KI 311:SEMANTIKI NA PRAGMATIKI KISWAHILI








SEMANTIKI NA PRAGMATIKI    KISWAHILI
   SEMANTIKI
  Semantiki ni  nini?
Wataalamu mbali wanakubaliana  kuwa:- Ni utanzu wa Isimu unaochunguza maana katikalugha za binadamu.
: Ni utanzu wa Isimu unaoshughulikia maana katikalugha.  Taaluma hii hufanya kazi ya kuunganisha Tanzu nyingine za Isimu.
Mofolojia
 



                                     
                                      

                                              Sintakia                                     Fonolojia
Ø  ALAMA / ISHARA NA MAANA.   
Taaluma ya Semantiki ni sehemu ndogo tu ya taalumapana zaidi iitwayo SEMIOLOJIA (Semiolojia/Semiotiki)     
Ø  SEMIOLOJIA                                                               
Ni taaluma inajikita katika kuchambua mfumo wa alama na Ishara kwa ujumla.
Semiontiki huchunguza alama na Ishara za lugha za binadamu na maana zake.  Inaangalia alama na Ishara zinavyotumika katika kuashiria maana.
        AINA MBALI MBALI ZA ALAMA NA ISHARA
   Kuna aina 3, Alama na Ishara.
        Ishara hutumika kimbadala
i)          Ishara za usababisho (Index)
ii)        Ishara za ufananisho (Incons)
iii)       Ishara nasibu (Sambolo)
      ISHARA ZA USABABISHI
Ni Ishara ambazo kunakuwa na ufungamano wa kiusababisho kati ya ishara na kinachoashiriwa
Mfano                                     Moshi                         -           Ishara ya moto
                                                Mawingu                   –          Mvua
     ISHARA ZA UFANANISHO
Ni Ishara ambazo kunakuwa na ufanano wa kipicha kati ya ishara na kile kinachoashiriwa
Mfano             Mchoro wa Ke na Me katika milango ya vyoo, michoro hiyo inatoa maana hapa ingia      Ke tu au Me tu.
 Kiti na kiti chenyewe, Meza na Meza yenyewe – ukiona Ishara / Alama unapata picha ya kitu halisi. 
      ISHARA NASIBU
Ndio zinzo chunguzwa zaidi na taaluma ya semantiki kwani ndizo zinanzojikita katika lugha.  Hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya ishara na kituchenyewe kinachoashiriwa hivyo uelewekaji wake hutokana na mazoea ya jamii.
Alalma nyingi za lugha zipo katika kundi hili.
Mfano             Bendera                     -           Nchi Fulani
                        Rangi nyekundu      -           Upendo au hatari
AINA ZA MAANA
Kwa mujibu wa Leech (1981) ambaye ana ainisha aina 7 za maana.

1.         Maana ya Msingi (conceptual meaning) Denotative / cognitive)
Hii ndio maana kuu ya neno isiyobadilika kutokana na mazingira.Aina hii ya maana hufafanuliwa kwa kuangalia nduni bainifu zinazobainisha kitu kinachotajwa na neno husika.Nduni bainifu ni sifa za msingi za neno au alama ambayo imetumika.Kwa lugha ya kisematiki nduni bainifu hujulikana kama vijenzi emantiki.
Hivyo  maana ya msingi ya neno Fulani hufafanuliwa kwa kuangalia kuwapo au kutokuwapo kwa vijenzi semantiki ambavyo vinajenga msingi wa kitu kinachofafanuliwa na neno hilo.
Mfano             Mwanamke               -           +          Binadamu / mtu
                                                                        +          Mzima
                                                                        +          Ke
·               Me

                        Mwaname                 -           +          Binadamu / mtu
                                                                        +          Mzima
                                                                        +          Me
·               Ke

                        Shoga                         -           +          Binadamu / mtu
                                                                        +          Mzima
                                                                        +          Me
·               Ke

2.         MAANA DOKEZI (Connetative meaning)
Ni ile maana ambayo hupatikana kwa njia ya kitu kingine maana hii hutokana na sifa
kuu 3:-
a)      Sifa ya Kiumba ya kitu
Sifa za umbo za kitu kinachodokeza maana ya kitu kizima yaani sehemu ya kitu fulani inayo ashiria  kitu kizima.
Mfano             Ndevu                        -                       Mwanaume
Sehemu to ya Me inafafanua kitu kizima ya Me.
Mimba                       -                       inaashiria Ke
Maziwa                      -                       Ke
Hivyo sehemu ya kitu fulaniambayo  inaishiria
b)     Sifa za Kisaikolojia za kitu.
Mfano                   Huruma, Upendo, Uvuilivu, Heshima Maneno hayu yanamrejelea Mwanamke.

c)      Mitazamo ya watu kuhusu kitu hicho
Mfano                   Mwoga, dhaifu, Mwepesi kulia,
                              Asiye na msimamo              -           Mwanamke
*    Kalam                               -           Elimu
3.         MAANA MTINDO
Ni maana inayohusisha Muktadha wa kimatumisi Inahusisa mitindo mbalimbali ya matumizi ya lugha.  Baadhi ya mitindo hiyo ni mitindo ya kilahaja, kiwakati, kieneo / Taaluma au famine kihadhi, kiuwasilishaji, Binafsi n.k.
            Kuna namna tunavyotumia lugha kutegemea na mtindo
                                                                           Zanziba       -           bomba
Mfano             Mfereji                          TZ - mtalo 
Mfano             Juma ni mshenzi wa hesabu
                                    Maana ya msingi ya Mshenzi ni tusi
4.         MAANA   HISIA
Ni maana inayotegemea hisia au mtazamo wa msemaji kuhusu kitu anachokizungumza.  Maana hii hujengwa kwa namna mbili:-
(a)   Kwa kutumia maana ya msingi au dokezi
-     Unahusisha maana ya msingi ya hivho kitu a unahusisha sifa za maana dokezi
Mfano                   Wewe Mwanamke kweli kweli   
-           Ke wa tofauti
-           Jasiri
-           Hodari
                 Lakini hapa anaonyesha hisia
Mfano                   Mume wangu amekuwa samba.  
-           Mkali
(b)   Kwa kutumia njia isiyo ya moja kwa moja kutoa ujumba au hisia zako.
Mfano                   Wanafunzi wanapiga kelele – unawambia ongezeni kelele kidogo
5.         MAANA TANGAMANI (Collocational meaning)
Ni maana inayopatikana katika mktadha wa kimatumizi kwa kuangalia jinsi maneno mawili au zaidi yanavyotangamana yaani yanavyokubali kutumika pamoja ili kuleta maana fulani iliyokusudiwa.
Mfano                         Msichana       -           Mrembo
                                    Mvulana                    Mtanashati
                                    Usiku wa                   Manane
                                    Mchana                      Kutwa
                                    Uwiku                        Kucha
                                    Mchana                      Kutwa
                                    Kujifungua                Binaadamu
                                    Kuzaa                         Mbwa
6.         MAANA  MWANGWI  (Reflected meaning)
Ni maana inayopatikana kwa kuhusianisha maana moja na dhana nyingine ya kitu kile kile yaani maana moja inaakisi maana nyingine.
            Mfano                         Ejaculate        -           Ejaculation
                                                Erect               -           Erection
Hapa awali yalikuwa na maana zake mfano Ejaculate   -   kuondoa   Erect   -   kusimamisha kama vile jengo.  Maana hizi za msingi zilianza kupata maana Mwangwi.
Maana mwangwi zimepata mashiko zaidi hadi sasa
            Mfano             Tia, Simamisha, Panua, Comeka, Ingiza
            Maneno haya yamepata maana mwangwi ambazo zimekuwa na mashiko zaidi.
7.         MAANA  DHAMIRA  (THEMANTIC MEANING)
Ni maana ambazo hutegemea kile ambacho msemaji au mtoa ujumbe anakusudia kukipa umuhimu mkubwa au kukipa msisitizo mara nyingi kwa kukitaja mwanzoni.
            Mfano             1.         Mtoto amevunja kikombe
                                    2.         Kikobe kimevvunwa na mtoto
                                    3          Msichana yumo darasani
                                    4.         Darasani kuna msichana

            Sentensi         1.         Msisitizo ni nani amevunja
                                    2.         Nini kimevunjwa
                                    3.         Nani yumo darasani
                                    4.         Wapi mahali alipo msichana)

Kwa ujumla Aina za maana zimegawanyika katika sehemu kuu 2 :-
1.         Maana ya msingi
2.         Maana ya ziada
DHANA ZA UTAJO, UREJELEO NA  FAHIWA
Dhana hizi zinauhusiano wa moja kwa moja na maana
     UTAJO (Denotation)
Ni uhusiano baina ya Leksimu au kipasho cha kiisimu (Expression kiyambo cha lugha) na seti ya vitu ambavyo vinarejelewa na Leksimu Meza ni vitu vyote katika dunia ambavyo kwa hakika vinaitwa Meza.Utajo wa Leksimu Nyumba ni viu vyote katika dunia ambavyo kwa hakika vinaitwa Nyumba.
      UREJELEO
Ni uhusiano baina ya viyambo vya kiisimu au vya lugha na viwakilisho vyake duniani wakati maalum wa semo au usemi wako. Ili uhusiano huo uwe na urejeleo lazima uoneshe umahususi Mfano Kiti hiki, kiti cha miguu minne, meza ya mviringo.
Mfano  Mwanamke huyu  
Utajo wa Leksimu nyumba Urejeo wake Nyumba ya msonge.
    FAHIWA
Ni seti ya mahusiano yaliyopo baina ya kiyambo kimoja na viyambo vingine katika lugha au  seti ya mahusiano katik ya neno moja na jingine katika lugha .Mahusiano hayo huitwa mahusiano ya kifahiwa au mahusiano ya Kisemantiki.
Mahusiano ya kifahiwa ni kama vile Usinonimia, Unyume, Utata n.k.
Mfano Pesa, hela, fedha  - Maneno haya yanauhusiano wa kifahiwa unaoitwa Usinonimia na maneno yenyewe yanaitwa Sinonimia.Chini, juu Uhusiano wa Unyume.
Utajo wa Urejeleo huhusu vipengele vya lugha na  nje ya vipengele vya lugha lakini fahiwa inhusu vipengele ndani ya lungha.
Tofauti kati ya utajo na Urejeleo Utajo ni wa jumla lakini Urejeleo ni mahususi yaani wakati maalum wa semo.Dhana hizi hutusaidia kufafanua maana katika lugha.
   NADHARIA ZA MAANA
Zipo nadharia nyingi zinazojadili masuala ya maana.  Hii ni kutokana na:-
Dhana yenyewe ya maana ni tata na telezi na ni vigumu kusema maana hasa nini?
Kuna nadharia 4 ambazo tunaziteua
i)  Maana kama kitajwa au kirejelewa (referencial)
ii) Maana kama dhana / Tasurira (Idiotional)
iii) Maana kama mwitiko (Behavioral)
iv)Maana kama matumizi (operational au contextional  than of meaning)
1.         MAANA KAMA  KITAJWA AU  KIREJELEWA
Nadharia hii inadai kuwa maana ya umbo la kiisimu hurejelea kitu halisi kinachotajwa na umbo hilo.  Maana ni kitu halisi kinachorejelewa na neno hilo au umbo hilo la kiisimu.  Hivyo basi kama umbo lolote la kiisimu lina maana basi lazima liwe na kirejeleo chake.

Nadharia hii inasisitiza kuwa kama maumbo 2 yanatenelea kitajwa kile kile basi mambo hayo yana maana moja.
Nadharia hii inahusu hasa majina maalumu ambayo hutokwa kipekee na kuwakilisha kitu halisi.

UBORA
i) Ni kweli kwamba lugha ina kiambo ambacho tuaweza kupata maana kwa kuirejelea latika mazingira halisi.
MAPUNGUFU
i)  Sio kila Leksimu au kiambo chake japo maneno mengi katika lugha yenye maana pasipo kuwa na verejeleo vyake .  Mfano           Viunganiuhi   -   kwa, na, ya   -   vibaisahi hivi havina viwakilishi vyake.

ii) Tunaweza kuwa na viamb  matamko maweili au zaidi yanayorjelea kitajwa kimoja lakini si lazima matamko hayo yawe na maana sawa.  
Mfano             Mtu anaweza kuitwa / kurejelewa kwa jina lake, cheo cha kazi, cheo cha uzazi n.k. nab ado akawa ni mtu yule yule japokuwa maana za maneno yaliyotumika ni tofauti.
                        Mfano             -           Mwalimu Kibiki
                                                -           Mwalimu wa DULE
                                                -           Mke wa Mbata
                                                -           Mwanachama wa UDASA
                                                -           Mwalimu Mlezi wa CHAWAKAMA
                                                -           Mwenyekiti wa kikundi cha kina mama
iii)       Kuna maneno ambayo hayarejelei kitu kinachotajwa ingawa htumia tamko au jina la kitu hicho.
Mfano             Kupe                          -           John ni kupe
                                                                        -           kupe mduu
                                                                        -           Unyonyaji
                                    Utapaswa useme      -           John ni mdudu anayeitwa kupe
iv)       Kunamaneno yanayotaja vitu dhahania hivyoni vigumu kurejea vitu halisi vinavyo rejelea kitu dhahania.
                        Mfano             Shetani, Uchovu, Furaha, Huzuni, Malaika
2.         MAANA KAMA   DHANA
           Nadharia hii inadai kuwa maana au taswira inayoibliwa na umbo hilo la kiisimu akilini mwa wana lugha pindi umbo hilo la kiisimu litumikapo, yaani maana ni picha /Taswira zinazoibuliwa pindi umbo la kiisimu linapotumika.
Hivyo badala ya kuhusisha maana na vitu halisi moja kwa moja nadharia hii inahusisha maana na wazo ama Taswira.  Viambo dhahania kama mallaika, shetani, upepo hapa zinaweza kupata maana kwani mnaangalia kitu mmoja ana picha au Taswira gani kujusiana na dhana hiyo.
Nadharia hii inaisitiza kuwa mawasiliano hujafanikiwa pale ambapo maneno au kiambo huchochea mawazo sawa kati ya msikilizaji na msemaji.
Hivyo hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya neno au umbo hilo a kiisimu na kitajwa halisi lakini uhusiano upo kati ya kitajwa na Taswira halisi aliyonayo mtu.



UBORA
i)                   Kwa kiasi Fulani maana hutokana  na dhana na ndio maana vitu dhahania huweza kupata maana.

UDHAIFU
i)                   Nadharia hii inaibua maswali mengi:-
Je dhana / Picha / Taswira ya mtu na mtuhufanana?
Wakati mwingine hutofanana
Nani huamua kuwa dhana hiyo ni kweli kama ilivyotumika
ii)                 Tunaweza kuwa na dhana tofauti juu ya kitu kilekile
msonge
Mfano             Neno                          Nyumba                    ghorofa

                                                            Mke                            kuangalia     
                                                                                                Maumbile
iii)              Si kweli kwamba kila kiambo kina husishwa na Taswina mfano na, lakini, ingawa.
3.         MAANA KAMA MWITIKO
            Mwasisi wa nadharia hii ni Bloomfield – alliasisi 1935
Nadharia hii imetokana na wana Utabia (behaviourism) kama B.F Skinner, Parlon waliofanya utafiti kwa wanyama.
            Misingi ya nadharia ni kwamba Tamko huwa ni kichocheo ambacho huamsha mwitiko kwa msikilizaji.  Nadharia inahusu hasa kila mtu anavyoitikia katika nafsi yake yaani kila mtu anaposikia neno Fulani huibua hisia Fulani ndani ya nfsi yake inayomfanya aitikie maana ya neno hilo.
            Nadharia hii uliona neno kama kichocheo na maana ni ule mwitiko hivyo maana ya kitu au Tamko fulani ule mwitikio wa msikilizaji.
            UBORA
i)                   Kwa kiasi fulani una ukweli kwa sababu mwitiko unaweza kutusaidia kupata maana.
UDHAIFU
i)                   Namna watu wanavyoitika si sawa wakati wote.  Watu huweza kutika tofauti tofauti kwa tamko hilo olo moja.
ii)                 Yapo maneno ambayo ni vigumu kupata miitikio yake
Mfano             -           Viunganishi              -           na, kwa, ingawa, ni vigumu
kutenda tendo lolote linalotokana na mneno hayo pia maneno dhahumia .
                        Mfano             -           Njaa
iii)              Nadhani hii inakazia zaidi mwitiko na kusahau kuwa lugha ni chombo kinachohusisha jamii nzima
4.         NADHARIA YA MAANA KAMA MATUMIZI
Mwasisi wake ni Ludwig Wittegn (1953).Katika  kitabu chake “Philosophical Investigation”.Alifanya mapinduzi makubwa katika kueleza maana.
Anasema ni kosa kubwa kuweka mipaka ya maana kama ambavyo nadharia ya maana kama kitajwa, Maana na Mwitiko zinavyofanya “Kwani kufanya hivyo ni sawa na kuweka mipaka ya thamani ya umbo lenyewe la kiisimu. Kinachopaswa kuzinyatiwa ni matumizi yaani jinsi neno au kiumbo cha kiisimu kinavyotumika.  Haina haja ya juuliza neno hili lina maana gani bali angalia neno hili linatumikaje.

UBORA
i)                   Inasaidia kuondoa uvulivuli wa maana za maneno kwa kujikita katika mktadha wa kimatumizi.
ii)                 Nadharia hii haibagui umbo lolote la kiisimu, maneno ambayo hayajengi, taswira, dhana yeyote inaweza kupata maana kulingana na matumizi yake.
UDHAIFU
i)                   Baadhi ya wanaisiimu wanahoji kuwa Nadharia hii haiweki wazi mipaka ya kimatumiz.  Je mipaka ya kimatumizi ni ipi?
ii)                 Kuna mamemo ambayo yanaweza kupata maana kabla ya matumizi.
Mfano vifaa vya kieledromic vinavyogunduliwa, mfano Kinukushi – Fax
Je ni namna / Nadharia ipi ni Bora kwa kueleza Maana?
SEMANTIKI YA MANENO
Tutajikita kuangalia maana katika ngazi ya neno na sentensi
1.         SEMANTIKI YA MANENO VIKOA VYA MAANA
Dhana hii inahusu mahusiano na mpangilio wa msamiati wa lungha.  Maneno katika lugha yeyote  hayapo kiholele bali yapo katika utaratibu au mpangilio maalum.  Wanasemantiki wanaamini kuwa “Maneno yangekuwa yanaonekana katika ubongo wa binadamu basi maneno hayo yangeonekana yakiwa yamepangwa katika makundi madogo madogo kulingana na jinsi maneno hayo yanavyohusiana.
            Hayo makundi madogo madogo ya kidhahania ya maneno yaliyojitenga kulingana na mahusiano yake ndiyo huitwa Vikoa vya Maana.
            Mfano wa Vikoa vya maana, kunakuwa na Neno kuu na Memba wa kikoa hicho
Mfano             Wanyama      -           Simba, Pak, Mbwa, Kunguni
Matunda        -           Embe, Pela, Nanasi
Nyani             -           Sokwe, Kima, Tumbili, Komba, Ngedele
Mbwa             -           Mbwa, Mbweha, Fisi, Mbwa mwitu
Embe              -           Dodo, Embe maji, Ng’ong’o
Chungwa       -           Chungwa, Limau, Chenza Ndimu
            Kikao cha thamani za kukalia kiti, sofa, kochi
Rangi -           Nyeusi, Nyeupe, Nyekundu n.k.
            SIFA ZA VIKOA VYA MAANA
i)                   Maneno yaliyo katika kikoa kimoja yanauhusiano wa kisiganifu yaani kuwa na ufanano kimaana na kutofautiana pia.
Mfano             Samani inajumuisha vitu vyote vinavyotumika kukatia lakini ukiangalia kimoja kimoja na matumizi yake vinatofautiana.
2.         Kikoa kimoja kikubwa au kipana huweza kuwa na vikoa vidogo vidogo vya maana ndani yake.
Mfano             Wanyama      -           mbali mbali tunaweza kuchukua kikoa kidogo tukapata vikoa vingine.
3.         Maneno katika vikoa Fulani hayana mpangilio maalumu yaani hakuna utaratibu maalum wa neno lipi lianze na lipi lifuate.
            Angalizo :   Upo mpangilio maalum katika Vikoa vya siku, miezi, mwaka na vipimo mbalimbali.
MAHUSIANO YA KIFAHIWA
Mahusiano ya kifahiwa ni seti ya mahusiano yliyopo baina ya kiambo kimoja na kingine au neno moja na jingine.  Mahusiano ya kifahiwa yapo ya aina sita:-
i)                   Usionimia / Usawe
ii)                 Uantonimia / Unyume
iii)              Uhomonimia
iv)               Upolisemia
v)                 Umenonimfa
vi)               Uhiponimia
USINONIMIA / USAWE
Ni mahusiano ya kimaana baina ya maneno mawili au zaidi ambapo maana ya maneno hayo huwa ni sawa au hukaribiana.
Maneno yenye maana sawa au maana zinazokaribiana huitwa Usawe au Usinanimia.
Mfano             Pesa, hela, fedha maneno haya yanauhusiano wa Usinonimia au Usonee kwani maana  zake hukaribiana.
Dunia wakati mwingine Ulimwengu
Shimo, tobo, Tundu yanakaribiana
Uzinzi, Kahaba, Malaya, Usherati ni maneno yanayokaribia.
Mjinga, mpumbavu, Bwege.
AINA ZA SINONIMIA
i)                   Sinonimia za kimantiki /logica / synomimes.
Ni sinonimia zinazotokea pale ambapo leksimu mbili au zaidi huweza kubadilishana nafasi katika sentensi afifu zhote pasipo kuathiri masharti ya ukweli ya sentinsi hizo.
Mfano -Lengo, Kusudi, Nia, Dhumuni, Mama anatembea pole pole / Taratibu.  Haraka haraka, Upesi upesi.
ii)                 Sinonimia Kuntu (Absolute Synomimes)
Ni Sinonimia ambazo hutokea pale ambapo Leksimu mbili au zaidi huweza kubadilisha nafasi katika miktadha yote bila athari yeyote ya maana.  Watafiti wanakubaliana kuwa hakuna lugha yeyote duniani yenye sinonimia kuntu.

Hivyo ni vigumu kupata maneno yenye maana sawa kwa asilimia moja.
“Eneo moja wapo linaloaza kuwa na Sinonimia kuntu ni eneo la Silabi”
Mfano             Ving’ong’o au Nazali wakati wote vinaweza kubadilishana
                        Sintaksia        -           Saruji miundo
                        Fonolgia        -          
                        Mofolgia
Elimu viumbe          -           Baiologia
            VYANZO VYA SINONIMIA / SABABU
            Habwe ba jaranja
i)                   Ukopaji wa misamiati
Maneno yakiwa na asili tofauti huleta hali ya Usinonimia.  
Mfano             Neno Shule limetoholewa toka lugha ya kijerumani “Schule “ lakini kuna neno “Skuli “ hili limtokana na School la kiingereza.
Maneno haya yanatumika katika lugha ya Kiswahili wengine wanatumia Skuli na wengine Shule/

ii)                 Jinsia
Hutokana na maneno yanayolejelea ama mwanmke au mwanaume.
Mfano             Hali ya kutokuwa na uwezo wa kuzaa kwa m-ke ni Utasa na Ugumba kwa mwanaume.  Msichana mrembo lakini Mvulana mtanashati Mwanamke aliyefiwa na mume  -  Mjane
Mwanaume aliyefiwa na mke      -  Mgaje
Mwitiko Abee na Naam

iii)              Tofauti za kijiogorafia au Maeneo  Wazungumzaji wa  lugha moja ambao wanaisi katika maeneo tofauti ya kijiografia wanaweza kuwa na maneno tofauti yanayorejelea dhana au kitu kile kile.
Mfano             Zanzibar                    -           Markiti
                        Tanzania bara           -           Soko
                        Tanzania bara           -           Umeme
                        Kenya                         -           Stima
                        Tanzania                    -           Bomba
                        Zanzibar                    -           Mfereji
                        Tanzania                    -           Dala dala
                        Kenya                         -           Matatu

iv)               Taaluma au Uwanja
Taaluma mbili mbili huwa na maneno mbali mbali yanayotumiwa kurejelea kitu au dhana ile ile.
Mfano             katika riwaya kuna Aya lakini ushairi kuna Ubeti, maneno hayo yote hutejelea kitengo au mfululizo wa maandishi.

v)                 Wakati
Baadhi ya Sinonimia huzuka kutokana na wakati.
Mfano             Habwe na Karanja
Kuna neno kama soko kuna mahali liliitwa Utuku
Mfano             Zamani wanyonyaji  - Mabepari  kwa sasa Mafisadi

vi)               Urasimi
Tunarejelea neno lipi ni sanifu kuliko lingine
Mfano             Hela, fedha, pesa – neno rasmi ni fedha 
                        Mpumbavu, mjinga – yanaonekana rasimi kuliko fara, bwege n.k.

vii)            Ujumla na Umahususi  yapo maneno ambayo hutumika kwa jumla na wakati mwingine hutumika kwa umahususi
Mfano             Hamu  neno la jumla  kiu – kinywa, njaa.

viii)          Rika au Umri
Tofauti za umri na rika, yapo maneno ambayo yanaonekana ni ya kitoto zaidi mengine ni ya kiutu uzima.
Mfano             Piga  - mtu mzima / kutandika  chapa – mtoto

ix)               Elimu au Hadhi
Watu wenye elimu tofauti tofauti hutumia maneno tofauti, wakati mwingine huwa ni kutofautisha.
Mfano             neno  Afya – kawaida  na Siha – kitaaluma njema

x)                  Dini
Dini tofauti huwa na maneno tofauti kwa ajili ya kuelezea dhana zinazolingana hasa Waislamu na Wakristo
Mfano             Dhana ya kujinyima chakula kwa minajili ya kupata fadhila za kidini Waislam  -  Saumu na Wakristo   -  Kwaresma  
Mahali pa kuabudia Wakristo  -  Kanisa
Waislamu  –  Msikitini,  Sala  -  Swala
NAMNA YA KUBAINI KAMA NI SINONIMIA KUNTU AU SIO KUNTU
Kuna mbinu kuu 2:-
i)                   Kuangalia miktadha mbalimbali ya matumizi husika ya Sinonimia
ii)                 Katika mazungumzo au katika maandishi
1.         KUANGALIA MIKTADHA MBALIMBALI YA MATUMIZI YA SINONIMIA HUSIKA KATIKA MAZUNGUMZO AU MAANDISHI
            Mfano             Fahamu, Jua, Elewa,  je maneno haya yanatumika kote
·         Nilielewa atakuja, Nilifahamu atakuja
-     Muasherati, kahaba, mzinzi  -  utofauti kidogo kimaana
2.         *  Kutunga sentensi kahaa tofauti kwa kutumia kila Sinonimia kwa sentensi moja kishi kubadilisha nafasi ya kila Sinonimia katika sentensi hizo na kuweka Sinonimia nyingine
            Mfano -Shimo, Tobo, na Tundu
i)                   Hamis alichimba shimo.
ii)                 Suruali ya Festo ina tobo
iii)              Chandarua change kima matundu mengi
iv)               Ni rahisi ngamia kupenya kattika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
Hizo ni Sinonimia lakini sio Sinonimia Kuntu.
Shimo  -  kubwa, Vifaa  jembe n.k.
Tundu  -  Dogo zaidi
UANTONIMIA / UNYUME
Ni uhusiano wa kimaana baina ya maneno mawili ambayo maana zake ni vinyume yaani maana ya neno moja ni kinyume cha maana ya neno jingine
Mfano             Neno  - Nenda - Rudi          Cheka - Lia                Kubwa  - Dogo
Kuna aina kadhaa
AINA ZA UNYUME AU UANTONIMIA
i)                   Unyume kamilishani / complimentary or simple antonyms.  Ni Unyume ambao unampaka usiopitika ambapo ukanushi wa upande mmoja ni unenetezi wa upande wa pili
Mfano             Mwanamke   -           Mwanaume
                        Hai                  -           Mfu
                        Pata                -           Kosa
                        Kweli                         -           Si kweli
ii)                 Unyume  kadilifu (Gradable)
Ni unyume ambao hamna mpaka usiopitika hivyo huweza kuelezwa kwa makadirio yaliyopo baina ya pande mbili husika.  Ukamohi wa upande mmoja si lazima uwe ni unenko wa upande mwingine (wa pili) kubwa  -  ndogo si lazima kinyume cha kubwa iwe ndogo kwani inaweza kuwa ndogo wastani n.k.
Zito  -  nyepesi inaweza kuwa nzito wastani n.k..
iii)              Unyume elekeana (Relational Antonyms)
Ni unyume unaokuwepo pale ambapo uhusiano baina ya leksimu mbili katika jozi huwa ni wa kiuelekeano yaani Leksimu nyingine kutegema na Uelekeo yaa upande ambako tendo linaelekewa.
Mfano             Nenda            -           Rudi   -    Uelekeo Fulani yaani tenda linaelekewa wapi
                        Panda             -           Shuka
                        Sukuma         -           Vuta
                        Kushoto         -           Kulia
                        Mbele             -           Nyuma
                        Juu                  -           Chini
                        Chomeka       -           Chomoa
iv)               Unyume Rejezi au Tenduzi
Ni unyume ambao huhusisha Leksim ambayo kwazo tendo la Keksim mojawapo kuweza kubadilishwa ili kurejelea kinyube chake.
Mfano             Chomoa         -           Chomeka
                        Ezeka             -           Ezua
                        Ziba                -           Zibua
UHOMONIMIA
Ni hali au uhusiano ambao umbo moja la kiisimu huwa na maana nyingi zisizohusiana.
Mfano             Panda
·         Kusia mbegu
·         Kwea mlima au mti
·         Tawi la mti
Kaku
·         Ugonjwa wa vidole
·         Ganda la yai
·         Ndugu mkubwa wa kiume
UPOLISEMIA
Ni Sifa ya neno moja kuwa na maana nyingi zinazohusiana, au ni hali ya neno kuwa na maana nyingi zinazo husiana yaani maana inakuwa moja lakini inahusiana na vitu vingi
Mfano             Mdomo
                        (N) wingi wake midogo
                        i)  Ni sehemu ya nje ya kinywa inayomwezesha kiumbe kupitisha
     kitu chakula.
ii) Uwazi wa kitu kama chupa ya birika n.k.
iii) Kinywa
Kichwa
i)  Ni sehemu ya mwili wa kiumbe hai
ii)  Ni injini ya gari moshi inayokokota mabehewa
iii) Ni kiongozi wa familia
iv)  Mtu hodari sana katika masomo
              
             UHIPONIMIA
Ni uhusiano wa kiwima baina ya  Maneno ambapo fahiwa ya neno moja hujumuishwa katika fahiwa ya neno jingine.Ina maana kwamba maana za neno Fulani ni sehemu ya maana y neno jingine.  Kuna  neon  moja  jumuishi na madogo madogo na ili uelewe maana ya neno kubwa lazima uhusishe maneno madogo madogo.
Neno lenye maana pana huitwa neno jumuishi nayale yenye maana finyu huita Haponimia
MATUNDA

                                                  Ndizi    Chungwa   Embe  Parachichi
Fahiwa ya neno Ndizi ni sehemu ya fahiwa ya matunda hivyo ukitaka kuifasili ndizi utasema ni aina ya matunda, ili uweze kuelewa maana ya ndizi, chungwa, embe, parachichi ni sehemu ya fahiwa ya neno jumuishi ambayo ni Matunda
UMERONIMIA
Ni uhusiano ulipo baina ya Leksimu inayotaja sehemu na ile inayotaja kitu kizima.
Mfano             Mwili
-          Shingo
-          Kichwa
-          Mabega
-          Miguu
-          Tumbo
Meronimia inahusu kitu na sehemu zake, nikitaka kujua kichwa ni nini nitarejelea sehemu mbali mbali za kichwa
MAANA KATIKA NGAZI YA TUNGO AU SENTENSI
Kuna vipengele 5
i)                   Usawe
ii)                 UtataUkinzani
iii)              Ukinzani
iv)               Upotoo
v)                 Uziadu – dufu
USAWE
Ni uhusiano baina ya sentensi mbili au zaidi zenye kudhihirisha maana moja ya msingi.
Mfano             Sikujua kwamba usingeongea naye abadani
                        Sikufahamu kuwa usingezungumza naye katu
Katika sentensi hizimaneno yanaetofautiana lakini maana ile ile
-          Maelezo yako yalikuwa magumu kueleweka
-          Ilikuwa vigumu kuelewa maelezo yake
Katikasentensi hizi kinachotofautisha ni mpangilio.
AINA ZA USAWE
i)                   Usawe wa kilekisika
ii)                 Usawe wa kimuundo
1.         USAWE  WA KILEKSIKA
Ni Usawe unaotokana na sentensi mbili au zaidi kuwa na maneno yenye maana ile ile ya msingi katika nafasi ile ile.
Mfano            Sikujua kwamba usingeongea naye abadani
                        Sikufahamu kuwa usingezungumza naye katu
Maneno yaliyotumika katika nafasi ile ile yanabeba maana ya msingi
2.         USAWE WA KIMUUNDO
Hutokana na maana ya msingi ya sentensi mbili au zaidi hubaki ile ile japo sentensi zina mpangilio tofauti.  Hapa kinachozingatiwa saidi na muundo wa ile sentensi.
Mfano             Maelezo yake yalikuwa magumu kueleweka
·         Ilikuwa vigumu  kuelewa maelezo yake.
Kilichotofautisha hapa ni mpangilio tu.
Mfano             Hakuna aliyelewa maneno yake ya ajabu
·         Maneno yake ya ajabu hakuna aliyeelewa.
UTATA
Ni hali ambayo sentensi moja huwa na maana au tafasiri zaidi ya moja au huwezi kuelewaeka kwa namna zaidi ya moja.
AINA ZA UTATA
i)                   Utata wa Kileksia / Kileksika
ii)                 Utata wa Kimuundo
UTATA WA KILEKSIA
Ni Utata unaosababishwa na matumizi ya Homonimia na Polisemia
Mfano             Baada ya shida nyingi alifannikiwa kumleta Papa nyumbani
                        Papa               -           Mnyama
                                                -           Mkuu wa kanisa.
Siku hizi bei ya kanga na sh 10,000
-           Ndege
-           Nguo.
            UTATA WA KIMUUNDO
Hutokana na jinsi sentensi ilivyo pangiliwa au umbo la neno au kirai kuwa katika nafasi malumu katika sentensi.
Mfano             -           Wanawake na wanaume waangalifu walikaa  kando.
1.            -           Wanawake walikaa kando
-           Wanaume waangalifu nao walikuwa kando
2.            -           Wanaume waangalifu na Wanaume waangalifu walikaa
Kando
                                    *  Mtoto alilalia maziwa
                                                -           Alikunywa maziwa akalala
                                                -           Alilala juu ya maziwa.
                                    * Ananipenda zaidi kuliko wewe
                                                -           Nyinyi nyote wawili mnanipenda
                                                -           Wewe unanipenda lakini mwenzio ananipenda zaidi yako
            UKINZANI
Ni hali itokeayo pendi kiyambo cha lugha kinapokuwa na sifa Fulani na wakati huo huo hakina sifa hiyo.
Kiambo cha namna hii hunena kwamba mtu au kitu Fulani kina sifa Fulani na wakati huo huo hakina sifa hiyo.
Mfano             Mwanamke Yule ni mwanamke kweli kweli
                        + Me
                                    - Ke
Bibi yangu nikijana kabisa.
                        + Uzee
 - Uzee
            Yule kijana ni mwizi mtakatiu
                        + Mtakatifu
 - Mtakatifu
            Huyu mtoto ni mtu mzima
                        + Uzima
 - Uto Uzima au
                        + Utoto
 - Utoto
Nilikwenda mbele nikarudi nyuma
                        + mbele
 - mbele
            UPOTOO
Ni Ukiushi wa kisemantiki utokeao pindi vijenzi semantiki viwili singanifu vinapounganishwa kueleziea jambo au kitu.
Mfano             Alichora barua kwa guu wa kushoto
·         Viatu vyake vinacheka
·         Kaptura yake inwasha taa
·         Kuchora – haliendani na neno “barua” kifaa kinachotumika kuchora hakiendani na mguu (wa kushoto)
·         Barua – haichorwi
Viatu vyake vinacheka
            *Matumizi holela ya maneno katika lugha na husababisha upotoshaji
  UZIADA – DUFU
Ni urudiaji wa maneno usio wa lazima au usiohitajika ambao hauifany sentensi kueleweka zaidi au haufafanui zaidi maana.
Mfano             -     Mke wangu ni mke wangu
·         Mwizi ni mwizi tu
·         Mwanafunzi ni mwanafunzi tu
·         Mwalimu ni mwalimu
PRAGMATIKI
Ni tawi la isimu linalohusu maana kama inavyowasilishwa na mzungumzaji na kutafsiriwa na msikilizaji
Progamatiki inahusu kitu kinacho maanishwa zaidi a kile kinachosemwa au kuandikwa.
Progmatiki inahusu kinachomaanishwa na mzungumzaji katika muktadha fulani na namna muktadha unavyosaidia kutafsiri maana.
Progmatiki ni maana ktika mtagusamo (meaning in interaction ) maana haijikiti katika maneno pekee wala haichukiliwi na msemaji pekee na wala haitesemei utashi wa msikilizaji pekee.  Kujenga maana ni mchakato chanamni unaohusisha mnafaka baina ya msemaji, msikilizaji, muktadha wa mzungumzo pamoja na maana ya msingi ya kilichosemwa.  Wanaisimu – Pragmatiki ni taaluma ambayo inhusu mahusiano yaliyopo baina ya maumbo au alama za lugha na watumiaji wa maumbo au alama hizo.
Katika Pragmatiki suala la msingi ni muktadha.  Muktadha hutumanishi tu mahali, sehemu au mazingira ambapo mazungumzo yatafanyika hivyo ni kipengele kimoja tu katika vipengele vingi.  Muktadha inahusisha yafuatayo:
Nani anazungumza?
Anazungumza na nani?
Anazungumza na mtu huyo akiwa na nini pembeni.
Wanazungumzia nini?
Wanazungumza wakiwa wapi?
Wanazungumza wakati gani?
Je wanamtazamo gani kuhusu wao wenyewe na watu wengine?
Wapo katika hali gani?
Nini kilichotangulia kusemwa kabla ya hicho kilichosemwa sasa?
Je wanauzoefu au historia sawa au tofauti?

DHANA YA SKIMA (SCHEMA – SCHEMATA)
Skima ni ramani dhahania zilizopo akilini mwa binadamu ambzo hutusaidia kupata na kuelewa taarifa mpya.  Hizini ramani majumuni za maarifa au utambuzi ambazo kila mtu anazo akilini mwake.  Kwa kawaida tunatumia skima mara zote tupatapo habari mpya, hivyo skima zetu huboreshwa na kurekebishwa pindi tupatapo habari au maarifa mapya.

Skima ndizo ambazo hutusaidia kuelewa kile ambacho kinasomwa katika miktadha mbali  mbali
Mfano             Skima zinazohusu watu au tukio kama vile harusi, akilini utajua ni tukio gani kulingana na jinsi tunavyopata maarifa mapya.

Mfano             Amina aliingia akajazi mahitaji yake ya wiki nzima katika kapu lake na kuyapakia kwenye torori ambalo aliliburuza mpaka alipoegesha gari, akapakia kapu garini na kwenda zake.

Katika hali ya kawaida tukio hili linafanyika sokoni au supermaketi
-           Uelewa huu na maana hii ni kwa sababu ya skima ya sokoni au supermarket
NJIA ZA KUPATA TAARIFA MPYA ZIPO 3
1.            Kupokea na kuhifadhi
Ni kitendo cha kuchukua taarifa mpya na kujaribu kuhifadhi bila kuifanyia marekebiso au mabadiliko yoyote.  Unapopata taarifa mpya unaiimarisha au kuiboresha skima yako.
2.            Kupokea na kuboresha
Hii hutokea pale uapatpo taarifa mpya na kisha kuifanyia markebisho kwa sababu haiendani na skima yako iliyopo
3.            Kuunda Upya
Ni kitendo cha kutengeneza skima mpya pindi hupokeapo taarifa mpya ili kuirekebisha au kuondoa Ukinzani uliopo akilini mwako.
            AINA ZA SKIMA
i)                   Skima ya mtu
ii)                 Skima ya kitu
iii)              Skima ya tukio
iv)               Skima ya dhima
1.         SKIMA YA MTU
Ni skima inayohusu sifa ya mtu fulani mahususi kama inavyofahamika na mtu mwingine.
            2.         SKIMA YA KITU
Ni skima inayohusu sifa za kitu fulani mahususi kama zinavyo fahamika na mtu mwingine  Mfano             Meza, Darasa n.k.
            3.         SKIMA YA TUKIO
                        Ni skima inayohusu mchakato shughuli au njia ya kutenda jambo Fulani
                        Mfano             Msiba, Harusi
            4.         SKIMA YA DHIMA
Ni  Skima inayohusu matarajio ya wanajamii juu ya dhima au wajibu wa mtu fulani katika jamii hiyo.Kila mtu katika jamii ana dhima Fulani ambayo wanajamii wanatarajia aihimize.
            MCHANGO WA WANAFALSAFA KATIKA TAALUMA YA PRAGMATIKI
Taaluma hii kwa kiasi kikubwa imeathiriwa zaidi na michango ya wanafalsafa kuliko wanaisimu.  Hii imewafanya watukujiuliza Pragamatiki ni tawi la Isimu au falsafa.
Michango ya wanafalsafa 3 muhimu:-
i)                   John L. Austiri (1962)
ii)                 John R. Searie (1969)
iii)              Herbet (H.P Grice.) Paul Grice (1975)
JOHN L. AUSTIN (1962)
            -           Aliasisi na dharia ya TENDO – UNENI John R. Searie
            -           Aliboresha nadharia ya Tendo Uneni iliyoasisiwa na Austin.  H. P Grice
                        Ni mwasisi wa kanuni ya ushirikiano  katika mawasiliano.
            KANUNI YA USHIRIKIANO  KATIKA MAZUNGUMZO
            HERBET PAUL GRICE (1975)
Aliasisi kanuni ya ushirikiano katika mazungumzo . Aliiasisi katika makala yake iitwayo “Logic and Compesation” ilihusu Mantiki katika mazungumzo.  Kwa mujibu wa H. P. Grice “kanuni ya mazungumzo inasema “ “Toa mchango wako katika  mazungumzo kadri inavyohitajika wakati wote uzungumzapo kwa kuzingatia lengo linalokubalika na mwelekeo wa mazungumzo unaojihusisha nao”.
Hivyo H. P. Grice “Mawasiliano ni kitendo cha ushirika ambacho kinahitaji jitihada za pamoja kati ya msemaji na msikilizaji”
Pia kuna kuwa na seti ya malengo ambayo yanafahamika kati ya mzungumzaji na msikilizaji
-           Kuna kuwa na muelekeo wa mazungumounaoelekeza nini cha kusema nini si cha kusema ktika mawasiliano.
VIKANUNI  VYA KANUNI KUU YA USHIRIKIANO  (Comperative Principles)
Inajengwa na vikanunu (axims) vidogo vidogo 4:-
            1.         Kanuni ya kiasi  (maxims of quantity)
Inasema “Toa taarifa inayohitajika kulingana na lengo la mawasiliano, usitoe taarifa zaidi ya ile inayohitajika na pugufu ya ile inayohitajika.
            2.         Kanuni ya ukweli (maxims of quality)
Inasema “Usiseme jambo lolote unaloamini kuwa ni uongo”  usiseme jambo uliloweza kulidhibitisha.
            3.         Kanuni ya Uhusiano (maxim of relation)
                        Inasema “sema yanayohusiana na mada au jambo linalozingumzwa”
            4.         Kanuni ya Njia au Jinsi (maxims of manner)
Inasema “Epuka maneno au miundo isiyoeleweka.  Epuka utata, sema kwa
kifupi , sema kwa mpangilio mzuri.
            UKIUKWAJI WA KANUNI YA USHIRIKIANO
            Pamoja na kwamba Grice anaisisitiza kanuni ya ushirikiano kwa wasikilizaji
huivunja kanuni hii kwa kuvunja vikamini vidogo vidogo.
Hali hii ya kutozingatia vikanuni vidogo vidogo vya ushirikiano anapojitokeza msikilizaji hulipua na kunyamaa maana za msemaji katika muktadha husika hat kama maan hiyo hikutamkwa na mzungumzaji.
            Maana inayobaliwa na kung’amuliwa na msikilizaji huitwa VIMANILIZI
            VIMANILIZI (IMPLICATIVE)
            Ni maana anyegundua msikilizaji hata kama haikuelezwa bayana na msemaji, au
Ni yale yasiyosemwa ambayo tunagundua kupitia yaliyosemwa, au
Ni kile kinachomaanishwa na msemaji ingawa hakikusemwa bayana.
            Mfano
1.            Msemaji         A:        Mzee yupo?
B:         Gari lake halipo
                        Kimanilizi hapa ni hayupo            -           Angekuwapo na gari lake lingekuwepo

2.            Niliposikia kuwa mwanafunzi amejinyonga nilijua tu kuwa ametoka Iringa

3.            A:        Ninaonekanaje leo
B:         Kiatu chako kizuri
Maana hujapendeza ila tu kiatu chako .
            AINA ZA VIMANILIZI ZIPO 2:
i)                   Vya Mazungumzo
ii)                 Vya kaida
VIMANILIZI  VYA MAZUNGUMZO
Ni vile ambavyo utokeaji na uelewakaji wake hutegemea muktadha wake mazungumzo..
Ndio hasa hutokana na ukiukwaji wa kanuni ya ushirikiano kwa kuvunja vikanuni vyake vidogo vidogo.
Mfano:            -           Mzee hapo juu
·         Naonekanaje
A         -           Tutakwenda kwenye shoo ya Diamond Dar live jumapili usiku?
B          -           Nina jaribio la semantiki Jumatatu kimanilizi ni sitakwenda

A:        Hilo dirisha lililowazi linapitisha baridi kalli
B:         (Haongei kitu) – anafunga tu dirisha kwa kutenda)
            Kwasababu anang’amua maana ya msemaji A isiyo ya moja kwa moja.
            Kimanilizi ni fungu dirisha
A:        Nimeishiwa mafuta kabisa katika gari langu
B:         Kituo cha mafuta kiko pale kwenye kona.
A:        Umeolewa?
B:         Nina watoto sita
Kimanilizi     -           Nimeolewa na kwa muda mrefu
                        -           Amevunja kanuni ya kiasi
A:        Vipi boom limeisha
B:         Unauliza makoji polisi?
A:        Mume wangu kati yangu na bia nani bora?
B:         Ebu acha kufananisha mambo ya kijinga na bia wewe.  Kimanilizi – Bia ni bora kuliko mke.
            2.         VIMANILIZI KAIDA (CONVENTANAL)
Ni vile ambavyo upatikanaji, utokeaji na uelewekaji wake hautegemei kwa kiasi  kikubwa muktdha wa mazungumzo.
Hazitegemei zaidi kanuni ya ushirikiano na hivyo havitokani na ukiukwaji na uvunjwaji wa vikanuni ya kanuni hiyo badala yake vimanilizi  hivi hutegemea maana ya kipagmatiki ipatiikanayo moja kwa moja kutokana na maneno fulani fulani yaliyotumika.  Baadhi ya maneno hayo ni kama kikini, ingawa, kwa hiyo, kwasababu japokuwa n.k.
Mfano             -           Amina ni mchaga kwa hiyo anajua sana kutafuta hela.  Kimanilizi   -            Wachaga wanajua kutafuta hela
Kijana Yule ni mfupi lakini sio mbishi hata kidogo.
Kimanilizi     -           Wafupi ni wabishi.
-           Huyu wa sasa atakuwa mke mwema kwasababu alizaliwa na kukulia kijijini.
Kimanilizi     -           Wanawake kutoka kijijini, ndio wema
                        -           Katika harusi ya nuru hata James alihudhuria
Kimanilizi     -           Haikutarajiwa James ahudurie katika harusi hiyo.
            NADHARIA YA TENDO UNENI (SPEECHPERIOD)
John Austin (1962) anajadili kuhusu Nadharia ya TENDO – UNENI katika kitabu chake kiitwacho “How To Do Thing With Word” (Jinsi ya kutenda kwa kunena).  Ndiye alituzindua kwamba tunweza kutenda matendo fulani fulani kwa kunena tu, yaani kwa maneno usemayo.
Mfano:            -           Naahidi kuishi nawe katika shida na raha.
Natangaza rasmi kuwa mkutano umefunguliwa
Nakuonya  kuwa sheria itachukua mkondo wake
Nambatiza mtoto huyu “Zebedayo”.
Ingawa sentensi hizi zipo katika muundo wa kimaelezo lakini zifanye  kazi zaidi ya kueleza au kuto taarifa ya jambo.  Sentensi hizi ni vitendo au sehemu ya vitendo ambavyo msemaji anatenda kwa njia ya kusema.

Hii humaanisha kuwa kwa kusema tu sentensi basi msemaji anakuwa ametenda tendo husika vipengele 2 muhimu:
(a)         Sema tendeshi (Pperfomantive Uherance)
(b)         Vitenzi tendeshi (Performative base)
SEMO TENDESHI
Ni zile ambazo kusemwa kwake ndio kutendwa kwa vitendo vinavyodokezwa na vitenzi vilivyo tumika katika sehemu hiyo.
VITENDI TENDESHI
Ni vile ambavyo kusemwa kwake ndiyo kutendwa kwa tendo lililobebwa na kitenzi hicho.
Mfano             Ahidi, Tangaza, onya, Batiza, Pinga, Alika, Kemea, Shauri, Shukuru,
Samehe n.k.

Hata hivyo ni vizuri kwamba si kitu kitenzi ni tendeshi na si kitu semo ni semo tendeshi hivyo zipo semo na vitenzi ambavyo si tendeshi kwa sababu kusemwa kwake si kutenda tendo lolote
Mfano:            Ninafundisha darasani, Mwajuma anasema  -    Hizi ni semo lakini si tendeshi
                        Soma, fundisha – si vitendi tendeshi.
MASHARTI YA TENDO UNENI
Austin anadai leunu “Matendo Uneni haya kamiliki ati tu mtu Fulani ameona hivyo na
wala haya  kamiliki tu kwa semo au vitenzi tendeshi tu hivyo kuna masharti ambao
lazima yatimia ndipo tendo uneni husika likamilike.  Masharti hapo katika makundi 3 na
kila kundi lina masharti mawili.
KUNDI A
a)            Lazima kuwe na utaratibu wa kiulimwengu juu ya utendaji wa tendo hilo na
kwamba athari au matokeo ya tendo hilo yajulikana mahali pote.

b)           Mazingira na watu wanaohusika katika uneni wa tendo husika lazima wawe
muafaka (rasimi)
      Mfano             Hukumu        -           Atoe  hukumu na awe mahakamani
            KUNDI B
i)                   Utaratibu wa kutenda au kutekeleza tendo husika lazima ufatwe kwa usahihi.
ii)                 Utaratibu huo lazima ufuatwe kwa ukamilifu.
KUNDI C
i)                   Aghalabu wahusika lazima wawe na mawazo, hisia na dhamira ya kweli ya kufanikisha tendo husika.
Mfano             Naahidi kukupa million moja mwishon mwa mwezi 
-           Unapaswa kutekeleza.
ii)                 Iwapo wajibu ambao unatakiwa kutimizwa baada ya tendo uneni unafahamika basi watu wanaohusika wautimize au wautekeleze.
HALI MARIDHAWA KATIKA MATENDO UNENI
Austini anasema Mbali na masharti ya matendo uneni, ili tendo uneni litimie lazima kuwa na hali maridhawa
Ni jumla ya vigezo au sifa ambazo teno uneni husika huhitaji kukidhi ili tendo uneni hilo liwe halali au hilimivu.
a)            Hali za jumla
      Hujumuisha wahusika kufahamu au kuelewa lugha inayotumika.
b)           Hali zinazohusu muda au wakati yaani uzingativu wa muda ambapo tendo uneni
husika linapaswa kutekelellzlllllllllwa na kukamilika.
                        Mfano             Ahadi             -           hukamilika baadaye
                                                Amri               -           muda huo huo

c)            Hali za kimaandalizi yaani mazingira au mamlaka ya msemaji katika kutimiza
tendo uneni husika.
d)           Hali zinazohusu dhamira zinahusu msemaji au wahusika kuwa na dhamira ya
dhati katika tendo litendwalo
e)            Hali madhubuti yaani ubadilikaji wa ukweli wa mambo au ulimwengu baada ya
Uneni ikilinganishwa na hali iliyokuwa kabla ya tendo uneni.

            AINA ZA MATENDO UNENI
            Austini (1962) aliainisha aina 3 za matendo uneni:
i)                   Kisemwacho (semo) Locutionary act)
Huusu usemaji wa sentensi yenye maana inayoeleweka na yenye kitu kinachorejelewa.
Mfano             Ninakushauri uacha tabia mbaya.
ii)                 Lengo la kusema (illocutionary act)
Huhusu lengo la msemaji atika kile akisemacho
Mfano             Ninakushauri uacha tabia mbaya   -  Kuonya au kushauri
iii)              Athari au matokeo (Perocutionary) ya semo.
Huhusu athari au matokeo ya kile kisemwacho kwa msikilizaji.
Mfano             Ninakushauri uache tabia mbaya 
- Athari itategemea msikilizaji kama ataacha hiyo tabia au hataacha
                        Matokeo / Athari inaweza kuwa yale yaliyokuwa yametarajiwa au kukusudiwa
au la
Ni majibu ya msikilizaji kimwili kimaneno, kisaikolojia, kiakili n.n.
            AINA ZA MATENDO UNENI ZILIZO BORESHWA NA SEARLE (1969)
Ameboresha za Austina “Searle anasema kuna aina nyingi za matendo uneni na labda hazina ukomo.
Hii ni kwasababu aina hizo hutegea lengo, muktadha na hata lugha husika. Searle anapendekeza aina za ziada kama zifuatazo:
i)                   Ahadi (Commisives)
Ni matendo uneni ambayo humfunga msemaji katik  utekelezaji wa kilichonenwa hapo baadaye.
Mfano             Ahidi, Zawadia n.k.
ii)                 Maelekezo (Directives)
Ni matendo uneni ambayo hulenga kuchochea jambo fulani lifanyike na msikilizaji kama atakavyo msemaji.
Mfano             Amrisha, Amuru, Omba, Onya, Shauri, Pendekez, Sihi n.k.
iii)              Hisia (Expressives)
Ni matendo uneni ambayo huthirisha hisia imani, mitazamo au mawazo ya msemaji juu ya jambo fulani.
Mfano             Fariji, Laumu, Samehe
iv)               Matamko
Ni matendo uneni ambayo kunenwa kwake hubadili ukweli fulani wa mambo katika dunia.
Mfano             Jiuzulu, Taliki Talaka, Fungua (mkutano) au funga (mkutano,
hukumu, Oza, Tangaza n.k.
v)                 Uwakilisho (Representatives)
Ni matendo uneni ambayo hueleza kile ambacho msemaji huamini kuwa kweli au si kweli.  Hujumuisha maelezo – shadidio, na mahitimisho
Mfano             Lulu hakumuona Kanumba.  Wasichana wa mjini hawana mapenzi ya kweli.
            DHANA ZA PRAGMATIKI
            Ushanilizi
            Uolezi
            Uchopezi
UDHANILIZI
Unahusu maana inayoibuliwa katika mktalha ambao msemaji  hudhani kuwa msikilizaji ana taarifa za awali juu ya kile kisemwacho sasa.
            Mfano             Simu yangu ni ya kichina taarifa ya awali ni kwamba nina simu
            AINA ZA UDHANILIZI
1)            UDHANILIZI WA KWELI
Ni udhanilizi ambao hujikita katika ukweli wa mambo ambapo jambo au tukio linalodhanilizwa huwa limetokea au imetendeka kweli.
Udhanilizi huu una vitenzi maalum kama vile:
Mfano             Sikujua kuwa Eli ni Mchumba
Nasikitika sana Musa kufukuzwa kazi
Najuta kupenda nipopenda
2)            UDHANILIZI USIOKWELI
Ni udhanilizi ambao hujikita katika taarifa ambayo kinachodhaitizwa au kinachosemwa hakina ukweli wowote.
      Hutumia vitenzi kama vile Out, dhania, fakiri, jifanya, hisi n.k.
Mfano             Niliota ni mekuoa.
                        Udhamilizi hajanisa
3)            UDHANILIZI ULIZI
Ni aina ya udhanilizi ambao hudhaniliza kwamba kauli inayofuatia neno ulizi ni kweli
Mfano:            -           Lini ulializa chuo kikuu?
Udhamilizi:   -           Nilimaliza Chuo kikuu.
                                    -           Mume wako ameachalini kutembea na watoto wa shule?
Udhanilizi:   
i)                   Una mume
ii)                 Mume wako anatabia ya kutembea na wanafunzi
UOLEZI
Ni uoneshaji maalum wa vitu, watu, mahali, hali n.k. katika muktadha husika kwa kutumia maneno yaani violezi.
Ni tofauti na uoneshaji wa kawaida ambao hutumia viungo vya mwili hususani vidole.
Kuna maneno maalumu katika lugha ambayo hutumika kufanya ulejelezi wa kimuktadha, maneno hayo huitwa VIOLEZI
Mfano             Viwakilishi Yule, hapa, kule huyu n.k. maneno yatumikayo katika uolezi yaani violezi aghlabu hayana maana ya kudumu bali kupata maana zake kutokana na kila kinacholejelewa kutokana na muktadha husika.
Mfano             Ukija YEYE utamkuta PALE itabidi usubiri kwa dakika 40 kisha MIMI nikija tutakwenda kuwaona ili tuwarejese HUKU nao watupatie KILE kingine.
AINA ZA UOLEZI
1)            UOLEZI NAFSI
Ni uolezi unaotumia viwakilishi vya nafsi kama violezi vyake mfano katika kisu vipo sita
                        Mimi              -           Sisi
                        Wewe             -           Ninyi
                        Yeye               -           Wao
Mimi sipendi tabi hiyo
*   Mimi / Sisi hurejelea wazungumzaji
*   Wewe /Ninyi  hurejelea wasikilizaji
*   Wao / Yeye hurejelea mtu mwingine watatu ambaye ama hayupo mahali / wakati wa mazungumzo au kama yupo basi hajihusishi moja kwa  moja na mazungumzo.
2)            UOLEZI WAKATI
      Ni ulejelezi wa kimuktadha unaohusu mda / wakati wa utendekaji wa jambo,
violezi vyake ni vielezi vya wakati ie Sasa, kesho, leo, baadaye, mtondogoo n.k.
Mfano             Nitakuja kesho.
3)            UOLEZI MAHALI
Ni uolezi unaohusu msemaji na msikilizaji kuhusishwa na mahali ambapo
mawasiliano yanatokea.
Mfano             hapa, huku, humu vinarejelea mahali ambapo ni kirani na  
Mzungumzaji.
*   hapo, humo, huko                Mahali jirani na m sikilizaji
*   Pale, mule, kule                     huonyesha mahali ambapo ni mbali kwa wote
wawili.  Vipo violezi vya mahali ambavyo vinafahiwa ya ndani ya mfano humu,
humo na mule
4)            UOLEZI MWELEKEO
Ni uolezi unaohusu nafasi ya kitu kimoja kimwelekeo kikilinganishwa na nafasi ya kitu kingine .
Mfano             Mbele, Nyuma, klia, kushoto,  juuu, chini
                        Njoo mbele / Nyuma.
5)            UOLEZI JAMII
Ni uolezi ambao hutokea ambapo maana ya tungo inategemea uhusiano wa kijamii kuweza kueleweka na uhusiano huu hurejelewa na maneno fulani fulani hupata maana yanapotumika kwa kuhusianishwa na watu wa kaida fulani katika jamii.
Mfano             Mzee, Mama, Bwana.
                        -   Ndio mzee nimekuelewa ie hutumika kuonesha heshima
                        -   Samahani mama hivi kituo cha dala dala kipo wapi?
                        -   Ngoja tutamwendea kwa babu
·         Mtu fulani mahususi anayetumika kutatua matatizo ya watu.
·         Kikombe  -           hurejelea pombe
·         Kiti           -           Jamani tuheshimu kiti – hurejelea mamlaka (mkutanoni)

DHANA YA UCHOPEZI
1)            Ni uhusiano wa sentensi mbili ambapo ukweli wa sentensi ya pili huridhishwa na
sentensi ya kwanza.
Mfano             :           Athumani amemuoa Asha
                                    :           Asha ameolewa na Athumani
                                    :           Mwalimu amefundisha somo la Sintaksia
                                    :           Somo la Sintaksia limefundishwa
                                    :           Jakaya Kikwate ni Raisi wa Tanzania
                                    :           Tanzania inaongozwa na Raisi
            Ni kama unahusisha sentensi

2)            Kimantiki hatuoni uhusiano wake wa moja kwa moja na taaluma ya pragmatic.
      Mfano             -           Viongozi wengi wa Tanzania si Waaminifu
-           Tanzania ina viongozi ambao si waaminifu.
           
            Ili mawasiliano ya lugha yaweze kufanyika maneno ya lugha yapangwe kwa mpangilio
maalumu.  Jadili kauli hii kwa mifano kuntu nay a kutosha.

            KANUNI
            Fonolojia
                        Mkazo wa sauti
                        Barabara
                        Lafudhi
           







Powered by Blogger.