ACT-Wazalendo Kuvuna Wabunge Kutoka CCM na CHADEMA

Baada ya vumbi la uchaguzi mkuu kuanza kumtika tumeona kura za maoni zinazoendelea kupigwa kutoka Chadema na CCM kwenye kila jimbo.

Chadema wanachagua wagombea ili baadae watakapokubaliana na wenzao CUF, NCCR Mageuzi, NLD, itabidi baadhi ya Majimbo wapewe vyama hivyo ambavyo vipo kwenye umoja huo UKAWA.

Na hapo ndiyo utazuka mgogoro mkubwa wa baadhi ya wagombea ambao majimbo yao watapewa UKAWA, hapo ndipo ACT-Wazalendo watakapojipatia wagombea wanaokubalika na kuwasimamisha kama wagombea wa ACT-Wazalendo.

Vile wagombea wa CCM ambao watakatwa pia kuna uwezekano mkubwa wakakimbilia ACT-Wazalendo.

Hapo ndiyo kauli ya Zitto kuwa wagombea hamsini watahamia ACT-Wazalendo itatimia.

Huu ndiyo ukweli ingawa unauma kuusoma hii hali kwenye siasa uwa inatumika sana.

Wale wote waliofanyiwa fitna watatumia mbinu hii ambayo imewahi kutumiwa na Dr.W.Slaa wakati yupo CCM kabla ya kutimkia Chadema na kushinda ubunge.


Powered by Blogger.