MAENDELEO YA KISWAHILI

MAENDELEO YA KISWAHILI
Ushahidi wa Kimsamiati na Kimuundo unaothibitisha Ubantu wa Kiswahili
Onesha ushahidi wa kimsamiati na kimuundo unaothibitisha ubantu wa Kiswahili
Neno asili ni jinsi kitu au jambo lilivyotokea au lilivyoanza. Kutokana na fasili hii tunaona kwamba jambo au kitu kinaweza kutokea kibahati kama ilivyo katika lugha au linaweza kuanzishwa.
Hivyo basi asili ya lugha ya Kiswahili bado ni mjadala mrefu ambapo wataalamu mbalimbali wanahitilafiana juu ya asili au chimbuko la lugha ya kiswahili. Wapo wanaokinasibisha kiswahili na kiarabu kwa kutumia kigezo cha msamiati na dini ya kiislamu. Wengine wanashikilia msimamo kuwa kiswahili ni kibantu kwa kutumia hoja za kiisimu na kihistoria. Wapo wanaokinasibisha kiswahili na uchotara baadhi yao wanaoshikilia msimamo huu ni Freeman Grenville na Homo Sasson
Kuna nadharia mbalimbali zinazojaribu kuelezea asili ya Kiswahili, miongoni mwa hizo ni pamoja na hizi zifuatazo:
Kiswahili ni Kiarabu
Hapa Kiswahili kimefasiliwa kuwa asili yake ni kiarabu, wanaoshikilia mtazamo huu wanahoji kwamba katika lugha ya Kiswahili kuna maneno mengi ya Kiarabu. Pia wanaeleza kuwa asili ya Kiswahili ni pwani na kwa kuwa wenyeji wa pwani ni Waislamu na kwa kuwa uislamu uliletwa na Waarabu basi hii lugha ya pwani nayo itakuwa imeletwa na Waarabu. Vigezo hivyo vyote vina udhaifu mkubwa kwa sababu havikukitwa katika misingi ya kitaalamu ya uainishaji lugha.
Kiswahili ni lugha Chotara
Mtazamo huu umezua ubishi mkubwa kwani hata baadhi ya wazawa wamejinasibisha na uarabu na ushirazi. Wanaofasili Kiswahili kama lugha chotara wanadai kuwa Kiswahili kimetokana na mchanganyiko wa lugha ya Kiarabu na lugha za Kibantu. Hivyo Waswahili ni watu waliotokana na wanaume wa Kiarabu na wanawake wa Kibantu.
Kiswahili ni lugha ya Vizalia
Waumini wa mtazamo huu wanadai kuwa Kiswahili kilianza kama pijini ya Kiarabu na baadae kukomaa na kuwa kreoli. Pijini ni lugha ambayo imetokana na mchanganyiko wa lugha mbili tofauti yaani Kiarabu na lugha za Kibantu. Na kreoli ni lugha inayozungumzwa na watoto waliozaliwa na baba Mwarabu na mama Mbantu.
Kiswahili ni Kikongo
Nadharia hii inafafanua kuwa lugha ya Kiswahili ilianzia huko Kongo na kusambaa katika pwani ya Afika Mashariki. Wabatu walipofika Afrika Mashariki waliingia kwa makundi na katika nyakati mbalibali. Makundi hayo yalianza kujigawa na kutawanyika, matokeo ya kugawanyika huko ni kutokea kwa makundi mbalimbali ya wabantu. Inasadikika kuwa baadhi ya Wabantu walifanya maskani yao ya kudumu katika mabonde ya kaskazini mwa mto tana. Kikundi hiki cha wabantu ndicho inasadikiwa kuwa chimbuko la Kiswahili
Kiswahili ni Kibantu
Mtazamo huu ni ule unaoamini kuwa Kiswahili ni lugha ya Kibantu ambapo lugha za Kibantu zilikuwepo hata kabla ya majilio ya wageni kutoka Ajemi, Arabuni, India, China na kwingineko. Katika mtazamo huu lugha ya Kiswahili inaingizwa katika kundi la lugha za Kibantu. Ama kwa hakika mtazamo huu ulipata mashiko sana kuanzia karne ya ishirini, ulishadidiwa kutokana na tafiti mbalimbali zilizofanywa na weledi wa isimu, historia, akiolojia na ethnografia. Wanaisimu waliothibitisha kuwa Kiswahili ni lugha ya Kibantu ni pamoja na Bleek (1862), Meinholf. C (1932), Malcom Guthrie (1967, 1970, 1971), Doke (1935, 1945) na wengineo. Vigezo vilivyotumika kufafanua kuwa Kiswahili ni kibantu ni pamoja na:
  • Msamiati
  • Mofolojia
  • Mfumo wa sauti
  • Mfumo wa toni
  • Mfumo wa ngeli
  • Mpangilio wa maneno
Ubantu wa Kiswahili: Kigezo cha Kiisimu
Kigezo hiki cha kiisimu kimetumiwa na wataalam mbalimbali katika kuonesha ubantu wa Kiswahili Massamba (1999) amewataja wataalam mbalimbali ambao wamehusika na utafiti juu ya ubantu wa Kiswahili, wataalam hao ni pamoja na Carl Meinhof katika kitabu chake chaIntroduction to the phonology of the Bantu language,Duke (1935 – 1945), Malcom Guthrie (1967), Dereck Nurse na Thomas Spear (1985). Hawa walijadili ubantu wa Kiswahili kwa kutumia kigezo cha kiisimu, kihistoria na kiakiolojia.
Katikakigezo cha kiisimu vipengele vinavyoangaliwa ni kama vile kufanana kwa msamiati wa msingi, muundo wa kifonolojia, muundo wa kimofolojia, muundo wa kisintaksia mpangilio wa ngeli za majina.
Mizizi ya msamiati wa msingiwa lugha za kibantu na Kiswahili hufanana kwa kiasi kikubwa, mifano ifuatayo huweza kuonesha ukweli huu.
Example 1
Mfano
KiswahiliKikuryaKinyihaKijita
MajiAmancheAminziAmanji
JichoIrisoIryinsoEliso
Katika mifano hiyo hapo juu tunaona kuwa mizizi maji, manche, minzi, manji inafanana kwa kiasi kikubwa, kwa hiyo huu ni ushahidi tosha kutuonesha kuwa kuna uhusiano wa kinasaba kati ya Kiswahili na lugha za kibantu.
Piamofolojia ya Kiswahili na lugha za kibantuhufanana kwa kiasi kikubwa, yaani mfumo wa maumbo ya maneno ya lugha ya Kiswahili na lugha za kibatu hufanana. Kwa mfano, namna viambishi vinavyopachikwa katika mzizi wa maneno hufuata kanuni ileile kama inavyotumika katika lugha ya Kiswahili yaani viambishi vinaweza kupachikwa kabla au baada ya mzizi na huwa na uamilifu bayana.
Example 2
Hebu tuchunguze mifano ifuatayo:
KiswahiliKisukumaKisimbitiKinyiha
A-na-lim-aa-le-lem-aa-ra-rem-ai-nku-lim-a
a-na-chek-aA-le-sek-aa-ra-sek-aa-ku-sek-a
Kwa kuangalia mifano hii utagundua kwamba katika kutenganisha viambishi hufuata kanuni moja kwamba mahali kinapokaa kiambishi kwa mfano cha njeo, ndipo pia hukaa kwa upande wa lugha za kibantu, kwa mfano –na- na –ra- katika lugha ya kisimbiti. Hivyo tunaweza kusema kuwa kuna unasaba baina ya lugha hizi
Vilevilesintaksiaya lugha ya Kiswahili na lugha za kibantu hufanana kwa karibu sana. Kwa mfano jinsi yampangilio wa vipashio na kuunda sentensihufanana yaani mpangilio wa maneno hufuata kanuni maalum ambazo hufanana katika Kiswahili na lugha za kibantu. Katika Kiswahili sentesi inakuwa na pande mbili yaani upande wa kiima na upande wa kiarifu, katika upande wa kiima kipashio chake kikuu ni nomino na katika upande wa kiarifu kipashio chake kikuu ni kitenzi. Hii inamaana kwamba katika kuunda sentensi ni lazima nomino ianze na baadaye kitenzi.
Example 3
Hebu tuangalie mifano ifuatayo:
KiswahiliMama / anakulaN (K) T (A)
KijitaMai / kalyaN(K) T (A)
KiheheMama/ ilyaN(K) T(A)
KihayaMama / nalyaN(K) T(A)
Katika mifano hii tumeona kwamba muunndo wa kiima-kiarifu katika lugha za kibantu unafanana sana na ule wa Kiswahili yaani nomino hukaa upande wa kiima halikadhalika kitenzi hukaa upande wa kiarifu, kwa hiyo kwa mifano hii tunaweza kusema kuwa lugha ya Kiswahili ni jamii ya lugha za kibantu.
Piamfumo wa sauti (fonolojia)wa lugha za kibantu unafana sana na ule wa Kiswahili, yaani mpangilio wa sauti katika kuunda silabi, na miundo ya silabi kwa ujumla hufanana. Kwa mfano katika lugha ya Kiswahili hakuna muundo wa silabi funge yaani silabi ambayo inaishia na konsonanti, muundo asilia wa silabi za Kiswahili ni ule unaoishia na irabu vilevile katika lugha za kibantu hufuata muundo wa silabi wazi, yaani silabi zote huishia na irabu.
Example 4
Mifano ifuatayo hufafanua zaidi:
KisawhiliBabaK+I+K+I
KikuryaTataK+I+K+I
KihaDataK+I+K+I
KijitaRataK+I+K+I
KipareVavaK+I+K+I
Tanbihi: K= konsonanti I= irabu.
Kwa mifano hii tunaona kwamba mifumo ya sauti katika lugha za kibantu hufanana na ule wa Kiswahili, kwa hiyo tunaweza kuhitimisha kwa kusema kuwa lugha hizi ni za familia moja.
Pia vilevilemfumo wa ngeli za majinakatika lugha ya Kiswahili hufanana sana na ule wa kibantu hususani katika upachikaji wa maumbo ya umoja na wingi na maumbo ya upatanisho wa kisarufi. Katika lugha ya Kiswahili viambishi vya umoja na wingi hupachikwa mwanzoni kabla ya mzizi wa neno, hivyohivyo katika lugha za kibantu
Example 5
Kwa mfano:
UmojaWingi
Kiswahilim-tuwa-tu
Kikuryamo-ntoabha-nto
Kihaumu-ntuabha-ntu
Kikwayamu-nuabha-nu
Mifano hiyo hapo juu inadhihirisha wazi kwamba vipashio vyote vya umoja na wingi hujitokeza kabla ya mzizi wa neno, hivyo ni dhahiri lugha hizi zina uhusiano wa nasaba moja.
Vilevile katikaupatanisho wa kisarufilugha za kibantu na Kiswahili huelekea kufanana viambishi vya upatanisho wa kisarufi hususani viambishi vya nafsi.
Example 6
Mfano wa viambishi vya nafsi
KiswahiliMtotoa-nalia
KizanakiUmwanaa-rarira
KisukumaNg’wanaa-lelela
KikuryaOmonaa-rakura
Tunaona hapo juu kwamba kiambishi ‘a’ cha upatanisho wa kisarufi hujitokeza katika lugha zote, hivyo tunashawishika kusema kuwa Kiswahili kina uhusiano mkubwa na kibantu.
Pamoja na ushahidi wa kiisimu kutupatia vithibitisho tosha juu ya ubantu wa Kiswahili pia kuna ushahidi mwingine kama vile ushahidi wa kihistoria, kiakiolojia na kiethinolojia.
Ushahidi wa Kihistoria
Ushahidi wa kihistoria huchunguza masimulizi na vitabu mbalimbali vya kale ambavyo huelezea asili na chimbuko la wakazi wa upwa wa Afrika Mashariki. Vilevile ugunduzi wa kiakiolojia huonesha kuwa kulikuwa na wakazi wa asili wa upwa wa Afrika Mashariki ambao walikuwa na utamaduni wao na maendeleo yao hata kabla ya kuja kwa wageni. Katika ushahidi wa kiethinolojia, huchunguzwa tarihi mbalimbali zinazojaribu kutoa historia ya watu wa pwani ya Afrika Mashariki na lugha yao.
Kwa ujumla vyanzo hivi vyote huonesha kuwa pwani ya Afrika mashariki ilikuwa na wakazi wake wa asili ambao walikuwa na lugha yao, utamaduni wao na pia maendeleo yao, vyanzo hivi pia huhitimisha kwa kusema kuwa lugha ya wakazi hawa ilikuwa ni Kiswahili.
Jinsi Miundo ya Kiswahili inavyofanana na Miundo ya Lugha nyingine za Kibantu
Fafanua jinsi miundo ya Kiswahili inavyofanana na miundo ya lugha nyingine za Kibantu
Miundo ya lugha ya za kibantu inafanana na lugha ya Kiswahili na kufanana huko hutokea katika miundo silabi ambapo zote huishia na irabu na siyo konsonanti, miundo ya sentensi, miundo ya vitenzi vya Kiswahili ni sawa na ile ya Kibantu. Kwa mfano vitenzi vya Kiswahili na kibantu vina uhusiano mkubwa hasa katika viambishi, mnyumbaliko na pamoja na mianzo na miisho ya vitenzi. Mada hii imefafanuliwa vizuri katika mada iliyotangulia hapo juu.
Powered by Blogger.