FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI NA KIAFRIKA MODULE 1; UTANGULIZI FASIHINSIMULIZI YA KISWAHILI-2


UHUSIANO  WA FASIHI SIMULIZI NA TAALUMA NYINGINE
 Fasihi simulizi haipo katika upweke au Ombwe bali inahusiana na taaluma mbali mbali .Hii inatokana  na ukongwe  wake yaani dhima zake,sifa zake,utendaji wake, na n.k vinafranya ihusiane na taaluma nyingine.Miongoni mwa taaluma hizo ni Mziki,Sosholojia,Historia,Isimu ya Lugha,Etimolojia na hata Fasihi Andishi.
A.     UHUSIANO WA FASIHI SIMULIZI  NA  MUZIKI
Mziki ni nini? Au ni vitu gani vinafanya utambue kuwa huu ni mziki?
Ø  Ala za mziki kama vile zeze,marimba,ngoma,manyanga,n.k.Fasihi simulizi inahusiana na mziki katika utendaji kwani katika    Fasihi simulizi kwani vipera mbali mbali vya fasihi simulizi vinahusisha ala fulani za muziki,mfano Majigambo,Tenzi.
B.Historia
 ni taaluma  inayochunguza matukio kisayansi ya wakati uliopita na uliopo.Ni taaluma inayoshughulika na uchunguzi wa maisha ya binadamu ambayo yanatuwezesha kujua maendeleo na mabadiliko ya binadamu. Fasihi  ananafasi kubwa katika historia ya binadamu kwa kupitia baadhi ya vipera vya fasihi simulizi.Hivyo  Fasihi simulizi  inatusaidia kuelewa historia yetu (sayansi fulani) mfano Tenzi,baadhi ya tenzi za kiswahili zinazungumzia mashujaa wa Afrika,Mfano Fumo Liyongo.Hii inatusaidia  kujua mtzamo wa jamii husika katika kipindi fulani cha kihistoria.Wanahistoria  pia wamechota baadhi ya mambo yao kutoka katika Fasihi simulizi.Data za fasihi simulizi zinasaidia kujenga rekodi za kihistoria .Vipera mbali mbali kama Tendi,Visakale,Tarihi,Shajara n.k vinatusaidia kuelewa historia ya jamii japo kwa kiasi kidogo kuhusu matukio ya watu au mashujaa katika jamii hiyo.
Suala la utendaji/Utofauti wa vipera vya fasihi simulizi  zamani na sasa vinaweza  kutusaidia kuelewa historia ya jamii fulani.Fasihi simulizi inasaidia kuhifadhi na kuendeleza historia katika jamii mfano majigambo.
C.      SOSHOLOJIA (Elimu viumbe,Athropolojia)
Ni taaluma inayoichunguza jamii kisayansi ili kujua mienendo yake na nguzo mbali mbali zinazoongoza jamii hiyo.Mfano Matabaka ,Dini,kijadi,.Vingele hivi  tunavipata  katika sosholojia na vinatusaidia kuelewa namna ambayo vinweza kuzuia  mienendo.
  Hivyo  Fasihi simulizi tangu hapo mwanzo inatusaidia kujua hiyo mienendo  au mifumo mbali mbali ya jamii,kipera kinaweza kuwa chombo cha kutetea utabaka au kuchochotea  utabaka.
 Fasihi simulizi kilikuwa chombo pekee cha kuwasilisha maadili ya jamii kupitia vipera  kama vile kitendawili au nyimbo.Kupitia Fasihi simulizi tunaweza kurithishwa utamaduni ,mila na desturi za jamii hiyo.Taarifa za kisosholojia pia zinapatikana katika kazi za kifasihi.Mienendo na mabadiliko  mifumo ya kiuchumi na kijamii inapatikana kwa kurejelea kazi za Fasihi simulizi.

D.     UTAMADUNI
Utamaduni unapatikana katika fasihi simulizi  kwani fasihi simulizi ni chombo kizuri cha kurithisha utamaduni wa jamii husika na utamaduni huo hurithishwa kupitia utendaji wake katika baadhi ya vipengele kama vil;Maleba (mavazi),Utendaji,Mazingira ya utendaji,Vifaa,Fani husika.
Hivyo uhusiano kati Fasihi simulizi na utamaduni pia upo katikaLugha kwani Fasihi simulizi hutumia lugha,na lugha ni nyenzo muhimu za fani husika  hivyo fasihi kama chombo na sehemu ya utamaduni inasaidia mambo kadha wa kadha kama vile;
Ø  Inakuuza utamaduni
Ø  Inahifadhi utamaduni
Ø  Inaeneza utamaduni
Ø  Kueleza utamaduni wa jamii hiyo.
  Kwa ujumla fasihi simulizi ipo katika kila hatua ya maisha yetu.
E.      ETHIOLOJIA
Fasihi simulizi inatumika  katika dini kama vile nyimbo na maandiko ya kidini ambayo yanaweza kuwa hadithi ,nyimbo ambazo zimo katika biblia na vitabu vya nyimbo za kidini.mfano Utenzi wa sundiata.
F.FASIHI ANDISHI
Uhusiano kati ya Fasihi simulizi na Fasihi andishi utafiti unaonyesha kuwa karibu tanzu zote za Fasihi   andishi zimetokana na Fasihi simulizi.
Ø  Maigizo yanazaa tamthiliya,pia uhusiano huu unajitokeza katika nafasi ya fasihi simulizi  katika  tanzu za fasihi andishi.Fasihi andishi inanufaika kwa kiwango kikubwa kutoka katika fasihi simulizi  kifani na kimaudhui kama vile vipera,matumizi ya lugha n.k vipengele hivi vya fasihi simulizi vinatumiwa katika fasihi andishi.Vitu hivi vinaleta athari kubwa katika fasihi simulizi.
Ø  Pia  kuna mianzo maalum katika tamthiliya kuna fomula za kihadithi mfano,Niendelee nisiendelee?
Ø  Vile vile matumizi ya wahusika wanyama,ndege,mazimwi,majitu n.k, pia matumizi ya wahusika bapa,matumizi y mbalimbali kama vile taswira,ucheshi n.k
Ø  Suala la kuingiliana kwa tanzu,katika fasihi  andishi kuna tanzu za fasihi simulizi kama vile hadithi,ngano,nyimbo n.k
Ø  Pia katika mashairi kuna utambaji ,malumbano na vipera vingine vya fasihi simulizi.


Powered by Blogger.