FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI NA KIAFRIKA


MODULE 2:
            ISTORIA YA FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI
(a)         Historia ya ushairi mulizi
(b)         Historia ya masimulizi
(c)          Historia ya Thieta.
HISTORIA YA MASIMULIZI
Ili kupata historia ya msimulizi hatuna budi  kuwaangalia wataalamu mbalimbali.  Tafiti zilifanywa Afrika kama ya 19 na 20 kuhusu maisha ya muafrika,  Na wanazuoni hao walikuja na mitazamo yao
Wazungu / Wageni pia walifanya utafiti kuhusu utamaduni wa mwafrika.
1.            NADHARIA YA UBADILIKAJI TARATIBU. (EVOLUTIONS) Hawa wanafanya tafiti mbalimbali Ulaya na Afrika.  Nadharia hii iliasisiwa na Charles Darwin (Mwingereza) hivyo wataalamu wengine wanatumia mtazamo huo kuasisi Fasihi Simulizi.
Lengo la Darwin ni kuchunguza viumbe hai.
Darwin  aliona kuwa kama kuna viumbe hai ambao wanasifa zinazo fanana basi viumbe hai hao wanatoka katika asili moja ila wamepitia mabadiliko hadi kufikia hali yao ya sasa.
            Mtazamo kama huo wa mabadiliko ya viumbe pia ulitumiwa na wataalamu wa
masuala ya kiutamaduni
                        -           Pia metumika katika mamla ya kifasini kwa kuchanganya Chimbuko la
fasihi simulizi ya afrika kwa kulinganisha na Wataalamu:  Edward Burnet Toylor, James George Frazer ni wafuasi wa mkabala wa mabadiliko ya viumbe hai katika kuchunguza fasihi simulizi.
                        -           Wanaangalia binadamu na mazingira yake
                        -           Wanaona kuna kanuni Fulani muhim zinazochangia maanzi ya binadamu.
Ili kuelelwa utamaduni wa kijadi na jamii yeyote ile lazima uilinganishe na jamii nyingine.
                        -           Walichunguza mila na desturi za jamii kwa kina kama vile mivigha, uchawi.
                        -           Walichunguza katika jamii zao za Ulaya baadaye wakaja Afrika.
-           Watu wengi walishiriki katika kutafiti fasihi simulizi katika nchi mbali mbali Mfano S. A                 Heri Junob alifany utafiti huko
John Roscoe alifanya utafiti katika jamii ya Baganda  Robert Battray alifanya katika
jamii ya Akan huko Ghana.
-           Walichunguza hadithi, nyimbo, Methali na vipera vingine.
-           Katika uchunguzi wao “Finegan” na “Okpewho” wanasema “Wametafiti Ulaya na Afrika”, kuna ukoo au jamii moja ambayo imezagaa ulimwenguni kote hivyo kama tuachungua jamii mbili katika kipindi kila kitu cha ukuaji wa utamaduni matokeo yake ni kuwa mila na desturi zao zituonyesha kufanana.
Heri chatelaine alifany uchunguzi kuhusiana na hadith huko Angola na anasema Kimsingi watu wa Afrika ni kama watu wengine ulimwenguni na hadith au agano za kiafrika ni tawi toka katika mti mmoja wa kiulimwengu.
-           Kazi yeyote ya kifasihi simulizi ya kiafrika ni masalia au mabaki ya fasihi iliyotanguli (Ulaya)
            NADHARIA YA MSAMBAO (DIFFUSSION)
Pia ni wageni toka Uswisi, Marekani n.k. pia walitafiti masimulizi hata hadithi, waliangalia maisha ya hadithi Fulani maalumu.
   Mtaalam Stith Thampson aliangalia jinsi hadith zinavyo fanana kiproti kai ya hadith za Kiafrika na India, Ulaya Arabuni na sehemu nyingine ambazo watumia toka Afrika walipitia.
-           Wanachunguza asili ya hadithi zinazopatikana Afrika kihistoria na kijiografia.
-           Wanachunguza athari kutoka nje
-           Wanahitimisha kama hadithi mbili kutoka jamii mbili zikionyesha sifa zinazo
fanana ni kwasababu kuna kipindi Fulani huko nyuma jamii hizi mbili ziliingiliana.
            Mwingiliano huo unasababisha jamii  moja kukopa vipengele vya utamaduni vya
mwingine.
            Wanazuoni wa Ulaya wanatafuta njia ya vipengele mbali mbali vya utamaduni
vinavyo fanana
Wanasema asili yake ni India Ulaya ndo unaenea kwingine duniani.
            Wataalam: Jacob  Grimm na Wilheton Grimm (wajerumani) walikusanya kazi
nyingi kutoka India na Ujerumani na wakaja na kitabu “House hold tolies” 20.  Walisema “kama kuna ufanano wowote kati ya hadithi zinazosimuliwa Afrika na Ulaya hizo za Afrika ni chpukizi ya hadith Mama ambao ni utamaduni wa India Ulaya”.
“Kwa kawaida utamaduni huenea toka kwa watu wengi nguvu (superior) kwenda watu wa chini na si vinginevyo” Thompsona”The Anasema “ kama kuna ufanano kati ya hadithi za ulaya na Afrika ni kutokana kwamba wa Ulaya walizileta Afrika kipindi cha biashara ya watumwa”
            (3)        KIAFRIKA/ UTAIFU
                        Katika mkabala wa kiafrika kimsingi, wanapinga mawazo yaliyotolewa na wageni
hawa.
Finegan:“Wanaubadilikaji na wanamoambao walishindwa kuona kuwa hadith za kiafrika zimetoka na miktadha yao ya kijamii na wala sio masalio hivyo anaona kuwa mtazamo huu si sahihi kabisa.
Hivyo mkabala huu wa   kiafrika unachochewa na mawazo finyu ya kimagharibi.
Hivyo mawazo ya waafrika yapo pia kwa waafrika wengi na wanasema wanazuoni wengi, hawakuelewa vizuri fasihi yetu.  Alexis Kayame (Ruanda) Alifanya utafiti katika ushairi simulizi wa Rwanda.
Kwabena Nkryis      -           Alitafiti Fasihi Simulizi na muziki huko Ghana.
Adebayo Babalola   -           (Nigeria)
Amadu ba                 -           Mali
T. Y. Sengo                -           Tanzania
M. M. Mulokozi       -           Tanzania
P. Mramu                  -           Tanzania
Mfano:            Sengo (1985) anaelezea asili na chanzo cha ngano, alichunguza jamii ya Wazanzibar
-           Anasema “Ipo pale tangu jamii ilipokuwepo pale”
Binadamu alitung ngano ili imfae katika maisha yake ya kiuchumi, kijamii na kisuikolojia.
-           Mazingira yanayomzunguka binadamu ndiyo yanayojua chanzo cha ngano (fasihi simulizi)
Mfano:            Ngure (2003) “Utanzu wa mwanzo kabisa wa fasihi simulizingano au hadithi”.
Anasema”Ngano hizi zilitokana na Uwoga na haja ya mtu kuanza kuijiuliza maswali kuhusu vyanzo vya asili ya dunia, binadam kifo n.k.
            HISTORIA YA USHAIRI SIMULIZI
Mulokozi (1996) anasema “Ushairi simulizi ni utungo wa kinadhumu unaofuata kanuni fulani za urari wa sauti, mapigo ya lugha na mpangilio wa vipashio vya lugha.Chanzo cha fasihi hakiwezi kutenganishwa na utamaduni fulani, maisha na lugha yao. Hivyo asili ya ushairi wowote ni nyimbo.  Asili ya ushairi wa Kiswahili / kiafrika ni nyimbo za wantu pamoja na utamaduni wao.Ushairi ulianza pale binadamu alipogundua lugha baada ya kuacha hatua ya uhaywani na kuwa razini, ubunifu wa lugha ulirahisisha mawasiliano.
Pamoja na kugundua zana mbalimbali za uzalishaji pia alitumia sanaa ili kurahisisha kazi hizo.  Ushairi unaojitokeza katika nyimba ulitumika kama chombo cha kuzalisha mali.  Nyimbo zilimsaidia kuchapuza azi kwani zilimpa nguvu na kumsahaulisha ugumu wa kazi.  Wimbo wa kazi uliimbwa kwa kufuata mapigo ya zana za kazi.
Kwasababu kazi zilifanywa kwa umoja (upamoja), kulikuwa na  kiongozi aliyeimba wimbo na wngine waliitikia kwa kufuata milio maalumu ya zana za kazi.  Kazi izo ni kama kilimo, uvuvi, uwindaji n.k.
Ushairi pia ulianza kutumika katika matambiko ambayo ni ibada za kijadi.  Matambiko huwa na sala /maombi maaalumu kwa mizimu au miungu.  Matambiko haya yalifanywa kwa matukio maalumu na vipindi maalumu.
Mfano:Kumaliza na kuanza mwaka, kuomba mvua n.k.
Wimbo ni kazi ya sanaa hivyo lazima uwe na ubunifu wa vinana mizani pamoja na maudhuni maalum.  Kiongozi wa nyimba anaitwa manju / malenga ambay huwa ni fundi stadi wa kuimba.  LAKINI Si kila wakati wote kulikuwa na vina vya mwanzo, kati na mwisho bali vina vya upande mmoja au mbili vilijitokeza.
Pia nyimbo zilizingatia idadi ya mistari katika wimbo husika.  Na mizani ilizingatiwa.  Dhima za nyimbo hizo ziliimbwa kwa lengo lakutmbiza ambako kuliambatana na kuchapuza kazi.
USAHIRI SIMULIZI ULIANZA LINI?
Si rahisi kueleza kuw aushairi ulianza lini kwani utanzu huu una historia ndefu na ni mkongwe ukilinganisha na tanzu zingine.
Wengine wanasema utanzu huu ulianza kabla ya kama ya 10 kutokana na tungo simulizi za kibantu hususani nyimbo na ngoma.
Aman Abeid (    ) katika kitabu kilichoandikwa na Mathias Mnyampala (1965) “Waadhi wa Ushairi” anasema kabla ya watu hawajajua kuandika, mashairi yalitungwa na kuimbwa katika jando, unyago, ngoma, harusi n.k. kwani mashairi si kitu kingine ni nyimbo.  Waliokuwa wanaimba na kutunga nyimbo waliitwa Manju au Malenga.
Mabadiliko yalianza kujitokeza taratibu hususani walipokuja waarabu waliofundisha kusoma na kuandika.  Ndipo ushairi ukanza kufungamana na maisha ya binadamu kuanzia kuzaliwa mpaka kufa.
Hivyo maudhui yalianza kumhusu binasamu na mazingira yake.
Ngure Alex (2003) anathibitisha kuwa asili ya ushairi ni nyimbo ambazo zilianza kuimbwa bila kufuata utaratibu maalumu.  Ushairi huo haukuandikwa kwasababu watu hawakujua kusoma na kuandika bali zilifungwa hovy hovyo bali zilifuata tukio husika.
Wamitila (2004) Ushairi ulitokana na nyimbo.  Ushairi una vipera vingi
(a)               Nyimbo
Nyimbo za mapenzi
Nyimbo za jadia
Nyimbo za Harusi
Nyiso
Mbolezi
(b)               Maghani
Vighani vya watoto
Ghani simulizi (Tendi & raru).
(c)                Sifo
Majigambo
Bembezi
Tondozi
(d)              Ngonjera
Ushairi wa Malumbano
Ushairi wa Masemezano
(e)               Shairi
Mashairi ya aina mbalimbali
Katika ushairi kuna tendi ambapo Finnegan (1970, 2012) anasema ushairi katika bara la Afrika hususani tendi hazikuwepo.  Yeye anatoa sifa za jumla za tendi nazo ni:
a)            Utungo wa kishairi / nudhumu
b)           Lazima uwe mrefu
c)            Upatanifu ie visa vinavyoungana kimantiki
d)           Uwe na maudhui
e)            Husimulia maisha na tendo la kishujaa kuanzia kuzaliwa kwake mpaka kufa
kwake.
            Watafiti waliofuata baadaye wakaona kuwa sifa hizo hazitoshelezi na wakaongeza
a)            Masimulizi
b)           Masimulizi yatolewe kishairi
c)            Tendi hufungamana na tukio la kihistoria u kijamii
d)           Zielezee ushujaa
e)            Tendi huimbwa / hughanwa
f)             Tendi hufungwa pao kwa papo
g)           Tendi huzingatia muktadha wa tukio
HISTORIA YA THIETA NA DRAMA
Wamitila (2008) anasema thieta hitwa “Sanaa za maonyesho”
Penina Muhando anasema “Sanaa za maonyesho ni Sanaa ambazo huwasilishwa ana kwa ana, wao kwa hadhira, hutimia usanii kiutendaji.  Anaona kuna aina kuu mbili za sanaa za maonyesho ambazo ni:-
a)            Sanaa za Maonesho za jadi
b)           Sanaa za Maonyesho za Mamboleo.

SANAA ZA MAONYESHO ZA JADI
Ni zile ambazo zimechipuka katika jamii ya Tanzania kama vile Mivigu, Majigambo, ngoma.  Mivigha-Jando, Unyago, Matambiko
Utambaji hadithi n.k  Sanaa hizi zinasaidia sana jamii kuwasiliana na miungu, mizimu, mapepo n.k. kwa lengo la kuwaeleza matatizo yanayowakabili jamii kama vile Ukame, njaa, uzazi magonjwa n.k.
Pia huwa na mafunzo ndani yake na heleza historia ya jamii.
-           Kueleza tabia / tajiliba za jamii husika.  Sanaa hizi zilianza kabla ya ujio wa
wakoloni.
Sanaa hizi huambatana na :-  Vitendo kisanaa
a)            Muziki
b)           Kucheza ngoma
c)            Kutongoa mashairi
d)           Matendo ya mwili
e)            Matumizi ya lugha
Sanaa za Maonyesho (wamagharibi) huwa na mambo yafuatayo:
(a)         Lazima uwe ni mchezo
(b)         Uwanja wa kiutendaji
(c)          Mtendaji
(d)        Watazamaji
Sanaa za maonyesho za jadi zilifungamana na utamaduni wa jamii na ulizingatia:-
(a)         Dhana inayotendeka
(b)         Wambaji / Hadhira
(c)          Uwanja wa kutendea
(d)        Watazamaji
SANAA ZA MAONYESHO ZA KIMAMBOLEO
Hizi zimetokana na ujio wa wageni hususani tamthilya katika Tanzania tamthilia zililetwa na Waingereza kwa lengo la:-
(a)         Kujifurahisha
(b)         Kujikumbusha maisha ya huko kwao
Drama inauhusiano wa karibu kabisa na tamthiliya.  Tamthiliya za mwanzo ziliiga tamthiliya za Shakespeare na zilitafsiriwa kutoka kazi za Shakespare ili kufifisha utamaduni wa mwafrika.  Tamthiliya hizi zilisambazwa kwa kutumia
(a)         Elimu
(b)         Dini ya Kikristo
Dhima zake:
(a)         Kuchekesha
(b)         Kufundisha kuwatii wakolono
(c)          Kuwapumbaza wafrika wasifikirie juu ya kupambana na ukoloni.
Baaada ya Ukoloni sanaa hizi zilibadilika kwani zilianza kusisitiza siasa ya ujamaa na kujitemea ustawi wa maisha ya mtanzania.  Mnamo 1970 zilisisitiza ujamaa, usawa kwa binadamuk kulinda uhuru, haki za wanawake na watoto n.k.
Drama ni maigizo yenye mambo ya fuatayo:
(a)         Mpangilio
(b)         Wahusika
(c)          Utendaji
Sifa za drama ni uigaji wa uhalisia yaani kuiga jambo halisi ambalo liko katika maisha yetu ya kila siku.
Wamitila (2004) anasema kuna aina nyingi za maigizo
(a)         Mivigha
(b)         Ngomezi
(c)          Utumbi
(d)        Michezo ya jukwani
(e)         Ngonjera
(f)           Utani
(g)         Majigambo
(h)         Vichekesho
(i)           Mazungumzo
Mulokozi (1996) anasema maigizo yanatumia watendaji ambao juiga tabia na matendo ya watu au viumbe wengine kwa lengo la kubanidisha au kutoa ujumbe Fulani.
Aina za Maigizo:-
(a)         Maigizo ya watoto
(b)         Maigizo ya msibani
(c)          Maigizo ya Sherehe
(d)        Maigizo ya Kidini
Vipera vya Thieta ni pamoja na Mirvigha, Dansi, Sarakasi, Masimulizi ya kidrama, Ngoma, Majigambo, Sherehe za jando na Uyago, Matambiko, Ngomezi Utambaji wa Hadithi n.k.
Thieta ya jadi ilifungamana na kazi za maisha ya kila siku ya jamii husika, ilijikita katika mila na desturi au utamaduni wa jamii hizo, zilikuwa na lengo maalumu la kijamii na kiutamaduni ili kurithisha amani kwa vizazi vya jamii hizo.  Pia zilikuwa kwa ajili ya mawasililano kama vile Ngomezi, Matambiko ni kuwasiliana na miungu ili kutatua matatizo mbalimbali katika jamii.  Wageni walileta vichekesho na Drama ambayo kwa wao thieta au sanaa za maonyesho zilikuwa na mamba 4 :-
Jukwaa
Mchezaji
Watazamaji
Thieta ya jadi ilihitaji
Dhana inayotendeka / kipera husika
Mtendaji
Jukwaa
Watazamaji
Sehemu za kutendea zilkuwa tofauti kulingana na kipera husika.
BUBWI (MIME)
Nikipera kilichoanzia ulaya (Wagiriki na Warumi)
Ni aina ya utendaji wa kisanaa ambapo hadithe husimuliwa kwa kutumia matendo ya mwili,  Ishara za uso na matendo.
Kwa kutumia vitendo unaweza kuwasilisha hadithi ikieleweka vizuri.  Inahitaji ujuzi wa viungo vya mwili na kujua utamaduni wa jamii husika.  Kipera hiki ni maarufu ulimlwenguni pamoja na Afrika.
NGOMA:
Ni chombo cha kimuziki, ni Uchezaji ni sherehe katika kufanikisha vipera mbali  m bali.  Ni kifaa cha kimuziki katika jamii za kiafrika.

Ngongi hutumia ngoma inayoongea katika jamii za jadi huwezi kuzungumza Thieta bila kutaja ngoma katika Fasihi Simulizi na utamaduni ni lazima uitaje ngoma katika kutoa taarifa n.k.
Baadhi ya misiba pia kutumia ngoma katika tawala za kijadi ngoma huweza kutumika:-
                        Kumsalimu Chifu
                        Kumsifu Mfalme
                        Kutoa taarifa
Ngoma huambatana na Nyimbo hivyo Nyimbo ni kipera muhimu cha Thieta
-           Hutumika katika utendaji wa vipera mbalimbali kama vile Matambiko huambatana na nyimbo
Nyimbo ikiambatana na ngoma huonesha hali ya jamii kama furaha, huzuni
MALEBA
Ni muhimu katika utendaji ingawa si kila kipera huhitaji mavazi maalum.  Baadhi ya
vipera Majigambo, Ngoma, Jando na Unyago huhitaji mhusika avae Maleba maalum.
-           Maleba hutegemea ubunifu wafanani.  Mfano:  Nyimbo za uganga, hivyo Maleba huweza kuambatana na zana mbalimbali katika utendaji kama vile kibuyu.  Maleba hayavaliwi kwa kuvutia tu hadhira bali huwa na dhima mbalimbali
                        Husaidia kufikisha ujumbe mbalimbali
                        Husaidia kuvuta hisia miongoni mwa hadhira.
                        Husaidia kutofautisha kipera kimoja na kingine.
>>>>>>>>>>>INAENDELEA>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>


Powered by Blogger.