha mwanzo sharti kishazi cha pili kitumie kiangama hicho hicho. Hali kadhalika‘ngeli’, ‘ngali’,
ZOEZI:
Ainisha sentensi zifuatazo .
a)  Haya ni maelezo ya mtu mwingine.
b) Mbuzi aliyenunuliwa juzi amechinjwa leo asubuhi.
c) Nitakuja lakini nitachelewa
d) Angeondoka mapema asinge chelewa
e)Ng’ombe aliye nunuliwa amechinjwa ili wananchi wapate kitoweo.
UCHANGANUZI WA SENTENSI
            Kuchanganua sentensi maana yake ni kufafanua vipengele vinavyojenga sentensi katika madaraja mbalimbali.
Kila sentensi huweza kufafanuliwa au kuchanganuliwa na kubainishwa vipashio vinavyoijenga.
Hatua za uchanganuzi wa sentensi
(i)Kutaja aina ya sentensi, yaani kama ni sentensi ambatano, sahili,  changamano au shurutia         
(ii)Kutaja sehemu kuu za sentensi yaani kiima na kiarifu
(iii)Kutaja vipashio vya kiima na kiarifu yaani vikundi nomino,vikundi tenzi ,vikundi vielezi nk
(iv)  Kutambua vijenzi vikuu vinavyounda sentensi hiyo yaani vishazi vyake
(v)Kutaja aina zote za maneno yaliyomo katika sentensi.
Vifupisho vitumikavyo katika uchanga nuzi.
S – Sentensi                    K -   Kiima
A-  Kiarifu                 KN-  kikundi nomino
KT- Kikundi tenzi       KE-  Kikundi kielezi  -  Kapa
           
Njia za uchanganuzi wa sentensi.
a)  Njia ya jedwali/ Visanduku
b)  Njia ya matawi / Miti.
c)  Njia ya mishale
d) Njia ya maelezo.
Katika kidato cha tatu,hata hiyo tutatumia njia ya jedwali na matawi peke yake.
Mfano:  1.
               K                               A
   Ng’ombe huyu/ anakula majani makavu
          N          V          T           N       V
           usiku na mchana .
                        E
Njia ya jedwali
.
                             S   SAHILI           
          K
              A                                                                 
         KN
KT
         KN
           KE
    N             V
T
     N        V
     E
Ng’ombe   huyu
anakula
Majani makavu
Usiku na mchana
                           Njia ya matawi.
                                                                                     
                           SAHILI
Ngo,mbe huyu anakula majani makavu usiku na mchana
        S . SAHILI
                  
    K                      A
                                                  
                     KT       KN       KE                                             
   KN                     
N +  V            T       N + V        E      
Ng,ombe huyu  anakula  majani  makavu 
                                                                 
                                          Usiku na mchana
Mfano:2
                   K                       A
 Samaki aliyeletwa / amechina kabisa  
      N            V                 T            E
   S . CHANGAMANO
           
JEDWALI
           
               S     CHANGAMANO
              K
A
               KN
KT
KE
           N+V
T
E
     Samaki aliyeletwa
Amechina
Kabisa
          
                           
MATAWI:
        
                                                       CHANGAMANO:
                       S. CHANGAMANO:                                                       


 


                                                                             
           K                  A
                                                                             
         KN       KT            KE  
      N  + V      T               E
Samaki   aliyeletwa   amechina   sana
3. Mfano:
Wanafunzi wanasoma sana lakini wanacho kisoma hawakizingatii.
      AMBATANO:
     S1.    Wanafunzi wanasoma sana.
      S2.    Wanafunzi wanacho kisoma hawakizingatii.
JEDWALI
                               S    AMBATANO
S1.       K
                A
S2.        K
        A
       KN
 KT
KE
      KN
     KT
   N
  T
   E
U
     W
       T
wanafunzi
wanasoma
sana
lakini
Wanacho kisoma
Hawakizingatii.
MATAWI:
                                                                        AMBATANO
                                                           
                          S.  AMBATANO                                                                  
                        
                                                                               
        S1                                   S2                                                                                                                                      
K             A
                          K                    A
KN      KT      KE
                            KN                  KT
N           T          E       U     W               T
                                
                             Sana     lakini       hawakizingatii
                                                wanachoikisoma
Wanafunzi wanasoma
4.  Mfano:.
           A
K/Ondoka hapa   S.     SAHILI
        T         E
JEDWALI
                            S                SAHILI
                K 
                        A
                
          KT
    KE
           T     
     E
     Ondoka
     hapa
MATAWI:
                             S.       SAHILI
     K                     A
                     KT      KE






 


                 
                                    T         E
          O ndoka         hapa
K             A
5.  Mimi / niseme kitu gani sasa.  SAHILI
         W         T       N      V     E
JEDWALI:
               S .              SAHILI
      K
                            A
     KN
KT
 KN
KE
     W
    T
N+V
   E
    Mimi
niseme
Kitu gani
Sasa.
MATAWI:
                            S.  SAHILI
                K                         A
KN                KT       KN        KE
     
       W                         T      N+ V         E
   Mimi                   Niseme  kitu  gani  sasa
        K                    A
6 . Haya/ni  maelezo ya mtu mwingine
        W   t       N                   V
JEDWALI :
 
                    S.            SAHILI
         K 
                        A
         KN
   KT
         KN
             W
      t
         N+V
 Haya
ni
Maelezo ya mtu mwingine
       
MATAWI
 S.   SAHILI


 


K                  A






 


      KN             KT         KN
    W                   t          N  +    V
 Haya        ni     maelezo  ya mtu mwingine
                               
                
                          
   
             K                     A
7.Mwalimu wetu/ angali anafundisha vizuri SAHILI                     
         N            V       Ts           T             E
                                  S.               SAHILI
                 K
                               A
                 KN
               KT
               KE
               N+V            
TS        +   T
                  E
   Mwalimu  wetu
 Angali
anafundisha   
 Vizuri
MAJEDWALI:
                                
             S. SAHILI
    K                    A
KN               KT        KE


 


N  + V        TS  +  T    E


 


    Mwalimu  wetu   angali
                       Anafundisha    vizuri
ZOEZI
            .
1.Changanua sentensi zifuatazo kwa Njia ya matawi na majedwali
     
(a)  Maria ni mwalimu wetu.
(b)  Mtoto aliyeanguka jana usiku na Kuvunjika mkono
      amelazwa    Hospitali.
                              .
(c)  Bosi aliyefukuzwa kazi amekufa
(d) Katika nchi ya vipofu chongo ni  Mfalme.
   (e ) Huko shinyanga misitu Imeyeyuka kama siagi.
( a )     CHATI (Chemsha Bongo)
1           2         3         4        5         6        7
1
3
5
Kwenda Chini
1.  Majengo ya kusomeshea Wanafunzi.
3.  Malipo kwa huduma fulani
5.  Sikukuu ya Waislamu
7.  Sehemu ya Wizara au Kampuni
Kwenda Kulia
1.  Mtu anayetoa  maelezo ya kuthibitisha
3.  Lia kama fahali

5.  Kuwa juu ya maji bila kuzama.  
 
Powered by Blogger.