FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI NA KIAFRIKA



MATATIZO YA TAFSIRI
            Tafsiri
Ni kuchukua mawazo yaliyo katika maandishi kutoka  lugha chanzo na kuyaweka mawazo yanayolingana nayo katika lugha lengwa.
 Ni zoezi  la uhawilishaji wa mawazo katika maandishi kutoka lugha moja kwenda nyingine.
Mwansoko (2006) Kitangulizi cha Fasihi Tafsiri ni daraja linalounganisha jamii zinzotumia lugha mbili tofauti.  Husaidia kueneza utamaduni maarifa na fasihi toka jamii moja hadi nyingine.
Katika karne 20 Tafsiri zilitumika katika kuleta  maarifa kwa jamii.
-           Pia hadithi mbalimbali za mataifa mengine zimetafsiri kuwa Kiswahili
Mfano:            Hekeya za abunuasi,  Tafsiri mbalimbali zinafanyika katika tanzu mbalimbali lakini tafsiri hizi zina changamoto zake.
Matatizo hayo yanaweza tokana na tofauti ya lugha, utamaduni, Umahiri wa anayetafsiri, Itikadi ya anayetafsiri.
                        Lugha ya matusi ni mbinu muhimu katika nyimbo (utamaduni) wa kiafrika.
            *           Wageni walitafsiri vitu kwa ufinyu na kumba mambo ambayo ni muhimu
            Mfano:            Okpewho jamii (2004) Bacha alifanya utafiti katika kiswhili alisema “katika
jamii za Afrika mashriki hakuna ushairi, vina, mizani, hisia, wala chochote cha kukonga”
Katika kutafsiri, mtafsiri anaweza kupunguza au kuongeza vitu.
-           Unapotafsiri ni lazima ujue suala la utamaduni hivyo utapaswa kutafsiri japokuwa
inakuwa ngumu katika jamii lengwa.
-           Kukosekana kwa radha na vionjo katika jamii lengwa, hivyo mtafsiri hapaswi kupuuza vipengele vya lugha bali anapaswa kufany kama inavyostahiri.
Tafsiri ni dhana muhimu katika taaluma yeyote ila ikiwemo fasihi simulizi lakini kuna changamoto zake
Mwansoko et al (2006) changamoto za kutafsiri:-
i)          Tofauti za kiitikadi, kihistoria na kimazingira kutoka lugha chanzi kwenda lugha
lengwa.
ii)        Tofauti za kiisimu, ufasiri wa matini ya kifasihi huna budi kuwa mahiri wa lugha
zote mbili zinazoshughulikiwa yaani miundo ya sentensi, maneno, Matamshi pamoja na Isimu kwa ujumla.  Kwani vipengele hivi hutofautiana kati ya jamii moja na nyingine.
            iii)       Istalahi Mpya / Kuibuka                 
                        Inapojitoeza istalahi mpya katika fasii simulizi kutokana na maendeleo ya Sayansi
na Teknolojia huleta shida kutafsiri.  Mfano:     katika TEHAMA.
            iv)       Tofauti ya Kiutamaduni,
                        Utamaduni ni jumla ya mambo yote yanayotawala katika jamii.
            v)         Fasihi Simulizi kama kazi ya sanaa hasa ushairi wa kiafrika unahitaji kuwa na
vionjo kama vina n.k. lakini kazi hizi zinapo tafsiri ubora wake hapotea yaani vipengele vyake vya kisanaa hupotea.
Waliofanya tafsiri ni wasomi wa kigeni, wazungu hivyo vionjo walgusin kwa kiasi kidogo sana hivyo ukiviacha vipengele vya kisanaa unaifanya tafsiri kuwa pungufu.
            vi)       Udhaifu wa Tafsiri uliofanywa na wageni, walifanya jitihada kubwa lakini 
hawakuzijua lugha chanzi kiasi cha kutosha hivyo hawakufikia viwango.
            MKABALA WA KIDHAMIRA KATIKA FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI
NA YA KIAFRIKA
Tunaangalia
                        Dhamira zinazojitokeza zaidi au Dhamira mardudi au Dhamira radidi
                        Fasihi Simulizi ya Kiswahili na Kiafrika au mfumo wa maisha
DHAMIRA RADIDI
Kwa kawaida Fasihi Simulizi ina Fani na Maudhuni na Maudhuri ina hisisha:-
-           Mwanzo
-           Falsafa
-           Historia
-           Maisha ya waafrika
Fasihi Simulizi ya waafrika inajengwa na dhumira.  Hiki ni kipengele cha maudhui na kiutamaduni
-           Tunapoangalia dhamira radidi tunarejelea vipera.  Mfano:    katika ushairi
Dhina inaweza kuhusu Dini, Mapenzi, Uwindaji, Michezo ya watoto, Jando na Unyago Shukrani, Kuzaliwa kwa mtoto.
Dhamira radidi / Marudidi lazima uwe umesoma, umesikiliza na kutazama kazi mbalimbali za fasihi vyakutosha.
Urudidi ni dhana ya kitakwimu Udofao yaani kujitokeza mara nyingi zaidi kuliko dhamira nyingine(mchomozo) katika Fasihi Simulizi dhamira zipo nyingi zipo zile ambazo husisitiza maadili, Tabia njema, Masuala ya uzazi, Umoja na mshikamo Ujasiri, Uganga wachawazi, Uhai na kifo, Malezi n.k.
Mfano:            Katika Mithali kunaweza kuwa na dhamira kama Wema, Umoja Malezi,
Bidii ya kufanya kazi, Imani kwa Mungu, kukemea uvivu n.k.
Mfano:            -           Mkataa wengi ni Mchawi,
-           Monagana upwa hali wali mkavu
-           Wema ni hakiba
            Jando na Unyago.     -           Kufanya kazi, usafi, malezi
            Mfano:            -           Majigambo
            Samweli M (  ) anasema majiga yanaweza kuhusu ushujaa, namna gani mtu anapendwa
katika wengine, ufanyaji kazi n.k.

Masimulizi
-           Hadithi hubeba dhamira mbalimbali
Mfano:                        Mapenzi na ndoa , Uzazi chuki, wivu, Ukewenza
FASIHI NA MFUMO WA MAISHA
Hapa tunaangalia Dhima ya Fasihi Simulizi katika maisha / au kwa jamii yake kwa kurejelea mifano mbalimbali kutoka katika Fasihi Simulizi.
Mwanadamu amepitia katika mifumo mbalimbali ya maisha na katika mifumo hiyo Fasihi Simulizi imekiwa ikitenda kazi yake.
Dhima ya Fasihi Simulizi  iliweza kua chany au hasi kutegemea mfano wa  maisha japokuwa katika kipindi cha ukoloni.  Fasihi Simulizi ilitazamwa kama hasi eti walisema ni ya kishenzi.  Hapa tunapitia tanzu kama :
i)          Ushairi Simulizi
Umefungamana na maisha ya mwanadamu.  Mfano Nyimbo zilituiwa na mwanadamu kuchapuza kazi na kuifanya kazi kuwa rahisi
-           Pia nyimbo zilielimisha, onya na kuhamasisha shughuli mbalimbali.  Jamii
nyingi kwa Fasihi Simulizi ilikuwa nyenzo muhimu katika kutoa maarifa.
-           Nyimbo ziliambatana na shughuli za maendeleo kama :  kazi
            -           Burudani
            -           Za kubembeleza watoto
                        Fasihi Simulizi ilifungamana na maisha kwani kulikuwa na nyimbo mbali za kazi
kama za Vita, Uvuvi, Kilimo, Bembesi,
katika Jando na Unyago Nyimbo zilihimiza
-           Kazi
-           Usafi
-           Malezi
-           Kutii
-           Kufanya kazi kwa bidii
Za Harusi zilihimiza:-
-           Kupendana
-           Kuacha Uongo
-            Uvumilivu
-           Kuwajibika
Za Dini zilihimiza
-           Mahusiano kati ya wanadamu na Mungu au Miungu yao
Za Sifa
-           Maudhri yake ya majigambo
Za Misiba
SEMI
Vitendawili   (Dhima yake) kuna fomula maalumu yaani mianzo na miisho yake.
Dhina ya kujenga udadisi na kurekodi historia ya maisha ya mwanadamu na husaidia kujenga kumbukumbu.
-           Pia husaidia jamii kutambua mazingira yanayomzunguka.





Methali
Hubeba Maudhiri na Dhamira.
Dhina zake,
Methali ni uti wa mgongo wa Fasihi Simulizi kwani hurejelea katika kila jambo linalozungumzia.
            -           Methali hutia radha katika mazungumzo.
            -           Hupamba mawasiliano zina dhima ya kiujumi yaani uzuri katika sanaa.
            -           Hutoa maadili, kama kuonya, kushauri kukejeli, kuadhibu.
            -           Pia methali zina busara
-           Huibua tafakuri
-           Huweka msisitizo juu ya jambo fulani linalozungumziwa
Fasihi Simulizi
Mlokozi (1996) anasea Fasihi Simulizi inabeba dhima zake ilibeba dhima hizo za kijamii tangu zamani yaani tangu wakati wa kina Alstotte,
-           Huburudisha kuvura hisia za mwili.
-           Ilikuwa inajenga tabia ya jamii
-           Ilikuwa inastarehesha                 kumpumzisha mtu baada ya kazi nzito.
Horace  anasema Dhima ya Fasihi Simulizi imekuwa ni sanaa tamu na tumizi.  Kama 19 na 20  wahikiki wa kimrx wanasema  Dhina ya Fasihi na Fasihi Simulizi ilibeba maktadha mahususi ulikuwa ni kuburudisha, kuulimisha, kuhifadhi amali za jamii kuonyesha kweli wa maisha, kuonyesha harakati za jamii, kuhfadhi lugha.
Kwa ujumla
Wahakiki wa Fasihi na Fasihi Simulizi ni kama John Ramadhani, Penina Mhando Balisidya, Kahigi, Mulokozi, F.  Nkwera Sengo na Kiango, F. E. M Senkoro, Musokile, Mazrui, hawa wamejadili sana kuhusu fafasi ya Fasihi Simulizi katika j amii, wamesema Fasihi Simulizi indhima kubwa katika kuelezea utubaka yaani Masusiano kati ya kundi moj la jamii na kundi jingine.
-           Wanadai kuwa Fasihi Simulizi ina dhima ya Kiitikadi (umwinyi, ubepari ujamii utabaka, katika jamii kuna wenye nacho na wasio nacho hivyo Fasihi Simulizi hutafuta usanii.
Itikadi ina mambo mengi kama:-
-           Musuala ya maslahi kati ya mtu mmoja na mwingine
Mfano             -           Vitendawili, misemo
Dhima ya kiuchumi – huhusu kazi, kilimo, uvuvi, kuwinda n.k.
Nyimbo zilistarehesha mtu baada ya kazi nzito.
Dhima ya kiutamaduni kama vile:- 
*           kuhifadhi mila za jamii
*           kuhifadhi imani
*           Desturi
*           Historia
            Mfano             -           Mivigha, ngoma, ngemezi
            Dhima ya Kisiasa
            Mfano             -           Nyimbo zinatumika katika siasa.
            Mfano             -           Uchaguzi, kubadili  mifumo mbali nyimbo hutia hamasa.
FASIHI SIMULIZI NA FALSAFA YA K IAFRIKA
Fasihi Simulizi na Falsafa ya Kiafrika ni dhana ambazo zina tegemeana na kushikana zinafanana sana.  Neno Falsafas “Philesophy” “Philo” LOVE na Sophia means Wisdom.
:   Philosophy mean study of Love of Wisdom Dhana hizi mbili zinashikamana kwa vipengele vinavyounda Fasihi Simulizi ni hivyo hivyo huunda falasafa ya kiafrika.
Mbili (2011) anasema Falsafa ya Kiafrika ni mtazamo muelekeo na itikadi ya waafrika na wasio waafrika kuhusu mila na desturi za kiafrika.
Falsafa ya Kiafrika imejikita katika mila na desturi na vipengele vya Fasihi Simulizi.  Hivyo Falsafa ya  kiafrika inachota vipengele vya Fasihi Simulizi
Matambiko, Uhai na Kifo
Malezi, Jando na Unyago, Dini za kijadi (matambiko) kuabudu mizimu na wahenga vyote hivyo ni vipengele vinavyounda fabafa ya Kiafrika.
Vipengele vya Ontolojia ya kibantu inafanna na ile ya Fasihi Simulizi.
Mfano             -           Wanaimani dhabiti katika miungu na hiyo Miungu ipo katika darajia kama Mahoka, Mizimu
            Katika Falsafa ya Kiafrika wabantu wanaamini       sana katika uhai na hoja ya kifo
(Temples) hata salamu ya Mwafrika ina hofu ya kifo
Kuna nguvu inayoongeza uhai kama waganga na nguvu inayo punguza uhai kama wachawi.
            Wanaabudu mapangoni n.k.
*           Heshima na Umri
Waafrika wanaheshimu sana umri kuwa mtu mzima anasadikiwa kuwa anabusara zaidi.
            Temples         -           Waafrika wanapenda vitu vya uduara
Mfano            -           nyumba, vyombo
            Uduara pia katika kutoa majina.
Katika Fasihi Simulizi dhana hii ya uduara na ujumi inaooa kuwa vitu bora ni vile vilivyo katika uduara.

Si jambo rahisi kutenganisha Fasihi Simulizi na Falsafa ya Kiafrika kwani ni dhana zinazotegemea.

Fasihi Simulizi inategemea sana Falsafa ya Kiafrika kama nyenzo au rasilimali yake pia Falsafa ya Kiafrika inategemea vipengele vya Fasihi Simulizi.
>>>>>>>>>MWISHO>>>>>>>>>>>
Powered by Blogger.