FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI NA KIAFRIKA


FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI NA KIAFRIKA
MODULE 1:  UTANGULIZI
FASIHI SIMULIZI YA  KISWAHILI      -Senkoro (1988 : 10 – 11)
            Ni ile inayojitambulisha na kujihusisha na utamaduni wa waswahili popote pale walipo ulimwenguni.  Utamaduni wa waswahili ni ule unaohusu desturi na mila za waswahili, sayansi sanaa zao, uchumi wao na maisha yao kwa ujumla.  Hali kadhalika inawahusika, Maudhui, fabafa, mawazo, historia n.k. vinavyoenda na na maisha ya waswahili.
            Kwa upande wa lugha, fabafa ya Kiswahili ni ile inayotumia lugha au lahaja ya Kiswahili.
FASIHI SIMULIZI YA KIAFRIKA
            Ni ili inayojitambulisha na kujihisisha na utamaduni wa Afrika kupitia jamii na lugha zao.  Hivyo utamaduni wa waafrika ni ule unaohusu mila zao, sanaa zao, siasa na uchumi wao kwa ujumla.
            Hivyo fasihi simulizi ya kiafrika ina mawazo, fabafa, wahusika, maudhui , na dhamira zinazoendana  na maisha yao.  Imefungwa kwa lugha za kiafrika au lahaja za lugha hizo.
            Je fasihi simulzi ni ya kiafrika?
            Je fasihi simulzi inayotumia llugha za nje zinazotumika Afrika ni ya Kiafrika pia?
Je fasihi simulzi ya kiafrika inapaswa kuandikwa na nani?  Mwafrika au hata Mzungu?
FASIHI SIMULIZI
Mgullu (2003:16)
Ni sanaa itoayo maudhui yake kwa lugha ya maneno ambayo hutamkwa ama hutendwa.
Ni fasihi inayohusu mkusanyiko wa kazi za kisanaa za binadamu zinazowasilishwa kwa njia ya mazungumzo au utendaji.  Siku hizi fasihi simulizi huhifadhiwa kwa kuandikwa vitabuni, kanda za video, redio na santuri.
Mlacha (1980 – 16)
Ni Nyanja ya maisha ya jamii ambayo huchangia sana katika kuendeleza na kudumisha historia ya jamii husika.
Fasihi simulizi huchangia katika kuelimisha jamii kuhusu asili yake, chanzo chake na maendeleo ya utamaduni wake na maisha ya jamii hiyo tangia zamani.
WAMITILA (2003 : 44)
Ni dhana inayotumika kurejelea kazi ambazo kimsingi hudokeza na kwa njia ya msimulizi au mdomo.  Hutumika katika jamii kama njia ya kupashana maarifa kama njia a kupashana maarifa yanayohusu utamaduni Fulani historia ya jamii na matamnio yao.
OKPEWHO (1992 : 3)
Ni matini bunifu ambazo huvutia fikra zetu, au hisia zetu, kama vile hadithik mashairi na michezo ya kugiza (matini).  Sio kwa matini za ukweli kama vile ripoti za magazeti au rekodi za kihistoria, hata hivyo nazo zikiandikwa kwa kuvutia zinaweza kuwa fasihi.
MLOKOZI (1996 : 24)
Ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia yam domo na vitendo bila kutumia maadishi.
Hivyo ni tukio linalofungamana na muktadha Fulani ya kijamii na kutawaliwa na muingiliano wa mambo sita, fanani (msomi).  Hadhira, fani inayotendwa, tukio, mahali na wakati.  Fasihi simulizi inaendana na Tukio.
SEMINA:Swali la 1:
Mbali na jitihada za wataalam mbali mbali katika kufasili fasihi simulizi na fashi simulizi ya kiafrika mpaka sasa hakuna fasili iliyotoshelevu.  Jadili dai hili na pendekezani fasili yenu.
KUFANANA NA KUTOFAUTIANA KWA FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI NA KIAFRIKA
i)          Zote zinahifadhi mila, desturi na historia pamoja na lugha za jamii husika.
ii)        Zote zinahitaji utendaji (maleva – mavazi)
iii)       Vipera na Tanzu vinaingiliana na kufanana
iv)       Muktadha, maudhui ya lugha maalum dhana hizi zinajitokeza kote.
UTOFAUTI
a)         Fasihi Simulizi ya kiafrika ni pana lakini Fasihi ya Kiswahili ni finyu kwani fasihi ya Kiswahili huchota vipengele fulani katika fasihi simulizi ya kiafrika.
b)         Fasihi Simulizi ya kiafrika ni kongwe
c)         Utamaduni wa Fasihi Simulizi ya kiafrika ni tofauti na ule wa kiafrika
TANZU ZA FASIHI SIMULIZI NA UAINISHAJI WAKE
            Tanzu ni matawi, Matawi ya fasihi simulizi ni mitindo yake.  Uainishaji wa Tanzu za Fasihi Simulizi si jambo rahisi.  Wataalamu wengi wamejaribu kuainisha lakini wamepambana na matatizo kadha wa kadha kwani:-
i)          Afrika ina utajiri mkubwa wa fasihi simlizi.
ii)        Tanzu hizi zinafanana .
iii)       Tanzu hizo zinaingiliana.
Wageni walipokuja kama vile Finegan (1970), Matteru (1977) Mlokozi (1966) Catheline Jovi & Kitula Kingei (2005) Wajula & C. Nungo (1993) Liongo (1992), Wajula R. & Kiman Njogu (2007) na wengine wamefanya jitihada za kuainisha Tanzu za Fasihi Simulizi.  Si rahisi kuainisha Tanzu kwani hakuna mipaka bayana kati ya utanzu mmoja na mwingine
Hadithi, methali, vitendawili na mafumbo vinaweza kuwekewa katika kundi moja.Wapo wataalamu walioainisha Tanzu za watoto na tanzu za watu wazima.  Mfano Methali ni tanzu za watu wazima.Pia ni upi utanzu bora kuliko mwingine, wapo wataalamu waliosema methali ni uti wago wa mazungumzo.           
VIGEZO VYA UAINISHAJI WA TANZU ZA FASIHI SIMULIZI
Wafulu R. & Kimani Njogu wanasema ili tuweze kuainisha tanzu za fasihi simulizi lazima tuwe na vigezo:
            Majina ya tanzu
            Miundo
            Mianzo na miisho
            Mitindo yake
Maudhui
            Kujipambanua kwake kitabaka
            Jinsi ikiwa tanzu zake name)
            Mahali na wakati
Wa husika
Materru (1983) ameainisha Tanzu za Fasihi Simulizi katika makundi 3:-
1.         Nathari           -           Masimulizi au mazungumzo ngano, visasili , misendu
2.         Ushairi           -                       Mashairi
                                                            Nyimbo
                                                            Tumbuizo
Utenzi
Maghani
Ishibu
3.         Semi               -                       Mafumbo
                                                            Misemo ya kilinge
Methali
Vitendawili                                      
KITULA KINGEI & CATHERINE KISOVI
Wametaja makundi 4 ya tanzu;
1.         Semi               -                       Misemo
                                                            Methali
Mafumbo
                                                            Vitanza ndimi
Majina
Utani
2.         Hadithi                      -           Ngano / Hekaya
                                                -           Visasili
Mighani
                                                            Visakale
3.         Maigizo                     -           Michezo ya kuigiza
Sarakasi
Majigambo
                                                            Ngomezi
                                                            Utani
Mawaidha
                                                            Mipasho / Michongoano
Ngonjera
Vichekesho
4.         Ushairi                                    Nyimbo kama Rege, Chakachu,
Nyimbo za harusi, Mbolezi, Wawe za kazi , Mkwaju ngoma, Nyimbo za unyago, Bembelezi
Jando
                                                            Ngonjela
                                                            Mashairi
Tenzi
                                                            Kirumbikizi
MLOKOZI M. M. (1996)
                            Ametumia vigezo
                  Umbile na Tabia ya Utanzu.
Muktadha wa uwasilishaji.  (wakati na mazingira).
                  Namna ya uwasilishaja wake kwa hadhira (mtindo)
Dhima ya fani ya utanzu huo.
Mlokozi ameainisha Tanzu Fasihi Simulizi katika makundi 6 ambayo:-
1.         Mazungumzo
2.         Masimulizi
3.         Maigizo
4.         Ushairi
5.         Semi
6.         Ngomezi

1.         MAZUNGUMZO
            Utanzu una vipera 4:
       Hotuba
Malumbano ya watani
      Mizaha.

Sala                 Dua
                        Maapizo
                        Tabano
2.         Masimulizi
Vipera vyake            Hadithi za kubuni               Vigano
                                                Istiara
Mbuzi
Michapo
                       
Salua                                      Visakale
                                                Mapisi
Tarihi
Dhajari
Kumbukumbu

Visasili                                   Visasili vya uzuri
                                                Visasili vya ibada  na sini
                                                Visasili vya miungu na mizimu
                       
3.         MAIGIZO                 -           ya watoto, misiba, sherehe, kidini

4.         USHAIRI SIMULIZI VIPERA                  
                  Nyimbo
-          Tumbuizo                       Bembea
Mbolezi 
Nyiso 
Janda

-          Tukuzo                            Kongozi
Nyimbo za dini
Nyimbo za Taifa 

-          Chapuzo kazi au kimai             Nyimbo kuthinga
Za watoto
Za vitu
-          Tenzi na Tendi
      Maghani
-          Ghani nafsi – kuikomba
-          Ghani Tumbuizi
-          Sifa                        Vivugo – Majigambo
Tondozi
-          Maghani simulizi                       Rara
Tendi
5.         SEMI
v  Methali
v  Vitendawili
v  Mafumbo                         Chemsha bongo
Fumbo jina
v  Simo / Misimo
v  Kauli Taulia

6.         NGOMEZI
            MAZUNGUMZO
Ni mazungumzo yenye sanaa ndani yake yaliyosheheni mbinu za kifani (fani na Maudhuni)            Mfano :           Tamathali za Semi kama vile Sitiari, Jashibia.
MBAZI
Ni hadithi fupi zenye lengo la kuonya.
SALUA
Ni hadithe zinazosimulia matukio ya kihistoria / zamani
VISAKALE
Visa vya kimapokeo vya mashujaa
MAPISI
Ni historia ya matukio ya kweli
TARIHI
Ni maelezo au jedwali la matukio muhimu na tarehe zake
VISASILI-Hadithi za kale zinazo zungumzia, asili ya kitu au imani ya mtu.
                        Mfano:Asili ya binadamu
MAIGIZO     -Kulielezea matukio ya dunia kwa namna ya dunia kwa namna ya
kucheza / utani
            USHAIRI       -           Ni utungo wa kinathumu unaozingatia urari wa vina na mizani
            MBOLEZI     -           Nyimbo za kuliwaza katika msiba
NYISO            -           Nyimbo za jando na unyago
WAWE           -           Nyimbo za kazi
KONGOZI    -           Nyimbo za kuaga mwaka mara nyingi zinaendana / kuambatanana
Matambiko
            CHAPUZO    -           Nyimbo za kazi
            KIMAI           -           Nyimbo za wavuvi
            TENZI            -           Ni  utungo unaozungumzia tukio fulani
            TENDI            -           Utungo unaozungumzia tukio la kiuhujaa
            SIFO               -           Ni nyimbo za kusifu
            TONDOZI     -           Tungo za kusifu watu wanyama n.k.
            RARA                        -           Ni maghani ya kusimulia au tukio fulani la kihistoria na huenda
sambamba na ala za muziki.
            FUMBO -JINA  -Ni mafumbo ya nayotaja majina. Mfano:  Mwamvua alizaliwa
kipindi cha mvua nyingi
            LAKABU       -           Kupewa jina kulingana na tabia.  Mfano:  Mwalimu Nyerere - Baba
wa Taifa.
            KAULI TAULIA       -Ni kauli zenye mfuatano wa sauti
            NGOMEZI    -           Ni tango za ngoma au zinazoambatana na ngoma
 >>>>>>INAENDELEA >>>>>>>>>>>>>>
Powered by Blogger.