FASIHI SIMULIZI YA KISWAHILI NA KIAFRIKA


KILONGO MASIMULIZI / MATINI SIMULIZI
Inaweza kuwa ya kipera chochote, tunaangalia Matumizi ya lugha katika muktadha fulani
wa kijamii yaani Lugha inayotumika kuelezea Miktaha mbalimbali.  Pia katika kilongo
tunaangalia vitu vinavyoonekana / vionwa au vinanvyotokaa / vionwa au vinavyotokaa
katika kipera kila Mfano:  Maleba yanawasilisha kitu gani, Lugha, Matendo, Ishara
mbalikbali katika utendaji wa Fasihi Simulizi zana mbalimbali ambazo huwa tunaziona. 
Ili kuelewa kilonzo simulizi ni lazima uelewe utamaduni wa jamii husika .
SIFA /JIRABAINIFU NDUNI ZA KIFANI ZA FASIHI SIMULIZI YA
KISWAHILI NA KIAFRIKA
Fani ni mbinu na mtindo wa namna ya kuwasilisha mandhui ya kazi ya fasihi
Fani ni ufundi unaotumiwa na msanii kuwasilisha kazi yake, inajumuisha Mandhari,
Lugha, Mtindo,
                        Kimundo, Mtindo, Lugha, Utendaji
MUUNDO
Ni kipengele cha fani, Miundo ya vipera vya Fasihi Simulizi ipo mingi kulingana na muundo wa kipera husika.
Muundo katika Fasihi Simulizi ni mpango na mtiririko wa kazi ya Fasihi Simulizi kwa upande wa visa na Matukio.  Tunaangali namna mtunzi anavyounganisha wazo moja na lingine, Motari mmoja na mwingine yaani jinsi kazi ilivyofunywa kazi nyingi za Fasihi Simulizi muundo wake huwa hauwi mrefu sana bali huwa mfupi, ingawa hutegemewa fanani anaye simulia.
VIPERA MBALIMBALI NA JINSI M IUNDO YAKE INAVYOJITOKEZA
Semi
i)          Methali
Umbo lake muundo wake ni wa pande mbili ambao hunyesha hali tendo Masharti na upande wa pili huonyesha matokeo
Mfano:            Mfifha uchi hazai
Methali nyingi huwa namuundo wa kishairi, yaani Mapigo ya kimuziki, urari wa kimizani, mpangilio fukani wa vina.
Mfano:Haba na haba hujaza kibaba
ii)        Vitendawili
Huwezi kuwa katika sentensi neno moja au miundo ya kishairi.  Vitendawili huwa na miundo ya kiformula huwezi kubadilika na mamii husika.
Mfano:Kitendawili !!!   Tegaa  !!!  kupata jibu na kama jibu si sahihi unaomba upewe zawadi fulani, kama mji katika jamii nyingine huweza kupewa mume au  mke na baada ya mtegaji kuridhika anatoa jibu.
            iii)       Hadithi / Ngano
Ni masimulizi ambayo si ya kishairi, hadhithi nyingi hutumia muundo, rahisi /sahihi au wa moja kwa moja, utakuwa na Mwisho – kati – Mwisho hivi vyote vinakuwa nas formula maalumu.  Muundo sahihi husaidia sana hadhiru kufuatilia hadithi husika.  Muundo husaidia fanani kuzingatia kusikia kwa usikivu, muundo huwa moja kwa moja haya hayakatazi kuchomeka vipera vingene ndani yake kama nyimbo, Methali.
            Safari
            Hadithi nyingi zinahusu safari
            Pia kuna muundo wa ndani ambao husaidia kuibua maudhiri mbalimbali
Mfano:Falsafa Mila na desturi
Ushairi
i)          Shairi
Vipengele vya kimuundo ni vipande (Shairi la kimapokeo), Misharoro (la kisasa) Beti, Mizani, Vina, lakini hutegemea shairi linalozungumziwa.
King’ei & Amata (2001 : 02)  Taaluma ya Ushairi
“Muundo ni Luray a nje nay a ndani ya dhairi”.  Ni Luray a utungo kama unavyosikika au onekana kutokana na midundo au mapigo yake.  Katika shairi Luray a nje ya shairi inajidhirisha katika umbo lake, je linatumia kanuni za kiamdhi au la na muundo wa ndani unaangalia, Lugha, Falsafa, funzo Maudhui.  Hivyo basi muundo ni jumla ya fani na maudhui.
            ii)        Majigambo
            Huweza kutumia formula Fulani ya kufungulia jigambo hilo,
Mfano: huanza kwa kujitambulisha, kisha huanza kutama na hitimisho ni
kumshukuru Mfalme n.k.  hivyo yanamtiririko Fulani / maalum.
            SIFA ZA KIMTINDO KATIKA FASIHI SIMULIZI
Ni jinsi zinavyojitokeza katika utunzi au utendaji wakeDhana ya mtindo ni pana maana ya Mtindo;
Senkoro (2001 : 24)  Ni upangaji wa fani na maudhui katika kazi ya fashihi ambayo hudokeza nafsi na hat upekee wa mtungaji wa kazi hiyo.
Mulokozi (1996 : 101) Mtindo hujidhihirisha katika vipengele mbali
-           Matumizi ya lugha
-           Utenzi wa maneno
-           Mpangilio wa maneno
-           Wizani (urari wa mapigo ya sauti)
-           Mpangilio wa sauti za lugha ili kuleta athari Fulani.
Mtindo ni upekee wa mtunzi haufundishiki kwa kutegemea uwezo mazoea ufundi, hisia na unafsi wa mtunzi.
watoto, wazee. 
Tamathali mbalimbali za Semi:
Kila fanani ana upekee wake katika kutunga kazi, kipera kimoja kinaweza kuchomoza zaidi kuliko kingine.
-           Mtindo wa kimajibizano
-           Kimolojia
-           Mtindo wa kimasimulizi
Mfano:            Methali                      Lugha             -           Matumizi makubwa ya Takiriri,
Picha, Ishara, Tanakali Sauti.
            VIPENGELE VYA LUGHA
a)            Ishara
Ni wazo, tendo, au dharia, kitu kimoja kinachowakilisha dhana au tendo au kitu kingine kuwa ishara za lugha kama vitendo, lugha, mawazo, Mavazi.  Ishara inaweza kuwa kitu h alisi, kikarejelea kitu ambacho ni cha kidhahama.  Matumizi ya Ishara hutegemea ufundi wa fanani.  Ishara hutumika katika vipera mbali mbali kuna ishara za kiutamaduni Fulani na ishara za kiulimwengu.  Ili kuelewa utendaji lazima ujue mbinu  za kisanaa kama hadhira na kama fanani.
-   Matumizi ya Ishara utendaji Fasihi Simulizi hutegemea maarifa na utamaduni wa jamii hiyo.  Ishara ni mbinu ya kuumba picha ya jambo katika mawazo ya msikilizaji, msomaji kwa kutumia lugha.
            Kuna Taswira mbalimbali
                                    Za kuonekana
                                    Za mawazo
                                    Za hisi
            TASWIRA
Ni neno au maelezo ambayo hutumika ili kuunda / kuchora picha ya kitu Fulani hali dhana au wazo Fulani akilini mwa msikilizaji au msomaji.
            Katika akili unaweza kuona, kuonja kuchukia, kudharau n.k. na husaidia kushirikisha
ubongo kufanya kazi.
-           Husaidia picha kupanda akilini.  Mbinu hizi hutuika katika vipera mbalimbali.
TAARUKI
Ni mbinu inayotumiwa sana
-           Ni tamathali ambayo inamsimamisha hadhira, haimfikishi kule mwisho haraka;
kutokana na shauku ya kutaka kujua mambo yaliyo au yatakayojiri.
-           Ni tamathali ambayo inaonesha kutoonyesha kitu kwa muda fulani au hadi
mwisho. Hutumika katika kazi za fasihi.  Mfano:          -           Ngano
            TAKRIRI
Ni kujjirudia, kujirudia kunaweza kuwa kiirabu, konsonanti, neno kipandi cha mstari katika shairi, mstari mzima, vina, wazo muundo.
Mfano:            Hadith hadith
                        Husaidia kuweka kumbukumbu
                        Husaidia kuleta usikivu kwa hadhira
TABAINI
Ni tamathali ambayo huundwa na maneo au mawazo yanayokingana ili kuleta msisitio wa wazo hilo
Mfano: Asiyejua maana haambiwi maana.  Chuku, Tashibira, Sitiari, Tashihisi, Usambamba, Tanakali Sauti
USAMBAMBA
Ni kauli ambazo zinafanana kimuundo au kimaana na huwekwa pamoja.  Miongoni mwa mifanano hiyo.  Pia mbinu nyingine ni kama wahusika halisi na wasio halisi.  Maudhari inaweza kuwa halisi au ya kufikirika.
MOTIFU
Ni kujirudia kwa dhana fulani au kitu fulani.
Mfano:            Motifu ya Safari        -           Hadithi nyingi zina safari
Motifu ya Namba
Katika hadithi namba Fulani inaweza kujirudia mara kadhaa.
USHAIRI
Lugha ni nyenzo muhimu katika uwasilishaji wa fasihi simulizi. 
Ushairi una uhuru wa kutumia maneno yake na mipangilio tofauti tofauti ya sentensi.
-  Pia katika ushairi kuna matumizi makubwa ya Ishara, mafumbo ya taswira.
Katika ushairi lugha ya kishairi ina m iundo ya sentensi na mpangilio wa maneno ambayo ni adimu kupatikana katika tanzu ngingine za kifasihi hutumia lugha ya  mkato ili kuleta radha.Lugha ya kistari ina utaraibu Fulani jaalumu na inaleta radhu Fulani ambayo inaweza ikahuzunisha au kukuamsha.
Lugha ya kishairi huwa ni ya mkato hfupishwa ili kupata mlingano wa silabi.  Mshairi anaaweza kubadili maneno kama anaweza kubadili maneno kama anvyotaka ili kupata vina, mizani n.k.
BAADHI YA MBINU ZINATOA UHURU WA KUCHEZA NA MANENO
a)         Hujitokeza kwa njia ya kubadili mpangilio wa maneno
            Mfano:            Mtoto mzuri              -           Mzuri mtoto 
b)           Kwa kutumia  Inkthari                    -           kufupisha maneno
Mfano:            -           Wataka nini                           Wataka ni?
c)            Mzada
Ni kurefusha neno ili kupata mizani inayohitajika bila kupotosha maana iliyokusudiwa.
Mfano:            Lemba                        Lembesha
                        Tanza                         Tanzia
d)           Tabiri
Ni kubadili mpangilio wa herufi au vitambwa katika neno ili kupata vina unavyo vitaka
Mfano:            Dunia                         niachu
                        Tabidhi                      Tabidha
            SEMIOTIKI YA UTENDAJI KATIKA FASIHI SIMULIZI
            Semiotiki
Ni taaluma ya mipangilio ya ishara inayomwezesha binadamu kuona vitu au hali  kama ishara zenye maana. (Wafula na Njogu 2007 : 103)
Wamitilal (2003 : 90 – 91)  Semiotiki ni aina ya nadharia ya kimuundo inayojishughulisha na ishara na maana za ishara hizo katika kazi za fasihi.
Semiotiki ni namna hadhira inayo fasili ishara mbalimbali kazi ya fasihi inayotendwa.  Ishara hizo huweza kuwa katika neno, vitendo, shamfas, sauti n.k.  Katika utendaji kitu chochote kitakuwa na  maana kama utakifasili.
Mfano:            Maleba ya mhusika yanaashiria nini n.k.
Katika Ishara / Semiotiki kuna usimbaji yaani kuelewa  mitindo mbalimbali katika matini.
Katika Semiotiki kuna Misimbo au kaida muhimu katika kufasili kazi ya fasihi.  Kuna aina 5 za Misimbo:
1.            Msimbo wa Matukio
Katika kazi ya fasihi matukio mbalimbali yanasaidia kuielewa kazi ya fasihi hiyo.
2.            Msimbo wa Kihemenitiki
Husaidia kupata maana ya neno au maneno kama yanavyotumika katika kazi hiyo.
3.            Msimbo wa Kiseme
Huhusisha kuelezea elementi nasibishi za Kisemantiki.  Unasaidia kuwaelewa wahusika wa kazi ya fasihi kwa kupitia sifa ambayo wahusika wanapewa.
4.            Msimbo wa Kiishara
Unahusisha jinsi ambavyo wasomaji wanavyosumbua maana za kiishara za kazi za fasihi
5.            Msimbo wa Kiutamaduni
Hujengwa na viashiria mbalimbali vya kiutamaduni ili kuweza kujua maana ya viashiria hivyo
>>>>>>>INAENDELEA>>>>>>>>>>>>>>>>
Powered by Blogger.