MTIHANI WA KUJIPIMA KIDATO CHA SITA KISWAHILI - 2

MTIHANI WA KUJIPIMA
KIDATO CHA SITA
121/2                                                  KISWAHILI - 2
Muda: Saa  3:00                                                                                      
Maelekezo
1. Karatasi hii ina maswali kumi (10) katika sehemu A, B, C, D na E.
2. Jibu maswali matano (5) kwa kuchagua swali moja (1) kutoka kila sehemu.
3. Kila swali lina alama ishirini (20).
4. Simu za mkononi haziruhusiwi katika chumba cha mtihani.
5. Vikokotozi haviruhusiwi katika chumba cha mtihani.
6. Swali lisilo na namba halitasahihishwa.


SEHEMU A (Alama 20)
FASIHI KWA UJUMLA
   1.  “Mhakiki wa kazi za Fasihi Andishi ni mnyonyaji wa mwandishi asilia.” Kubali au         kataa dai hili kwa hoja tano.
    2.    Fafanua kwa hoja nne (4) juu ya nadhariya za chimbuko la sanaa na fasihi kwa            ujumla.
SEHEMU B (Alama 20)
USHAIRI
                              Kimbunga                    –    Haji  Gora  Haji
                              Mapenzi     Bora          –    Shaaban   Robert
                              Chungu      Tamu        –   Theobald   A.  Mvungi
                              Fungate   ya  Uhuru    -   Mohamed  S.  Khatibu  
     3.    “Mshairi ni mwalimu wa jamii kwani hugusa nyanja zote zinazohusu maendeleo ya jamii.” Thibitisha kwa hoja tatu toka kila diwani miongoni mwa vitabu viwili ulivyosoma.
  4. Jadili dhamira ya mapenzi kama inavyojitokeza katika vitabu viwili kati ya vilivyoorodheshwa hapo juu. Toa hoja tatu kila diwani.
SEHEMU C (Alama 20)
RIWAYA
                              Usiku Utakapokwisha      –   Mbunda  Msokile
                              Kufikirika                          -   Shaaban Robert
                              Mfadhili                              -   Hussein  Tuwa
                              Vuta  N’kuvute                   -   Shafi Adam Shafi
  5. “Kuwepo kwa fasihi katika jamii ni tarajio la kimsingi, inapokosekana jamii hupungukiwa katika ukamilifu wake.” Kwa kutumia vitabu viwili ulivyosoma kubali au kataa kauli hii ukitoa hoja tatu toka kila riwaya. 
   6.    Jina la kitabu husadifu yaliyomo ndani ya kitabu. Thibitisha kauli hii kwa hoja tatu toka kila kitabu miongoni mwa riwaya mbili ulizosoma.
SEHEMU D (Alama 20)
TAMTHILIYA
                              Kwenye Ukingo wa Thim   –  Ebrahim  Hussein
                              Morani                                  –  Emmanuel  Mbogo
                              Kivuli Kinaishi                     –  Said  Mohamed
                              Nguzo Mama                        –  Penina  Muhando
7.     Miongoni mwa majukumu  ya msanii ni kuzungumzia matatizo mbalimbali yanayoikumba jamii. Thibitisha kauli hii kwa hoja tatu toka kila kitabu ukitumia tamthiliya mbili kati ya ulizosoma.
8.    Waandishi wa Tamthiliya kwa kawaida hawatenganishi Fasihi Simulizi na Fasihi Andishi. Jadili ukitoa hoja tatu toka kila kitabu miongoni mwa tamthiliya mbili ulizosoma.
SEHEMU E (Alama 20)
USANIFU WA MAANDISHI
9.    Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yanayofuata:
Soma mtoto wa kike, soma usitetereke,
Soma usishawishike, hadi mwishoni ufike,
Soma nyadhifa ushike, nchi hii utumike,
Soma nakutegemea, soma mtoto wa kike.
Soma usibabaike, mafudisho uyashike,
Soma nami nifurahike, vishawishi uepuke,
Soma kisha utumike, katu usihangaike,
Soma nakutegemea, soma mtoto wa kike.
Soma na ufundishike, na vikwazo uvivuke,
Soma nami niridhikr, moyo nisisononeke,
Soma kesho unizike, mahali papa niweke,
Soma nakutegemea, soma mtoto wa kike.
Soma usirukeruke, bongo zako zichemke,
Soma yote ukumbuke, masomo yasiponyoke,
Soma usirubunike, mwanangu usipotoke,
Soma nakutegemea, soma mtoto wa kike.
Soma usipaparike, raha zina muda wake,
Soma nisifesheheke, wenzangu wasinicheke,
Soma nami nitukuke, Unasi niheshimike,
Soma nakutegemea, soma mtoto wa kike.
Soma nisinyanyasike, wenye wivu watapike,
Soma nami ninyanyuke, wenzangu wasinicheke,
Soma nisiwe mpweke, tamati nitamatie,
Soma nakutegemea, soma mtoto wa kike.
MASWALI:
(a)  Kwa sentensi moja eleza ujumbe anaoutoa mshairi.
(b) Mwandishi ana maana gani kusema, “…..soma usirubunike, mwanangu……”
(c)  Kituo cha shairi hili ni nini?
(d) Mshairi asemapo: “Soma nisifedheheke, wenzangu wasinicheke.” Haya maneno yanaelekezwa kwa nani?
(e)  Je, hili ni shairi la mkabala gani?
10. Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha eleza mbinu za kifani zilizotumika kufikisha ujumbe.
Mjomba! Mjomba! Mjomba angalia kule wale ni wanafunzi wamemzingira mama muuzaji wa mihogo. Wafanyaje? Hawana jinsi, ni mihogo tu wanayoweza kununua kwa shilingi mia moja walizopewa na wazazi wao. Ndiyo, ndiyo mjomba hali ni ngumu.
Mjomba angalia kule unaona njaa, vifo…….kila kitu kimezingira wazazi wa wanafunzi, maisha kama vita. Kila mtu anapambana. Maisha safari, kila mtu anasafiri.
Mjomba hali imekuwa mbaya. Watu wanajadiliana kila leo mtaani. Wanajiuliza na kuuliza maisha maswali magumu.
Watu: Maisha wapi unatupeleka?
Maisha: Hamna haki ya kuuliza hilo swali.
Watu: Lakini tulipoanza safari tulikubaliana kuwa utatupa taarifa ya kila
            tuendako.
Maisha: Nakumbuka tulikubaliana lakini haki hiyo imefutwa. Haipo tena. Kwa
               hiyo, fungeni midomo na mikanda msonge mbele.
Watu: Jamani tumegeukwa! Tumegeukwa! Tunanyanyaswa! Tunaonewa! Tumekwisha!
Mjomba sikia, siku zinakuja na siku zimefika ambapo mawe yanasema; jamani! Ee tulikuwa tumelala, tumeamka sasa mtatutambua; Tunakuja, Tusubirini…..
Mjomba unawaona walimu, waangalie wale pale wameegesha magari yao ya kifahari. Waone wanaondoa magari yao kwa kasi ya ajabu kurejea nyumbani kwao baada ya kazi. Wanaelekea Masaki, Mikocheni, Msasani, Mbezi Beach, Kinyerezi. Naam, ndiko wanastahili kuishi. Ndiko kwenye hadhi yao. CHANZO>>>>>>
Powered by Blogger.